Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,781
Chukua muda wa kuzipumzisha hisiaWanaume tumeumbwa na ujasiri sana, na siyo rahisi kuonyesha udhaifu wake ata pale anapoona ameumizwa sana na mahusiano
Wengi wao huwa tunazuga kama hali hiyo haituumizi kumbe moyoni mwetu kunafukuta maumivu ambayo yanauma na ata umeze Lori la panadol sio rahisi kupata nafuu,binafsi hali hiyo imenikuta na kuna wakati natamani ata nisitoke nje kuona kinacho endelea ila ndio hivyo lazima maisha yaendelee.
Natamani nibadili namba ya simu pengine nahisi naweza kupata utulivu na kumkwepa ila nahisi nitapoteza watu wengi sana ambao tunasaidiana kimaisha,nipo kwenye msongo mzito sana wa mawazo
Hapa JF ndio sehemu pekee naweza kueleza hizi hisia ambazo siwezi Ku share na mtu yeyote physical ila nina uhakika na hili litapita.