Simu ambayo imenitoa machozi..

Simu ambayo imenitoa machozi..

Mwl Mwakujonga

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2023
Posts
355
Reaction score
702
Leo wakati tunapiga story na rafiki yangu ambaye urafiki wetu sasa unakaribia miaka 20 tuliongea mambo mengi tu mara baada ya kuhachana miaka 15 iliyopita

Sio kwamba hatuwasiliana naye kabsa hapana siku ya leo ilikuwa ni ya tofauti sana

Kitu ambacho siku zote wala hatujawai kuzungumza ni habari ya maisha ya wokovu mara baada ya shule, maana tumekuwa tukizunguma mambo mengi yanayo husu maisha na namna ya kupambana na changamoto tunazokutana nazo

Kwa sababu mara baada ya kumaliza shule kila mmoja kuenenda katika wito ambao Mungu alimwitia na majukumu ya familia na jamii tumekuwa tunawasiliana kwa mambo ya msingi tu na wakati mwingine kukumbushia juu ya maisha ya shule


Jambo ambalo sikutarajia kwamba linaweza kuwa ajenda ya mazungumzo yetu ni juu ya rafiki zetu ambao tulikuwa nao shuleni ambao wengi walikuwa wameokoka na Kumpa Yesu Maisha kama Bwana na Mwokozi wa maisha yao

Jambo ambalo rafiki yangu aliniambia na likaniweka katika mtihani ni juu ya ndugu zangu hao ambao wengi wao hama wamehachana na wakovu au wamerudi nyuma katika imani na kumwacha Yesu

Wakati naongea na rafiki yangu huyu,kwa kuwa wengi wa rafiki zetu wako mji mmoja na rafiki yangu huyu na wamekuwa wakionana katika matukio mbalimbali

Kwa masikitiko makubwa rafiki yangu aliniambia maisha ya shule na maisha ya mtaani ni maisha mawili tofauti kwa ndugu zetu hawa

Wakati tunaendelea kuongea , rohoni mwangu kukaingia kitu kutoka kwa roho mtakatifu na machozi yakaanza kunilenga lenga

Sikutaka kuongea sana juu ya ndugu zetu hao, moyoni mwangu ninajua changamoto za wakovu ninazokutana nazo, hivyo nikamwomba Mungu wa Rehema awasaidie na kuwainua na kuwarejesha katika imani

Wakati tumemaliza kuongea nikawa natafakari miaka yangu 15 ya kutembea na Yesu, sio kwamba ni miaka raisi au ni mseleleko

Hayakuwa maisha raisi sana kwangu kwani mwaka mmoja baada ya kuokoka niliingia mtaani kuanza maisha mara baada ya kutoka shule

Kwakweli sikuweza kumwambia rafiki yangu nini kimenifanya kusimama katika imani lakini nachojua haikuwa raisi na wakati mwingine nilikata tamaa katika wokovu lakini Neema ya Mungu haikuwai kuniacha

Sio kwamba nimesimama imara ila nacho jua hiko Neema ya Mungu juu yangu, wakati naendelea kutafajari haya

Nilimwomba Mungu kama atanipa nafasi ya kuandika kitabu juu ya kile ambacho Mungu alinifundisha ili niweze kutembea katika wakovu katika dunia ambayo imejaa kila aina ya tamaa mbaya ambazo kwa kijana ni mlango wa kwenda jehanamu

Yako mambo kadhaa ambayo Mungu amekuwa akinisaidie ili niweze kutembea katika wakovu japokuwa vita ni kali

Mambo hayo nitayaweka hapa kadri Mungu atakavyokuwa ananipa kibali
 
Yako mambo ambayo Roho Mtakatifu alinifundisha na anaendelea kunifundisha kuyazingatia kwa ajili ya kulinda uhusiano wangu na Mungu kila siku za maisha yangu mambo hayo ni :_
Jambo la Kwanza

Uhusiano wangu na Mungu katika Utoaji wa Sadaka

Mahusiano ya Mwanadamua na Mungu yanapimwa kwa njia ya utoaji

Biblia inasema
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Yohana 3:16

Kwa hiyo kama Mungu alionyesha upendo wake kwa kumtoa Mwana wake tena wapekee ujue na sisi pia tunatakiwa kutoa

Kwanini utoaji unaonyesha ni kiwango gani unampenda Mungu

Kwa sababu mali yako inapokuwepo ndipo na moyo wako unapokuwepo, kwa hiyo kama unatoa sana maana yake moyo wako umeutoa sana kwa Mungu

Hata katika mahusiano kama unatoa sana mali zako kwa mwenzako hiyo ni dalili ya kwanza inayoonyesha jinsi unavyompenda mwenzako

maana, analipenda taifa letu, naye alitujengea sinagogi. Luka 7:5
Wazee wakiyahudi walimwomba Yesu amponye kijakazi wa akida mmoja ambaye kwa sababu aliwapenda wayahudi hata kuwajengea kanisa, kwa hiyo upendo wake ulipimwa kwa jinsi alivyo toa mali yake kwa wayahudi

Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa. Matendo ya Mitume 9:36.

tunaposoma habari ya Dorcas pamoja kuwa na matendo mema alikuwa anatoa sadaka, ndio maana hata alipokufa watu walimwomba Petro kwa ajili yake na Mungu akamfufua kutokana na sadaka zake

1 Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia,

2 mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima.
Matendo ya Mitume 10:2
Kornelio sifa kubwa ya utawa alikuwa anatoa sadaka

Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang'anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne. Luka 19:8

Zakayo baada ya kukutana na Yesu ili kuthibitisha kwamba anampenda Yesu alikubali kutoa mali zake kwa maskini
Hivyo basi njia moja wapo ya kutafakari uhusiano wetu na Mungu ni kwa njia ya utoaji wa sadaka

Kama mwakajana ulikuwa unatoa sadaka ya 10,000/=, mwaka huu unatoa 1000/= licha ya kipato kuongezeka, ujue upendo wa Mungu kwako umepoa hiyo ni taa ya njano unataliwa kuifatilia
kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.

Mathayo 6:21
Kwa kuwa hazina yenu ilipo, ndipo itakapokuwapo na mioyo yenu.
 
Jambo jingine ambalo Roho Mtakatifu amekuwa ananifundisha kwa ajili ya kusimana katika wokovu ni :-

Kumpenda Mungu,
Kumpenda Mungu kwa tafsiri ya biblia kama ilivyoandikwa

1 Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
1 Wakorintho 13:1

2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
1 Wakorintho 13:2

3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.
1 Wakorintho 13:3

4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
1 Wakorintho 13:4

5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
1 Wakorintho 13:5

6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
1 Wakorintho 13:6

7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
1 Wakorintho 13:7

8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
1 Wakorintho 13:8

9 Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;
1 Wakorintho 13:9

10 lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.
1 Wakorintho 13:10

11 Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto.
1 Wakorintho 13:11

12 Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.
1 Wakorintho 13:12

13 Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.
1 Wakorintho 13:13
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom