Usidanganyike, Wanawake hawana mapenzi ya kweli

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,877
Habari Wakuu!

Bila kupoteza muda. Kichwa cha habari hapo juu chahusika.

Wanawake ni Mama zetu, dada zetu, shangazi, Bibi na pia Wake zetu. Tunawapenda Kwa sababu Sisi ndio wenye Kupenda, upendo ni Asili yake ni kutoka kwetu.

Hata hivyo hatuwalaumu wanawake Kwa tabi zao kwani ndivyo hulka Yao ilivyo. Wai kimsingi wameumbwa kutii tuu, mioyo yao haipo connected na wanaume, bali ipo connected na watoto watakaowazaa tuu.

Wakati moyo wa mwanaume umeumbwa kumpenda na kumlinda Mwanamke.

Asije akakudanganya Mtu kuwa mwanamke anakupenda, sio kweli, unadanganywa wewe.
Labda mwanamke huyo awe Mama yako mzazi,

Mwanamke humpenda mtu atakayeona anampenda,
Hata Kama Mwanamke Hakuwa na hisia na wewe, lakini ukimpenda Kwa kumjali na kumhudumia atakupenda automatically.

Upendo ni nini?
Upendo ni Kutoa

Mwanamke kama huna chakumpa hawezi akakupenda nakuhakikishia.

Ili uwe na upendo lazima uwe na chakutoa, na ili uwe na chakutoa lazima uwe na kazi inayokuingizia mapato.
Ndio maana amri za Mungu zinaeleza kabisa ufanye KAZI Kwa siku sita kisha upumzike siku Moja. Tafsiri yake ufanye kazi ili uwe na Upendo (upate Chakutoa).

Kula Kwa jasho ni amri aliyopewa MWANAUME, yaani kufanya kazi ni kwawanaume tuu. Wanawake hawakuumbwa Kupenda isipokuwa kupendwa. Hawakuumbwa kufanya kazi ili wapate mapato kwani hawako Kwa ajili ya kutoa isipokuwa kupewa.

Watu wengi wanawalaumu wanawake Kwa sababu hawana elimu kuhusu hawa viumbe.

Huwezi ukasema unampenda mwanamke wakati huna chakumpa alafu utegemee atakutii. Sio kweli.
Mwanamke ili akutii lazima umpende( uwe na chakutoa), yaani umuhudumie.

Mioyo WA wanawake ni dhaifu hivyo inahitaji upendo wa kweli(kuhudumiwa haswa)

Udhaifu wa mwanamke upo katika kupewa Huduma. Hakuna mwanamke atakayesimama na kukataa kupendwa(kuhudumiwa)

Vijana lazima wafundishwe na waache kujidanganya kuwa mwanamke anaweza akakupenda pasipo Upendo (Mali au kitu chakutoa), huko ni kujidanganya. Na hizo ni hisia za kitoto ambazo madhara hujitokeza baada ya miaka mingi kupita.

Hata Mungu anaitwa anaupendo Kwa sababu Yeye ndiye mtoaji, anayetulea na kutuhudumia, mwenye Utajiri na ndio maana tunamuomba.

Wanawake hujisikia fahari kuomba na kupewa kutoka Kwa mwanaume. Ni mwiko Kwa mwanamke kuombwa, sio asili Yao. Watakuvumilia Mwanzoni lakini mwishoni watakupa Fedheha na aibu.

Upendo ni Kutoa Huduma
Upendo ni ulinzi
Upendo ni kujali,
Upendo ni kuthamini,

Yote hayo mwanaume lazima uyatimize ili mwanamke akutiii na sio akupende.

Mwanamke anaweza ishi na Mwanaume yeyote Yule ilimradi anapendwa na huyo mwanaume (anakitu cha kumpa)
Ila mwanaume hawezi ishi na Mwanamke Yeyote.

Mwanamke humuoa mwanamke anayempenda,
Tofauti na Wanawake, anaweza kuwa hakupendi(Hana hisia na wewe) na ukamuoa alafu baada ya wewe kumuonyeshea upendo akakupenda.

Mbali na kumhudumia mwanamke ambapo ndio huitwa Upendo.
Mwanamke ili akutii itakupasa umfikishe katika kilele cha mlima Kilimanjaro.

Huwezi kuwa na mamlaka Kwa mwanamke ukiwa hauna Upendo (yaani huwezi kumhudumia na huna chakutoa).

Kwa nini wanawake wanauhitaji upendo(kuhudumiwa na kutukuzwa)?

1. Wanawake maumbile Yao ni mepesi kuchakaa, hivyo pasipo kutunzwa huwa Wabaya zaidi ya wanaume. Ndio maana hutafuta wanaume wakuwapenda(kuwahudumia)

2. Wanawake pasipo urembo hawana lolote la ziada, wengi hawavutii.
Wanawake bila Mafuta mazuri, urembo WA mavazi, viatu, nywele kuhudumiwa vizuri wala hautawataka.
Wengi wao ni hawavutii.
Hivyo kumtunza Mkeo(kumpenda) Kwa kumpa pesa za Mafuta, mavazi, urembo wa usoni, kucha au nywele ndiko kutazidi kuufurahisha moyo wa mwanamke akutii.
Wanawake pesa zao nyingi huzielekezea kwenye urembo ili kuficha madhaifu ya maumbile Yao na kuwafanya wavutie.

Mwanamke asiyependeza huonekana Kama mumewe hampendi(kashindwa kumhudumia).

3. Wanawake hupenda kuheshimiwa.
Bila kupendwa hakuna heshima Kwa mwanamke. Heshima ya mwanamke ipo katika kupendwa.
Wanawake wapo Radhi wasalimishe kila kitu ilimradi wapendwe tofauti na wanaume ambao Sisi tunahitaji Kuheshimiwa na kutiiwa.

Mwanamke ukimpenda ndio ataona unamheshimu. Na hapa kupendwa inamaana ya kumhudumia na kumtunza Jambo ambalo Vijana wengi WA siku hizi hawalijui.

Mwanamke akipendeza kwake ndio Heshima, ukimjali mbele za watu na kumsifia kwake ndio huona sifa na heshima kubwa.

Ukiona mwanamke amekuambia haumheshimu tafsiri yake amekuambia humpendi.
Maana Kama ungekuwa unampenda, usingelala na wanawake wengine, usingemnyima pesa ya wigi, usingechelewa Kurudi bila kumpa taarifa.

Mwanamke anaamini kuwa ili umpende anatakiwa awe pekeake, tofauti na uhalisia wa upendo.
Upendo unagawanyika Ila utii haugawanyiki.
Hauwezi kutii mamlaka mbili Kwa wakati mmoja Ila unaweza Kupenda watu, vitu au mambo mawili Kwa wakati mmoja.

4. Wanawake wanapenda maonyesho na mashindano.
Sio ajabu wakapenda Harusi na sherehe za hapa na pale. Ni Kwa sababu wameumbwa hivyo. Wao ni Maua ya Dunia, huko huenda kuonyesha fahari zao, Kama sio uzuri wao, basi urembo wao, au mambo yote ya kuvutia waliojaliwa.

Mwanamke humtii mwanaume atakayemfanya muda wowote apendeze na kuwaringishia wanawake wenzake, Avae vizuri kwenye Harusi au sherehe apendeze, aende kanisani na nguo mpya kila mara.
Sio kila wiki nguo moja kama Sanda lazima utagombana na Mkeo na ataacha kukupenda(kukupa utiifu wake)

Wanawake hupenda kuangaliana wamevaaje, akipita mwanamke anajua anaangaliwa.
Sasa Kama umemvalisha masulupwete au kichwani anamsuko uleule usioeleweka unataka akuchekee, akupende(akupe utiifu wake)? Hilo haliwezekaniki.

Mwanamke anaacha kukupenda(kukupa utii wake) pale unapoacha kumpenda (kumhudumia na kumtunza)
Kadiri unavyohangaika kumpenda Mkeo ndivyo Naye anavyozidisha utiifu kwako.

Hivyo kanuni inaweza kuwa, Upendo unatangulia ndipo utiifu ufuate.

Sio mwanaume utake kutiiwa wakati hujatanguliza upendo(hujatoa chochote).

Vijana wa sasa hawajui falsafa na Miyazaki ya wanawake ndio maana wanapata shida kuhusiana nao.
Wanawashangaa mabinti pindi wanapokutana nao Kwa mara ya Kwanza alafu hata hawajazoeana wanaanza Kupiga vizinga, kuomba pesa sijui za nywele, sijui Kodi, sijui umeme miongoni mwa Huduma zingine.
Ndivyo wanawake walivyo, hawawezi kukupa utiifu wao kabla hujatanguliza upendo(kutoa Huduma na Matunzo Kwanza).

Wanaume wenye akili na wanaojua akili za wanawake huwaga hujifanya hawanaga haraka nao😀😀 pindi wakutanapo huwapa vizawadi mara nguo, mara elfu hamsini, mara Out Kula Dinner,
Mtoto wa kike anaingia kingi automatically, huanza kuhisi anapendwa hata Kama Mwanaume hampendi.

Hakuna mwanamke mwenye nguvu ya kukataa kupendwa(kuhudumiwa na kutunzwa) hayupo chini ya jua.

Mwanamke anaupendo wa kweli Kwa mtoto wake tuu.
Kwa Mimi na Wewe wanaume itategemea na Upendo tulionao dhidi yake.

Kumbuka kila mwanamke anamatarajio yake ya maisha mazuri, hivyo unapokuwa Naye lazima uyatimize matarajio hayo ili azidi kukupenda(kukupa utiifu wake). Tofauti na hapo lazima akuadhibu uzeeni Kama sio Kwa maneno basi kupitia watoto wako uliyemzaa Naye.

Nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
 
FB_IMG_16453663968245784.jpg
 
Habari Wakuu!

Bila kupoteza muda. Kichwa cha habari hapo juu chahusika.

Wanawake ni Mama zetu, dada zetu, shangazi, Bibi na pia Wake zetu. Tunawapenda Kwa sababu Sisi ndio wenye Kupenda, upendo ni Asili yake ni kutoka kwetu.

Hata hivyo hatuwalaumu wanawake Kwa tabi zao kwani ndivyo hulka Yao ilivyo. Wai kimsingi wameumbwa kutii tuu, mioyo yao haipo connected
Upendo = Mwanaume Kutoa = Mwanaume Kuhudumia
Vipi kuhusu hawa wanawake/ Wakina Mama wanaowalea vijana na kuwapa kila kitu? Hebu elezea na hiyo "falsafa" pia...
 
Wewe mwandishi ni misogynist (mchukia wanawake) uliyekubuhu unayejaribu kwa nguvu zako zote kutuaminisha maoni na mitazamo yako binafsi kuhusu wanawake iliyojaa chuki. Siyo kweli hayo unayoandika.

Ungekaa nchi zilizoendelea ungejua kuwa wanawake na wanaume tabia zao huendana na tamaduni, mila, values, morals na uchumi wa jamii husika.
 
Habari Wakuu!

Bila kupoteza muda. Kichwa cha habari hapo juu chahusika.

Wanawake ni Mama zetu, dada zetu, shangazi, Bibi na pia Wake zetu. Tunawapenda Kwa sababu Sisi ndio wenye Kupenda, upendo ni Asili yake ni kutoka kwetu.
Inakuwaje sasa.Mwanamke anayependwa na kutimiziwa mahitaji yake yote anachepuka na kumpelea Mbususu yake dereva wa boda boda asie na kitu??
 
Habari Wakuu!

Bila kupoteza muda. Kichwa cha habari hapo juu chahusika.

Wanawake ni Mama zetu, dada zetu, shangazi, Bibi na pia Wake zetu. Tunawapenda Kwa sababu Sisi ndio wenye Kupenda, upendo ni Asili yake ni kutoka kwetu.

Hata hivyo hatuwalaumu wanawake Kwa tabi zao kwani ndivyo hulka Yao ilivyo. Wai kimsingi wameumbwa kutii tuu, mioyo yao haipo connected
Unaweza pamoja na sarakasi zote za kuandika apa ukawa huna mke,mpenzi wala kimada
Wanawake tuishi nao kwa akili kama bibilia inavyosema
 
Back
Top Bottom