Hii ishu ya Mwalimu kuipiga Malawi mmeitoa wapi?
Kuna hotuba moja nilimsikia Mwalimu, wakati anaongelea ishu ya vita ya Uganda, alisema alilazimika kutuma ujumbe Malawi kwani Wafukunyuku walikuwa wameanza kuzusha kwa Kamuzu kuwa Mwalimu kamaliza kwa Amini sasa anakuja kwako.
Kwa hiyo kwa kifupi Mwalimu alisema Wazushi ndio walikuwa wanaeneza hizo habari ili hali hakuwa na sababu ya kupigana na Malawi.
Ingawa kweli Mwalimu alitofautiana na Kamuzu kwa ishu ya SA, hayo ya kupigana ilikuwa ni kazi za Wazushi.
Sasa nawe hapa naona umemuongeza na Machel.