Using'ang'anie kazi inayokupa mateso

Using'ang'anie kazi inayokupa mateso

joshydama

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2016
Posts
4,623
Reaction score
5,051
Habari zenu wana JF? Ni matumaini yangu kila mmoja wetu hapa ameweza kuiona siku ya leo. Bila shaka ni jambo la kushukuru sana maana siyo wote waliolala jana na wameamka leo.


Bila kupoteza muda ngoja niende kwenye hoja ya msingi. Ni kwamba Mwana JF usipende kung'ang'ania kazi inayokuletea maumivu na mateso mengi na kila ukijitahidi mwisho wa siku unaambulia tu maumivu bila hata kuona faida ya hiyo kazi.

Ngoja niwape historia fupi ya maisha yangu kielimu. Ni kwamba nilisomea ualimu katika chuo fulani hapa Tz. Baada ya kumaliza niliajiriwa hapa jijini Dar. Pamoja na kuwa mwalimu maisha yalizidi kuwa magumu sana mpaka ikapelekea nikate tamaa. kwa sababu kila nilipopata mshahara watumiaji walikuwa wengi sana mfano nyumbani kwetu walitaka hela, hela ya nauli kwenda kazini, Hela ya kununua chakula, Hela ya kunununua nguo na kodi ya nyumba etc.

Hivyo basi, nilijikuta nachukia jiji la Dsm na kazi ya ualimu kutokana na adha nilizokuwa nakumbana nazo. Ingawa niliendelea kumuomba Mungu asaidie maisha yangu yawe mazuri lakini niliishia kuwa mkopaji mkubwa na hatari katika maduka ya mtaani kwangu. kitu kilichopelekea kuchukiwa kwa sababu ya kutolipa madeni. Nilikuwa sifanyi hivyo kwa kupenda bali ukata ndiyo uliyoniandama kwa kiasi kikubwa.

Pia kutokana na hali kuwa ngumu nyumbani kwetu yani kwa wazazi wangu walianza kuniona kama nina roho mbaya maana walipoomba hela nikawanyima walinilaumu sana bila kujua kwanini wananyimwa hela.

Hali ilizidi kuwa mbaya sana mpaka pale nilipokutana na rafiki yangu pale Posta ya zamani nikiwa nimechoka sana nimekuwa kama zee la miaka kwa sababu nilikuwa navaa mibwanga ya nguo kama pepekale na viatu vimelika kisigino kama mtu aliyetoka kijijini jana kuingia mjini.

Ilibidi tukae sehemu tuongee kidogo ingawa alinishangaa sana kwa ile hali. katika kumpa mchakato mzima kuhusu maisha nayopitia alisikitika sana na akanishauri niachane na fani yangu ili nihamie kwenye fani yake kwa kunihakikishia kuwa hakika nitaishi maisha mazuri sana.

Rafiki yangu alikuwa ni Wakili na alikuwa na maisha safi sana. Hivyo basi alinishauri nianze kusoma fani ya sheria mara moja. Ilibidi nijiunge na Open University nikaanza kuchimbua madini na vitu vingine akiwa ananisaidia yeye.

Mwisho wa siku nikahitimu masomo yangu akanipa ajira kama Legal officer katika LAW FIRM yake. baada ya miezi sita akaniambia nifanye taratibu za kuwa wakili baada ya kuona nimeanza kuwa smart katika fani ya sheria.

Nilifanya taratibu zote za kuwa wakili na nikawa nimekubaliwa na kikaapishwa mara moja. Hivyo niliendelea kupiga kazi katika LAW FIRM nikiwa kama ASSOCIATE ADVOCATE. Kiukweli nilianza kushuhudia maisha yanabadilika kwa kiwango kikubwa kwa sababu hela niliyokuwa napata katika fani yangu ilikuwa ni mara kumi ya hela niliyoipata kwa muda huo na mpaka sasa hivi katika fani hii ya sheria.

Kiukweli maisha yalibadilika mpaka wote walionizunguka na walionitegemea walikuwa hawaamini kabisa. Hivyo basi ilipelekea kuendesha maisha yangu vizuri sana bila wasiwasi wala kubahatisha.


Mwisho, Fanya uamuzi sahihi using'ang'anie unachokifanya wakati kinakupa mateso na huenda hiyo kazi ndiyo chanzo cha umasikini wako. Badilika kwanza wewe hakika utakuwa mtu yeyote hapa duniani. Sina nia ovu yoyote wala kuleta dharau kwa mtu yeyote.

"BADILIKA WEWE KWANZA, KUTOBOA KATIKA MAISHA NI SUALA RAHISI SANA"
 
Mi niliacha kazi kiwanda kikubwa cha bia kwa ukiritimba mwingi, majungu, kutiana presha. Siku naacha kazi kwa mshahara ule hakuna alie amini.

Niliingia kitaa na kamtaji kangu na kuanza kupiga ruti za Nairobi kupeleka mali na kurudi na mali.
Mambo yakaenda sawiaaa.

Japo sasa mziki wa magufuli nausoma vzr, nishapigika sana na TRA. Nafikiria kutafuta kazi tena, sasa sijui nitapata ya mshahara ule?
 
Mkuu hongera ila ulipata bahati ya mtu kukushika,kuna jamaa yangu kamaliza sheria yupo tu mtaani ikabidi ajishikize tu kwenye ualimu.Ukiwa na mtu ni rahisi sana kutoboa kwanza tayari huyo jamaa yako alikuwa na Law firm anajulikana michongo ipo na ndio maana nawe ukatoboa kiurahisi.
 
Mi niliacha kazi kiwanda kikubwa cha bia kwa ukiritimba mwingi, majungu, kutiana presha. Siku naacha kazi kwa mshahara ule hakuna alie amini.

Niliingia kitaa na kamtaji kangu na kuanza kupiga ruti za Nairobi kupeleka mali na kurudi na mali.
Mambo yakaenda sawiaaa.

Japo sasa mziki wa magufuli nausoma vzr, nishapigika sana na TRA. Nafikiria kutafuta kazi tena, sasa sijui nitapata ya mshahara ule?
Hongera na pole pia kwa muziki mnene wa TRA Mkuu.
 
Mkuu kwanza hongera saana kwa kupata wa kukushika mkono!! Umenipa nguvu ya kusonga mbele na maamuzi ninayotaka kuyafanya!! Inabidi tufike wakati tujitathimini: hivi kazi ninayofanya naifurahiaa?? Nafikia malengo yangu?? Au ni ili mradi tuu mateso kwenda mbele!! Watu wengi tunaogopa mabadiliko ( get rid of the fear of the unknown!!)
 
Mkuu hongera ila ulipata bahati ya mtu kukushika,kuna jamaa yangu kamaliza sheria yupo tu mtaani ikabidi ajishikize tu kwenye ualimu.Ukiwa na mtu ni rahisi sana kutoboa kwanza tayari huyo jamaa yako alikuwa na Law firm anajulikana michongo ipo na ndio maana nawe ukatoboa kiurahisi.
Mhhhh muulize kama alishaenda Law School na Kufaulu? Kama bado mwambie akajiunge huko akishapata muhuri wake mshauri akapige michongo nje ya Dar ni rahisi sana kutoboa maana kama ujuavyo wasomi wengi wanakimbilia Dar wakati kwa kipindi hiki fursa zipo mikoani. Hakika hatojutia kabisa.
 
Mkuu kwanza hongera saana kwa kupata wa kukushika mkono!! Umenipa nguvu ya kusonga mbele na maamuzi ninayotaka kuyafanya!! Inabidi tufike wakati tujitathimini: hivi kazi ninayofanya naifurahiaa?? Nafikia malengo yangu?? Au ni ili mradi tuu mateso kwenda mbele!! Watu wengi tunaogopa mabadiliko ( get rid of the fear of the unknown!!)
Exactly brother. Mtu inabidi unafanya uamuzi mgumu ili kuleta maendeleo. Huu siyo muda wa kuanza kulalamika ooh mshahara hautoshi mara nafanya kazi ktk mazingira magumu. Fanya uamuzi sahihi.
 
Ingawa hii stori inahamasisha sana lakini kwa tuliosoma sheria tunajua huyu bwana amefanya advertiaing..kwa namna moja au ingine
 
Mm ni kaka yako,nimeanza mambo haya tangu wewe hujabalehe '83.
Qualified Marioo. Nakumbuka nikiwa chuo ilikuwa ndiyo michezo yangu. Nilikuwa na jimama moja hivi bila kulikojoza kara 8 hakuelewi. Ila ni muda mrefu tangu nilipos
 
Ingawa hii stori inahamasisha sana lakini kwa tuliosoma sheria tunajua huyu bwana amefanya advertiaing..kwa namna moja au ingine
Hujasoma sheria Mkuu. Kwa uandishi wako huu nimekupinga kwa nguvu. utamu wa kuwa wakili ni kwamba ni fani ambayo haina kustaafu wala nini. Hivyo ukijenga jina utafaidi mpaka unaingia kaburini ni tofauti na ualimu. Ndicho kilichonishawishi kwa nguvu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom