Usimpime kwa macho hii kitu ni ya ajabu

DeMostAdmired

JF-Expert Member
Oct 7, 2017
877
2,427
HABARINI FJ PEOPLE

Nimependa leo niseme kitu kidogo juu ya tatizo la HIV/AIDs. Hamna asiyejua kwamba HIV ni janga kubwa hasa katita nchi zinazoendelea. Am sorry najua humu kuna baadhi wapo na HIV+ status lakini ni lazima waelewe kwamba ni jukumu letu sote kupambana na kutokomeza hii kitu.

Kilichonifanya niandike uzi huu ni kitu hiki. Ilikuwa ni week ilopita tar 13/ 01/ 024 nilikuwa naenda zangu hospital kumchek mshikaji wangu alipataga ajali na toyo yake, sasa nimebakisha kama hatua 30 kufika hosii nikapishana na sistee mmoja mkali nikisema mkali hapa naomba muelewe yule binti ni mrefu, chocolate color, anahips na anasura nzuri nzuri nzuri zaidi ya malkia wa shebah. Mimi uzalendo ukanishinda ikanibidi nimpige mkono bila ajizi akaitikia, nikamsalimia akaitika na alikuwa anaonesha kuwa ni mcheshi sana na mkarim kila nilichomwambia au kumuuliza aliitikia vizuri tu.

Tulibadirishana namba na kuachana. Sasa nilipofika hosii mapokez kushoto pembeni kulikuwa na mahema yanayoshughulika na clinic za watu wenye HIV na kifua kikuu nilishangaa kuona warembo wengi wengi mno pia wazee na watoto pia vijana wengi wao hasa wale warembo walikuwa wanaonekana kuwa na afya nzuri sana kifupi walikuwa wanavutia sana.

Sasa nikapita kuelekea wodin kwa msela nilitumia kama dk 4 tu maana muda ulikuwa ushaisha wa kuwaona wagonjwa ikabidi nitoke zangu sasa ile nimefika mlangoni nilimuona yule sistee nilomsimamisha na kumuomba namba akiwa miongoni mwa wale walokuja clinic nayeye pia aliniona na hakuonesha kustuka wala sikupenda pia anotice kwamba mimi nishamsuspect kwamba yawezekana yeye ni muathirika.

Niliendelea na safar na nikampungia mkono wa kwaheri, sas ulipita muda kidogo nikaona mesej inaingia na alikuwa ni yule bint tulichat sana na hatukuongelea maswala ya hospital ila zilikuwa stor zngne tu. Sasa kesho yake ilikuwa j pili mida ya saa kumi niliona cm inaingia nikaangalia alikuwa yeye bas nikapokea na tukaanza kuongea na alianza kunigusia kuhusu mambo ya HIV nikaona imekuwa afadhar yeye mwenyew kaanzisha mada.

Yalikuwa maongezi mazito lakini mwishon aliweza kuniweka wazi kwamba yeye ni HIV+ na nilimpongeza sana kwa kitendo cha kiuungwana kunisanua maan kiukweli kwa uzur na afya yake sidhani kama endapo tungefanikiwa kuwa wapenz ningegusia swala la kwenda kupima yani ningeenda mzima mzima bila hata ya kinga na ningempelekea moto kwa kumkomoa kwasbb ni mali inayostahili kupigwa show ambayo isingeweza kusahaulika kirahisi lakini niliepukana na kikombe hiko kwasbb ya uungwana wake na nilishangaa sana kunitamkia kwa ujasiri kuwa ni muathirika.

Ananisisitiza sana nisimtenge kwan tunaweza kuwa wapenz na asiniambukize na tukaenjoy maisha ashanichukua tukaenda kwa dokt wake tukapima nikajithibitishia mwenyewe kwamba ana hali hiyo na dkt akatupa elimu juu ya ngono salama ambayo haitanifanya nipate maambukizi, lakin kiukweli bado nina ugumu sana wa kumpiga show na anafanya kila njia kuniaminisha kwamba inawezekan tukaishi na nikawa sawa maisha yangu yote lakini waaapi moyo unakataa japo sijamtenga yani tupo katika mahusiano kifupi lakini tendo ndo bado sijapata huo ujasiri. Yeye alipata kutoka kwa wazaz wake nawish niwe naye katika maisha yangu kama mke wangu kwasbb ni wife material kiukweli lakini moyo unagoma kwasabb tu ya tatizo alonalo.

Nitoe RAI kwa vijana wenzangu wa kike kwa waume KAMWE USIMUAMINI MTU NENDA NAYE KUPIMA KWANZA AU TUMIA KONDOM HII KITU NI SERIOUS NA MAAMBIKIZI MENGI YANATOKA KWA HAWA TUNAOWAITA MA BROTHERMEN NA MASLAY QUEEN HAWA NDO WANAUSAMBAZA KWA KASI SANA KWASABB NI KAZI KUWASTUKIA NA NI RAHISI KUWAAMINI KWAMBA HAWANA MAAMBUKIZI.
 
Samahani,
Nje ya mada, nipo serious.
Ukitaka kunguni na mbu wakung'ate ila usisikie uendelee na usingizi unafanyaje?
Yaani naanisha kila mtu aendelee na yake?
Nenda kitandani kwa lengo moja tuu, kulala.
Yaani Ushalewa au umeshachoka haswa yaani ile una tua tuu, usingizi huo..
Au jizime data.
 
Ananisisitiza sana nisimtenge kwan tunaweza kuwa wapenz na asiniambukize na tukaenjoy maisha
Ushaelewa ulichokiandika hapo? Sometimes ni assassination tu hua wanafanya Ila wakiamua kukulinda hupati Mimi nishajaribu kufanya nilitest sumu kwa kuilamba sijawahi kuupata Ila kuna mmoja TU nilimgomea maana ile stage aliyofikia hata ungekua wewe akikupa ule huli
 
Usiogope!mzoee kwanza !!

Yaani muwe mnatoka out pamoja mguso kidogo was hapa na pale !

Mara nyingi hao jamaa wenye hiyo kitu huwa wana joto kama la homa muda wote!

Yaani iwe jua au baridi lakini temperature Yao ipo juu!nadhani ni hiyo chemical ya mchongo iliyotengenezwa ku control population iitwayo HIV virus!

Ukiigusa ngozi Yao Ina ka ulaini Fulani hivi ambako Huwa kana leta uoga fulani hivi kwa sisi!!

Na Huwa Wana mapenzi ya dhati hao balaa yaani Wana care sana!!

Kale kauoga tu huwa kanafanya jogoo asiwike kabisa hata kama no pisi Kali Hadi umzoee sana!!
 
al
Ushaelewa ulichokiandika hapo? Sometimes ni assassination tu hua wanafanya Ila wakiamua kukulinda hupati Mimi nishajaribu kufanya nilitest sumu kwa kuilamba sijawahi kuupata Ila kuna mmoja TU nilimgomea maana ile stage aliyofikia hata ungekua wewe akikupa ule huli
ikuwa kashaisha?
Ushaelewa ulichokiandika hapo? Sometimes ni assassination tu hua wanafanya Ila wakiamua kukulinda hupati Mimi nishajaribu kufanya nilitest sumu kwa kuilamba sijawahi kuupata Ila kuna mmoja TU nilimgomea maana ile stage aliyofikia hata ungekua wewe akikupa ule huli
alikuwa kashafikia hali mbaya?
 
Ukielewa ujumbe wa U = U haitakupa shida. Kifupi kama anatumia dawa vizuri unaweza kuishi nae na usiambukizwe.
Pia kama bado una wasiwasi sasa hivi kuna PreP (wasiliana na wataalam wa afya kwa ushauri zaidi),unaweza kutumia hizo mkaendelea na mahusiano yenu.
 
Back
Top Bottom