Using'ang'anie kazi inayokupa mateso

Using'ang'anie kazi inayokupa mateso

Mi niliacha kazi kiwanda kikubwa cha bia kwa ukiritimba mwingi, majungu, kutiana presha. Siku naacha kazi kwa mshahara ule hakuna alie amini.

Niliingia kitaa na kamtaji kangu na kuanza kupiga ruti za Nairobi kupeleka mali na kurudi na mali.
Mambo yakaenda sawiaaa.

Japo sasa mziki wa magufuli nausoma vzr, nishapigika sana na TRA. Nafikiria kutafuta kazi tena, sasa sijui nitapata ya mshahara ule?
Mkuu Pressure Na Majungu Kazini huwezi Kuviepuka Especially Tanzania,cha Msingi ni Kutafuta Namna bora ya Kupunguza Pressure,Na Jitahidi Upande wako usimpige MTU jungu....Penye Riziki hapakosi Fitina,Unaweza hata Ambiwa kuwa Ohh Kazi Umepewa,Mara Huna qualifications,Au tuu Mchango wako Kazini Bosi zako wasiutambue....ila Nasema Pigs Kazi,MUNGU huwa Hamtupi mja wake,jiendeleze Kwenye hiyo Fani tumia Fursa Kujifunza Kwenye Eneo lako,jenga Tabia ya Kupuuza na Kusamehe...hapa lazima pia Uwe Unamuomba MUNGU.
 
Habari zenu wana JF? Ni matumaini yangu kila mmoja wetu hapa ameweza kuiona siku ya leo. Bila shaka ni jambo la kushukuru sana maana siyo wote waliolala jana na wameamka leo.


Bila kupoteza muda ngoja niende kwenye hoja ya msingi. Ni kwamba Mwana JF usipende kung'ang'ania kazi inayokuletea maumivu na mateso mengi na kila ukijitahidi mwisho wa siku unaambulia tu maumivu bila hata kuona faida ya hiyo kazi.

Ngoja niwape historia fupi ya maisha yangu kielimu. Ni kwamba nilisomea ualimu katika chuo fulani hapa Tz. Baada ya kumaliza niliajiriwa hapa jijini Dar. Pamoja na kuwa mwalimu maisha yalizidi kuwa magumu sana mpaka ikapelekea nikate tamaa. kwa sababu kila nilipopata mshahara watumiaji walikuwa wengi sana mfano nyumbani kwetu walitaka hela, hela ya nauli kwenda kazini, Hela ya kununua chakula, Hela ya kunununua nguo na kodi ya nyumba etc.

Hivyo basi, nilijikuta nachukia jiji la Dsm na kazi ya ualimu kutokana na adha nilizokuwa nakumbana nazo. Ingawa niliendelea kumuomba Mungu asaidie maisha yangu yawe mazuri lakini niliishia kuwa mkopaji mkubwa na hatari katika maduka ya mtaani kwangu. kitu kilichopelekea kuchukiwa kwa sababu ya kutolipa madeni. Nilikuwa sifanyi hivyo kwa kupenda bali ukata ndiyo uliyoniandama kwa kiasi kikubwa.

Pia kutokana na hali kuwa ngumu nyumbani kwetu yani kwa wazazi wangu walianza kuniona kama nina roho mbaya maana walipoomba hela nikawanyima walinilaumu sana bila kujua kwanini wananyimwa hela.

Hali ilizidi kuwa mbaya sana mpaka pale nilipokutana na rafiki yangu pale Posta ya zamani nikiwa nimechoka sana nimekuwa kama zee la miaka kwa sababu nilikuwa navaa mibwanga ya nguo kama pepekale na viatu vimelika kisigino kama mtu aliyetoka kijijini jana kuingia mjini.

Ilibidi tukae sehemu tuongee kidogo ingawa alinishangaa sana kwa ile hali. katika kumpa mchakato mzima kuhusu maisha nayopitia alisikitika sana na akanishauri niachane na fani yangu ili nihamie kwenye fani yake kwa kunihakikishia kuwa hakika nitaishi maisha mazuri sana.

Rafiki yangu alikuwa ni Wakili na alikuwa na maisha safi sana. Hivyo basi alinishauri nianze kusoma fani ya sheria mara moja. Ilibidi nijiunge na Open University nikaanza kuchimbua madini na vitu vingine akiwa ananisaidia yeye.

Mwisho wa siku nikahitimu masomo yangu akanipa ajira kama Legal officer katika LAW FIRM yake. baada ya miezi sita akaniambia nifanye taratibu za kuwa wakili baada ya kuona nimeanza kuwa smart katika fani ya sheria.

Nilifanya taratibu zote za kuwa wakili na nikawa nimekubaliwa na kikaapishwa mara moja. Hivyo niliendelea kupiga kazi katika LAW FIRM nikiwa kama ASSOCIATE ADVOCATE. Kiukweli nilianza kushuhudia maisha yanabadilika kwa kiwango kikubwa kwa sababu hela niliyokuwa napata katika fani yangu ilikuwa ni mara kumi ya hela niliyoipata kwa muda huo na mpaka sasa hivi katika fani hii ya sheria.

Kiukweli maisha yalibadilika mpaka wote walionizunguka na walionitegemea walikuwa hawaamini kabisa. Hivyo basi ilipelekea kuendesha maisha yangu vizuri sana bila wasiwasi wala kubahatisha.


Mwisho, Fanya uamuzi sahihi using'ang'anie unachokifanya wakati kinakupa mateso na huenda hiyo kazi ndiyo chanzo cha umasikini wako. Badilika kwanza wewe hakika utakuwa mtu yeyote hapa duniani. Sina nia ovu yoyote wala kuleta dharau kwa mtu yeyote.

"BADILIKA WEWE KWANZA, KUTOBOA KATIKA MAISHA NI SUALA RAHISI SANA"
Hongera sana Sana Mkuu
Ulisomea Combination Gani A-Level?
Pia Ni Somo Kuwa unaweza Kufanya Kazi yeyote na ukaifanya Vyema sana sana Hata Kama Hukuisomea
Au Uka Diversify Masomo!
 
Najiuliza kutoboa katika maisha kuna siri gani? Unakuta msomi wa hali ya juu lakini maisha magumu. Unaweza ukawa na refa na usitoboe!! Ndugu yangu Mshana Jr nisaidie, hivi hakuna uhusiano wa kutoboa na ulimwengu wa roho?? Nimepigika sana na juhudi ninazo, au nicheze tatu mzuka?
 
Mkuu Pressure Na Majungu Kazini huwezi Kuviepuka Especially Tanzania,cha Msingi ni Kutafuta Namna bora ya Kupunguza Pressure,Na Jitahidi Upande wako usimpige MTU jungu....Penye Riziki hapakosi Fitina,Unaweza hata Ambiwa kuwa Ohh Kazi Umepewa,Mara Huna qualifications,Au tuu Mchango wako Kazini Bosi zako wasiutambue....ila Nasema Pigs Kazi,MUNGU huwa Hamtupi mja wake,jiendeleze Kwenye hiyo Fani tumia Fursa Kujifunza Kwenye Eneo lako,jenga Tabia ya Kupuuza na Kusamehe...hapa lazima pia Uwe Unamuomba MUNGU.
Siyo kwenye ualimu. Utakula vumbi chaki weee. Ukianzsha twisheni utakula vumbi pia na wanafunzi 10,20
 
Siyo kwenye ualimu. Utakula vumbi chaki weee. Ukianzsha twisheni utakula vumbi pia na wanafunzi 10,20
Mkuu nimezungumzia kazi kwa ujumla sio ualimu tuu nimezungumza GENEARL...
 
Mm binafsi kazi zangu ni za kijasiria Mali, ila kila Mara huwa nabadilika na kujichanganya na issue yoyote .
Nimefanya kazi tofauti kama kumi.
 
Hongera sana Sana Mkuu
Ulisomea Combination Gani A-Level?
Pia Ni Somo Kuwa unaweza Kufanya Kazi yeyote na ukaifanya Vyema sana sana Hata Kama Hukuisomea
Au Uka Diversify Masomo!
Maisha yakikusaliti unajikuta unakuwa mtaalamu kila eneo mkuu.
 
Sasa mimi niliyeishia form 4 na sasa ni mbeba maboksi nina options gani mimi?

Life sucks man.

I have a dead-end job. I'm not smart.

*** it.
 
Sasa mimi niliyeishia form 4 na sasa ni mbeba maboksi nina options gani mimi?

Life sucks man.

I have a dead-end job. I'm not smart.

*** it.
Mkuu umepotea sana sana Mkuu
Anzisha hata thread kuwa yu alive Mkuu....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom