Usichojua kuhusu makanisa ya kiroho

shalet

JF-Expert Member
Feb 12, 2013
3,430
3,547
Wakuu pokeeni salamu zangu,

Kutokana na kuhangaika na maradhi sugu nilijikuta naenda katika haya makanisa ya kiroho kuombewa hiki ndicho nilichokiona huko.

1. Pesa kwanza; hufanyiwi maombi mpaka ulipishwe pesa tena ukifika siku ya kwanza unaulizwa kazi unayofanya kabisa alafu watakuambia roho mtakatifu kakuambia utoe shilingi ngapi.

2. Unatolewa unabii feki kabisa; nilienda mara ya kwanza nikaambiwa tatizo langu nimerogwa kuna binti niliahidi kumuoa nikamkimbia, kwa kijana kuahidi kuoa mtu na kukimbia ni jambo la kawaida nikakubali ila naenda kuombewa tena mara ya pili akawa kanisahau kwenye unabii akasema tatizo langu linasababishwa na vifungo ambazo wazee wangu waliingia hivyo nahitaji kutoa sadaka ya ukombozi kumbuka huyo ni mtumishi mmoja anatoa unabii tofauti kwa mtu mmoja na tatizo moja.

3. Maombi hayasaidii kupona; kila ugonjwa kuna uwekano wa kupona na kutokupona wanachofanya hawa watumishi ni kucheza na probability wale wakupona wakija kutoa ushuhuda wanawavuta na wengine waje kuombewa, wale wasiopona hawana nafasi ya kuja kushuhudia tena hivyo tunawasikia waliopona tu wasiopona hatuwasikii, hivyo kuonekana watu wanapona kweli ila si kwa ajili ya maombi ni natural selection tu.

Baada ya kusema hayo naomba kuwasisitiza msidanganywe na matangazo ya redion kuhusu uponyaji ni feki uponyaji ni suala la asili hata bila kuombewa kuna watu wanapona wengine hawaponi, kazi hata bila kuombewa kuna watu watapata wengine hawawezi pata na mafanikio yoyote yale ni hivohivo.

NB: Unaweza ongeza matatizo uliokumbana nayo ulivoenda kuombewa.
 
Mtoa mada usidanganywe na shetani kwasababu ya hao watumishi feki. Uponyaji kwa jina la Yesu upo na hata maandiko matakatifu yanakiri hivyo. Kiukweli kumekuwa na makanisa mengi ya kitapeli yanayojiita ya kiroho. Binafsi baada ya kugundua ujanja ujanja huu mimi na familia yangu tumeamua kusali Kanisa Katoliki tu na kama ni maombezi ni humo humo kupitia Karistimatiki Katoliki Emaus Centre ubungo badala ya kutangatanga na watumishi wa makanisa ya kiroho feki.
 
wakuu pokeeni salamu zangu,
kutokana na kuhangaika na maradhi sugu nilijikuta naenda katika haya makanisa ya kiroho kuombewa hiki ndicho nilichokiona huko.

1. Pesa kwanza; hufanyiwi maombi mpaka ulipishwe pesa tena ukifika siku ya kwanza unaulizwa kazi unayofanya kabisa alafu watakuambia roho Mtakatifu kakuambia utoe shilingi ngapi.

2. Unatolewa unabii feki kabisa; nilienda mara ya kwanza nikaambiwa tatizo langu nimerogwa kuna binti niliahidi kumuoa nikamkimbia, kwa kijana kuahidi kuoa mtu na kukimbia ni jambo la kawaida nikakubali ila naenda kuombewa tena mara ya pili akawa kanisahau kwenye unabii akasema tatizo langu linasababishwa na vifungo ambazo wazee wangu waliingia hivyo nahitaji kutoa sadaka ya ukombozi kumbuka huyo ni mtumishi mmoja anatoa unabii tofauti kwa mtu mmoja na tatizo moja.

3. Maombi hayasaidii kupona; kila ugonjwa kuna uwekano wa kupona na kutokupona wanachofanya hawa watumishi ni kucheza na probability wale wakupona wakija kutoa ushuhuda wanawavuta na wengine waje kuombewa, wale wasiopona hawana nafasi ya kuja kushuhudia tena hivyo tunawasikia waliopona tu wasiopona hatuwasikii, hivyo kuonekana watu wanapona kweli ila si kwa ajili ya maombi ni natural selection tu.


Baada ya kusema hayo naomba kuwasisitiza msidanganywe na matangazo ya redion kuhusu uponyaji ni feki uponyaji ni suala la asili hata bila kuombewa kuna watu wanapona wengine hawaponi, kazi hata bila kuombewa kuna watu watapata wengine hawawezi pata na mafanikio yoyote yale ni hivohivo.

NB: unaweza ongeza matatizo uliokumbana nayo ulivoenda kuombewa.
The power of healing and success is within every one who believe being healed and being successful in anything. The only problem is lack of knowledge for most people. That's why most American church don't preach offering=healing, they only preach faith, if you give you're likely to receive blessing if you believe in offering. It's a complicated phenomenon especially in Africa, because those who claims to have healing power from our creator (of which they get it for free) they're so rich, and their followers are very very poor.
 
Mtoa mada usidanganywe na shetani kwasababu ya hao watumishi feki. Uponyaji kwa jina la Yesu upo na hata maandiko matakatifu yanakiri hivyo. Kiukweli kumekuwa na makanisa mengi ya kitapeli yanayojiita ya kiroho. Binafsi baada ya kugundua ujanja ujanja huu mimi na familia yangu tumeamua kusali Kanisa Katoliki tu na kama ni maombezi ni humo humo kupitia Karistimatiki Katoliki Emaus Centre ubungo badala ya kutangatanga na watumishi wa makanisa ya kiroho feki.
Sikatai kwamba hakuna wahubiri waongo ila kuhusu RC hapo hunidanganyi maana ni weupe ktk mambo ya kiroho maana hata mimi nilikuwa huko ukitaka wahubiri wa kweli nende kwenye hayo makanisaa ya kiroho japo wahubiri wa uongo wako hukohuko na ukitaka mapokeo baki haphapo RC
 
Sikatai kwamba hakuna wahubiri waongo ila kuhusu RC hapo hunidanganyi maana ni weupe ktk mambo ya kiroho maana hata mimi nilikuwa huko ukitaka wahubiri wa kweli nende kwenye hayo makanisaa ya kiroho japo wahubiri wa uongo wako hukohuko na ukitaka mapokeo baki haphapo RC
Karibu Emaus centre ubungo kuanzia saa nane mchana leo jumapili then uje kutoa ushuhuda hapa.
 
wakuu pokeeni salamu zangu,
kutokana na kuhangaika na maradhi sugu nilijikuta naenda katika haya makanisa ya kiroho kuombewa hiki ndicho nilichokiona huko.

1. Pesa kwanza; hufanyiwi maombi mpaka ulipishwe pesa tena ukifika siku ya kwanza unaulizwa kazi unayofanya kabisa alafu watakuambia roho Mtakatifu kakuambia utoe shilingi ngapi.

2. Unatolewa unabii feki kabisa; nilienda mara ya kwanza nikaambiwa tatizo langu nimerogwa kuna binti niliahidi kumuoa nikamkimbia, kwa kijana kuahidi kuoa mtu na kukimbia ni jambo la kawaida nikakubali ila naenda kuombewa tena mara ya pili akawa kanisahau kwenye unabii akasema tatizo langu linasababishwa na vifungo ambazo wazee wangu waliingia hivyo nahitaji kutoa sadaka ya ukombozi kumbuka huyo ni mtumishi mmoja anatoa unabii tofauti kwa mtu mmoja na tatizo moja.

3. Maombi hayasaidii kupona; kila ugonjwa kuna uwekano wa kupona na kutokupona wanachofanya hawa watumishi ni kucheza na probability wale wakupona wakija kutoa ushuhuda wanawavuta na wengine waje kuombewa, wale wasiopona hawana nafasi ya kuja kushuhudia tena hivyo tunawasikia waliopona tu wasiopona hatuwasikii, hivyo kuonekana watu wanapona kweli ila si kwa ajili ya maombi ni natural selection tu.


Baada ya kusema hayo naomba kuwasisitiza msidanganywe na matangazo ya redion kuhusu uponyaji ni feki uponyaji ni suala la asili hata bila kuombewa kuna watu wanapona wengine hawaponi, kazi hata bila kuombewa kuna watu watapata wengine hawawezi pata na mafanikio yoyote yale ni hivohivo.

NB: unaweza ongeza matatizo uliokumbana nayo ulivoenda kuombewa.

Samahani Ndugu Je!unaamini Mungu yupo!? Je! unaamini katika Krsto?
 
Kwani nn kipya zaidi ya biashara, wanajua hao kuwekza kwenye biashara na biashara ni matangazo kaka na wakati gani.watu wanapiga Pesa so mchezo kaka.
 
Mkuu kumbuka wao ndio wanatangaza hayo maombezi sasa ukiwa na shida utaacha vipi kwenda
Shida yako uliliendea Kanisa kwa dhana ile wanawake waliokata tamaa wanawaendea SANGOMA. Kwanza jirudi, nenda kanisani na sio kwa wapiga dili. Nani alikwambia kanisani watu wanaaguliwa? Ina maana shida yako ikiisha hutaenda tena?

Nenda pale Kibamba kwa Pastor John, utaombewa mapepo yako yaishe bure.
 
Mtoa mada unaweza ukawa na point lakini umeshindwa kufanya presentation vizuri. And I can only assume hii imetokana na ukweli kuwa umefanya conclusion based on kile kilichokutokea wewe na siyo kile ambacho Mungu anaongea juu ya manabii wa uongo. Manabii wa uongo hawapo kwasababu wewe ulienda kanisani ukatabiriwa mambo mawili tofauti na mtumishi mmoja. Manabii wa uongo wapo kwasababu Yesu alitabiri miaka 2000 iliyopita kuwa watatokea.

Mtu wa kwanza kutabiri kuwa kutatokea manabii wa uongo ni Yesu mwenyewe. Alisema katika Mathayo 24:5 kuwa wengi watakuja kwa jina lake wakisema wao ni Kristo. Lakini kwenye Mathayo 24:24 Yesu anarudia tena kuonya kuwa "watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo nao watatoa ishara kubwa na maajabu wapate kuwapoteza hata walio wateule". Kwenye Yohana 5:43 anaendelea kuonya tena kuwa "mimi nimekuja kwa jina langu wala hamnipokei mwingine akija kwa jina lake mtampokea".

Mifano hiyo michache kutoka kwa Kristo ni uthibitisho tosha kuwa suala la uwezekano wa kuwepo manabii wa uongo siyo habari mpya tena. Ni dhahiri kuwa lazima wawepo hata mtu asipotuambia kuwa wapo.

Kitu cha msingi ni kuelewa kuwa huwezi kuwa na NABII WA UONGO kama hayupo NABII WA UKWELI. Yaani neno uongo linatokana na neno ukweli. Huwezi kumwambia mtu anakudanganya kama hujui ukweli unafananaje. Kwa mfano, huwezi kusema simu hii ni FAKE ilihali hujui sifa za kuifanya simu kuwa ORIGINAL ni zipi. Hutaweza.

So Yesu aliposema tujihadhari na manabii wa uongo, alichokuwa anamaanisha wakati huohuo ni kuwa tujifunze ni sifa zipi zinamfanya mtu kuwa nabii wa ukweli. Alikuwa hana lengo la kutufanya kustick na kufocus kutafuta manabii wa uongo popote walipo halafu tuanze kudraw dangerous conclusions kuwa MANABII WOTE NI WAONGO TU, halafu hatufanyi jitihada zozote kuwatafuta wale walio wa ukweli. Huko kutakuwa ni kujidanganya na tutakuwa tunamsaidia Shetani kutupumbaza tu. Hatupaswi kutoa msaada wa aina yoyote kwa Shetani.

Sasa ili usitoe msaada wa aina hiyo kwa Shetani. Yaani ili uache kuhangaika kuishi kwa kutafuta makosa (faultfinding) ya watumishi na uanze kuconcentate on sifa nzuri zinazofanya mtumishi awe NABII WA KWELI, ni lazima uzame kwenye NENO LA MUNGU. Ukijifunza vizuri Neno la Mungu, utajua ni jinsi gani ufalme wa Mungu unafanya kazi na ni sifa zipi zinamqualify mtu kuwa mtumishi wa Mungu wa ukweli. In fact Biblia ina majibu ya matatizo yote binadamu anayokutana nayo kiasi kwamba ukiwa msomaji mzuri wa Neno, itafikia kipindi wala hautahitaji tena kwenda kuonana na nabii ili atatue tatizo lako. NENO la Mungu linatosha kabisa kumaliza matatizo yooooooooote unayokutana nayo makubwa au madogo. Kitu muhimu ni kuamini tu. PERIOD.

Kwahiyo anza leo kusoma Biblia yako kwa utulivu huku ukiomba uongozi wa Roho Mtakatifu ili uachane na habari za kwenda kutafuta msaada kwa manabii--wawe wa uongo au wa ukweli.
 
Back
Top Bottom