Usimpeleke mwanao shule za bweni

Usimpeleke mwanao shule za bweni

Gaddaf i06

JF-Expert Member
Joined
Nov 14, 2022
Posts
1,770
Reaction score
2,845
Siko hapa kukupangia namna ya kuishi na familia yako, ila naomba nikushauri kitu;

Kumpeleka mwanao akaishi bweni kwanza ni ulimbukeni, kama mtoto ana akili, hata akisoma day atafaulu tu.
wapo wanaosoma wakiwa boarding awali mpaka form4.. na bado wanafeli!

Hasara kubwa anayoipata mtoto ni kukosa malezi ya wazazi. Mtu aliesoma katika mazingira hayo, hata ukubwani utamjua tu!

Sasahivi tuna vijana mpaka wazee wa hovyo sana lakini cha ajabu ni wasomi (walikosa malezi ya wazazi)

Tunawapa wanawake lawama za kila rangi kumbe sio wao bali "walikosa malezi bora ya wazazi": binti wa form 4 & std7 alielelewa na wazazi ni bora (anaweza kuwa mke bora) kuliko degree holder aliekulia boarding kipindi chote cha makuzi yake.

Kuna msemo huu:- "asiyefunzwa na wazazi dunia itamfunza"

Umekosa nini mpaka mwanao ukamkabidhi mikononi mwa walimwengu wamfunze?

Kaa karibu na mwanao kwa faida yake, huko mbele kuna hatari.

NB. Nazungumzia watoto under 18
 
Inatagemea ila kama ni mijini lazima boarding maana ushawishi wa kuharibikiwa asilimia kubwa ni mjini.
 
Umeongea ukweli
Kuna mfanyakaz mwenzetu amesoma bodi kuanzia primary hadi chuo ni wa hovyo
Yeye mwenyewe anakiri wazazi wake ndiyo wamemuharibu kumpeleka bodi school
Hakuna raha anayoipata mtoto kama kuwa karibu na wazazi! Yaani anajihisi perfect sana
 
Tafuta mkwanja mkuu. Maneno yote hayo tushatambua huna hela ya kumsomesha Mtoto bodng
 
Hakuna bingwa wa malez ndugu, kama una watoto tema mate chini.

Hii dunia haijanyooka kama upeo wa akil yako unavyokwambia...
Mifano ni Mingi na waliopotea ni wengi kwa kutegemea akili zao kwenye malez.
Mtoto alelewavyo ndivyo akuwavyo. Usitegemee mwalimu akufundishie mwanao kila kitu

Hujanishawishi
 
Back
Top Bottom