Uncle bright
JF-Expert Member
- Feb 9, 2023
- 1,040
- 4,081
Sina maana ya kuwa mmbea ama kumkandia dada yangu ila hii ndio hali halisi ya matatizo haya ya sasa yanayofanya ndoa nyingi kubomoka, mimi nimeleta case study.
Mifano ipo mingi sana juu ya wanawake wasomi wa vyuoni kuwa wasumbufu kwenye ndoa ila wacha niweke kisa cha mtu naemjua kabisa wala si wa kihadithiwa.
Ni dada yangu huyu kabisa, aliitafuta sana ndoa na akaipata kimbebe kikawa kwenye maisha halisi ya ndoa.
Dada alikuwa kakariri sana maisha ya miss independent, haki sawa, ndoa za kitamthilia, n.k kwa bahati mbaya ama nzuri mme wake alikuwa hawezi vumilia haya mambo, kapata kazi hapa mjini na ni msomi ila kakulia sana maisha ya kijijini.
Dada alianza kuleta kiburi kumfulia mme wake nguo akashauri watafte house girl, mme wake akamwambia hata wakimleta house girl bado nguo zake haziwezi fuliwa na house girl, hilo ni jukumu la mwanamke wa ndoa.
Dada alianza kiburi kuamka asubuhi kumpashia mme wake maji, anamwambia mme wake apashe, walikuwa wanakorofishana sana.
Uvivu wa kupika, kuna muda anamwambia mme wake ale huko huko, yeye kachoka kupika.
Dada alikuwa bado hana kazi anashinda nyumbani, anaachiwa hela kila siku nje ya matumizi.
Vitimbwi vilikuwa ni vingi sana ila kwa ustaarabu wa kipekee wa yule bwana dada hakuwahi kupigwa hata kibao.
Baada ya miezi minne ya ndoa nikaanza kuona dada anapost status za kimafumbo za taasisi za kukemea uonevu kwenye ndoa, haki sawa kwenye ndoa, n.k.nikimpigia anadai anateswa na vitu vingine kibao, hio ilikuwa ni mbinu ya kupata tundu la kuchomoka / exit strategy, vitu vingi alikuwa anadanganya.
Alirudi nyumbani na mpaka sasa yupo nyumbani, mzazi hawakuwa na tatizo lolote kwa yeye kuridi na hata anavyoondoka chumba chake kilifungwa asilale mti mwengine.
vikao kama viwili hivi haonyeshi nia ya kurudi, nyumbani karudi na mtoto kuna house girl, anapikiwa, n.k.
Bwana yule anatoa laki 3 ya kumtunza mtoto kila mwezi lakini dada hakuwahi kusema hili, tulikuja gundua baadae, hapa nikaona kabisa sista alikuwa anataka atuvute upande wake tumuone mme wake hafai.
Pia napata stori pale nyumbani kwamba yule bwana akienda kumuona mtoto kuna mchezo mchafu unachezwa, dada anamwambia house girl ampeleke mtoto mtaa wa pili washinde huko hadi baba yake akiondoka, ni dada yangu lakini kwa kuwa nami pia ni baba, nikiona mwanaume mwenzangu anafanyiwa haya inaniuma.
Majukumu ya ndoa kwa mabinti wengi wa vyuoni ni tatizo, wanataka kuendelea na lifestyle za vyuoni ambazo haziwezi kuendana na maisha ya ndoa, wanataka haki sawa bila kutekeleza majukumu yao, wamekuwa brain washed na tamthilia, n.k.
Mifano ipo mingi sana juu ya wanawake wasomi wa vyuoni kuwa wasumbufu kwenye ndoa ila wacha niweke kisa cha mtu naemjua kabisa wala si wa kihadithiwa.
Ni dada yangu huyu kabisa, aliitafuta sana ndoa na akaipata kimbebe kikawa kwenye maisha halisi ya ndoa.
Dada alikuwa kakariri sana maisha ya miss independent, haki sawa, ndoa za kitamthilia, n.k kwa bahati mbaya ama nzuri mme wake alikuwa hawezi vumilia haya mambo, kapata kazi hapa mjini na ni msomi ila kakulia sana maisha ya kijijini.
Dada alianza kuleta kiburi kumfulia mme wake nguo akashauri watafte house girl, mme wake akamwambia hata wakimleta house girl bado nguo zake haziwezi fuliwa na house girl, hilo ni jukumu la mwanamke wa ndoa.
Dada alianza kiburi kuamka asubuhi kumpashia mme wake maji, anamwambia mme wake apashe, walikuwa wanakorofishana sana.
Uvivu wa kupika, kuna muda anamwambia mme wake ale huko huko, yeye kachoka kupika.
Dada alikuwa bado hana kazi anashinda nyumbani, anaachiwa hela kila siku nje ya matumizi.
Vitimbwi vilikuwa ni vingi sana ila kwa ustaarabu wa kipekee wa yule bwana dada hakuwahi kupigwa hata kibao.
Baada ya miezi minne ya ndoa nikaanza kuona dada anapost status za kimafumbo za taasisi za kukemea uonevu kwenye ndoa, haki sawa kwenye ndoa, n.k.nikimpigia anadai anateswa na vitu vingine kibao, hio ilikuwa ni mbinu ya kupata tundu la kuchomoka / exit strategy, vitu vingi alikuwa anadanganya.
Alirudi nyumbani na mpaka sasa yupo nyumbani, mzazi hawakuwa na tatizo lolote kwa yeye kuridi na hata anavyoondoka chumba chake kilifungwa asilale mti mwengine.
vikao kama viwili hivi haonyeshi nia ya kurudi, nyumbani karudi na mtoto kuna house girl, anapikiwa, n.k.
Bwana yule anatoa laki 3 ya kumtunza mtoto kila mwezi lakini dada hakuwahi kusema hili, tulikuja gundua baadae, hapa nikaona kabisa sista alikuwa anataka atuvute upande wake tumuone mme wake hafai.
Pia napata stori pale nyumbani kwamba yule bwana akienda kumuona mtoto kuna mchezo mchafu unachezwa, dada anamwambia house girl ampeleke mtoto mtaa wa pili washinde huko hadi baba yake akiondoka, ni dada yangu lakini kwa kuwa nami pia ni baba, nikiona mwanaume mwenzangu anafanyiwa haya inaniuma.
Majukumu ya ndoa kwa mabinti wengi wa vyuoni ni tatizo, wanataka kuendelea na lifestyle za vyuoni ambazo haziwezi kuendana na maisha ya ndoa, wanataka haki sawa bila kutekeleza majukumu yao, wamekuwa brain washed na tamthilia, n.k.