Usichojua kuhusu makanisa ya kiroho

Usichojua kuhusu makanisa ya kiroho

Wakuu pokeeni salamu zangu,

Kutokana na kuhangaika na maradhi sugu nilijikuta naenda katika haya makanisa ya kiroho kuombewa hiki ndicho nilichokiona huko.

1. Pesa kwanza; hufanyiwi maombi mpaka ulipishwe pesa tena ukifika siku ya kwanza unaulizwa kazi unayofanya kabisa alafu watakuambia roho mtakatifu kakuambia utoe shilingi ngapi.

2. Unatolewa unabii feki kabisa; nilienda mara ya kwanza nikaambiwa tatizo langu nimerogwa kuna binti niliahidi kumuoa nikamkimbia, kwa kijana kuahidi kuoa mtu na kukimbia ni jambo la kawaida nikakubali ila naenda kuombewa tena mara ya pili akawa kanisahau kwenye unabii akasema tatizo langu linasababishwa na vifungo ambazo wazee wangu waliingia hivyo nahitaji kutoa sadaka ya ukombozi kumbuka huyo ni mtumishi mmoja anatoa unabii tofauti kwa mtu mmoja na tatizo moja.

3. Maombi hayasaidii kupona; kila ugonjwa kuna uwekano wa kupona na kutokupona wanachofanya hawa watumishi ni kucheza na probability wale wakupona wakija kutoa ushuhuda wanawavuta na wengine waje kuombewa, wale wasiopona hawana nafasi ya kuja kushuhudia tena hivyo tunawasikia waliopona tu wasiopona hatuwasikii, hivyo kuonekana watu wanapona kweli ila si kwa ajili ya maombi ni natural selection tu.

Baada ya kusema hayo naomba kuwasisitiza msidanganywe na matangazo ya redion kuhusu uponyaji ni feki uponyaji ni suala la asili hata bila kuombewa kuna watu wanapona wengine hawaponi, kazi hata bila kuombewa kuna watu watapata wengine hawawezi pata na mafanikio yoyote yale ni hivohivo.

NB: Unaweza ongeza matatizo uliokumbana nayo ulivoenda kuombewa.
Umeongea ukweli mchungu..
 
Sikatai kwamba hakuna wahubiri waongo ila kuhusu RC hapo hunidanganyi maana ni weupe ktk mambo ya kiroho maana hata mimi nilikuwa huko ukitaka wahubiri wa kweli nende kwenye hayo makanisaa ya kiroho japo wahubiri wa uongo wako hukohuko na ukitaka mapokeo baki haphapo RC
Wahubiri wa kweli ni wapi. ? Hawa wanaopayuka payuka hovyo kama waganga wa kienyeji..??
 
Mtoa mada unaweza ukawa na point lakini umeshindwa kufanya presentation vizuri. And I can only assume hii imetokana na ukweli kuwa umefanya conclusion based on kile kilichokutokea wewe na siyo kile ambacho Mungu anaongea juu ya manabii wa uongo. Manabii wa uongo hawapo kwasababu wewe ulienda kanisani ukatabiriwa mambo mawili tofauti na mtumishi mmoja. Manabii wa uongo wapo kwasababu Yesu alitabiri miaka 2000 iliyopita kuwa watatokea.

Mtu wa kwanza kutabiri kuwa kutatokea manabii wa uongo ni Yesu mwenyewe. Alisema katika Mathayo 24:5 kuwa wengi watakuja kwa jina lake wakisema wao ni Kristo. Lakini kwenye Mathayo 24:24 Yesu anarudia tena kuonya kuwa "watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo nao watatoa ishara kubwa na maajabu wapate kuwapoteza hata walio wateule". Kwenye Yohana 5:43 anaendelea kuonya tena kuwa "mimi nimekuja kwa jina langu wala hamnipokei mwingine akija kwa jina lake mtampokea".

Mifano hiyo michache kutoka kwa Kristo ni uthibitisho tosha kuwa suala la uwezekano wa kuwepo manabii wa uongo siyo habari mpya tena. Ni dhahiri kuwa lazima wawepo hata mtu asipotuambia kuwa wapo.

Kitu cha msingi ni kuelewa kuwa huwezi kuwa na NABII WA UONGO kama hayupo NABII WA UKWELI. Yaani neno uongo linatokana na neno ukweli. Huwezi kumwambia mtu anakudanganya kama hujui ukweli unafananaje. Kwa mfano, huwezi kusema simu hii ni FAKE ilihali hujui sifa za kuifanya simu kuwa ORIGINAL ni zipi. Hutaweza.

So Yesu aliposema tujihadhari na manabii wa uongo, alichokuwa anamaanisha wakati huohuo ni kuwa tujifunze ni sifa zipi zinamfanya mtu kuwa nabii wa ukweli. Alikuwa hana lengo la kutufanya kustick na kufocus kutafuta manabii wa uongo popote walipo halafu tuanze kudraw dangerous conclusions kuwa MANABII WOTE NI WAONGO TU, halafu hatufanyi jitihada zozote kuwatafuta wale walio wa ukweli. Huko kutakuwa ni kujidanganya na tutakuwa tunamsaidia Shetani kutupumbaza tu. Hatupaswi kutoa msaada wa aina yoyote kwa Shetani.

Sasa ili usitoe msaada wa aina hiyo kwa Shetani. Yaani ili uache kuhangaika kuishi kwa kutafuta makosa (faultfinding) ya watumishi na uanze kuconcentate on sifa nzuri zinazofanya mtumishi awe NABII WA KWELI, ni lazima uzame kwenye NENO LA MUNGU. Ukijifunza vizuri Neno la Mungu, utajua ni jinsi gani ufalme wa Mungu unafanya kazi na ni sifa zipi zinamqualify mtu kuwa mtumishi wa Mungu wa ukweli. In fact Biblia ina majibu ya matatizo yote binadamu anayokutana nayo kiasi kwamba ukiwa msomaji mzuri wa Neno, itafikia kipindi wala hautahitaji tena kwenda kuonana na nabii ili atatue tatizo lako. NENO la Mungu linatosha kabisa kumaliza matatizo yooooooooote unayokutana nayo makubwa au madogo. Kitu muhimu ni kuamini tu. PERIOD.

Kwahiyo anza leo kusoma Biblia yako kwa utulivu huku ukiomba uongozi wa Roho Mtakatifu ili uachane na habari za kwenda kutafuta msaada kwa manabii--wawe wa uongo au wa ukweli.
Asee umeongea vema sana.
 
Halafu hayo makanisa ya mtaani wanavyojua kuomba kwa makelele,yaani hadi saa saba za usiku ndo wanaanza kuporomosha maombi na na kufukuza mapepo kwa makelele mpaka basi,mwanzoni nilikua nashindwa kulala, lakini siku hizi walaa,najilalia zangu uzuri ,wanatoana mapepo wee mi ndo kwanza nakoroma tu, ila kuna uwezekano ya hao manabii wengine ni wasanii tu,yaani mtu anajua mistari miwili mitatu ya Bibilia na yeye kashakua mtume na Nabii na haijulikani kapewa na nani hichi cheo,maana huyu wa jirani anatia mashaka na unabii wake kwani watu wanamzungumzia kwa ubaya mara nyingi ina wezekana na yeye akawa feki,ila ndo hivyo ya ngoswe mwachie ngoswe mwenyewe kwani watu na imani zao bwana.
 
Kuna huyu bwana wa Mwanza anajiita sijui nabii Malisa,siku hiyo nyumbani sina kazi nikaona nipoteze muda kwenye tv..anawahubiria waamini kwamba watoe sadaka mpaka ziwaume na kila atakayetoa sadaka yake itarudi kwake maradufu kupitia tigopesa,m-pesa na airtel money sikuamini nilichokisikia nikajiuliza kwanini yeye asiziombee zaka zake zikarudi kwake,na watu wanaamini,muhubiri ibada nzima anasisitiza toeni sadaka toeni sadaka,zinakoenda hapajulikani wala matumizi yake hamsomewi watu hawashtuki tu.mie ni RC tukitoa sadaka zinaelezwa matumizi yake,tukiambiwa mchango kwa ajili ya kuongeza sehemu either darasa la watoto,may be kununua chochote kwa matumizi ya Parokia mahalia tukishachanga tunaelezwa zimetumikaje,salio lililobaki na litatumika wapi na kama mtu una wasiwasi unaruhusiwa kuhoji na mwisho wa mwaka tunasomewa mapato,matumizi,balance iliyobaki siyo watu wanatoa sadaka mchungaji ananunua Hummer anaishi kwenye kighorofa na hamuwezi kuhoji,ukihoji unaambiwa una pepo,nitake kuujua ukweli uniambie nina pepo?hapo juu kuna mtu kasema kwamba Catholics tunasali kwa mapokeo,nakuhakikishia mkuu wewe hujapata kuufahamu Ukatoliki umehadithiwa tu.
Mkuu hawajui mapokeo ni kitu gani....Hawajui kuwa Biblia ni mapokeo ya kanisa Katoliki maana ni vitabu na nyaraka zilipokelewa sehemu mbalimbali zikachambuliwa ndo tukapa biblia..
 
Mimi ni wa imani nyingine ila umenifundisha vitu vizuri sana. Always i appreciate what u represent madamme. God bless u, ila kakidhungu kamekosa ata kidogo leo.
Sema sasa kuna saa anapandwa na kichaa unaweza usiamini kama ni yeye..
 
Amri 10 ilikuwa ni mwanga tu ila Roho Mtakatifu ndiye arabuni yetu na kutufunza.

Amri ni torati na zipo zaidi ya 600 na waliotangulia walizishindwa maana waweza shika zote ukikosea moja wewe ni wa motoni ila kwa sasa tunaishi kwa neema tu,ndio. Maana kila saa tunatubu,kama unataka kuishi kwa Amri kumi nenda KATOLIKI AMA ISLAM,hao ndo wanaishi kwa sharia,sisi wapentekoste tunaishi kwa neema
Huu upuuzi wa ' tunaishi kwa neema' ndo ulimfanya Martin Luther kupunguza vitabu saba vya biblia..
 
Acha tu ndg yangu, nlienda kwa mzee wa ipako nlisukumwa pale madhabahuni na zile tiles zinavyoteleza mpaka nikaanguka, nafight kunyanyuka ndo anazid kunikandamiza huku wanaonishika wananilazimisha kufumba macho ili nikose balance.
Pole sana..
 
unatumia nini kupima imani, mtu mpka atoke hospital bado unauliza kama ana imani
Na hilo ndiyo tatizo la wengi. Hawajui kuwa Yesu anafanya kazi kupitia imani, lakini wanataka kupokea matendo yake. Wanafikiri wanaponywa kwasababu ya huruma ya Mungu. Siyo huruma ya Mungu inayokuponya. Ni imani yako inayokuponya. Na ukiona hujaponywa, ujue imani yako haiko thabiti. Unaamini kwa Mungu lakini wakati huohuo huamini kwasababu unahisi anayekuombea ni MUONGO. Mungu hafanyi kazi hivyo. The fact kuwa mgonjwa ametoka hospitali halafu akaenda kwa maombi haimaanishi kuwa eti ndiyo ana imani. No way
 
Kamwe sitakuja kuibiwa na huwa nashangaa sana mtu akisema hivyo! mtoa mada sio mkristo halisi atakuwa ni mkristo jina! yule alie mkristo wa kwl maana ake ana kristo ndani yake na kristo akikaa ndani yako utazijua hizo roho zenye upotofu!! kiukwl hakuna makanisa yanayofundisha kumjua Mungu na roho mtakatifu kama makanisa ya kiroho!!! lakini pia nikuambie kitu mtoa mada Yesu alipokuwa anataka kuwaombea watu aliwauliza 'je waamini?? nao waliposema ndio hapohapo walipokea uponyaji sawasawa na kuamini kwao! kwhyo sio lazma uende kwa hao manabii unaweza ukaomba ww mwnyew na kitu kikubwa kinacheta uponyaji ni IMANI iliyo ndani yako! na hiyo ndio humgusa Mungu kule aliko na kuachilia uponyaji au kutenda kitu ndani yako lakini pasipo imani utaangaika makanisa yote duniani utaambulia patupu,na utambue pia kila tendo lisilotokana na imani ni dhambi
 
Mkuu kumbuka wao ndio wanatangaza hayo maombezi sasa ukiwa na shida utaacha vipi kwenda
siez kuongea mengi lakini nina mashaka kama unamwamini Mungu ama binadamu maana unaposema hata usipoombewa unapona sasa sielewi ulienda kutafuta nini huko maana nahisi ulienda kwa madhumuni ya research si kwa kuombewa so nahisi Mungu aliona imani yako .So usilalamike sie tumepona mengi kaa viuzuri na bwana dunia hii si salama bila Mungu.Mtafute kwa bidii umjue vizuri.
 
Yesu akamwambia 'inuka uende zako imani yako imekuponya'....ndugu kila kitu ni imani.


Wajinga ndo waliwao

Wenzenu wananunua hammer na private jet kwa kuwahubiria ilo neno jinsi walivyo elewa wao

Hahahahahahahaa aisee duniani kuna mambo sana mtu anajichanga mwaka mzima aende Nigeria kwa yule anaejiita TB Joshua dah vere interesting
 
Mambo ya dini magumu sana.! Kuna binti alini chekesha. Aliniambia alienda kuombewa kwenye mojawapo ya makanisa. Sasa alipofika aliona kila aliyeombewa kwa kuwekewa mkono na mtumishi wa Mungu alianguka. Ilipofika zamu yake akawekewa mikono na mtumishi wa Mungu akaombewa lakini hakuanguka hata baada ya kusukumwa ili aanguke alirudi nyuma hatua chache lakini hakuanguka. Akawa anasema anashangaa kwanini hakuanguka wakati wenzake walianguka.
 
Anaye ponya siyo Mchungaji in Yesu Kristo pekee,kwa kuwatumia wstumishi wake wa kweli,sijawai kutana na mtumishi anaye dai malipo kwa ajili ya maombezi,unions hivyo jua umekutana na nabihi wa uongo.
 
Imani ni hakika ya mambo yatarajiwayo bayana ya mambo yasiyoonekana
 
Back
Top Bottom