Ushuhuda wenye kuumiza mno

Inaumiza kweli. May his soul rest in eternal peace, amen.
 
Maisha ni kitu cha ajabu sana. Ila pamoja na hayo - elimu ya watu kuhusu makatazo mbalimbali ni shida kubwa sana. kama watanzania tungeelewa sheria na taratibu tukazifuata majanga kama hayo yangeweza kupunguzwa athari zake. Mfano tu, gari imeshaandikwa DANGER! ila tunaona nalo ni neno tu. Hii huanza kwa vitu vidogo kama kuvuka barabara eneo ambalo halina zebra na huku zebra iko pembeni tu kidogo.
Our Ignorance is incomprehensible
 
Maisha ni fumbo hivyo basi sisi kama binadamu kwasababu hatujui hatima yetu katika hii dunia tukipata nafasi ya kutoa msaada tufanye kwa moyo mmoja bila kusita kwani hatujui nani atakuja kutusaidia siku ambayo tutapata shida.
Leo ukimsaidia fulani Mwenyezi Mungu ataona huruma zako jinsi unavyojali wenzio wakati wa shida atawatumia watu wengine pia kukusaidia siku ukipata matatizo, usichukulie kwamba binadamu hawasaidiki hapana yule uliemsaidia anaweza asikusaidie lakini akajitokeza mtu mwingine ambaye humjui wala hakujui akakusaidia Mungu atamtumia huyo ili kulipa fadhila ambazo siku moja ulitoa kwa mtu mwingine, na katika kusaidia usibague saidia kila mtu awe mtoto au mkubwa mwenzio.
 
Kuna siri kuna. Siri kubwa sana dereva aliona kuna kifo abiria hakukiona kifo ndio maana dereva wa bodaboda alikuwa anashurutishwa kuondoka ila mwenzake hakuona masikini hapo ndipo tunasema wapo wanadam wakawaida ila wanaona vitu visivyo kuwepo na wanaweza kuviepa.
Labda niseme kuna ulimwengu tusio uwona na huu ni hatari sana.
 
Juzi nilikuwa nasikiliza radio. Kuna mama anaomba msaada analea mtoto wa mama yake mdogo ambaye ni mlemavu..hajazaliwa na macho pia tumbo linajaa anajisaidia bila kujitambua. Ni mtoto wa miaka 9 lakini kwa mtazamo utadhani ana miaka mitatu. Mama wa watu kahangaika kauza kila kitu ili kumtunza huyo mtoto.
Sasa unajiuliza kwanini Mungu anaumba watoto wa nanma hiyo? Mtoto kakosea nini hadi kuumbwa hivyo, na huyo maza ana maisha duni hawezi kumlea mtoto bila msaada.
Najiuliza why watu wasio na hatia wapate majanga kiasi hiki? Fikiria wanaoumwa magonjwa ya ajabu ajabu au wanaopata ajali. Halafu uniambie mungu ana upendo, upendo upi?
Mtu unasema haya niache madhambi labda ndio sababu lkn utakesha ukiomba ukilia na kusaga meno lkn matatizo ndo yanakuzidi Kama umeumbwa nayo vile.
Tena unakuta wenye midhambi ya wazi wazi wanabarikiwa kila kukicha, unajiuliza hivi huyu Mungu hanioni au ni bas tu kaamua kukutesa kwa makusudi hupati jibu.
Halafu tunasema ni mipango ya Mungu...kwahiyo hizi ajali na majanga mengine kasababisha yeye? Ni upendo upi Sasa alionao yeye mi hata sielewi
 
Inavyoonekana haupo tayari kueleweshwa imani yako ngumu sana mkuu
 
Angalau abiria wa bodaboda amekutwa na kifo wakati wa kutenda mema. Kufa kwake ni faida...maandiko yanasema.

Wengine sijui tutakutwa na vifo vyetu katika mazingira gani!

Mkuu usiandike hivyo yaani ni faida yeye kuungua Moto mpaka kuteketea, hivi umewahi kuungua na Moto hata mkononi ???
 
Nikibahatika kisikiliza hicho kipindi cha SITOSAHAU cha radio free kweli kuna wakat unafikiria haya mambo hupati jibu
 
Nikibahatika kisikiliza hicho kipindi cha SITOSAHAU cha radio free kweli kuna wakat unafikiria haya mambo hupati jibu
Yaani mtu unawaza na majibu hupati. Cases zipo nyingi
 
Na Mungu ana siri kubwa juu ya maisha yetu huyo mtu alietaka kuwasaidia akaishia kufa pamoja nao ukute hiyo ndo ilikuwa Neema yake ya mwisho ya kuiona pepo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…