Usiyoyajua sakata la shamba la Sumaye

Usiyoyajua sakata la shamba la Sumaye

Una Ng'ombe 1500 na shamba la ekari 1500 unashindwa kuchimba visima kweli hadi uhamishe mifugo yote kwa sababu ya ukame ? Utetezi wa Sumaye ni wa ki Mr Zero Mr Zero.
Hao ngombe 1500 anaosema alihamisha ni ngombe hewa hamna uthibitisho wala ushahidi wowote Ha ha ha
 
Ng'ombe 60 na mbuzi 150 wanahitaji hekari 450 kwa ajili ya kula?

Na wale wafugaji wenye ng'ombe elf 10 je?!wapewe mkoa mzima?
Kila mtu ana size yake anayohitaji kulingana na mapendekezo yake, hatuwezi kufanana kila kitu.
 
Nipe kwa ufupi Kama inawezekana
Alipelekwa kahaba ili ahukumiwe na hakimu (Bwana Yesu) akawauliza "asiyekuwa na dhambi awe wa kwanza kumpiga mawe" baada ya muda hapakuwa na aliyebaki zaidi ya yule kahaba.Hivyo kwa viongozi wetu wakikutana na hakimu mkuu hakuna wakubaki.
 
Sasa mnanaka chatu waishi wapi endapo kika mwenye eneo lake atawafukuza? Chat naye si rasmali ya taifa. Hivi hakuna viongozi wa juu wa CCM wanaomiliki maeneo au mashamba makubwa? Akina Ben "wapumbavu na malofa" nao watanyang'anywa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sumaye amechangia umwagaji wa damu Morogoro baina ya wakulima na wafugaji kwa kuhodhi ardhi kubwa peke yake Wilayani Kilosa. .Hali iliyowafanya wakulima na wafugaji wakose ardhi ya kufanyia shughuli zao na kuamua kupigana na kupelekea wauane kwa kugombea ardhi kidogo iliyopo.

Lakini tangu mpango huo uanze wa kunyang'anya mashamba yasiyoendelezwa visa vya mapigano Mkoani Morogoro hususani Wilayani Kilosa vimeisha kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwandishi angesaidia pia kujua huyo mwenye ekari 100,000/= ingekaa njema!!!

Nimepata shaka pia kutokana na majibu ya Lukuvi. Hivi huko Sekondari tunafundishwa kuwa Agriculture inahusisha Kilimo na Ufugaji. Sasa Sumaye kalima sehemu na nyingine anaitumia kufuga.

Je, kwa uelewa wa tunayoyafundisha kwa watoto wetu, hapo Sumaye ana kosa hadi afutiwe hati kwa kufuga?

Mchanganyo mchanganyo. Ila hizo 100,000/= wakisaidia tukajua ni za nani na ziko wapi itakaa njema sana.

Ekari 300-1000 hata raia wa kawaida tu wanamiliki na wengine hata Dar es Salaam na sasa hivi ndiyo mabingwa wa kukata Viwanja kwa vipimo vya Miguu huko Madale, Mbezi Louis, Chanika, Masaki (ya Kisarawe), Kiluvya (huku nako Sumaye alikuweko), etc.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sahihi Kabisa!

Sumaye alitakiwa aombe radhi kwa Wizi na uporaji aliofanya kwa kutumia Mamlaka yake ya Uwaziri Mkuu

Mbona hatujasikia kuwa ameshitakiwa kwa wizi. Inakuwaje mtu anunue kitu halafu aitwe mwizi tena? Kisa lake ni kuwa waziri mkuu?

Hata akina Accacia tumeingia nao mikataba sisi wenyewe la ajabu tunageuka tena na kuwaita wezi halafu tena tunaingia kujadiliana bao.

Hivi wezi huwa wanakaa na mwenye mali kujadiliana? Hebu tujiongeze kidogo jamani vinginevyo tunajidhalilisha. Ukinunua gari kihalali na kulipark nyumbani bila kulitumia unanyang'anywa??!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waandishi wetu ni Uchwara kweli kweli na Ndio Sababu wamevamiwa na kudhalilishwa na Makonda na baadae wao ndio wakaja kumuomba radhi Mvamizi!

Mwandishi Makini wa Habari ya Kiuchunguzi alipaswa kuelezea Historia ya Awali ya Sumaye kupata Shamba hili na Mgogoro ulioibuka wa Wananchi kupinga Sumaye kujimilikisha Eneo hili kwa jina la Mkewe kwa kutumia nafasi yake ya Uwaziri Mkuu!

Alipora hiki Eneo kutoka kwa Chama cha Ushirika na ililalamikiwa sana Hali hii mpaka kwenye Media na Majukwaa ya Kisiasa lakin Leo kwa unafiki wanajifanya kumhurumia

Shamba la Wizi haligeuki kuwa halali kwa kuw kuna maeneo umelima Lima kuzuga
Huyu mwandishi na muhariri wake wachukuliwe hatua na media council na serekali kwa uchochezi/mis reporting
 
Hivi! Kufuga pia si aina ya kilimo!!!
Huyu lukuvi kachanganyikiwa!!

Inakuaje mtu anathubutu kumiliki eneo kalibu kata nzima pekeako.
Sasa wewe umesimamia wapi? Unajua sijakuelewa kabisa upo kwa Lukuvi au Sumaye?
 
Alipelekwa kahaba ili ahukumiwe na hakimu (Bwana Yesu) akawauliza "asiyekuwa na dhambi awe wa kwanza kumpiga mawe" baada ya muda hapakuwa na aliyebaki zaidi ya yule kahaba.Hivyo kwa viongozi wetu wakikutana na hakimu mkuu hakuna wakubaki.
Kahaba mwenyewe awe Richmondi.....!
 
Back
Top Bottom