Usiipite hii post tafadhali...hebu ichungulie

Usiipite hii post tafadhali...hebu ichungulie

me naona hakuna tatizo mzee..kama una uhakika umerizika nae na hutahangaika na dogodogo generation mana wanakuja kwa kasi balaa...dogo dogo achia ma senior bachelors
 
Tamaa ya mali na ngono ndio inakusukuma lakini kiuhalisia hakuna mapenzi ya dhati hapo. kinachokusukuma ni huku kutaka kulelewa. Vijana Wa siku hizi mnatia aibu sana kwa kupenda mteremko.
 
kumbe bado unabeef na mimi wee nguruwe...angalia hoja usiangalie nani aliyeitoa shetani wewe sio kuachama domo tu kama jibwa from no where na kusema eti hakuna hoja...ukiendelea na tabia hiyo utaolewa we pakamapepe

Hamna hoja hapo !
 
upo wapi Neylu?
ebu njoo umshauri huyu dogo!

Wadau mm nina umri wa miaka 26 now, nimemaliza Sheria Chuo Kikuu Mzumbe ila sijabahatika kupata kazi bado. Imetokea nimependana sana na dada mmoja ambaye ni Kaimu Mchumi wa Halmashauri fulani ya Mji, tatizo ni kwamba ana umri wa takribani miaka 35 sasa, na wkt namuapproach moja ya sababu iliyopelekea asite kunikubalia ni age difference ila at last nikafanikiwa kumshawishi...washkaji na kaka zangu wananionea wivu sana wanadai huyu dem ananilea na kuna tetesi kwamba anapata mshahara mkubwa sana coz ameajiriwa zamani na ana masters degree.

Mara nyingi nalala kwake, nimebahatika kumiliki usafiri(gari) mapema so nikiamka nampeleka kazini asubuhi then narudi zangu maskani. Juzi kati nikamuuliza kwa kumtega kwamba nataka anipe mtoto akakubali! Jana nikamwambia nataka nimuoe akakubali! Ana uzuri wa kawaida tu ila ni mstaarabu sana, muwazi, hana mambo mengi na ananiheshimu sana ingawa kanipita umri! Nafikiria kumuoa mara tu nikipata kazi, je kuna tatizo lolote hapo wajameni?
 
Last edited by a moderator:
Nick Canon na m\Mariah Carey age diffrence ni miaka 10, na wanaoenekana wanapendana vizuri na wamezaa watoto wao wawili. Umri sio tatizo alimradi mnapendana na mnaelewana vema.
 
swali la busara la kujiuliza mkuu ni kwamba kwann ana umri wa miaka 35 na hajaolewa? pia kama aliwahi kuolewa kwann aliachika na hujaeleza kama ni MJANE, take care bro magonjwa mengi
Mmeanza wivu wenu...
 
Age aint nothimng but a number. Pia wanaume huwa wanakufa mapema huyo atakusaidia kwa umri wake. Pia uwe umekuwa kidogo sio kumpenda mtu kwa sababu ya masters au muruju (pesa).
 
first akusaidie kazi huko halmashauri
hata ya kufagia tu
utaanzia hapo
halafu ndo umuoe
 
hiv kwanini mnashindwa kuinjoi mapenzi yenu kwa sababu zisizomithilika jamani!
kwani miaka 35 ana pembe mabegani!kama umeweza kuwa naye kwa furaha muda wote huo nini shida akiwa mkeo!
ila sasa natamani huyo dada asome hiki ulichoandika hapa!
kwa lugha jamii yangu niliyonayo kijana uko hapo for what tht sis of mine has!
UNABISHA?
angalia ulivyoharakisha kusema kuwa huyo dada ana nini?
tabia zake na undani wake umeviweka mwiiiisho
so nahis sio a worthy person to her kihiiivyo!
NAWAZA TU kwa sauti lakini!

Hakika umenena vyema



Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Chamsingi na muhimu ni kuikubari hali yako. Mimi niliyemuoa kanizidi miaka miwili ila nimeishi naye kwa miaka minane hivi sasa na tuna watoto wawili. Tofauti yetu ni kuwa huyu wangu hana pesa kama alivyo wako na mimi kama baba wa famila ndio kila kitu. Kutokana na elimu yake ya Form Four, bado hajabahatika kupata kazi ya maana na hivyo nimemfungulia cafe pale anauza soda, maji juice, ice cream, barafu na anauhakika wa angalau elfu kumi kwa siku. Naiona hiyo elfu kumi ni ya maana kuliko kumtafutia kazi kwani kwa elimu hiyo sidhani kama anaweza kupata mshahara wa maana zaidi ya hiyo anayoipata hapo nyumbani. Hata hivyo, pesa hiyo inatusaidia kula siku zote na mshahara wangu, kwasababu haukatwi kwenda kwenye chakula, umetuwezesha kujenga nyumba nzuri, kumsomesha mtoto wetu mkubwa ktk moja kati ya shule nzuri za English Medium hapa Dar na hivi sasa tunatembelea ki Toyota Raum chetu tunapokwenda kuwatembelea ndugu na marafiki. Haya yote tumeweza kuyafanya ndani ya miaka mi5 tu kwani nilichelewa kumkubari kuwa ndio mke wangu pamoja na kuwa nilimtaka mwenyewe na yeye hakunificha kuhusu umri wake. Wakati namuoa, yeye alikua na miaka 28 huku mimi nikiwa na 26. Baada ya kumuoa, ndipo ndugu waliingilia kati na kunisema sana kwa uamuzi wangu huo. Ilinichanganya sana akili haswa ikizingatiwa kuwa mimi ni graduate so nisingekosa msichana msomi mwenzangu niliyemzidi umri. Hali hiyo ilichangia sana kuchelewesha maendeleo ndani ya familai yangu. Tangu niamue kukubariana na hari yangu hiyo, nayaona maisha ni mteremko sana. Ninampenda sana na ananipenda pia. Ndugu zetu (pande zote mbili) wanajua wakija kwetu waseme lililowaleta na waondoke bila kutuharibia maisha kwani tunachokifanya ni kwa ajili ya watoto wetu. Kama unampenda, basi epuka maneno ya marafiki na ndugu na uwe serious kuwa hautayumbishwa.

Wadau mm nina umri wa miaka 26 now, nimemaliza Sheria Chuo Kikuu Mzumbe ila sijabahatika kupata kazi bado. Imetokea nimependana sana na dada mmoja ambaye ni Kaimu Mchumi wa Halmashauri fulani ya Mji, tatizo ni kwamba ana umri wa takribani miaka 35 sasa, na wkt namuapproach moja ya sababu iliyopelekea asite kunikubalia ni age difference ila at last nikafanikiwa kumshawishi...washkaji na kaka zangu wananionea wivu sana wanadai huyu dem ananilea na kuna tetesi kwamba anapata mshahara mkubwa sana coz ameajiriwa zamani na ana masters degree.

Mara nyingi nalala kwake, nimebahatika kumiliki usafiri(gari) mapema so nikiamka nampeleka kazini asubuhi then narudi zangu maskani. Juzi kati nikamuuliza kwa kumtega kwamba nataka anipe mtoto akakubali! Jana nikamwambia nataka nimuoe akakubali! Ana uzuri wa kawaida tu ila ni mstaarabu sana, muwazi, hana mambo mengi na ananiheshimu sana ingawa kanipita umri! Nafikiria kumuoa mara tu nikipata kazi, je kuna tatizo lolote hapo wajameni?
 
Kk kwanza pole sn kw hilo,
Pili napenda kk shauri ya kwamba
Miongoni mwa kanuni za mapenzi ni
upendo wa zati na sio UMRI nk.
Je,nakama mngekkua lika sawa halafu yy ni kilema
kw namna yeyote ile wangesemaje?
Binadamu ndivyo tulivyo kk ww baku na msimamo wako.
ONE LOVE KAKA:nono:
 
Umri sio shida kabisa katika mapenzi,cha muhimu ni mapenzi, kama unampenda kweli muoe,ila kama upo kwa ajili ya pesa zake, usimuoe kabisa
 
kitu muhimu cha kujiuliza ni hiki?
JE, UNAMPENDA KWA DHATI au sababu ya kazi na pesa zake?
JE, ANAKUPENDA WEWE KWA DHATI just the way you are?
kama majibu ni ndio mi nakushauri go for it, marry her and be happy nad rest of the world an the ''words'' are just ''background noise''!
goodluck..
 
hujakua kiasi cha kutaka kuoa, kama ungekuwa umekua kiakili kiasi cha kuweza kuoa usingeandika ulichoandika.
Kuoa au kuolewa lazima yawe maamuzi yako muoaji au muolewaji bila shinikizo/shurutisho/ushauri, lazima wewe mwenyewe ufanye maamuzi kwa akili yako..
Kama huna hoja ya kutaka kuoa halafu unataka sisi tukupe hoja ya kuoa/kutooa unapotaka kuoa, hujakua kiasi cha kutosha kuoa!
 
Ingia uwanjani kwanza uanze kuicheza ngoma ndio ujue utamu wake. Dogo kupishana umri sio shida, ila that is too much....hapo mimi sikushauri kabisa yani 26 kwa 35?

Mh!kweli kupishana umri sio issue,bt it depend umri mliopishana!....even mi nimempita 2 yrs,bt 26 to 35!! Mh!parefu jamani
 
Kwa thread hii umeonesha hujiamini na hufai kuwa na familia
'
Kama ungekua unajiamini usingekuja hapa,kusema unaonewa wivu ni dalili ya kushindana na woga ulio ndani mwako
'
Pia kelele za rafiki zako zinakuchanganya sana
'
Halafu inaonekana vitu vya huyo dada ndo vimekuchanganya zaidi maana hapa hujazunguzia chochote kuhusu hisia wala mapenzi yako kwa huyo dada
'
I feel sory for her!

Hili nalo neno!?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom