Usiri wa mali katika ndoa

Usiri wa mali katika ndoa

utajiskiaje vibaya na mali za mwenzio?? tafuta zako. kwani mlioana ili urithi mali au umrithishe za kwako? ah! sijui bwana, mtajua wenyewe na ndoa zenu huko. Mi nahaingikia zangu kivyangu upande huu mwingine.

Hahaa haya bwana, nimekupata vizuri
 
Wanaume wengi ni watu hatari sana. Mi nimeshaona mwanaume anafariki ndipo anajitokeza mwanamke mwingine na watoto akidai kuwa ni mkewe pia. Watu tunamfahamu huyo mmoja aliyekuwa akiishi naye lkn kumbe kuna mwingine ambaye wengi wetu hatukumjua. Muda na siku alizokuwa akienda hata mkewe hajui. Ni hatarii sana.
 
[/B][/COLOR]

Naona una jazbaaa sana. rejea vitabu vitakatifu vinamtaka mwanaume afanye nini na mwanamke afanye nini.

Yan mwanamke ukinifanyia hivyo. Utafute mume kabisa.. Maana hapo itakuwa mwisho wa ndoa.. Hata kama ina 30yrs. Bora kuwa peke yako kuliko kuwa na kansa ndani ya nyumba.
 
Kwa kweli hii ni hatari sana,na kama unajijua ni mbinafsi unaoa kwaajili gani? Ni bora mwanaume huyo aendelee kutafuta kwaajili ya hiyo familia yake tu aliyozaliwa nayo......Ila bora hata huyo anawaambia hata ndugu zake mwingine hata ndugu zake hawaambii chochote mambo yake anafanya siri tu.

Sema wanawake pia hawaamniki, na wakioneshwa mali zote wanawaaondoa waume zao, lkn pia kama watoto ni wakubwa nini vema kuwashirikisha ,kuweka ktk maandishi
 
Tatizo unakuta mtu umekosea kuoa ndy matokeo ya hayo yote kujitokeza ever link

Mdada kila ukimpeleka mguu sawa yeye anabaki mguu upande...Ukimwambia mbelee geuka ye ndy kwanza anabaki kaduwaa kama sanamu la michellin

Ila amini kuwa mpaka mtu anakushirikisha jambo lake jua ana heshimu mawazo yako na ana imani na ww ...ukiona hujahusishwa na ww ni mtu wa karibu jua kuna walakini juu yako
 
Last edited by a moderator:
hali hii husababishwa na mwanamke kwa nionavyo mimi, kama unakuwa umejenga hali ya kutokuaminika kwa mumeo na ubinafsi wa kupitiliza.

ila basi wanaume muwakumbuke hata watoto wenu sio muwaache bila kitu.
 
Babu Dark City alishaelezea hapa kuhusu hili suala la kuandikisha mali kwa majina ya watoto. I hope atakuja atoe ufafanuzi zaidi kwa ajili ya wengi

Sijui watu tuwaelezeje. Kuandika mali kwa majina ya watoto haisaidii kitu kama zimepatikana ndani ya ndoa. Kama mtu anahisi mwezi wake hafai katika utunzaji wa mali achukue hatua mapema.
 
Sijui watu tuwaelezeje. Kuandika mali kwa majina ya watoto haisaidii kitu kama zimepatikana ndani ya ndoa. Kama mtu anahisi mwezi wake hafai katika utunzaji wa mali achukue hatua mapema.

Babu Dark City kwa faida ya wengi tufafanulie kwanini haisaidii , na mtu achukue hatua kama zipi?
 
Last edited by a moderator:
Sijui watu tuwaelezeje. Kuandika mali kwa majina ya watoto haisaidii kitu kama zimepatikana ndani ya ndoa. Kama mtu anahisi mwezi wake hafai katika utunzaji wa mali achukue hatua mapema.

Vevee.... wacha maneno yako hata kama ni Hakimu au jaji...kama tulifunga ndoa kimila na tuliafikiana suala la mali na mirathi kulingana na mila zetu zinavyotaka?
 
Vevee.... wacha maneno yako hata kama ni Hakimu au jaji...kama tulifunga ndoa kimila na tuliafikiana suala la mali na mirathi kulingana na mila zetu zinavyotaka?

Kama kuna ushahidi kuwa ni ndoa ya kimila au kidini basi uamuzi utafanyika kwa misingi hiyo. Ila lazima kuwe na ushahidi na pia nadhani lazima pande zote ziridhie.
 
Back
Top Bottom