Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,777
- 41,071
Utamu wa embe dodo, nawaambia vijana,
Ni embe lisilo nyodo, mfano wake hakuna,
Hamuye ninayo bado, kwa mengine mimi sina,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Nilipoona bolibo, nilidhani nimepata,
Nikalipigia chabo, tamaa ikanikuta,
Sikutaka embe robo, lilo zima nikangata,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Mdomo nikajilamba, bolibo nikisifiya,
Na wimbo nikauimba, utamu nikisikiya,
Na mguno kama komba, mtini akirukiya,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Harufu nikanusiya, embe dodo li mtini
Hamu ikaniingiya, bolibo sikutamani,
Haraka nikakimbiya, nisiingizwe mjini,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Mwili ukinitetema, nikashika mkononi,
Huku miye ninahema, dodo embe la thamani,
Nikaliminya kupima, jinsi lilivyo laini,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Kwa upole nikamenya, dodo nililotungua,
Na kidole kikapenya, nikaanza kutumbua,
Bolibo sikuyasanya, madodo nikachukua,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Kufurahia utamu, ni kufyonza kokwa lake,
Dodo litakupa hamu, mengine usiyatake,
Mimi leo ni mwalimu, mengine yana makeke,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Beti zangu nazifunga, embe langu najinoma,
Madodo hasa ya Tanga, hakika hayana noma,
Mdudu hatanivunga, na wala sitamtema,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!!
Ni embe lisilo nyodo, mfano wake hakuna,
Hamuye ninayo bado, kwa mengine mimi sina,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Nilipoona bolibo, nilidhani nimepata,
Nikalipigia chabo, tamaa ikanikuta,
Sikutaka embe robo, lilo zima nikangata,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Mdomo nikajilamba, bolibo nikisifiya,
Na wimbo nikauimba, utamu nikisikiya,
Na mguno kama komba, mtini akirukiya,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Harufu nikanusiya, embe dodo li mtini
Hamu ikaniingiya, bolibo sikutamani,
Haraka nikakimbiya, nisiingizwe mjini,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Mwili ukinitetema, nikashika mkononi,
Huku miye ninahema, dodo embe la thamani,
Nikaliminya kupima, jinsi lilivyo laini,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Kwa upole nikamenya, dodo nililotungua,
Na kidole kikapenya, nikaanza kutumbua,
Bolibo sikuyasanya, madodo nikachukua,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Kufurahia utamu, ni kufyonza kokwa lake,
Dodo litakupa hamu, mengine usiyatake,
Mimi leo ni mwalimu, mengine yana makeke,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!
Beti zangu nazifunga, embe langu najinoma,
Madodo hasa ya Tanga, hakika hayana noma,
Mdudu hatanivunga, na wala sitamtema,
Nimekula embe dodo, bolibo sitaki tena!!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)