RoadLofa
JF-Expert Member
- Mar 22, 2017
- 1,347
- 2,957
Maana kuna jamaa ni mfanyakazi mwenzangu nimekuwa na urafiki naye wakikazi kwa muda wa miezi mitano ila sijawahi kukaa naye sehemu hata moja kula naye bata, ila juzi tukiwa kwenye kikao cha kazini tukaenda kupanga lodge moja kila mtu room yake sema zinaangaliana milango.
Sasa mimi nilimwamini sana, kumbe wakati natoka kwenda nje jamaa alizama room kwangu na kuingia kwenye bag langu ambapo kulikuwa na Tsh 300,000 nakuiba 80,000, na nilijua kesho yake baada ya kuzihesabu pesa na kukuta zipo 220,000 badala ya 300,000 nikajua ni jamaa tu, tena nina bahati hakuamua kuniibia pesa zote yaani aliingia kwenye bag na kuzichambua vizuri na kuzirudishia kama alivyozikuta.
Nina bahati pesa nyingine nilikuwa natembea nazo kwenye pochi mfukoni na nina bahati mwizi aliamua kunihurumia.
Kiukweli hilo suala limenifanya kupunguza mazoea ya karibu sana na watu tunaokutana tu bila kuwajua vizuri na kwa mazingira ninayoishi sitokubali kupeleka mwanamke au mshikaji kushinda ghetto kwangu la sivyo natakiwa kuwa makini sana.
Sasa mimi nilimwamini sana, kumbe wakati natoka kwenda nje jamaa alizama room kwangu na kuingia kwenye bag langu ambapo kulikuwa na Tsh 300,000 nakuiba 80,000, na nilijua kesho yake baada ya kuzihesabu pesa na kukuta zipo 220,000 badala ya 300,000 nikajua ni jamaa tu, tena nina bahati hakuamua kuniibia pesa zote yaani aliingia kwenye bag na kuzichambua vizuri na kuzirudishia kama alivyozikuta.
Nina bahati pesa nyingine nilikuwa natembea nazo kwenye pochi mfukoni na nina bahati mwizi aliamua kunihurumia.
Kiukweli hilo suala limenifanya kupunguza mazoea ya karibu sana na watu tunaokutana tu bila kuwajua vizuri na kwa mazingira ninayoishi sitokubali kupeleka mwanamke au mshikaji kushinda ghetto kwangu la sivyo natakiwa kuwa makini sana.