kifupi kirefu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2018
- 539
- 3,507
Nimegundua ipo nguvu kubwa sana katika kusoma kitu kabla ya kusaini. Nimeona Kampuni yetu ikifilisika kwa sababu tu ya CO mpya alikuwa ni mtu wazimamoto asiyejipanga kupitia anachosaini. Jamaa kasaini mkataba wenye mapungufu lukuki akiamini cabnet yake watasoma. Kabinet nalo likaamini Wataalamu wa idara wamesoma na kitu hivyo wakapitisha kwa asilimia mia. Ilipofika kwa bosi akaisaini Kama nyaraka nyingine akiwa amesimama. Leo hii alichosaini kimepunguza wateja na malalamiko ni mengi sana mtaani kwa wateja wetu
Alichofanya kawaita watu walewale waliompotosha wakae watafute Suluhu ya ghasia na kunusuru mporomoko wa Kampuni. Watu walewale badala wakae wamshauri na kwakuzingatia wanajua ana mambo mengi na Hana muda wakutafakari wakaja na propaganda kwamba wanaolalamika wametumwa na Kampuni shindani. Bosi kwakutumia dola akaagiza walinzi wa Kampuni yetu wamkamate Mkurugenzi wa Kampuni kubwa shindani waakikishe hatoki ndani ili wateja wake wanywee wakati wakiandaa propaganda zaidi.
Lakini pia kwakuwa wateja wetu wanapenda soka, kabinet ikaelekeza msemaji wa timu kubwa mtaani kwetu atoe clip akionyesha kutoridhika na baadhi ya mambo ili wateja wetu waachane na malalamiko ya mkataba aliosaini CO Kampuni kidogo itulie. Mara paap msemaji akajitokeza akatoa audio aliyotoa watu kweli wakaanza kuijadili na masaa yakazidi kwenda.
Badala kabinet litumie muda vizuri kutekeleza maagizo waliyopewa na CO wao wanakalia propaganda na kusema tusiyumbishwe na kelele zao watatulia tu.
Sijui hata kampuni yetu kama itapata mafanikio, nawaza kwenda nchi jirani nikatafute kampuni iliyo seriuos isiyoishi kwa propaganda.
Lakini narudia kosa tulilofanya nikuruhusu kuwa na uongozi usiotenga muda kusoma, wanakimbizana na malipo ya safari wakiamini walio ofisini wanatenda kumbe nao wamelala
Alichofanya kawaita watu walewale waliompotosha wakae watafute Suluhu ya ghasia na kunusuru mporomoko wa Kampuni. Watu walewale badala wakae wamshauri na kwakuzingatia wanajua ana mambo mengi na Hana muda wakutafakari wakaja na propaganda kwamba wanaolalamika wametumwa na Kampuni shindani. Bosi kwakutumia dola akaagiza walinzi wa Kampuni yetu wamkamate Mkurugenzi wa Kampuni kubwa shindani waakikishe hatoki ndani ili wateja wake wanywee wakati wakiandaa propaganda zaidi.
Lakini pia kwakuwa wateja wetu wanapenda soka, kabinet ikaelekeza msemaji wa timu kubwa mtaani kwetu atoe clip akionyesha kutoridhika na baadhi ya mambo ili wateja wetu waachane na malalamiko ya mkataba aliosaini CO Kampuni kidogo itulie. Mara paap msemaji akajitokeza akatoa audio aliyotoa watu kweli wakaanza kuijadili na masaa yakazidi kwenda.
Badala kabinet litumie muda vizuri kutekeleza maagizo waliyopewa na CO wao wanakalia propaganda na kusema tusiyumbishwe na kelele zao watatulia tu.
Sijui hata kampuni yetu kama itapata mafanikio, nawaza kwenda nchi jirani nikatafute kampuni iliyo seriuos isiyoishi kwa propaganda.
Lakini narudia kosa tulilofanya nikuruhusu kuwa na uongozi usiotenga muda kusoma, wanakimbizana na malipo ya safari wakiamini walio ofisini wanatenda kumbe nao wamelala