Usilogwe ukaondoka nyumbani na kwenda usipopajua kwa kigezo cha kutafuta maisha

Akili Sina

JF-Expert Member
Jan 18, 2018
301
2,218
Nilizaliwa mwishoni mwa miaka ya themanini katika kijiji cha chabutwa wilaya ya Sikonge mkoa wa Tabora, nilifanikiwa kupata elimu yangu ya msingi hapo kijijini, shuleni nilikuwa vizuri sana, si walimu tu bali hata wanafunzi walinipenda. Familia yetu ilikuwa ya maisha ya kawaida sana kwani baba na mama wote ni wakulima wadogo wadogo tu, kwetu tulizaliwa wawili tu mimi na mdogo wangu wa kiume.

Basi baada ya kumaliza shule ya msingi nilichaguliwa kujiunga na shule ya skondari Chabutwa iliyopo pale katani. Kwa vile nilikuwa John kisomo basi maisha ya shule hayakuwa mabaya ki ufaulu, Paka namaliza form four nilikuwa naongoza pale shuleni, Baba yangu alipenda kunihusia kuwa nisipende kujionesha kwa watu kuwa nina akili maana si wote wanapenda kuona watoto wao hawafanyi vizuri alafu watoto wa wengine wanafanya vizuri

Basi nilijitahidi sana kufata ushauri wa mzee ingawa kama unavyojua haya mambo hayafichiki, Kata nzima ilikuwa inanifahamu, kwenye vikao vya shule ndo usiseme maana niligeuzwa sample space (Sehemu ya wengine kujifunzia).

Basi nikamaliza four pale na Mungu si Athumani nikafaulu vizuri na kuchaguliwa kujiunga na shule ya Pugu Secondary kwa ajili ya five na six. Mzee wangu alifurahi sana si kwa sababu ya kufaulu tu bali nilichaguliwa shule ya mbali na pale nyumbani maana mzee alikuwa hana amani kabisa na majirani wa pale katani

Basi bana, siku ya siku nikatimba shule ya baba wa taifa, Askwambie mtu nilikutana na life la kibabe sjawahi kuona
Picha linaanza shule haina maji, Maji utajua pa kuyapata, kama utaenda mtaani kununua utajua mwenyewe, Ukitaka uzame pondi ( Huko bondeni kuna visima wanatumia wanakijiji ila maji yake yana magadi na fangasi wa kutosha)

Kufupisha story sitaelezea sana life la Pugu, ila kiukweli lilikuwa la kiume, Miongoni mwa vitu sitavisahau ni bweni letu la Mapinduzi 3 ambalo ndo lilikuwa linaaminika bweni la watu wakorofi shule nzima, pia nikiwa bado mgeni nilikaribishwa kwa kupigwa nguo zangu zote nikabaki na nliizokuwa nimevaa tu, yaani siku hiyo nimetoka pondi nimefua nguo zangu nikaanika kwenye ukoka, nikaondoka kwenda kutembea majohe, kurudi jioni nakuta ukoka unanikodolea tu hakuna nguo yaani Hadi boxer walichukua wahuni wale.

Kingine sitasahau ni tukiwa karibu kumaliza six, tumebakiza paper ya practical ya chemistry, siku hiyo ilikuwa jioni ki giza ndo kinaingia, nimetoka kupiga zangu nguna maharage, najisogeza taratibu naelekea kwenye kipindi cha dini, Mara ghafla naona watu wanakuja wengi wanakimbilia eneo la shule, Wa baba, wa mama wengine wana watoto, nikajiuliza kimoyomoyo haya maandamano ya nini tena, nikiwa bado nashangaa ghafla nikaona kitu hicho ndo kilifanya nione hii issue ni serious, nikamwona teacher wetu wa darasa nae anakuja mbio, tena mbaya zaidi ana kitambi sasa akikimbia balaa, na alikuwa na spidi maana ilikuwa kawaida yake kila asubuhi anatukimbiza ambao hatuendi assemble.

Duuh, nlipoona hivyo na mimi nikaliunga tukaanza kukimbia, kuna sehemu wanafunzi wanapenda kuangalia tv nikakuta nao wamesepa wameacha tv pale, Daaah sasa wote tunakimbia halafu hatujui tunakimbia nini, Sasa wakati naendelea kukimbia nikakutana na mlemavu mmoja yupo kwenye kiti chake cha matairi (Maana ile shule ina wanafunzi walemavu pia),. Sasa hana mtu wa kumsukuma na kile kiti chake, kila mtu anaokoa nafsi yake, basi huruma ikaniiingia nikaanza kunsukuma huku tunakimbia, ebwanaeeh tumekimbia mwisho nikaona hapa nafeli, maana watu wanazidi kukimbia kuelekea bondeni huko alafu kelele zimekuwa nyingi, nikaona usintanie nikamwacha yule mlemavu nikaanza kukimbia mwenyewe.

Nikakimbia hatimae nikafika pondi, pale kidogo nikakuta watu wamerundikana kidogo,wanaulizana ni nini ila hakuna anaejua, ila juu angani anga limegeuka rangi, limekuwa jekunduuu kama vile jua lataka kushuka, alafu kelele kama vile watu wanapiga mabati huko angani au kama vile msitu unaungua sasa zile kelele za miti, daah hapo nikajua ndo mwisho wa dunia huu, wakati nageuka huku na kule mara namwona yule mlemavu ila saivi hayupo kwenye kiti bali anatambaa chini, nikajiuliza huyu kakimbia au kabebwa? Nikabaki nimestaajabu ila nikajichanganya asije kuniona akasema huyu broo ana roho mbaya, maana jinsi anga lilivyo jekundu yaani Hadi watu mna onana kabisa

Basi bana kelele zikazidi, watu woga ukaongezeka basi mbio zikaanza , tukapanda juu tukatokea Barbara kubwa ya pugu kajiungeni, Barabara imejaa watu wanakimbia, magari ndo usiseme, basi tukawa tunakimbia kelele zikizidi ukitazama juu unaona kama kimondo cha moto kinakuja hivyo unalala chini, kikipita unaamka tena unaaza mbio, Basi tukafika njia panda ya kisarawe na chanika, tukala kulia kuelekea kisarawe, mbio mbio unafika mahali unakutana na mdada anakimbia kanga inaanguka anabaki na chupi lakini hana muda wa kuokota kanga,ni kukimbia tu, mi pia sikuwa hata na hamu ya kutazama hayo mambo, maana unakimbia ukilala chini unasali ili likimondo lipite, basi ni kukimbia na kusali tu

Basi mara tukafika shule ya secondary Minaki , kulikuwa na wanafunzi pale nao wakaungana na sisi kukimbia, tukakimbia mara tukatoboa kisarawe,hapo ni usiku hata siijui saa ngapi, Basi pale kisarawe tukakuta watu wengi kinyama, yaanii pale ndo ikawa kama makutanio, watu wanaulizana ni nini,lakani hakuna anaejua dhahiri ni kitu gani kimetokea, Basi wakati tunashangaa pale mara ule mwanga na yale makelele yakawa takekaribia tena, watu wakaanza kuondoka kuendelea mbele,

Daah kwa jinsi nlivyokimbia na miguu ilivyokuwa inauma nikasema mi skimbii tena, kama kufa nife tu, basi nikaona cruzer moja imejaza watu nyuma inaondoka, nikaikimbilia nikaidaka, nikadandia yenyewe ikachanganya, sasa wakati natafuta sehemu ya kuweka mguu nikakosa, mikono ikachoka kubembea nikarudisha miguu kwenye lami, acha niburuzwe, nikaskia watu wanasema umeuaaaa, gari ikasepa nikaamka kujiangalia, nilikuwa nimevaa jinsi lakini ililiwa na lami paka ikakutwa Ngozi, nilichubuka vibaya, damu zinatoka balaa vidole vinatoa damu, ndala Sina maana zulikatika toka huko nikiwa nakimbia

Basi, mara nikaona cruiser moja imechorwa msalaba mwekundu, watu wanaikimbilia, na mimi nikazama, sasa wakati nazama kuna mama mmoja alikuwa mbele yangu, nikamvuta nyuma mi nikazama ndani, kumbe ni mke wa yule dereva anae endesha lile gari

Itaendelea

SEHEMU YA PILI

SEHEMU YA TATU

SEHEMU YA NNE

SEHEMU YA TANO

SEHEMU YA SITA

SEHEMU YA SABA
 
Mabomu ya Gongolamboto hayo nakumbuka nilikuwa na camera Aina ya Sony vile vidogo megapix 16 napiga passport size, kazi yangu ilikuwa kila linapodondoka bomu naenda kupiga picha na wananchi wanaokimbia.

Home walikimbia woote nikabaki peke yangu kwahiyo nazunguka halafu naenda home kuangalia usalama, kuna muda nikachukua wamama na watoto waliokimbia kutoka gomz nikawaifadhi home ndio nikapata muda mzuri huko nje, mimi nilikuwa Banana pale.

Mambo yalivyoisha watu walikuwa wanakuja kuangalia zile picha kwenye kibanda ngazette. Na brother, kama week hivi naenda nacheki camera picha zote zimefutwa roho iliniuma sana.

Bro alifanya makusudi maana ilikuwa kero na Camera ilikuwa ya kazi, kingine bro mtu wa tungi nahisi kuna mtu alifika bei akamuuzia maana niliziona baadhi kwenye gazeti.
 
Nilizaliwa mwishoni mwa miaka ya themanini katika kijiji cha chabutwa wilaya ya Sikonge mkoa wa Tabora, nilifanikiwa kupata elimu yangu ya msingi hapo kijijini, shuleni nilikuwa vizuri sana, si walimu tu bali hata wanafunzi walinipenda. Familia yetu ilikuwa ya maisha ya kawaida sana kwani baba na mama wote ni wakulima wadogo wadogo tu, kwetu tulizaliwa wawili tu mimi na mdogo wangu wa kiume.

Basi baada ya kumaliza shule ya msingi nilichaguliwa kujiunga na shule ya skondari Chabutwa iliyopo pale katani. Kwa vile nilikuwa John kisomo basi maisha ya shule hayakuwa mabaya ki ufaulu, Paka namaliza form four nilikuwa naongoza pale shuleni, Baba yangu alipenda kunihusia kuwa nisipende kujionesha kwa watu kuwa nina akili maana si wote wanapenda kuona watoto wao hawafanyi vizuri alafu watoto wa wengine wanafanya vizuri

Basi nilijitahidi sana kufata ushauri wa mzee ingawa kama unavyojua haya mambo hayafichiki, Kata nzima ilikuwa inanifahamu, kwenye vikao vya shule ndo usiseme maana niligeuzwa sample space (Sehemu ya wengine kujifunzia).

Basi nikamaliza four pale na Mungu si Athumani nikafaulu vizuri na kuchaguliwa kujiunga na shule ya Pugu Secondary kwa ajili ya five na six. Mzee wangu alifurahi sana si kwa sababu ya kufaulu tu bali nilichaguliwa shule ya mbali na pale nyumbani maana mzee alikuwa hana amani kabisa na majirani wa pale katani

Basi bana, siku ya siku nikatimba shule ya baba wa taifa, Askwambie mtu nilikutana na life la kibabe sjawahi kuona
Picha linaanza shule haina maji, Maji utajua pa kuyapata, kama utaenda mtaani kununua utajua mwenyewe, Ukitaka uzame pondi ( Huko bondeni kuna visima wanatumia wanakijiji ila maji yake yana magadi na fangasi wa kutosha)

Kufupisha story sitaelezea sana life la Pugu, ila kiukweli lilikuwa la kiume, Miongoni mwa vitu sitavisahau ni bweni letu la Mapinduzi 3 ambalo ndo lilikuwa linaaminika bweni la watu wakorofi shule nzima, pia nikiwa bado mgeni nilikaribishwa kwa kupigwa nguo zangu zote nikabaki na nliizokuwa nimevaa tu, yaani siku hiyo nimetoka pondi nimefua nguo zangu nikaanika kwenye ukoka, nikaondoka kwenda kutembea majohe, kurudi jioni nakuta ukoka unanikodolea tu hakuna nguo yaani Hadi boxer walichukua wahuni wale.

Kingine sitasahau ni tukiwa karibu kumaliza six, tumebakiza paper ya practical ya chemistry, siku hiyo ilikuwa jioni ki giza ndo kinaingia, nimetoka kupiga zangu nguna maharage, najisogeza taratibu naelekea kwenye kipindi cha dini, Mara ghafla naona watu wanakuja wengi wanakimbilia eneo la shule, Wa baba, wa mama wengine wana watoto, nikajiuliza kimoyomoyo haya maandamano ya nini tena, nikiwa bado nashangaa ghafla nikaona kitu hicho ndo kilifanya nione hii issue ni serious, nikamwona teacher wetu wa darasa nae anakuja mbio, tena mbaya zaidi ana kitambi sasa akikimbia balaa, na alikuwa na spidi maana ilikuwa kawaida yake kila asubuhi anatukimbiza ambao hatuendi assemble.

Duuh, nlipoona hivyo na mimi nikaliunga tukaanza kukimbia, kuna sehemu wanafunzi wanapenda kuangalia tv nikakuta nao wamesepa wameacha tv pale, Daaah sasa wote tunakimbia halafu hatujui tunakimbia nini, Sasa wakati naendelea kukimbia nikakutana na mlemavu mmoja yupo kwenye kiti chake cha matairi ( Maana ile shule ina wanafunzi walemavu pia),. Sasa hana mtu wa kumsukuma na kile kiti chake, kila mtu anaokoa nafsi yake, basi huruma ikaniiingia nikaanza kunsukuma huku tunakimbia, ebwanaeeh tumekimbia mwisho nikaona hapa nafeli, maana watu wanazidi kukimbia kuelekea bondeni huko alafu kelele zimekuwa nyingi, nikaona usintanie nikamwacha yule mlemavu nikaanza kukimbia mwenyewe.

Nikakimbia hatimae nikafika pondi, pale kidogo nikakuta watu wamerundikana kidogo,wanaulizana ni nini ila hakuna anaejua, ila juu angani anga limegeuka rangi, limekuwa jekunduuu kama vile jua lataka kushuka, alafu kelele kama vile watu wanapiga mabati huko angani au kama vile msitu unaungua sasa zile kelele za miti, daah hapo nikajua ndo mwisho wa dunia huu, wakati nageuka huku na kule mara namwona yule mlemavu ila saivi hayupo kwenye kiti bali anatambaa chini, nikajiuliza huyu kakimbia au kabebwa? Nikabaki nimestaajabu ila nikajichanganya asije kuniona akasema huyu broo ana roho mbaya, maana jinsi anga lilivyo jekundu yaani Hadi watu mna onana kabisa

Basi bana kelele zikazidi, watu woga ukaongezeka basi mbio zikaanza , tukapanda juu tukatokea Barbara kubwa ya pugu kajiungeni, Barabara imejaa watu wanakimbia, magari ndo usiseme, basi tukawa tunakimbia kelele zikizidi ukitazama juu unaona kama kimondo cha moto kinakuja hivyo unalala chini, kikipita unaamka tena unaaza mbio, Basi tukafika njia panda ya kisarawe na chanika, tukala kulia kuelekea kisarawe, mbio mbio unafika mahali unakutana na mdada anakimbia kanga inaanguka anabaki na chupi lakini hana muda wa kuokota kanga,ni kukimbia tu, mi pia sikuwa hata na hamu ya kutazama hayo mambo, maana unakimbia ukilala chini unasali ili likimondo lipite, basi ni kukimbia na kusali tu

Basi mara tukafika shule ya secondary Minaki , kulikuwa na wanafunzi pale nao wakaungana na sisi kukimbia, tukakimbia mara tukatoboa kisarawe,hapo ni usiku hata siijui saa ngapi, Basi pale kisarawe tukakuta watu wengi kinyama, yaanii pale ndo ikawa kama makutanio, watu wanaulizana ni nini,lakani hakuna anaejua dhahiri ni kitu gani kimetokea, Basi wakati tunashangaa pale mara ule mwanga na yale makelele yakawa takekaribia tena, watu wakaanza kuondoka kuendelea mbele,

Daah kwa jinsi nlivyokimbia na miguu ilivyokuwa inauma nikasema mi skimbii tena, kama kufa nife tu, basi nikaona cruzer moja imejaza watu nyuma inaondoka, nikaikimbilia nikaidaka, nikadandia yenyewe ikachanganya, sasa wakati natafuta sehemu ya kuweka mguu nikakosa, mikono ikachoka kubembea nikarudisha miguu kwenye lami, acha niburuzwe, nikaskia watu wanasema umeuaaaa, gari ikasepa nikaamka kujiangalia, nilikuwa nimevaa jinsi lakini ililiwa na lami paka ikakutwa Ngozi, nilichubuka vibaya, damu zinatoka balaa vidole vinatoa damu, ndala Sina maana zulikatika toka huko nikiwa nakimbia

Basi, mara nikaona cruiser moja imechorwa msalaba mwekundu, watu wanaikimbilia, na mimi nikazama, sasa wakati nazama kuna mama mmoja alikuwa mbele yangu, nikamvuta nyuma mi nikazama ndani, kumbe ni mke wa yule dereva anae endesha lile gari


Itaendelea
Kama mwenyewe unajiita akili huna tukusaidieje sasa
 
Back
Top Bottom