Nikiwa katika mji wa Dodoma kwa takriban wiki tatu sasa nimebahatika kuzungumza na makundi tofauti ya watu katika maeneo ya Kikuyu, Mkonze, Ipagala, Swaswa, Chang'ombe, Majengo na Mailimbili.
Pamoja na ukweli Mitaa ya Dodoma mjini inapendeza sasa kwa kutandazwa lami bado raia wengi wanaonyesha kuichoka CCM.
Sababu nilizozigundua ni hizi kuu 4 ingawa zipo sababu nyingi zinazoashiria anguko la CCM kwa viunga vya Dodoma
1. CCM imechokwa. Kwa kuwepo kwake madarakani kwa muda mrefu kumewafanya wengi watamani mabadiliko. Vijana wengi wenye miaka 35 kushuka chini wamezaliwa wameikuta CCM. Wameenda shule kwa level zote wapo na CCM. Wameanza kazi wapo na CCM na sasa wana familia wapo na CCM. Wana Dodoma wanasema kuna ndugu zao wamezaliwa hadi wametangulia mbele za haki bado wapo na CCM. Ndipo nilipokumbuka usemi usemao KITU CHOCHOTE KITAKACHOISHI MIAKA MINGI KINACHOFUATA NI KIFO. Kwenye Product life cycle theory, baada ya stage ya Maturity kinachofuatia ni Decline(Death). CCM imeshaishi miaka mingi. Tumezaliwa tunamsikia Wassira, Kikwete, Mangula, Kinana na wengineo. CCM imeshapita Maturity stage na sasa inaanguka. Wakazi wa Dodoma wamethibitisha.
Ili kujihalalishia uhalali wa utawala CCM imeamua kumwaga damu.
2. Wakazi wengi wa Dodoma nilioongea nao Wanaiona CCM ya sasa kama genge la wahuni. Wapo watu zaidi ya Wanne waliosema CCM ni majambazi. Sababu kuu ni kuwa wapo tayari kuua mradi tu mambo yao waende. Wanashindwa kuona natural death inayowakabili. Mkazi wa Msalato alisema CCM imeacha majukumu tuliyowapa wao kazi yao ni Chadema tu. Bungeni Chadema, Mahakamani Chadema, Mawaziri kutwa kucha Chadema. Huduma za jamii ambazo kimsingi CCM ndio wenye ridhaa ya kutekeleza zimewashinda. Wako busy kuua raia wasio na hatia na kufungua kesi zisizomsaidia mtanzania na kusahau majukumu yao. Kifupi ni kuwa Dodoma wanawaona CCM kuwa ni Chama cha Wauaji. Nilipotaka kupata maoni yao kuhusu mauaji ya bomu la Arusha walinijibu wengine kwa hasira' NANI HAJUI KUWA NI CCM WALIOUA? Kijana mmoja wa Chuo cha Mipango akamtaja kiongozi mmoja mwandamizi wa CCM anayetokea kanda hii ya kati kuwa ndiye anayepanga na kufadhili mauaji. Alikwenda mbali zaidi na kutabiri kuwa kiongozi huyo atakufa kifo kibaya sana.
3. Hali ngumu ya maisha ni jambo lililosemwa na wengi kuwa limesababishwa na CCM. Wanahoji kama tuna madini, gesi, mbuga za wanyama, bahari, Ardhi ya kutosha yenye rutuba iweje leo mtu aumwe akose huduma kwenye hospitali za umma? Iweje leo ukitoka tu kidogo mji wa dodoma hupati maji safi na salama? Iweje leo washuhudie anguko kuu la Elimu namna hii? Iweje leo Dodoma iwe na watu wanaokufa njaa?
Wapo walioamua kulima na kukamua alizeti. Hakuna masoko. Badala yake serikali imekazana na mfanyabiashara wa kiasia anayefanya biashara ya kuingiza mafuta ya alizeti akitokea nje ya nchi.
4. Vijana kukosa ajira. Wakazi wa Dodoma wameonyesha masikitiko yao hasa kwa namna vijana wanavyohangaika. Ni ukweli uliowazi kuwa vijana ndio wanao hold labour force kubwa Tanzania. Lakini VETA haijawasaidia, Elimu ya Chuo kikuu haijawasaidia, wapo wenye masters wanahangaika tu. Ukiwauliza viongozi wa kisiasa(wa CCM) wanawapa majibu mepesi eti waondoe dhana ya kuajiriwa wawaze kujiajiri. Hata mimi nilipowapa hiyo changamoto waliona kama ninawadhihaki. 'Brother mimi najiajiri naanzia wapi? Nitapata wapi uwezo wa kununua vifaa vya Capentry masikini mimi? Nani atanikopesha? Benki gani itaniamini bro? Alisema kijana mmoja wa Kikuyu aliyemaliza mafunzo ya Veta mwaka jana kwa level ya trade test two.
Madereva wa bodaboda wameponda sana sifa wasizostahili kupata CCM na serikali yake hasa kwa kuondoa ushuru wa bodaboda. Ingawa wameshukuru mkopo wa pikipiki wanaopewa na mbunge wao kwa masharti makali na magumu wamesema kabisa bila kupepesa kuwa ushuru ulioondolewa unawanufaisha wamiliki wa bodaboda na sio madereva wa bodaboda. Wao wangenufaika endapo tozo kwenye mafuta hasa petroli zingepungua na kushusha bei ya petroli hivyo kuwaongezea kipato kuliko bei ya sasa ambayo kwa madai yao kila wakipatacho kinaishia kwa mmiliki wa bodaboda.
Ni hayo tu kutoka Dodoma.