Usichojua kuhusu makanisa ya kiroho

Usichojua kuhusu makanisa ya kiroho

Hivi watanzania ndiyo mnaojua neno la Mungu kushinda ulimwengu mzima?mimi ningekuwa na mamlaka ningechoma vikanisa uchwala vya mtu mmoja mmoja.Hapa nchini hakuna Nabii wala mtumishi wote ni wezi tu.Ujinga wenu ndio unasababisha mhandike kwa kujipendekeza,yote ni ubatili afadhali uislaamu mara mia
Kwani huko uislamuni wamekufukuza au njia huijui?
 
Acha tu ndg yangu, nlienda kwa mzee wa ipako nlisukumwa pale madhabahuni na zile tiles zinavyoteleza mpaka nikaanguka, nafight kunyanyuka ndo anazid kunikandamiza huku wanaonishika wananilazimisha kufumba macho ili nikose balance.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji97] [emoji28] [emoji226] [emoji97] [emoji226] [emoji97] [emoji226] [emoji228] [emoji97] [emoji97] I'm crying rivers
.
 
Mkuu hawajui mapokeo ni kitu gani....Hawajui kuwa Biblia ni mapokeo ya kanisa Katoliki maana ni vitabu na nyaraka zilipokelewa sehemu mbalimbali zikachambuliwa ndo tukapa biblia..
Catholic mali yenu ni misali ya waumini Bible hamna mwenye hati miliki.
 
Imani si kitu cha ajabu, imani ni uhakika wa mambo yatarajiwayo - usiyoyaona!

Imani, imani jamani - kuweni na imani ili muwe na amani! Hata siku moja sitoweza kuwabeza waombaji / waombewa kwa sababu nimeishaona mengi, mama yangu kaugua nikiwa bado primary - kwa sasa nina mtoto yuko chuo - mama hajapona pamoja na kuombewa mara kibao.
Lakini wapo watu ambao waliwahi kuombewa na wakapona na kutoa ushuhuda! Mimi binafsi sijawahi kuombewa, huwa naomba mwenyewe kwa kadri ninavyoweza; majibu nayapata na huenda kama ningekuwa siombi nisingekuwa kama nilivyo!
 
Wakuu pokeeni salamu zangu,

Kutokana na kuhangaika na maradhi sugu nilijikuta naenda katika haya makanisa ya kiroho kuombewa hiki ndicho nilichokiona huko.

1. Pesa kwanza; hufanyiwi maombi mpaka ulipishwe pesa tena ukifika siku ya kwanza unaulizwa kazi unayofanya kabisa alafu watakuambia roho mtakatifu kakuambia utoe shilingi ngapi.

2. Unatolewa unabii feki kabisa; nilienda mara ya kwanza nikaambiwa tatizo langu nimerogwa kuna binti niliahidi kumuoa nikamkimbia, kwa kijana kuahidi kuoa mtu na kukimbia ni jambo la kawaida nikakubali ila naenda kuombewa tena mara ya pili akawa kanisahau kwenye unabii akasema tatizo langu linasababishwa na vifungo ambazo wazee wangu waliingia hivyo nahitaji kutoa sadaka ya ukombozi kumbuka huyo ni mtumishi mmoja anatoa unabii tofauti kwa mtu mmoja na tatizo moja.

3. Maombi hayasaidii kupona; kila ugonjwa kuna uwekano wa kupona na kutokupona wanachofanya hawa watumishi ni kucheza na probability wale wakupona wakija kutoa ushuhuda wanawavuta na wengine waje kuombewa, wale wasiopona hawana nafasi ya kuja kushuhudia tena hivyo tunawasikia waliopona tu wasiopona hatuwasikii, hivyo kuonekana watu wanapona kweli ila si kwa ajili ya maombi ni natural selection tu.

Baada ya kusema hayo naomba kuwasisitiza msidanganywe na matangazo ya redion kuhusu uponyaji ni feki uponyaji ni suala la asili hata bila kuombewa kuna watu wanapona wengine hawaponi, kazi hata bila kuombewa kuna watu watapata wengine hawawezi pata na mafanikio yoyote yale ni hivohivo.

NB: Unaweza ongeza matatizo uliokumbana nayo ulivoenda kuombewa.
huwa nafurahi sana nikiona mtu kawa na akili hivi,hongera ingawa umechelewa sana kuelevuka,wenzio tangu enzi tunalijua hilo,kuwa zile nazo ni hustle za watu,sawa tu na mpiga debe kituo cha daladala..
 
Mtoa mada usidanganywe na shetani kwasababu ya hao watumishi feki. Uponyaji kwa jina la Yesu upo na hata maandiko matakatifu yanakiri hivyo. Kiukweli kumekuwa na makanisa mengi ya kitapeli yanayojiita ya kiroho. Binafsi baada ya kugundua ujanja ujanja huu mimi na familia yangu tumeamua kusali Kanisa Katoliki tu na kama ni maombezi ni humo humo kupitia Karistimatiki Katoliki Emaus Centre ubungo badala ya kutangatanga na watumishi wa makanisa ya kiroho feki.
Ila msisahau ubatizo wa maji mengi !:,
 
Sikatai kwamba hakuna wahubiri waongo ila kuhusu RC hapo hunidanganyi maana ni weupe ktk mambo ya kiroho maana hata mimi nilikuwa huko ukitaka wahubiri wa kweli nende kwenye hayo makanisaa ya kiroho japo wahubiri wa uongo wako hukohuko na ukitaka mapokeo baki haphapo RC
kumbe ndio maana haufanikiwi,una umalaya wa dini...
 
Mtoa mada usidanganywe na shetani kwasababu ya hao watumishi feki. Uponyaji kwa jina la Yesu upo na hata maandiko matakatifu yanakiri hivyo. Kiukweli kumekuwa na makanisa mengi ya kitapeli yanayojiita ya kiroho. Binafsi baada ya kugundua ujanja ujanja huu mimi na familia yangu tumeamua kusali Kanisa Katoliki tu na kama ni maombezi ni humo humo kupitia Karistimatiki Katoliki Emaus Centre ubungo badala ya kutangatanga na watumishi wa makanisa ya kiroho feki.
Na mm ni hivyo hivyo naendaga karismatiki AGAPE mbezi kibanda cha mkaa nabarikiwa sana na hamna cha kudaiwa pesa na watu wanapona.
 
Yesu akamwambia 'inuka uende zako imani yako imekuponya'....ndugu kila kitu ni imani.
lakini yesu hakuja kwa ajili ya kuponya wagonjwa yesu alifundisha watu wamwamini na kuishi kama yeye, automatically hayo matatizo yatakuwa deleted, bila kuelewa hao waombeaji na waombewa wote ni wasanii
 
Wakuu pokeeni salamu zangu,

Kutokana na kuhangaika na maradhi sugu nilijikuta naenda katika haya makanisa ya kiroho kuombewa hiki ndicho nilichokiona huko.

1. Pesa kwanza; hufanyiwi maombi mpaka ulipishwe pesa tena ukifika siku ya kwanza unaulizwa kazi unayofanya kabisa alafu watakuambia roho mtakatifu kakuambia utoe shilingi ngapi.

2. Unatolewa unabii feki kabisa; nilienda mara ya kwanza nikaambiwa tatizo langu nimerogwa kuna binti niliahidi kumuoa nikamkimbia, kwa kijana kuahidi kuoa mtu na kukimbia ni jambo la kawaida nikakubali ila naenda kuombewa tena mara ya pili akawa kanisahau kwenye unabii akasema tatizo langu linasababishwa na vifungo ambazo wazee wangu waliingia hivyo nahitaji kutoa sadaka ya ukombozi kumbuka huyo ni mtumishi mmoja anatoa unabii tofauti kwa mtu mmoja na tatizo moja.

3. Maombi hayasaidii kupona; kila ugonjwa kuna uwekano wa kupona na kutokupona wanachofanya hawa watumishi ni kucheza na probability wale wakupona wakija kutoa ushuhuda wanawavuta na wengine waje kuombewa, wale wasiopona hawana nafasi ya kuja kushuhudia tena hivyo tunawasikia waliopona tu wasiopona hatuwasikii, hivyo kuonekana watu wanapona kweli ila si kwa ajili ya maombi ni natural selection tu.

Baada ya kusema hayo naomba kuwasisitiza msidanganywe na matangazo ya redion kuhusu uponyaji ni feki uponyaji ni suala la asili hata bila kuombewa kuna watu wanapona wengine hawaponi, kazi hata bila kuombewa kuna watu watapata wengine hawawezi pata na mafanikio yoyote yale ni hivohivo.

NB: Unaweza ongeza matatizo uliokumbana nayo ulivoenda kuombewa.
Wewe utakuwa unasumbuliwa na mapepo wa kuzuia kuamini.........

Muujiza wa uponyaji unatokea pale tu wewe unayeumwa ukiwa na imani kuwa Mungu aweza kukuponyesha kupitia maombi.....

Inapotokea wewe unayeumwa una doubt kuhusu muujiza huo, huwezi kamwe kupokea muujiza huo wa uponyaji.....
 
Amini hili mkuu, kumjua nabii wa ukweli au wa uongo kunahitaji muda, kupona ugonjwa sio kipimo chakumjua nabii wa ukweli au uongo, na sio ukienda kuombewa lazima upone pia unaweza kufaa tu, chamsingi omba mapenzi ya Mungu juu yako. kama ugonjwa wako ni wa kufaa kwa mujibu wa Mungu lazima ufe hata ukiombewa na nabii vingenevyo ongea na MUngu mwenyewe msawazishe wewe na yeye.

Kumbuka hukuna tatizo linamkuta mtu pasipo dhambi, dhambi ndiyo kila sababu ya uovu wote. ukikuta uovu wowote umeingia kwako au kwa watu wako au kwa familia yako au kwa ukoo wako, cha kwanza omba toba, mpaka mahusiano yako na Mungu yarudi, usikimbilie kuombewa wakati una dhambi na roho yako inakushuhudia, nabii sio mganga wa kienyeji nae anatafuta connection na Mungu huyo huyo uliyemtenda dhambi ili wewe upone.

Kwa mujibu agano jipya kuponywa kwako hakumuhitaji mtumishi yeyote, kunahitaji roho ya toba na moyo uliotiyari kuacha uovu wako kwenda na Mungu. Kumbuka wewe kwa MUNGU ni muhimu kuliko kitu chochote, akikutaka urudi kwake baada ya dhambi yako, anaondo ulinzi wake ili uovu na taababu vikujie, na kadiri unavyo kuwa mgumu ndiyo vinaongezeka ili uombe toba na akupate tene kwake, dhambi ni uasi kwake, magonjwa na shida ni check and balance ya uhusiano wako na MUNGU. Kwahiyo ukipata shida ujue check and balance ipo kazini.

Kazi kubwa ya watumishi ni kuutangaza ufalme wa Mungu, na kukuunganisha wewe na Mungu, pia ni kukuonyesha kweli ya Mungu ili wewe uwe na misingi ya kujisimamia. Lakini wengi tumewafanya watumishi kama waganga wa kienyeji na ndiyo maana uovu umekuwa mwingi makanisani, shetani naye amegundua udhaifu wetu wa kushindwa kujisimamia na umetufunga humohumo.

Mambo muhimu kati yako na Uhusiano wako na Mungu.

  • Ukiona uovu umeingia kwako tafuta sababu kwanini jambo hili limenikuta wakati huo omba toba kwani wote tumetenda na tunajua hakuna uganga juu ya yakobo wala uchawi juu ya israel, wakati unatafakari na kuomba toba yakufa na kupona, endelea kujitoa kwenye kila mlango wa dhambi. Kumbuka dhambi inayokusonga kwa kasi huo ndio mlango mkubwa. wengine ni uongo, wengine uizi,wengine uchawi, wengine uasherati nk

  • Tafuta maarifaa juu ya dhambi na namana ya kuzishinda, tafuta ukuu na rehema ya Mungu juu ya wenye dhambi, soma maandiko na utaona kadili siku zinavyosonga mbele mzigo wako moyoni unapungua na hamu ya kumtafuta Mungu inaongezeka na utaanza kutojali sana juu ya tatizo ulilonalo, kama ulikuwa hulali usingizi kwa sababu ya tatizo utaanza kulala, ili litimie neno lililoandikwa hakika amechukua masikitiko yetu....... na kwakupigwa kwake tumepona (Isaya 53.4-5)

  • Ukigundua uhusiano wako na Mungu umerudi anza kuomba tatizo lako likuondoke, na hata ukiomba wengine wakuombee ni sawa kwani uko online, hata ukienda kwa mtumishi akuombee hutakuwa na machukizo moyoni,na roho yako itakuongoza wapi pa kwenda hutakwenda kwa pressure ya ungonjwa bali uongozi wa roho aliyeko ndani yetu, hivyo ni rahisi kwenda kwa mtumishi sahihi, sio kila mtumishi ni sahihi kwa kila tatizo, hiyo ndiyo philosophy ya kwanini wawe wengi,wengine wako vizuri kwa kujenga imani, wengine kuondoa roho za umasikini, wengine magonjwa na miujiza, wengine neno la maarifaa na nk

  • Pia fahamu nguvu ya kupona ipo kwetu wenyewe na sio kwa watumishi, ni rahisi mtumishi kutoa pepo na sio kuponya ugonjwa, pepo anakemewa na kuondoka kwa mamlaka, ugongwa huondoka baada ya sababu iliyosababisha kuondolewa na toba na kuomba rehema ya Mungu, japo magonjwa mengine yanaweza kuondoka kirahisi pamoja na mapepo kwani hao ndiyo husababisha magojwa hayo, yaani magonjwa ya uonevu. Lakini magonjwa mengine yapo kwa watu kwa sababu yanahaki kuwepo hivyo ondoa haki hiyo harafu omba rehema ya Mungu uondoke.
Upo vizuri mkuu, bila shaka wewe utakua mfuatiliaji mzuri wa mafundisho ya mwl Mwakasege
 
Wakuu pokeeni salamu zangu,

Kutokana na kuhangaika na maradhi sugu nilijikuta naenda katika haya makanisa ya kiroho kuombewa hiki ndicho nilichokiona huko.

1. Pesa kwanza; hufanyiwi maombi mpaka ulipishwe pesa tena ukifika siku ya kwanza unaulizwa kazi unayofanya kabisa alafu watakuambia roho mtakatifu kakuambia utoe shilingi ngapi.

2. Unatolewa unabii feki kabisa; nilienda mara ya kwanza nikaambiwa tatizo langu nimerogwa kuna binti niliahidi kumuoa nikamkimbia, kwa kijana kuahidi kuoa mtu na kukimbia ni jambo la kawaida nikakubali ila naenda kuombewa tena mara ya pili akawa kanisahau kwenye unabii akasema tatizo langu linasababishwa na vifungo ambazo wazee wangu waliingia hivyo nahitaji kutoa sadaka ya ukombozi kumbuka huyo ni mtumishi mmoja anatoa unabii tofauti kwa mtu mmoja na tatizo moja.

3. Maombi hayasaidii kupona; kila ugonjwa kuna uwekano wa kupona na kutokupona wanachofanya hawa watumishi ni kucheza na probability wale wakupona wakija kutoa ushuhuda wanawavuta na wengine waje kuombewa, wale wasiopona hawana nafasi ya kuja kushuhudia tena hivyo tunawasikia waliopona tu wasiopona hatuwasikii, hivyo kuonekana watu wanapona kweli ila si kwa ajili ya maombi ni natural selection tu.

Baada ya kusema hayo naomba kuwasisitiza msidanganywe na matangazo ya redion kuhusu uponyaji ni feki uponyaji ni suala la asili hata bila kuombewa kuna watu wanapona wengine hawaponi, kazi hata bila kuombewa kuna watu watapata wengine hawawezi pata na mafanikio yoyote yale ni hivohivo.

NB: Unaweza ongeza matatizo uliokumbana nayo ulivoenda kuombewa.
Imani iko complicated ndugu...
Ninasali kwenye kanisa la kiroho kama unavoita ila nadhani uutetumakanisa ya kilokole. Hamna suala kama ilo na ata siku moja usiamini mchungaji anaetaka pesa ili akuombee. Na swala la kupona, nimeshuhudia wengi wakipona na matasa wakibeba mimba.... Hii ni ishu ya imani.
Tatizo watu wanapenda miteremko ndo maana manabii feki wako wengi sana kudanganya watu... Na wengine si manabii ila waganga wa kienyeji. Kutulia sehemu moja ndio siri. Acha kutangatanga.
 
Catholic mali yenu ni misali ya waumini Bible hamna mwenye hati miliki.
Hahaha..Hebu wacha kunifurahisha bana...Kama hujui historia ni bora kukaa kimya bana...Utaja aibika mkuu....

Wewe biblia umeijulia wapi..?? Kanisa lilikuwa toka ilipoitwa siku ya kwanza....Halafu ngoja nikupe hii! Unajua biblia imekamilika mwaka 300AD chini ya mtaguso wa Efeso..hahahaha ...

Kama hujui historia kaa kimya utaja aibika...Nikisema Biblia ni mali ya Kanisa Katoliki na maanisha na wala sibabaishi .....

Vipi wataka nikupe historia..

Daah...
 
Back
Top Bottom