Usiende Dar kama hauna ramani ya uhakika

Usiende Dar kama hauna ramani ya uhakika

Duuuhhh.......umetema sana cheche mjomba, vp kuna jambo lolote limekukuta kaka!!!????

Ingawa kuna ka ukweli in between
Nasikitika sana kuona vijana wanalala kwenye vibaraza vya fremu za maduka yakifungwa, watoto wa kike wanapewa pombe na kupelekwa gesti/magetoni wakiwa hawajitambua na kuishia kuingiliwa kinyume na maumbile. Vijana wanaishi maisha ya kubangaiza wakati wangebaki uko kwao mikoani wangeishi vizuri tu
 
Nasikitika sana kuona vijana wanalala kwenye vibaraza vya fremu za maduka yakifungwa, watoto wa kike wanapewa pombe na kupelekwa gesti/magetoni wakiwa hawajitambua na kuishia kuingiliwa kinyume na maumbile. Vijana wanaishi maisha ya kubangaiza wakati wangebaki uko kwao mikoani wangeishi vizuri tu
Ila dar palinishinda hasa jambo la usafiri.
 
Mkuu tuondoe mawinga kwenye uzi wako please[emoji1787]
[emoji3][emoji3][emoji3] nina mwanangu winga maisha tunayoishi ndio haya haya tu, nikisikiaga story eti winga anapiga laki per day naishia kucheka tu. Laki kwa siku ni ni milioni 3 kwa mwezi kibongo bongo ni mshahara wa boss wa taasisi kubwa tu.
 
Kwa kweli dar ni nzuri na ina ufahari wote wa nchi hii. Dar ndiyo Tanzania yenyewe kila raia wa nchi hii anapaswa kufika dar kuona utukufu wa nchi hii. Ila kama huna ramani utataka kurudi haraka sana ulikotoka, kila kitu ni gharama tu, usafiri wenyewe utakuchosha kwenda na kurudi kibaruani mshahara wote unaweza kuishia kwenye usafiri tu
Wapo wanaoishi peponi wakiwa Dar ila ni asilimia ndogo sana ukilinganisha na wanaotaabika
 
Hapo watoto wa kike wanategemea kunini.. aisee tunashukuru kwa kututukana[emoji25]
Huo ni kweli labda mmetofautiana strategies tu. Kuna wanaojiuza directly mitandaoni, kumbi za starehe, barabarani n.k na kuna wanaojiuza indirectly kupitia mahusiano ya kimapenzi wengine wanaingia mpaka kwenye ndoa ila target yao ni maokoto. Hata wewe mwanaume akikutongoza lazima uangalie msuli wake kiuchumi upo vipi kwa mategemeo ya kupata financial benefits hapo ni sawa tu na kujiuza indirectly
 
Sawa wasiende dar bila ramani Ila Wapi huko wanatakiwa kwenda na kufanikiwa bila ramani mkuu

Kuna mkoa utaenda tu kwa kuvamia na kufanikiwa chap bila kupitia ugumu flani mwanzoni??..

By the way mkuu kuna watu Dar wanaishi bhana, si kila mtu Dar anateseka
 
Acha uoga wewe njoo hapa Vingunguti tuuze matikiti na mananasi. Kipande miambili kwa jero hukosi liteni kwa siku. Mnakuja mjini hamjasoma halafu mnachagua kazi.
Nyie ni waongo tu. Story kama zako sio mara ya kwanza kukutana nazo. Kuna jamaa aliniletea sound kama hizi, kuna mishe ilinipeleka dar nikasema ngoja nimcheki mwamba akaanza siasa. Nina uhakika nikija pm unipe ramani za huo mchongo hapo vingunguti utaishia kuleta blah blah tu
 
Back
Top Bottom