Heavy Metal
JF-Expert Member
- Feb 7, 2017
- 1,050
- 2,500
Daaaaah we jamaa bhanaSasa unaweka ac ya nini wakati fridge unayo? Washa fridge acha mlango wazi ule upepo.

Anyways, operation ya fridge ina violate the second law of thermodynamics: iko hivi, always heat inaflow from hot body/ area to cold body/ area and never the reverse: yani mfano unapokua unapasha kitu moto lazima upande ambao uko contact na moto utaanza kupata joto then joto hilo litaflow kuelekea maeneo ambayo hayana joto ama kwenye ubaridi, hiyo ndo principle na formula ya msingi ambayo inaapply hata kwenye maisha ya kila siku
Sasa fridge ina operate kwenye reverse direction yani heat inaflow from cold to hot body, hivyo ukifungua mlango wa fridge yako chumba chako kitapata joto zaidi ya ubaridi kwasababu heat itaanza kuflow kutoka kwenye fridge ambako kuna ubaridi yani cold body/ area kuja kwenye room yako ama sehemu ulipokaa ambako ni kwa muda huo tutapahesabu kama hot body/ area. Labda swali hapo ni kwanini inakua ivyo?! Compressor ya fridge inapokua inafanya kazi inazalisha joto jingi ambalo linatakiwa kua compressed into air kuleta ubaridi kwenye fridge yako. So ukifungua mlango wa fridge hiyo air haitokua converted/ compressed into cold air badala yake itatoka direct kwenye mfumo ule ule wa joto kama ambavyo imezalishwa na compressor ya fridge yako
Hata hivyo pamoja na yote hayo, hata kama mlango wa fridge yako ukiwa hauko wazi bado kuna kiasi cha joto kinachozalishwa na compressor kitaendelea kupotea nje kwasababu sio heat yote inayozalishwa compressor itakua converted into cold air kwenye fridge work must be done kuhakikisha hilo linafanikiwa matokeo yake ndo hayo kwamba efficiency of any heat engine (Carnot engine) is less than 100% and even far less than 50%. So hicho kiasi ambacho sisi tunakiona kidogo cha joto kinachopotea ndo kinazalisha joto nyuma ya fridge lako na hiyo heat ni sensible unaweza kuifeel kabsa kua inabadilisha halijoto room kwako hasa kama uko kwenye enclosed space kama kwenye karoom kadogo
Anyways nimetumia concept ndogo tu ya Physics kwenye applications of second law of thermodynamics (operation of heat/ carnot engines). Watu wa Mechanical Engineering ndo wataalamu wa haya mambo wanaweza kuja hapa kuongeza kitu ama kusahihisha pale ambapo sikua sawa kwenye maelezo yangu. Lakini pia mambo ya operation za AC, refrigerator na car engines ni ya kwao wanaweza kuja hapa kutoa ufafanuzi kuhusu mada ya huyu mdau kuhusu matumizi ya umeme kwenye AC
