Utajiri ni ile hali ya kumiliki mapesa mengi na kuwa na mali nyingi, utajiri ni mzuri kwa kuwa unakupa uwezo nguvu mamlaka sifa na umaarufu!kwa kifupi Utajiri ni kitu chema.
Watu wengi hutafuta utajiri kwa njia mbalimbali halali na haramu wao wanachotaka ni utajiri ili waweze kutimiza ndoto zao nyingi.
Sasa kuna wakati mtu hutafuta utajiri kwa njia za mkato hapa nazungumzia kwa njia za ushirikina na uchawi.
Utajiri huu ni mzuri na huja haraka lakini ukiwa na masharti mengi lakini kubwa likiwa ni kutoa kafara la damu kwa kuangamiza roho.
Unapoingia kwenye utajiri huu mwanzoni utafurahia na masharti utayaona mepesi lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda mambo hubadilika na tabu huanzia hapo.
Mwanzoni utaambiwa toa kafara la damu ya kuku baadae itakuja mbuzi, halafu itafuatia ng'ombe na mwishowe itakuja binadamu mmoja na hatimaye kwa makundi.
Hii yote ni kutaka kulinda utajiri wako usiporomoke na ukivunja masharti kila kitu kinaharibika .
Kuna pia masharti ya kujisaidia kulala kula kuvaa na hata matumizi ya vitu mbalimbali. Mwanzoni inakuwa ni rahisi tu kwenda sambamba nayo lakini mbeleni mambo hubadilika hasa pale watu wanapoanza kuhoji hiki au kile.
Wote tunajua jamii ya watu wenye ulemavu wa ngozi inavyoteketea kutokana na waganga wa kienyeji kuwaaminisha wateja wao kuwa viungo hivyo vikichanganywa na dawa nyingine huleta utajiri bahati nguvu na uwezo! Kuna zaidi ya waganga 300 kwenye mahabusu na Magereza mbalimbali wenye kesi zinazowahusisha na mauaji ya albino.
Jamani utajiri wa masharti ya namna hii haufai na mwishowe huwa na anguko kuu tunashuhudia visa vya kila aina kuhusiana na utajiri wa namna hii lakini kila uchao watu hawakomi kuendelea kuutafuta.
Hakika dunia inaumwa.
Mimi hii post naiangalia kwa mtazamo hasi kwakuwa mantiki yake ni kutuaminisha kuwa ni kweli utajiri wa ushirikina upo ila una masharti magumu. Katika kipindi hiki ambacho tuna pambana na imani POTOFU kwamba kumuua albino kunaleta utajiri au bahati, si kipindi cha kuwaeleza watu kuwa ukimuua albino utatajirika isipokuwa masharti yatakuwa magumu zaidi baadae.
Imani hizi huitwa POTOFU kwakuwa si kweli kwamba kumuua albino kutakufanya ufanikiwe ktk mipango yako.
Ndugu mshana, huoni kwamba post yako yaweza kuwahamasisha watu kutafuta utajiri kwa masharti yawayo yoyote yale ilhali si kweli.
Ndugu mshana hujagundua kuwa makabila au jamii zinazosifika kwa utajiri , nyingi husifika kwa ubahili pia???
Angalia WACHAGGA, WAKINGA, WAPARE....Makabila haya yanasifika kwa kufanikiwa ktk biashara, lakini pia yanasifika sana kwa Ubahili.
Ningependa kuwafahamisha wana JF ya kwamba, Hakuna kitu kinaitwa Utajiri wa ushirikina wenye masharti magumu, ila ili uwe tajiri lazima uzingatie "MASHARTI YA UJASILIAMALI" ambayo kimsingi ndiyo huitwa masharti ya kishirikina.
Nakuhakikishia ndugu Mwana JF, Fanya kazi kwa bidii, kuwa mbunifu, usiwe arrogant, fanya matumizi yale ya muhimu tu, epuka anasa, hakika utafanikiwa bila hata kuongeza kiungo cha albino au kumuua mtoto wako.
Acha kuua ndugu, acha kuua mtoto, acha kuua ALBINO. zingatia masharti ya Ujasiliamali, na utafanikiwa.
Mimi hii post naiangalia kwa mtazamo hasi kwakuwa mantiki yake ni kutuaminisha kuwa ni kweli utajiri wa ushirikina upo ila una masharti magumu. Katika kipindi hiki ambacho tuna pambana na imani POTOFU kwamba kumuua albino kunaleta utajiri au bahati, si kipindi cha kuwaeleza watu kuwa ukimuua albino utatajirika isipokuwa masharti yatakuwa magumu zaidi baadae.
Imani hizi huitwa POTOFU kwakuwa si kweli kwamba kumuua albino kutakufanya ufanikiwe ktk mipango yako.
Ndugu mshana, huoni kwamba post yako yaweza kuwahamasisha watu kutafuta utajiri kwa masharti yawayo yoyote yale ilhali si kweli.
Ndugu mshana hujagundua kuwa makabila au jamii zinazosifika kwa utajiri , nyingi husifika kwa ubahili pia???
Angalia WACHAGGA, WAKINGA, WAPARE....Makabila haya yanasifika kwa kufanikiwa ktk biashara, lakini pia yanasifika sana kwa Ubahili.
Ningependa kuwafahamisha wana JF ya kwamba, Hakuna kitu kinaitwa Utajiri wa ushirikina wenye masharti magumu, ila ili uwe tajiri lazima uzingatie "MASHARTI YA UJASILIAMALI" ambayo kimsingi ndiyo huitwa masharti ya kishirikina.
Nakuhakikishia ndugu Mwana JF, Fanya kazi kwa bidii, kuwa mbunifu, usiwe arrogant, fanya matumizi yale ya muhimu tu, epuka anasa, hakika utafanikiwa bila hata kuongeza kiungo cha albino au kumuua mtoto wako.
Acha kuua ndugu, acha kuua mtoto, acha kuua ALBINO. zingatia masharti ya Ujasiliamali, na utafanikiwa.
Utajiri una madaraja na kila daraja lina kafara lake mfano
Milioni 20-50 ni tofauti na milioni 100-200 na kila daraja huhitaji kitu kikubwa zaidi au damu nyingi zaidi
Lakini unaamini Biblia???
Ah wapi!
Siwezi kuamini kitabu cha riwaya mimi.
Wachagga ni kweli wanafanya hzo issue but zile ni mila (Mungu wa Asili) akina Musa, Ibrahim enzi hzo pia walikua wakitoa sadaka za wanyama. Ni mila na desturi kwa wachagga (Mara nyingi haitafuni watu).
Kama ni Mkristo (Lutheran) na uliwahi soma kipaimara miaka ya nyuma. Kuna topic inaelezea " Mungu wa Asili " as in beliefs za watu wa zamani kabla ya dini kuenea Africa (Dini ulio letewa na mzungu).
Tunachoongelea hapa ni Uchawi alias Ndumba. Issue za kishirikina (devil worshipping) mtu anafanya satanic things for unspeakable rewards.
Mimi ni mdau
Oh, ok. Wewe uko category gani kati ya hizo ulizotaja? Je nikitaka zaidi ya hizo inabidi nifanyeje?
boss hiyo ni imani yako tu.
wakinga wanatafuta hela mahali popote na wanaishi maisha ya kujibana ndio maana wanakuwa na mali pale wanapozipata.
matumizi mabaya ya kile kidogo unachopata yanakufanya usifanikiwe hata kidogo.
mkinga asubuhi anakunywa chai nyumbani, mchana analetewa chakula kutoka nyumbani, jioni anaenda kula nyumbani kwa nini asiwe na hela?
dukani kwake yupo yeye na mkewe ndio wauzaji akiweka msaidizi basi ni ndugu yake.
kwani wangapi wameenda kwa waganga na bado biashara zikagoma/kuanguka?
siku zote hata kwa anayetegemea mshahara, matumizi mazuri ya anachopata ndio mafanikio yake.
sio mtu kila siku asubuhi anaamkia supu ya kuku, mchana nyama choma na jioni kitimoto na bia juu.
huyu hawezi kufanikiwa.
post nzuri sema watu wapo kwenye mikutano ya kutangazia nia?
hapa si kweli mkuu, maofisini kumejaa uchawi sana. je hawa sio walioelimika? Adebeyo na kuishi ulaya ana amini mama yake anampiga juju,imani za kichawi zipo sana kwetu ngozi nyeusi.Kuamini sana ushirikina kunaenda sambamba na illiteracy level na umasikini.
Siku zote, jamii inayoamini sana ushirikina kwa kiasi kikubwa huwa haijaelimika na pia huwa ni masikini sana. Huo ndio ukweli, fanya observation utaliona hilo.
Hahaha,we OSOFIA ni sheeda sana.Halafu sijawahi ona albino Masai