joshydama
JF-Expert Member
- May 10, 2016
- 4,623
- 5,051
Habari zenu wana JF? Ni matumaini yangu kila mmoja wetu hapa ameweza kuiona siku ya leo. Bila shaka ni jambo la kushukuru sana maana siyo wote waliolala jana na wameamka leo.
Bila kupoteza muda ngoja niende kwenye hoja ya msingi. Ni kwamba Mwana JF usipende kung'ang'ania kazi inayokuletea maumivu na mateso mengi na kila ukijitahidi mwisho wa siku unaambulia tu maumivu bila hata kuona faida ya hiyo kazi.
Ngoja niwape historia fupi ya maisha yangu kielimu. Ni kwamba nilisomea ualimu katika chuo fulani hapa Tz. Baada ya kumaliza niliajiriwa hapa jijini Dar. Pamoja na kuwa mwalimu maisha yalizidi kuwa magumu sana mpaka ikapelekea nikate tamaa. kwa sababu kila nilipopata mshahara watumiaji walikuwa wengi sana mfano nyumbani kwetu walitaka hela, hela ya nauli kwenda kazini, Hela ya kununua chakula, Hela ya kunununua nguo na kodi ya nyumba etc.
Hivyo basi, nilijikuta nachukia jiji la Dsm na kazi ya ualimu kutokana na adha nilizokuwa nakumbana nazo. Ingawa niliendelea kumuomba Mungu asaidie maisha yangu yawe mazuri lakini niliishia kuwa mkopaji mkubwa na hatari katika maduka ya mtaani kwangu. kitu kilichopelekea kuchukiwa kwa sababu ya kutolipa madeni. Nilikuwa sifanyi hivyo kwa kupenda bali ukata ndiyo uliyoniandama kwa kiasi kikubwa.
Pia kutokana na hali kuwa ngumu nyumbani kwetu yani kwa wazazi wangu walianza kuniona kama nina roho mbaya maana walipoomba hela nikawanyima walinilaumu sana bila kujua kwanini wananyimwa hela.
Hali ilizidi kuwa mbaya sana mpaka pale nilipokutana na rafiki yangu pale Posta ya zamani nikiwa nimechoka sana nimekuwa kama zee la miaka kwa sababu nilikuwa navaa mibwanga ya nguo kama pepekale na viatu vimelika kisigino kama mtu aliyetoka kijijini jana kuingia mjini.
Ilibidi tukae sehemu tuongee kidogo ingawa alinishangaa sana kwa ile hali. katika kumpa mchakato mzima kuhusu maisha nayopitia alisikitika sana na akanishauri niachane na fani yangu ili nihamie kwenye fani yake kwa kunihakikishia kuwa hakika nitaishi maisha mazuri sana.
Rafiki yangu alikuwa ni Wakili na alikuwa na maisha safi sana. Hivyo basi alinishauri nianze kusoma fani ya sheria mara moja. Ilibidi nijiunge na Open University nikaanza kuchimbua madini na vitu vingine akiwa ananisaidia yeye.
Mwisho wa siku nikahitimu masomo yangu akanipa ajira kama Legal officer katika LAW FIRM yake. baada ya miezi sita akaniambia nifanye taratibu za kuwa wakili baada ya kuona nimeanza kuwa smart katika fani ya sheria.
Nilifanya taratibu zote za kuwa wakili na nikawa nimekubaliwa na kikaapishwa mara moja. Hivyo niliendelea kupiga kazi katika LAW FIRM nikiwa kama ASSOCIATE ADVOCATE. Kiukweli nilianza kushuhudia maisha yanabadilika kwa kiwango kikubwa kwa sababu hela niliyokuwa napata katika fani yangu ilikuwa ni mara kumi ya hela niliyoipata kwa muda huo na mpaka sasa hivi katika fani hii ya sheria.
Kiukweli maisha yalibadilika mpaka wote walionizunguka na walionitegemea walikuwa hawaamini kabisa. Hivyo basi ilipelekea kuendesha maisha yangu vizuri sana bila wasiwasi wala kubahatisha.
Mwisho, Fanya uamuzi sahihi using'ang'anie unachokifanya wakati kinakupa mateso na huenda hiyo kazi ndiyo chanzo cha umasikini wako. Badilika kwanza wewe hakika utakuwa mtu yeyote hapa duniani. Sina nia ovu yoyote wala kuleta dharau kwa mtu yeyote.
"BADILIKA WEWE KWANZA, KUTOBOA KATIKA MAISHA NI SUALA RAHISI SANA"
Bila kupoteza muda ngoja niende kwenye hoja ya msingi. Ni kwamba Mwana JF usipende kung'ang'ania kazi inayokuletea maumivu na mateso mengi na kila ukijitahidi mwisho wa siku unaambulia tu maumivu bila hata kuona faida ya hiyo kazi.
Ngoja niwape historia fupi ya maisha yangu kielimu. Ni kwamba nilisomea ualimu katika chuo fulani hapa Tz. Baada ya kumaliza niliajiriwa hapa jijini Dar. Pamoja na kuwa mwalimu maisha yalizidi kuwa magumu sana mpaka ikapelekea nikate tamaa. kwa sababu kila nilipopata mshahara watumiaji walikuwa wengi sana mfano nyumbani kwetu walitaka hela, hela ya nauli kwenda kazini, Hela ya kununua chakula, Hela ya kunununua nguo na kodi ya nyumba etc.
Hivyo basi, nilijikuta nachukia jiji la Dsm na kazi ya ualimu kutokana na adha nilizokuwa nakumbana nazo. Ingawa niliendelea kumuomba Mungu asaidie maisha yangu yawe mazuri lakini niliishia kuwa mkopaji mkubwa na hatari katika maduka ya mtaani kwangu. kitu kilichopelekea kuchukiwa kwa sababu ya kutolipa madeni. Nilikuwa sifanyi hivyo kwa kupenda bali ukata ndiyo uliyoniandama kwa kiasi kikubwa.
Pia kutokana na hali kuwa ngumu nyumbani kwetu yani kwa wazazi wangu walianza kuniona kama nina roho mbaya maana walipoomba hela nikawanyima walinilaumu sana bila kujua kwanini wananyimwa hela.
Hali ilizidi kuwa mbaya sana mpaka pale nilipokutana na rafiki yangu pale Posta ya zamani nikiwa nimechoka sana nimekuwa kama zee la miaka kwa sababu nilikuwa navaa mibwanga ya nguo kama pepekale na viatu vimelika kisigino kama mtu aliyetoka kijijini jana kuingia mjini.
Ilibidi tukae sehemu tuongee kidogo ingawa alinishangaa sana kwa ile hali. katika kumpa mchakato mzima kuhusu maisha nayopitia alisikitika sana na akanishauri niachane na fani yangu ili nihamie kwenye fani yake kwa kunihakikishia kuwa hakika nitaishi maisha mazuri sana.
Rafiki yangu alikuwa ni Wakili na alikuwa na maisha safi sana. Hivyo basi alinishauri nianze kusoma fani ya sheria mara moja. Ilibidi nijiunge na Open University nikaanza kuchimbua madini na vitu vingine akiwa ananisaidia yeye.
Mwisho wa siku nikahitimu masomo yangu akanipa ajira kama Legal officer katika LAW FIRM yake. baada ya miezi sita akaniambia nifanye taratibu za kuwa wakili baada ya kuona nimeanza kuwa smart katika fani ya sheria.
Nilifanya taratibu zote za kuwa wakili na nikawa nimekubaliwa na kikaapishwa mara moja. Hivyo niliendelea kupiga kazi katika LAW FIRM nikiwa kama ASSOCIATE ADVOCATE. Kiukweli nilianza kushuhudia maisha yanabadilika kwa kiwango kikubwa kwa sababu hela niliyokuwa napata katika fani yangu ilikuwa ni mara kumi ya hela niliyoipata kwa muda huo na mpaka sasa hivi katika fani hii ya sheria.
Kiukweli maisha yalibadilika mpaka wote walionizunguka na walionitegemea walikuwa hawaamini kabisa. Hivyo basi ilipelekea kuendesha maisha yangu vizuri sana bila wasiwasi wala kubahatisha.
Mwisho, Fanya uamuzi sahihi using'ang'anie unachokifanya wakati kinakupa mateso na huenda hiyo kazi ndiyo chanzo cha umasikini wako. Badilika kwanza wewe hakika utakuwa mtu yeyote hapa duniani. Sina nia ovu yoyote wala kuleta dharau kwa mtu yeyote.
"BADILIKA WEWE KWANZA, KUTOBOA KATIKA MAISHA NI SUALA RAHISI SANA"