Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Simulizi nzuri sana kaka UMUGHAKA kama kawaida ya simulizi zako, huwa zinahuzunisha, kufurahisha na kufundisha.
Naimani wengi tutakuwa tumejifunza, mengi katika maisha haya hasa vijana.

Mwenyezi Mungu akubariki, wewe pamoja na familia yako. Malengo yenu yatimie na siku moja muishi mkoa mmoja na familia yako.
Wakaka zetu wa Kikurya ni wapambanaji na wasio na uoga kabisa. Kanda maalumu Mara 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
 
Simulizi nzuri sana kaka UMUGHAKA kama kawaida ya simulizi zako, huwa zinahuzunisha, kufurahisha na kufundisha.
Naimani wengi tutakuwa tumejifunza, mengi katika maisha haya hasa vijana.

Mwenyezi Mungu akubariki, wewe pamoja na familia yako. Malengo yenu yatimie na siku moja muishi mkoa mmoja na familia yako.
Wakaka zetu wa Kikurya ni wapambanaji na wasio na uoga kabisa. Kanda maalumu Mara
Karibu Mara Karibu Tarime
 
yani tumetoka kote uko kumbe sababu ni Rehema ... nmekua disappointed sana
mi nilidhani sijui ulikumbwa na balaa gani, kumhe demu ndo kakulostisha Daaah!! yani matukio yote uliopiga umeangukia pua kisa Rehema... aah umezingua sana .... Bora ingekua unatakiwa kumtoa bi Mkubwa hapo ningesapoti yani Demu mwanangu Demuuu aah nmeumia sana
Huyo Demu aliyemuangusha UMUGHAKA alisema ndiye mke wake kwa sasa.
 
Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 23.



Sikutaka kabisa kupoteza muda,baada ya kufanikisha lile zoezi la ununuzi wa chupi nilimtafuta Rehema nikajaribu kuongea nae na kumshawishi kuhusu ile zawadi.

Rehema "baby sasa size yangu umeipatia kweli?"

Mimi "Nimejitahidi baby wala usijali!"

Rehema "Zikinibana utazirudisha?"

Mimi "Nitakununulia nyingine!"

Rehema "Mmh haya bwana!"

Aliendelea "Uko wapi?"

Mimi "Natoka mjini naelekea nyumbani"

Rehema "Umefika wapi?"

Mimi "Bado nipo mjini"

Rehema "Pita basi Sokoni unisubiri nikusanye madeni yangu halafu tuondoke wote nyumbani!"

Mimi "Ila sina gari nimeipeleka gereji!"

Rehema "wewe pita bana kwani mpaka uwe na gari?"

Mimi "sawa nakuja mama"


Niliondoka kupanda gari nikashukia pale Ilala sokoni ambapo nilimpigia simu Ray akawa ameniambia nimsuburi mahali kwanza achukue hela zake,sasa baada ya kumalizana na watu wake alikuja akiwa amevaa mini sketi na tisheti nyupe iliyompendeza kupita kiasi,jioni ile sasa ndipo niliuona uzuri na umbo la Rehema kwa umakini na kiukweli alizidi kuichanganya akili yangu,kiukweli ni mwanamke ambaye Mungu alimjaalia umbo zuri sana,ingawa alikuwa na sura ya kawaida na alikuwa ni mwanamke fulani asiyekuwa na makuu,ulikuwa ukimuangalia kichwani alipenda sana kusuka Yeboyebo,pamoja na shepu yake kunichanganya lakini nilijikuta tu kadiri siku zilivyokuwa zikisonga ndipo nilimpenda kuzidi.

Mimi "Umependeza!"

Rehema "Sasa nimependeza na nini!"

Mimi "Kwahiyo wewe hujioni?"

Rehema "mmh aya bwana"

Aliendelea "Nipe basi hela ninunue mahitaji twende tukapike!"


Nilichukua elfu 20 nikampatia akawa ameniachia mkoba wake nimshukie na yeye aliondoka kuelekea tena sokoni kwa ajili ya kununua mahitaji.Baada ya kukamilisha alirejea tena akiwa amefungasha mazaga ya kutosha kwenye mifuko.

Mimi "Madumu ya juisi umeyaweka wapi?"

Rehema "Leo namshukuru Mungu nimemaliza mapema,nilirudi tu kuchukua hela maana watu wateja wangu wengi huwa wananilipa jioni hivyo huwa narudi kwanza nyumbani"

Mimi "sawa"

Tulipanda gari kuelekea Gongo la mboto na tulipofika tu nyumbani Rehema hakutaka mambo yawe mengi,aliniambia nimpatie chupi zake nilizokuwa nimenunulia kama zawadi azijaribu,alichukua lile begi langu ambalo ndani niliiweka ile dawa pamoja na zile chupi akawa amefungua zipu na kutoa zile chupi akaanza kujaribu moja baada ya nyingine,chupi zote zilimtosha kana kwamba alikuwa ametengenezewa yeye!,alifurahi sana.

Rehema "Kweli unanipenda nimeamini!"

Mimi "Kwanini?"

Rehema "Kama nimekuvulia chupi mara moja na umekiona kiuno changu na hujakosea basi wewe ndiye mume wangu naamini!"

Kauli ile ya Rehema ilizidi kunichanganya sana kiakili.Nilipaswa zile chupi nizitie dawa kabla ya kuzivaa ili akishaivaa ile nyekundu kazi ianze mara moja lakini nilijikuta ndiyo upendo unakolea sana na nilipokuwa nikimtazama ile shepu yake wakati anabadili zile chupi ni hakika ni kichaa tu ndiye angekubali kumpoteza Rehema.
Sasa baada ya Rehema kuanza kuweka mazingira ya kupika kule nje,niliichukua ile dawa nikaiweka mfukoni nikawa nimetoka nje.Sasa mahali nilipokuwa nikikaa mimi hakukuwa mbali na lerini(leri ya kati),niliondoka kuelekea huko lerini na nilipofika niliitupa ile dawa pembezoni mwa leri vichakani kisha nikarudi zangu nyumbani mdogo mdogo!.

Nilipofika nyumbani nikiwa nimewasha luninga naangalia,ghafla simu ya Ally Mpemba ikawa inaita,niliingalia ile simu kidogo nisiipokee ila niliamua kuipokea.

Ally Mpemba "Habari ya jioni master"

Mimi "Nzuri kaka,za huko"

Ally Mpemba "Uko wapi?"

Mimi "Nipo nyumbani kaka"

Ally Mpemba "Nilikuamini ila umejikosesha mwenyewe,jitafakari?"

Aliendelea "Kuna mtu naomba umkabidhi funguo wa nyumba yangu"

Mimi "Lakini kaka nimefanya mistake tu "

Ally Mpemba "wewe bado dogo haya mambo yatakugahrimu,shauri yako!"


Baada ya jamaa kuniambia vile akawa amekata simu,mimi niliamua likalotokea ngoja litokee lakini kiukweli sikutaka kabisa kumtoa kafara mwanamke mzuri Rehema ambaye hakuwa na hatia hata kidogo ingawaje pia nilikuwa nikimpenda sana tu!.Wakati nikiwa sebuleni Rehema alikuja kuniita ndani akisema kuna mtu ananiita nje.
Sasa nilipotoka nje nilikutana uso kwa uso na Farah na kiukweli mwanamke yule alikuwa akifanana sana na Maya na sikuwahi kuelewa alikuwa ndiye wa dukani pale kkoo au huyu yeye alikuwa ni nani?maana yule wa kkoo yeye aliwahi kuniambia hakuwepo kwa muda wa wiki 2,sasa Je huyu ni nani?,hilo lilikuwa ni swali gumu sana kwasababu hakuna aliyeweza kunipatia majibu.

Farah "Habari yako Master?"

Mimi "Nzuri dada Farah "

Farah "Naomba funguo wa nyumba"

Niliingia ndani kuchukua funguo kisha nikamletea,baada ya kumpatia ule funguo akanishukuru kisha akawa anatoka nje nami nikawa namsindikiza,sasa lengo langu ni tutoke nje nimuombe aongee na Ally Mpemba aniombee msamaha kwa kile nilichokuwa nimekifanya,sasa baada ya kutoka nje niliikuta ile Range ikiwa imepaki na sikutaka kabisa kusubiri ikabidi nimuulize funguo wa ile gari ameitoa wapi wakati mara zote nilikuwaga nikiiacha ndani ya ile nyumba na funguo wa nyumba ndiyo alikuwa amekuja kuuchukua!.Nilibaki nikishangaa sana.

Mimi "Dada nilikuwa nakuomba niongee nawe kidogo!"

Farah "Kesho tuonane!"

Mimi "Sawa"


Alipanda kwenye gari akawa ameondoka.Nilidhani uenda yeye alikuwaga na funguo wa lile gari lakini nilizidi kuchanganyikiwa kwasababu lile geti la ile nyumba lilikuwa limefungwa.Sikutaka kabisa maneno na Ally Mpemba kwasababu ni mtu aliyekuwa akiniamini sana na nilitaka kufanya kila kinachowezekana nimuombe msamaha.

Rehema "Huyo ni nani?"

Mimi "Ni mdogo wake na bosi wangu!"

Ilikuwa ni mara chache sana mimi kulala pale nyumbani kwangu tangia nimejuana na Ally Mpemba kila mara anapokuwa akisafiri,mara zote ambazo anakuwa hayupo nilikuwa nikilala pale kwake kwenye ile gari ndogo ambayo alinipatia.Sasa kwakuwa nilikuwa nishaharibu alinikataza kabisa mimi kulala pale kwake hadi nifanye jambo nililokuwa nimeelekezwa na Mzee wa Chumbe.

Ilipofika asubuhi baada ya kuamka nilijiandaa ili nielekee kwenye kazi yangu ambayo ilinipeleka pale Kkoo,nilipoondoka nyumbani niliamuacha Rehema akiwa amelala na niliamuambia akiondoka afunge nyumba na funguo aziache kwa demu wa Steve.Sasa nilipofika kkoo nilikuta tayari dada Farah amekwisha kufungua duka na swali lake la kwanza ni mbona tangia juzi sikuonekana?.

Farah "Sijakuona tangia juzi,kwema lakini?"

Mimi "Tangia juzi dada wakati jana umekuja nyumbani!"

Farah "Nije kwako hata napajua?"

Mimi "Dada wewe si jana umefata funguo wa nyumbani kwa kaka Ally!?"

Farah "Weeeee!....mjini hapa,isije ukawa umetapeliwa funguo za nyumba ya watu!"


Aliponiambia vile ndipo nikazidi kuchanganyikiwa na nikaona yawezekana kuna mchezo akawa uenda ananichezea pasipo mimi kufahamu!.

Mimi "Kwani dada nyie kwenu mko mapacha?"

Farah "Kwanini?"

Mimi "Nimeuliza tu!"

Farah "Hivi kweli wewe uko sawa?,nisije kuwa nazungumza na chizi!"

Mimi "Tangu lini nimekuwa chizi Aunt Farah?"

Farah "Vitu unavyoongea sikuhizi havieleweki kabisa master,umekuaje?"

Mimi "Dada mimi mbona niko kawaida!"

Farah "Ni juzi tu umetoka kuniambia nimefungua duka wakati mimi sikuwepo,haya leo tena umekuja na mpya kwamba nimekuja kwako kuchukua funguo za Ally?"

Aliendelea "Umewahi kuniona hata sura?"

Baada ya swali lake sikujua nimjibu nini kwasababu kila nilochokuwa nikimwambia alikuwa akiniona kama mwendawazimu na mara zote imekuwa ngumu sana kumjua Farah kwasababu amekuwa akivaa Nicab asubuhi hadi atakapofunga duka.Sasa ile siku aliyokuja kuchukua funguo wa gari ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kumuona uso wake na wakati ananipigia simu aliniambia anaitwa Farah hivyo nikajua ni huyo mdogo wake na Ally Mpemba.Kiukweli hali ilikuwa mbaya sana.

Farah "Halafu pia umemfanya nini Ally?"

Mimi "Kwanini dada?"

Farah "Alinipigia simu akasema upishe karibu na duka "

Aliendelea "Ila sijamjibu"

Mimi "Mbona dada hakuna baya nililomfanya kaka Ally"

Basi baada ya yale maneno ya Aunt Farah nilifahamu kabisa hali ishakuwa mbaya sana,kibaya zaidi jamaa anahitaji niondoe biashara yangu kando ya duka lake,nilikaa kimya nikarudi kuendelea na kazi lakini kiukweli ni kama moyo ulikuwa ukinifukuta sana,nilinyanyuka kurudi dukani kwa Farah ili nimuulize swali na akinijibu nikishaelewa ningejua pa kuanzia.

Mimi "Kwani dada wewe huwa unapacha wako?"

Farah "Kwetu hatukuzaliwa mapacha!"

Mimi "Je,unamjua Maya?"

Farah "Maya?,ndiyo nani tena huyo mdogo wangu?"

Mimi "Kuna dada mmoja huwa mmefanana sana ndiyo maana nikadhani mlizaliwa mapacha"

Farah "Wewe unavituko sana,unamfananishaje mtu na mimi wakati hata sura yangu hujawahi kuiona!?"

Mimi "Sawa dada,Je Zahra unamjua?"

Farah "Zahra?"

Aliendelea "Eeh wewe umemfahamia wapi Zahra?"

Mimi "Unamfahamu?"

Farah "Ndiyo namfahamu!"

Mimi "Ni nani?"

Farah "Kwani wewe una nini?mbona naona mapicha picha tu!"

Mimi "Tafadhali Aunt Farah naomba uniambie kuna kitu utanisaidia na mimi nitakusaidia!"

Farah "Zahra alikuwa dada yangu toka ni nitoke ila kwasasa ni marehemu!"

Sasa kuna muda tunaongea tulikuwa tunasuburi wateja waondoke kisha wateja wakiondoka tunaendelea,kiukweli baada ya kumtajia Farah jina la Zahra alishituka sana na kushangaa,mimi kiukweli niliamua liwalo na liwe kwasababu ilivyoonekana ni kama Ally Mpemba alikuwa amenikataa na hata kama ningejipendekeza vipi asingenielewa.

Farah "Kaka Ally ndiyo alikwambia kuhusu Zahra?"

Mimi "Hapana dada!"

Farah "Ok wewe Zahra umejuaje na kuna kitu gani kumuhusu?"


Inaendelea: Sehemu ya 24
UMUGHAKA umeamua kumchomea kunguni ally mpemba 🤣🤣
 
Kwenye huu uzi kwa mara ya kwanza nimeshuhudia mambo mengi sana:-
1. Kuna wanaume wana wivu hadi kwa wanaume wanzao..
2. Kuna watu ni wajuaji wa kipumbavu kabisa...
3. Kwa mara ya kwanza nilikua nawahesabu warahabu/kiu ya simulizi...
4. Minyukano pia ilikua sio haba....
5. Kuna dogo mmoja alikua anataka kuazimisha umaarufu kupitia simulizi hii..
6. Mods wengi walikua wanafuatilia hii simulizi ya tata mulisya...
7. Ila huyu baba ametukanwa jamani...🤣 lakini alikomaa mpaka akamaliza simulizi na kufikia malengo yake.
 
Kwenye huu uzi kwa mara ya kwanza nimeshuhudia mambo mengi sana:-
1. Kuna wanaume wana wivu hadi kwa wanaume wanzao..
2. Kuna watu ni wajuaji wa kipumbavu kabisa...
3. Kwa mara ya kwanza nilikua nawahesabu warahabu/kiu ya simulizi...
4. Minyukano pia ilikua sio haba....
5. Kuna dogo mmoja alikua anataka kuazimisha umaarufu kupitia simulizi hii..
6. Mods wengi walikua wanafuatilia hii simulizi ya tata mulisya...
Hatari sana mkubwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom