Ushuhuda: Mungu amekuwa Mwema kwangu

Ushuhuda: Mungu amekuwa Mwema kwangu

Mtume paulo anaandika hivi: "maana kabla ya sheria dhambi ilikuwamo ulimwenguni, lakini dhambi haihesabiwi isipokuwapo sheria; [War5:13].

Andiko hili limechanganya sana wanaojiita wakristo wengi kudhani kuwa uwepo wa dhambi hauhitaji sheria na kwamba hata sasa sheria haihitajiki kufafanua dhambi ni nini? lakini hili ni kweli?

Ni kweli kwamba Mungu kama mtawala wa dunia yote hana sheria za kuongoza utawala wake???

Paulo anaposema kwamba kabla ya Sheria dhambi ilikuwepo ulimwenguni, hapa alikuwa akimaanisja kuwa kabla Sheria za Mungu kuandikwa katika vibao vya mawe na katika magombo ya Musa pale mlimani sinai, dhambi ilikuwepo.

Kwa wanadamu sheria huanza kutambulika na kuwa na mamlaka baada ya kuandikwa. Na hili ni kweli. dhambi ilikuwepo hata kabla ya tukio la mlima sinai la Mungu kuandika Amri zake katika mbao mbili za Mawe.

Lakini paulo yupo wazi kuwa dhambi haiwezi kuhesabiwa pasipo sheria. Maana yake ni kwamba kila penye dhambi, maana yake kuna sheria fulani ya Mungu imevunjwa. Haiwezekani dhambi kuwepo bila sheria kuvunjwa. Kwa hiyo ni wazi kwamba Sheria za Mungu zilikuwepo hata kabla ya tukio la Mlima sinai. Paulo anaposema kuwa dhambi ilikuwepo kabla ya sheria, hana maana kuwa dhambi inaweza kuwepo bila sheria, ila anamaanisha kwamba dhambi ilikuwepo kabla ya Mungu kuziandika rasmi amri zake katika mbao za mawe pale mlimani sinai.

Hivyo ni dhahiri kuwa Amri za Mungu zilikuwepo hata kabla ya tukio la Mlima sinai.

Hapo Mwanzo Mungu alipomuumba Mwanadamu aliiandika sheria yake katika dhamiri zao na mioyo yao[War2:15]. Hata baada ya Uasi, Sheria za Mungu zilibakia ktk Mioyo ya wanadamu. Hata wanadamu waasi wanajua kabisa kanuni za haki na kanuni ziziso za haki. Haihitaji kufundishwa na mtu kuwa ukichukua mke wa mwenzako, ama ukimwibia mwenzako, ama ukimtukana mwenzako ni jambo baya. Sheria ya Mungu ya Upendo imo mioyoni mwa wanadamu wote.

Ni hali ya uasi ambayo Mwanadamu amerithi baada ya uasi ndo inamsukuma mwanadamu kuichukia sheria ya Mungu na kuivunja. Lakini Katika moyo wa kila Mmoja Mungu amejiachia ushuhuda wa sheria zake.

Amri ya Sabato ilianzishwa na Mungu Mwenyewe tangu Uumbaji, na hivyo kuwa Amri iliyozeeka na ya zamani sana kama Umri wa dunia. Sabato iliwekwa na Mungu kuwakumbushia wanadamu kuwa waliumbwa na Mungu na hivyo wanawajibika kwake katika kumwabudu na kumtii. Msingi wa Ibada uliwekwa mapema sana pale Mungu alipoianzisha sabato. Taz Mwa2:1-3.

Amri zote Kumi, ambazo ni mafafanuzi ya Sheria ya Mungu ya Upendo zilikuwepo tangu Uumbaji. Baadhi ya wakristo wanawaza kwamba kwa sababu Amri kumi ziliandikwa katika Mbao mbili za Mawe pale mlimani sinai, basi Amri hizo ni torati ambayo haiwahusu wakristo kabisa. wanawaza na kufikiri kuwa kwa sababu Agano la kale liliundwa kwa misingi ya utii wa Amri kumi, pamoja na Sheria zile zingine na maagizo yake na hukumu zake, basi kuondolewa kwa agano la kale kunafagilia mbali Amri kumi na Sabato. Huu ni udanganyifu Mkuu.

Na udanganyifu huu kwa sababu unalenga sabato tu, unakuja udanganyifu mwingine kuwa injili imezitaja sheria zingine zote tisa katika zile kumi kasoro sabato tu,na hivyo tuna uhalali wa kuzishika sheria zingine zote tisa kasoro sabato!!! Huu ni udanganyifu wa makusudi unaolenga chuki dhidi ya amri moja tu ya Mungu katika zile kumi.

Bwana wetu Yesu Kristo akiongelea juu ya Umilele wa Amri za Mungu, na kuwaonya watu dhidi ya kuzitangua, aliweka bayana hivi: "Lakini ni vyepesi zaidi mbingu na nchi vitoweke, kuliko itanguke nukta moja ya torati. [Luka16:16].

Kama vile mbinguna nchi vitakavyoendelea kudumu, daima vitaendelea kushuhudia kuwa Sheria za Mungu ni za Milele. Amri za Mungu ambazo zilikuwepo kabla ya Agano la kale la mlima sinai; husimama kwa zenyewe hata bila Agano la kale.

Agano jipya halikuondoa Amri za Mungu bali linazirudisha Amri za Mungu katika sehemu yake ya hawali yaani mioyoni mwa wanadamu, na kuwawezesha wanadamu kuzitii Amri zake.
mstari wa mwisho tu hapo unakutosha. maana ya Mungu kuweka sheria mioyoni mwetu, au kuweka amri mioyoni mwetu unaelewa maana yake? ni pale Roho Mtakatifu anapoingia ndani mwetu na kutuongoza kututia kwenye kweli yote. sio kukariri vifungu vya biblia kimwili, kwa kufanya hivyo kimwili haikusaidii chochote zaidi ya kuwa mwanahistoria wa biblia. hiyo Biblia uliyonayo haitoshi kuandika mambo yote ambayo Mungu aliagiza, yapo mengine Yesu mwenyewe alisema wanafunzi wake wasubiri Yerusalem hadi atakapokuja huyo Roho, na huyo Roho atawatia kwenye kweli yote. Roho Mtakatifu anatuelekeza kutotenda dhambi hata zile ambazo hazijaandikwa kwenye hizo sheria zetu au Biblia kwa ujumla. huwezi kumwona Mungu ukienda kimwili kama ninyi wasababo, mnatakiwa kwanza muokoke kwa kumkiri Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

sijawahi kuona msabato hata mmoja amejara Roho Mtakatifu, na ninajua mafundisho yetu yanaelekeza kwamba sio wote wanatakiwa kujazwa. hii ndio sababu mnaishi kwa kukariri vifungu na kutumia nguvu kushinda dhambi, kwa nguvu za mwili huwezi kushinda dhambi ila kwa nguvu za Roho, na huwezi kupata Roho Mtakatifu hadi uokoke, na awaye yote asiyekuwa na huyo Roho wa Kristo huyo sio wake. ninyi wasababu sio wakristo kwasababu hamna Roho Mtakatifu na mnamkataa (hamtaki kujazwa). Roho Mtakatifu ni muhimu kwa ajili ya kututia kwenye kweli yote zaidi ya hizo amri kumi, na pia anatusaidia kuomba kwasababu sisi ni dhaifu tukienda kuomba kwa nguvu ya mwili tunaomba kwa tamaa zetu na hatujui kuomba ipasavyo, lakini yeye aomba ndani yetu akilia ABBA kwa kuugua kusikoweza kutamkwa....sasa ninyi kama hamna Roho, nani huwa anawasaidia kuomba kwa kuugua kusikoweza kutamkwa? no wonder hamna uwezo hata wa kukemea pepo na vibwengo. you are not different from the catholics and other unbelievers.
 
Usifanye dhambi au upuuzi Kama kufanya Ngono au kufanya uzinzi na hujaoa au kuolewa ukasema utatubu huu ni uhasi Mbele za Mungu na shetani ndo Binadamu Mwenyewe


Nimekuwa hapa madhabauni najionea uchafu wa walokole kuzini huku lawama wakimpa shetani this is not good


Swala la usafi wa Mwili
Roho na Matendo lipo ndani ya huwezo wa mwanadamu na sio SHETANI Wala Mungu Cha kuomba ni kuomba hekima ya Mungu iyawatale maisha yako.
wazinzi sio walokole (kwa dini) tu, wazinzi ni watu wote wa dini zote, wale tu wanaomwogopa Mungu na walioyatoa maisha yao ndio hawazini. kwa taarifa yako, kila mwanadamu ni mdhaifu, na hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kushinda dhambi iwe ya uzinzi au yeyote bila nguvu za Mungu. hii ndio maana Yesu alikuja ili kutupatia uwezo wa kushinda dhambi. ninyi mnakariri vifungu mkiamini kwa uwezo wenu mnaweza kupambana na dhambi, Yesu alikuja kufanya nini sasa? kama mlikuwa na uwezo kushinda dhambi kwa nguvu zenu, Yesu alikufa kwa ajili ya nini? kama ni kuzini, hata ukishinda kwa nguvu za mwili na sheria za kukariri kama ninyi kama bado huna nguvu za Mungu kukusaidia kushinda roho ya uzinzi bado tu utawaza uzinzi na kuchafua hekalu la Mungu na bado tu utazini kwa kutamani. pia, kama umeokoka ni kweli sio sababu kwamba unaweza tu kufanya dhambi/uzinzi kwasababu neema ipo, lakini Neno la Mungu linasema, kama tukitenda dhambi tunaye mwombezi Yesu Kristo, huyo ndiye kafara letu. shinda ni kwenu ambao mnaenenda kwa agano la Musa na hamjampokea Yesu na kuokoka, hamna mwombezi kwahiyo mnabeba mafurushi yenu ninyi wenyewe, na mtashindwa tu. wewe ni shahidi, ni msabato gani aliwahi kushinda dhambi kwa nguvu zake? tunaishi nao na tunafanya nao kazi...wengi wanaikimbia tu dhambi ya uzinzi au zile amri kumi, ila ni wachawi vizuri tu, ni waongo, na wanazini sana, sema hatuhukumiani, cha msingi tu yakabidhi maisha yako kwa Yesu awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako, uondoke kwenye usabato kwasababu huko hamuamini hilo na ukibaki huko hautaweza, ili upate mwokozi na mwombezi nawe utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu ili uongozwe na Mungu kushinda dhambi, sio kwa uwezo wako wa kibinadamu.
 
Nakushangaa unavyosema Ninachosali Mungu hakitambui ,kisa umejaa chuki dhidi ya SDA , pole Sana ,Mungu atakusaidia atakutoa huko

Chuki yote Ni sababu ya Amri ya 4 inayosema IKUMBUKE SIKU YA SABATO UITAKASE , Wala sio kingine


Unasema nije huko ,Ni wapi ? Kwenye haya madhehebu yenu yaliyojaa utapeli , haya mnayouziana maji , mafuta, udongo, keki ,na Upagani mwingine


Wakristo kwa mujibu wako unawaona Ni wale wanaobadili Amri za Mungu ,kuabudu na kuchonga masanamu, kula kenge,nguruwe, mende ,kuuza Mafuta, udongo,keki,leso kwa mgongo vina upako ,ibada za kipagani ,x mass paganism,Easter paganism,Dominica paganism, n.k

Watu Kama nyie mlikuwepo hata enzi za Yesu ,

Mathayo 7:7

6Akawaambia, Isaya alitabiri vema juu yenu ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa,

Watu hawa huniheshimu kwa midomo

Ila mioyo yao iko mbali nami;

7Nao waniabudu bure,

Wakifundisha mafundisho

Yaliyo maagizo ya wanadamu,

8Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu. 9Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu. 10



ILA YESU MUANZILISHI WA UKRISTO ANASEMA

“Msidhani [wengi mno leo mnadhani] ya kuwa nalikuja kuitangua torati [Sheria] au manabii;” akasema, “sikuja kutangua [kuifutilia mbali], bali kutimiliza [kuitekeleza]. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka [bado zipo], yodi moja [,] wala nukta moja [.] HAITAONDOKA hata yote yatimie [yaani, mpaka hapo mbingu na nchi zitakapoondoka].

Basi [kwa hiyo] mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo [Yak.2:10-12], na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa [mnyonge hataingia – Ufu.21:27] katika ufalme wa mbinguni; bali mtu ATAKAYEZITENDA [Amri Kumi] NA KUZIFUNDISHA, huyo ataitwa mkubwa [mtawala/mfalme – Ufu.20:4; Dan. 7:27] katika ufalme wa mbinguni.” Mathayo 5:17-19.
Yesu ni BWana wa sabato, na Biblia inakataza kuabudu siku, mwabuduni yeye aliyewafia msalabani. nakuambieni, sina chuki na wasabato, ila nisipowaambia ukweli nitadaiwa. sijasema uende kwenye makanisa ya kitapeli, utakuwa haujafanya kitu, kwasababu ukweli ni kwamba, hapo mlipo hamna tofauti yeyote na wauza mafuta kama mwamposa na waongo kama GEORDEVIE na wengine wanaojifanya manabii. hii ni kwasababu hao wanamtumikia shetani, na ninyi kwa upande wenu mpo kwenye kifungo cha shetani cha kuabudu siku na kukataa nguvu za Mungu. mnataabisha miili yenu kwa deni ambalo Yesu alishalilipa lote, mnapoteza muda.
 
Huyu Mungu mwache aitwe Mungu maana Kuna kipindi anakufanyia mambo mema mpaka unajiuliza moyoni hivi wewe mungu umewezaje kunifanyia hivi. Mwezi huu ndo nimegundua Mungu ni master kwa aliyonifanyia
 
Habari za Jioni ndugu zangu, Amani ya Bwana iwe nanyi ,

Nisipoteze muda niseme hakika Mungu amenitendea Wema na muujiza katika maisha yangu ,sio kwamba Ni mwema au Nini ,naweza kusema katika waovu ,wenye dhambi wa kutupwa nami Ni mmoja wapo ,ila huyu Mungu usipomuelewa utajihisi amekukataa kumbe sivyo, ukiuelewa upendo wa AGAPE utajua Nini naongea.

Mimi Ni muadventista Msabato , sio wa kuzaliwa .(nitakuja kueleza siku Moja nilivyotoka katika Uislamu na kuingia katika Ukristo )

Mara kadhaa nilihangaika kupata ajira ,nilijiunga na Ajira portal na kweli niliitwa interview nyingi lakini zilikuwa zinaangukia Jumamos ambayo Ni siku yangu ya ibada ,Hali hii ilinipa tabu Sana , kusema kweli awali nilienda kufanya zile interview Hadi jumamos , sikufanikiwa japo nilikuwa naingia Hadi Oral interview, siku Moja nilihisi hatia baada yakuwa nasikiliza mahubiri na kusoma Maandiko,na historia nikiona mashujaa wa imani walivyojitoa kuacha ya dunia na kumtetea Mungu, niliazimia sitafanya Tena Interview jumamos kipindi hicho Sina ajira ,Nina mke na ana mimba , kula yangu ya tabu Sana, nilimwambia Mungu naomba Hadi mwezi ujao nipate ajira , Mwanamke wangu nyumbani alikuwa akinisimanga ,akininyanyapaa ,yote Ni sababu Sina ajira Sina kipato Kodi ya nyumba Sina na sijui nalipa Nini , niliendelea kushikilia msimamo sitafanya Tena Interview jumamos na rasmi naitelekeza akaunt ya ajira portal .

Kwakweli sijui hata nilikuwa nakulaje ,naishije ,maana sikuwahi kulala njaa ,hata mwenye nyumba Kodi yake ilipofika hakuwahi kuja kunidai had nikasahau nadaiwa Bei gan maana nilikuwa nimelimbikiza nahisi hata miezi 6-8, Siku Moja mwenye nyumba alikuja akasema hanidai Kodi Bali Kuna miezi Kama miwili mbele yeye ndiye namdai ,nilishangaa Sana , kipindi hicho nilikuwa napata interview makapuni mengi tu lakini tulikuwa tunashindwa kwenye Swala la IBADA , .Kuna wakati nilikuta kwenye Emali yangu meseji kutoka bodi yangu ya uhandisi ,nitume detail zangu na namba ya benki, kwakweli nilifanya vile , haikupita wiki nikawekewa laki 9 ,bila kufanya kazi yoyote ,na ndio Kipind ambacho ile miezi miwili ya Kodi niliyoambiwa inaishia ( japo binafsi kwakumbukumbu zangu nilikuwa nadaiwa miezi 6-8),ile laki 9 ilinisaidia Sana kipindi hicho.Nyingine nilianzisha biashara ya matunda lakini haikufanikiwa (ukisikia mtu anakwambia jiajiri wewe msikilize tu)

Lakini bado swala la ajira lililuwa gumu Sana hasa upande wa IBADA ,Kuhusu interview huwa naiitwa kila wiki hata Mara 2 ,Awali nikiwa nimehitimu nilitafuta ajira nikapata katika kampuni ya Uzalishaji mikaa ya briquette huko kusini, nilikutana na meneja mtata Sana, hofu yake kubwa ilikuwa nimekuja kuchukua cheo chake ,alihangaika kwa waganga kunifanyia figisu lakini alishindwa kabisa ,mwisho niliamua kuacha kazi, sio sababu yake ila sikupenda mazingira ,binafsi nakanuni Moja katika maisha , huwa simkimbii mchawi popote pale iwe kwenye kazi au nyumba ,maana kumkimbia mchawi Ni Kumdhalilisha Mungu ambaye tunajinasibu ana nguvu kuliko upande wao .,

Baada ya kurudi nyumbani ,nilisemwa na majirani na jamaa wanaonizunguka maana wanaona unaamka asubuhi had Jioni unarandaranda tu ,nikamwambia Mungu nataka mwezi fulani usipite nipate hata ajira kwanza iniweke sawa , Nilikuwa na rafiki yangu tumehitimu wote chuo darasa Moja , alikuwa hamuamini Sana Mungu, nayeye alihangaika Sana kuhusu maisha na Ajira , kipindi nipo kusini nilimtumia tangazo la ajira kampuni Moja kubwa hapa TZ ya Gesi , aliomba ,niliporudi Dar , tukawa wote majobless , lakini nilikuwa nae karibu kuhusu Mungu anavyofanya kazi, tukisoma Sana Maandiko, (huyu ana stori ndefu jinsi Mungu alivyomtendea,) ,alikata Sana tamaa alifikia hatua hata ya kujiua ,siku Moja akiwa amejiandaa amepaki mizigo yake na vyeti akijiandaa kurudi kwao Kaskazini mwa TZ , asubuhi anapigiwa simu kutoka ile kampuni ya Gesi aende kwa interview , alijiandaa tukiwa wote ,tuliomba , nami nilimwombea nilimwambia Mungu naomba apate hii kazi ili UTUKUFU WAKO UDHIHIRIKE

Kwakweli alifanya interview 3 na zote alitoboa na kupata kazi katika hiyo kampuni ya Gesi, Imani yake kwa Mungu iliongezeka Sana, hirizi na mafuta ya manabii ,maji yote nilikuta amezichoma .

Kwangu hali haikuwa nzuri niliendelea kuwa Jobless ,maisha ya kuungaunga ,biashara ya matunda ilikwama kabisa , .Nikamwambia Mungu Sasa nahitaji kazi ,maana maadui zangu wananisema vibaya na kusema ona anamtegemea Mungu mbona hamsaidii Sasa, binafsi najua hatua zote hizi za maisha Ni shule ,Maana hata Waisrael walikaa jangwani miaka 40 ili kufundishwa .

Siku moja nikaitwa interview katika kampuni Moja ya Tajiri mkubwa hapa TZ , nikafanya interview nikapita ,kosa nililofanya nilisahau kuweka masharti ya ibada wakati nasaini mkataba , Nilipoanza kazi nikawa nasumbuliwa Sana nije jumamos , Bosi akaniita nikamwambia siwezi kuja Jumamosi hata kazi nipo tayari kuacha , Bosi akachukua peni akapiga hesabu pesa ambayo nitakatwa kwa mwaka mzima kwasababu ya kutokwenda jumamos tu, akanikazia macho akasema upo tayari kupoteza kiasi hichi Cha Pesa kisa kusali tu? Je ukienda kanisani unapata Nini ? Mwisho akasema fine sikufukuzi kaz maana umeshasaini mkataba ila Tutakukata pesa .

Kuanzia hapo Bosi akaanza figisu , Pesa za bonus, hanipi anazuia, pesa za communication, n.k zote anazuia ,wenzangu wanapewa Mimi natengwa, mshahara ukija nimekatwa pakubwa Sana , .Wafanyakazi wenzangu na watu wakaribu wakasema fanya uje kazini jumamos tu utakatwa pesa na mshahara unabaki kidogo .,hata mke wangu pia akasema Nenda kazini Jumamosi .

Nikawaambia Sitaenda , Hali ikawa mbaya Sana, Bosi akazidi kunikazia kamba , Nikamuuliza Mungu Nimekutetea kwa watu na wewe nijibu Sasa , Nahitaji unijibu , Nikaweka ratiba nikawa nasoma Sana Zaburi ya 40 .,na maombi na kufunga , Haikupita muda nikapokea simu kutoka mgodi mmoja hapa Tz, nikaandaliwa interview online ,nikafanya ,nikaulizwa hapo unalipwa Bei gani nikajibu , lakini nikasema ngoja nimuulize Mungu je amenijibu yeye ,nikasema Kama wataniruhusu ibada jumamos Basi hiyo kazi imetoka kwa Mungu, kweli wakasema Hilo halina shida , nikatumiwa nauli na hela ya kula , nikafika nikagharamiwa accommodation ya Hali ya juu,

Nikaambiwa unataka tukulipe Bei gani nikataja mshahara mzuri tu nikaambiwa tunakuongeza zaidi, nikaambiwa tunataka uwe meneja hapa na tutakupa nyumba kubwa hapa .

Nikasema hakika Mungu umenijibu

NB: MIMI NI MDHAMBI SANA , ILA MUNGU AMEKUWA MWEMA KWANGU , NINAPOMKOSEA NATUBU KWA KUTAJA DHAMBI JINA LAKE BILA KUPEPESA MACHO ILI ANIREHEMU

Nimejifunza hii kutoka kwa Daudi ,nilijiuliza kwanini MUNGU alimpenda Sana Daudi kuliko sauli ?

Ukisoma Maandiko utagundua Kati ya Sauli na Daudi, Daudi ndiye kavurunda Sana , ameua ,amezini, amenyang'anya wake za watu, lakini alikuwa mtu wa toba ya kweli ,imefikia hatua Daudi ana mji /mtaa mbinguni

Unaitwa MJI WA SAYUNI
Wasabato mna mawenge Sana usikute kuandika kite hukuni wishes tu na sio reality
 
Yesu ni BWana wa sabato, na Biblia inakataza kuabudu siku, mwabuduni yeye aliyewafia msalabani. nakuambieni, sina chuki na wasabato, ila nisipowaambia ukweli nitadaiwa. sijasema uende kwenye makanisa ya kitapeli, utakuwa haujafanya kitu, kwasababu ukweli ni kwamba, hapo mlipo hamna tofauti yeyote na wauza mafuta kama mwamposa na waongo kama GEORDEVIE na wengine wanaojifanya manabii. hii ni kwasababu hao wanamtumikia shetani, na ninyi kwa upande wenu mpo kwenye kifungo cha shetani cha kuabudu siku na kukataa nguvu za Mungu. mnataabisha miili yenu kwa deni ambalo Yesu alishalilipa lote, mnapoteza muda.
Maandiko yanasema hivi: " Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki. [War10:4].

Fungu hili halimaanishi kwamba Yesu ameiondoa sheria na kuifanya ifikie mwisho, Hapana. Fungu hili linamaanisha kuwa Yesu anayafanya madai ya sheria yafike mwisho. Sheria hudai kuwa mkosaji ni mwenye dhambi, lakini Yesu husamehe dhambi. Dai la sheria kwamba mtu ni mwenye dhambi hufika mwisho pale mdhambi anaposamehewa.

Sheria hufunua haki, wema, na utakatifu wa Mungu[War7:12], Lakini Sheria haina uwezo wa kumpa mkosaji haki kamilifu ya Mungu. Lakini Yesu sii tu anao uwezo wa kuondoa dhambi, bali pia anao uwezo wakumvika mdhambi kwa haki kamilifu, hata mdhambi akahesabiwa kuwa ameitii sheria kikamilifu, na kwamba hajawahi kukosa tangu azaliwe. Mdhambi aliyetubu anahesabiwa hana hatia na kuhesabiwa kuwa mtakatifu kama malaika wake watakatifu walioko mbinguni.

Sheria Hutoa hukumu ya kifo kwa wenye dhambi, lakini Yesu alikufa pale msalabani, ili kubeba adhabu ya mwanadamu, ili kwa namna hiyo mwanadamu afunguliwe toka kwenye adhabu ya kifo inayotangazwa na sheria.

Sheria Inataka wanadamu wote waitii na kuishika kikamilifu, lakini haina uwezo wa kuwafanya wanadamu waitii. Yesu anatoa uwezo wa kuwafanya wanadamu wote wanaomwamini waweze kutii sheria za Mungu. Wakristo huyaweza mambo yote katika Kristo anayewatia nguvu[Fil4:13].

Kila hoja inayotolewa na sheria juu ya mdhambi, inatimilika katika Yesu na kufikia Mwisho wake. Lakini Mwisho wa madai ya sheria hakuna maana kuwa ndio mwisho wa sheria Yenyewe. Mtume paulo anasema hivi: "Basi, je! Twaibatilisha sheria kwa imani hiyo? Hasha! Kinyume cha hayo twaithibitisha sheria. [War3:31].

Wokovu kwa imani hakuibatilishi sheria na kuiondoa, bali kunaanzisha msingi wake hasa kama sheria za haki. Wokovu upo kwa sababu sheria zimevunjwa na mwanadamu. Kifo cha Yesu mwenyewe ni ushahidi tosha kuwa sheria ipo na kwamba dhambi ni uasi wa sheria na kwamba mshahara wa dhambi ni mauti.
 
Yesu ni BWana wa sabato, na Biblia inakataza kuabudu siku, mwabuduni yeye aliyewafia msalabani. nakuambieni, sina chuki na wasabato, ila nisipowaambia ukweli nitadaiwa. sijasema uende kwenye makanisa ya kitapeli, utakuwa haujafanya kitu, kwasababu ukweli ni kwamba, hapo mlipo hamna tofauti yeyote na wauza mafuta kama mwamposa na waongo kama GEORDEVIE na wengine wanaojifanya manabii. hii ni kwasababu hao wanamtumikia shetani, na ninyi kwa upande wenu mpo kwenye kifungo cha shetani cha kuabudu siku na kukataa nguvu za Mungu. mnataabisha miili yenu kwa deni ambalo Yesu alishalilipa lote, mnapoteza muda.
Unapotea sababu huyajui maandiko


Je, kuna siku ambayo Mungu anaiita kuwa ni yake?

“Nalikuwa katika Roho, Siku ya Bwana.” Ufu. 1:10. “Kama ukigeuza mguu wako usiihalifu Sabato, usifanye anasa yako siku ya utakatifu wangu; ukiita Sabato siku ya furaha, na Siku Takatifu ya Bwana yenye heshima; ukiitukuza, kwa kutokuzifanya njia zako mwenyewe, wala kuyatafuta yakupendezayo, wala kusema maneno yako mwenyewe, ndipo utakapojifurahisha katika BWANA.” Isa. 58:13,14.

Je, Yesu Kristo ni Bwana wa siku ipi?

“Kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.” Mt. 12:8.

Jambo hili ni wazi – Yesu mwenyewe anatamka wazi kuwa yeye ni Bwana wa Sabato. Siku zote amezifanya yeye, lakini siku ya saba ameifanya kuwa yake.


Kuna sababu yo yote iliyomfanya Mungu aichague Siku ya Saba na siyo zile nyingine?

“Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.” Kut. 20:11. “Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya. Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.” Mwa. 2:2,3. “Tena naliwapa Sabato zangu, ziwe ishara kati ya mimi na wao, wapate kujua ya kuwa mimi, BWANA, ndimi niwatakasaye.” “Zitakaseni Sabato zangu; zitakuwa ishara kati ya mimi na ninyi, mpate kujua ya kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.” Eze. 20:12,20.

Siku ya saba ni kumbukumbu ya tukio maalum. Kuzaliwa kwa dunia na vyote vilivyomo. Mungu aliiweka ili tuendelee kumkumbuka yeye kama Muumbaji. Na kuwa ndiye anayetutakasa.

Kama Yesu ndiye Bwana wa Sabato, Yeye mwenyewe alikuwa na desturi gani kila siku ya Sabato?

“Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; na siku ya Sabato akaingia katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake, akasimama ili asome.” Luka 4:16.

Biblia iko wazi hapa! Ilikuwa ni desturi ya Yesu kwenda kanisani kila siku ya Sabato. Desturi siyo tukio la mara moja au mbili tu.
 
mstari wa mwisho tu hapo unakutosha. maana ya Mungu kuweka sheria mioyoni mwetu, au kuweka amri mioyoni mwetu unaelewa maana yake? ni pale Roho Mtakatifu anapoingia ndani mwetu na kutuongoza kututia kwenye kweli yote. sio kukariri vifungu vya biblia kimwili, kwa kufanya hivyo kimwili haikusaidii chochote zaidi ya kuwa mwanahistoria wa biblia. hiyo Biblia uliyonayo haitoshi kuandika mambo yote ambayo Mungu aliagiza, yapo mengine Yesu mwenyewe alisema wanafunzi wake wasubiri Yerusalem hadi atakapokuja huyo Roho, na huyo Roho atawatia kwenye kweli yote. Roho Mtakatifu anatuelekeza kutotenda dhambi hata zile ambazo hazijaandikwa kwenye hizo sheria zetu au Biblia kwa ujumla. huwezi kumwona Mungu ukienda kimwili kama ninyi wasababo, mnatakiwa kwanza muokoke kwa kumkiri Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

sijawahi kuona msabato hata mmoja amejara Roho Mtakatifu, na ninajua mafundisho yetu yanaelekeza kwamba sio wote wanatakiwa kujazwa. hii ndio sababu mnaishi kwa kukariri vifungu na kutumia nguvu kushinda dhambi, kwa nguvu za mwili huwezi kushinda dhambi ila kwa nguvu za Roho, na huwezi kupata Roho Mtakatifu hadi uokoke, na awaye yote asiyekuwa na huyo Roho wa Kristo huyo sio wake. ninyi wasababu sio wakristo kwasababu hamna Roho Mtakatifu na mnamkataa (hamtaki kujazwa). Roho Mtakatifu ni muhimu kwa ajili ya kututia kwenye kweli yote zaidi ya hizo amri kumi, na pia anatusaidia kuomba kwasababu sisi ni dhaifu tukienda kuomba kwa nguvu ya mwili tunaomba kwa tamaa zetu na hatujui kuomba ipasavyo, lakini yeye aomba ndani yetu akilia ABBA kwa kuugua kusikoweza kutamkwa....sasa ninyi kama hamna Roho, nani huwa anawasaidia kuomba kwa kuugua kusikoweza kutamkwa? no wonder hamna uwezo hata wa kukemea pepo na vibwengo. you are not different from the catholics and other unbelievers.

sijawahi kuona msabato hata mmoja amejara Roho Mtakatifu, na ninajua mafundisho yetu yanaelekeza kwamba sio wote wanatakiwa kujazwa. hii ndio sababu mnaishi kwa kukariri vifungu na kutumia nguvu kushinda dhambi, kwa nguvu za mwili huwezi kushinda dhambi ila kwa nguvu za Roho, na huwezi kupata Roho Mtakatifu hadi uokoke, na awaye yote asiyekuwa na huyo Roho wa Kristo huyo sio wake. ninyi wasababu sio wakristo kwasababu hamna Roho Mtakatifu na mnamkataa (hamtaki kujazwa). .

Bado inaonesha maandiko huyachunguzi, pia Hujui chochote kuhusu ROHO MTAKATIFU


Na umeshadanganywa kuropoka ule ujinga ndio kuwa na Roho mtakatifu

Matendo 6:5-8, KJV. Stefano alikuwa ame“jaa imani na Roho Mtakatifu”; “akijaa imani na uwezo.” Alikuwa “akifanya maajabu na ishara [miujiza],”

lakini yeye, kulingana na kumbukumbu inavyosema, alikuwa hana karama ya lugha, zaidi ya kuwa na karama ile ya kuitumia vizuri kwa utukufu wa Mungu lugha ile aliyozaliwa nayo.


Matendo 10:38. “Habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu.” Alitenda mema kila mahali, akiwaponya hata wale waliokuwa
wamepagawa na pepo, lakini alizungumza lugha ile tu aliyozaliwa nayo ya Kiaramu, kwa kadiri sisi tunavyojua. Marko 16:15-20.


Wanafunzi wake “wakahubiri kote-kote,” na mara nyingi walibishana nao na kuwapinga. Ndipo Mungu akawatumia ili wapate kuwagusa watu kwa uthibitisho wa “ishara zilizofuatana nao.”

Hakuna kumbukumbu zo zote zinazotaja kwamba walinena kwa lugha.”
 
sijawahi kuona msabato hata mmoja amejara Roho Mtakatifu, na ninajua mafundisho yetu yanaelekeza kwamba sio wote wanatakiwa kujazwa. hii ndio sababu mnaishi kwa kukariri vifungu na kutumia nguvu kushinda dhambi, kwa nguvu za mwili huwezi kushinda dhambi ila kwa nguvu za Roho, na huwezi kupata Roho Mtakatifu hadi uokoke, na awaye yote asiyekuwa na huyo Roho wa Kristo huyo sio wake. ninyi wasababu sio wakristo kwasababu hamna Roho Mtakatifu na mnamkataa (hamtaki kujazwa). sasa ninyi kama hamna Roho, nani huwa anawasaidia kuomba kwa kuugua kusikoweza kutamkwa? no wonder hamna uwezo hata wa kukemea pepo na vibwengo. you are not different from the catholics and other unbelievers.

Naona unalalamika tu ila hutaji ilo Kanisa ni lipi unalodai mna Mungu ,na sisi hatuna ,unalalamika kwanini natoa Maandiko


Halafu Nani kakudanganya ili uonekane una Roho Mtakatifu lazima uongee zile Lugha zenu za ajabu


Gwajima, Geo Devi, Mackenzie, Mashimo, nabii Tito , na matapeli wote wanaziongea ,

Yaani kwako wanaoongea hizo Lugha ndio Wana roho mtakatifu


Ok


Mimi namsikiliza Yesu sio wewe, naomba nitajie wapi hao wameokoka taja Jina la Dhehebu ,au Kanisa ,nitakuwekea List ya Upagani na mwanzilishi wa Hilo kundi



YESU MUANZILISHI WA UKRISTO ANASEMA

“Msidhani [wengi mno leo mnadhani] ya kuwa nalikuja kuitangua torati [Sheria] au manabii;” akasema, “sikuja kutangua [kuifutilia mbali], bali kutimiliza [kuitekeleza]. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka [bado zipo], yodi moja [,] wala nukta moja [.] HAITAONDOKA hata yote yatimie [yaani, mpaka hapo mbingu na nchi zitakapoondoka].

Basi [kwa hiyo] mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo [Yak.2:10-12], na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa [mnyonge hataingia – Ufu.21:27] katika ufalme wa mbinguni; bali mtu ATAKAYEZITENDA [Amri Kumi] NA KUZIFUNDISHA, huyo ataitwa mkubwa [mtawala/mfalme – Ufu.20:4; Dan. 7:27] katika ufalme wa mbinguni.” Mathayo 5:17-19.
 
....sasa ninyi kama hamna Roho, nani huwa anawasaidia kuomba kwa kuugua kusikoweza kutamkwa? no wonder hamna uwezo hata wa kukemea pepo na vibwengo. you are not different from the catholics and other unbelievers.

Soma hii huenda ukapata akili zaidi ,maana mmekaririshwa kupayukapayuka ndio roho Mtakatifu,



 
Kwahiyo uko hapo unaamini kabisa kutokufanya kazi jumamosi ndio kumekufanya ufanikiwe? Nyie watoto wa Ellen buana...


Any ways... Hongera
 
Hakika Mungu wetu ni mwema sana.Nikupongeze kwa kuja hapa jukwaani kumpa Mungu utukufu kwa mema aliyokutendea pasipo mastahili yako.
 
Kwahiyo uko hapo unaamini kabisa kutokufanya kazi jumamosi ndio kumekufanya ufanikiwe? Nyie watoto wa Ellen buana...


Any ways... Hongera
BIBLIA KISWAHILI CHA KISASA


ISAYA 58

13“Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato,

ukaacha shughuli zako siku yangu hiyo takatifu;

kama ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha,

ukaiheshimu siku hiyo takatifu ya Mwenyezi-Mungu,

ukaacha na shughuli zako na kupiga domo,

14utapata furaha yako kwangu mimi Mwenyezi-Mungu,

nitakupatia ushindi katika kila pingamizi nchini,

nitakulisha mali ya Yakobo, babu yako.

Mimi, Mwenyezi-Mungu, nimesema.”
 
Habari za Jioni ndugu zangu, Amani ya Bwana iwe nanyi ,

Nisipoteze muda niseme hakika Mungu amenitendea Wema na muujiza katika maisha yangu ,sio kwamba Ni mwema au Nini ,naweza kusema katika waovu ,wenye dhambi wa kutupwa nami Ni mmoja wapo ,ila huyu Mungu usipomuelewa utajihisi amekukataa kumbe sivyo, ukiuelewa upendo wa AGAPE utajua Nini naongea.

Mimi Ni muadventista Msabato , sio wa kuzaliwa .(nitakuja kueleza siku Moja nilivyotoka katika Uislamu na kuingia katika Ukristo )

Mara kadhaa nilihangaika kupata ajira ,nilijiunga na Ajira portal na kweli niliitwa interview nyingi lakini zilikuwa zinaangukia Jumamos ambayo Ni siku yangu ya ibada ,Hali hii ilinipa tabu Sana , kusema kweli awali nilienda kufanya zile interview Hadi jumamos , sikufanikiwa japo nilikuwa naingia Hadi Oral interview, siku Moja nilihisi hatia baada yakuwa nasikiliza mahubiri na kusoma Maandiko,na historia nikiona mashujaa wa imani walivyojitoa kuacha ya dunia na kumtetea Mungu, niliazimia sitafanya Tena Interview jumamos kipindi hicho Sina ajira ,Nina mke na ana mimba , kula yangu ya tabu Sana, nilimwambia Mungu naomba Hadi mwezi ujao nipate ajira , Mwanamke wangu nyumbani alikuwa akinisimanga ,akininyanyapaa ,yote Ni sababu Sina ajira Sina kipato Kodi ya nyumba Sina na sijui nalipa Nini , niliendelea kushikilia msimamo sitafanya Tena Interview jumamos na rasmi naitelekeza akaunt ya ajira portal .

Kwakweli sijui hata nilikuwa nakulaje ,naishije ,maana sikuwahi kulala njaa ,hata mwenye nyumba Kodi yake ilipofika hakuwahi kuja kunidai had nikasahau nadaiwa Bei gan maana nilikuwa nimelimbikiza nahisi hata miezi 6-8, Siku Moja mwenye nyumba alikuja akasema hanidai Kodi Bali Kuna miezi Kama miwili mbele yeye ndiye namdai ,nilishangaa Sana , kipindi hicho nilikuwa napata interview makapuni mengi tu lakini tulikuwa tunashindwa kwenye Swala la IBADA , .Kuna wakati nilikuta kwenye Emali yangu meseji kutoka bodi yangu ya uhandisi ,nitume detail zangu na namba ya benki, kwakweli nilifanya vile , haikupita wiki nikawekewa laki 9 ,bila kufanya kazi yoyote ,na ndio Kipind ambacho ile miezi miwili ya Kodi niliyoambiwa inaishia ( japo binafsi kwakumbukumbu zangu nilikuwa nadaiwa miezi 6-8),ile laki 9 ilinisaidia Sana kipindi hicho.Nyingine nilianzisha biashara ya matunda lakini haikufanikiwa (ukisikia mtu anakwambia jiajiri wewe msikilize tu)

Lakini bado swala la ajira lililuwa gumu Sana hasa upande wa IBADA ,Kuhusu interview huwa naiitwa kila wiki hata Mara 2 ,Awali nikiwa nimehitimu nilitafuta ajira nikapata katika kampuni ya Uzalishaji mikaa ya briquette huko kusini, nilikutana na meneja mtata Sana, hofu yake kubwa ilikuwa nimekuja kuchukua cheo chake ,alihangaika kwa waganga kunifanyia figisu lakini alishindwa kabisa ,mwisho niliamua kuacha kazi, sio sababu yake ila sikupenda mazingira ,binafsi nakanuni Moja katika maisha , huwa simkimbii mchawi popote pale iwe kwenye kazi au nyumba ,maana kumkimbia mchawi Ni Kumdhalilisha Mungu ambaye tunajinasibu ana nguvu kuliko upande wao .,

Baada ya kurudi nyumbani ,nilisemwa na majirani na jamaa wanaonizunguka maana wanaona unaamka asubuhi had Jioni unarandaranda tu ,nikamwambia Mungu nataka mwezi fulani usipite nipate hata ajira kwanza iniweke sawa , Nilikuwa na rafiki yangu tumehitimu wote chuo darasa Moja , alikuwa hamuamini Sana Mungu, nayeye alihangaika Sana kuhusu maisha na Ajira , kipindi nipo kusini nilimtumia tangazo la ajira kampuni Moja kubwa hapa TZ ya Gesi , aliomba ,niliporudi Dar , tukawa wote majobless , lakini nilikuwa nae karibu kuhusu Mungu anavyofanya kazi, tukisoma Sana Maandiko, (huyu ana stori ndefu jinsi Mungu alivyomtendea,) ,alikata Sana tamaa alifikia hatua hata ya kujiua ,siku Moja akiwa amejiandaa amepaki mizigo yake na vyeti akijiandaa kurudi kwao Kaskazini mwa TZ , asubuhi anapigiwa simu kutoka ile kampuni ya Gesi aende kwa interview , alijiandaa tukiwa wote ,tuliomba , nami nilimwombea nilimwambia Mungu naomba apate hii kazi ili UTUKUFU WAKO UDHIHIRIKE

Kwakweli alifanya interview 3 na zote alitoboa na kupata kazi katika hiyo kampuni ya Gesi, Imani yake kwa Mungu iliongezeka Sana, hirizi na mafuta ya manabii ,maji yote nilikuta amezichoma .

Kwangu hali haikuwa nzuri niliendelea kuwa Jobless ,maisha ya kuungaunga ,biashara ya matunda ilikwama kabisa , .Nikamwambia Mungu Sasa nahitaji kazi ,maana maadui zangu wananisema vibaya na kusema ona anamtegemea Mungu mbona hamsaidii Sasa, binafsi najua hatua zote hizi za maisha Ni shule ,Maana hata Waisrael walikaa jangwani miaka 40 ili kufundishwa .

Siku moja nikaitwa interview katika kampuni Moja ya Tajiri mkubwa hapa TZ , nikafanya interview nikapita ,kosa nililofanya nilisahau kuweka masharti ya ibada wakati nasaini mkataba , Nilipoanza kazi nikawa nasumbuliwa Sana nije jumamos , Bosi akaniita nikamwambia siwezi kuja Jumamosi hata kazi nipo tayari kuacha , Bosi akachukua peni akapiga hesabu pesa ambayo nitakatwa kwa mwaka mzima kwasababu ya kutokwenda jumamos tu, akanikazia macho akasema upo tayari kupoteza kiasi hichi Cha Pesa kisa kusali tu? Je ukienda kanisani unapata Nini ? Mwisho akasema fine sikufukuzi kaz maana umeshasaini mkataba ila Tutakukata pesa .

Kuanzia hapo Bosi akaanza figisu , Pesa za bonus, hanipi anazuia, pesa za communication, n.k zote anazuia ,wenzangu wanapewa Mimi natengwa, mshahara ukija nimekatwa pakubwa Sana , .Wafanyakazi wenzangu na watu wakaribu wakasema fanya uje kazini jumamos tu utakatwa pesa na mshahara unabaki kidogo .,hata mke wangu pia akasema Nenda kazini Jumamosi .

Nikawaambia Sitaenda , Hali ikawa mbaya Sana, Bosi akazidi kunikazia kamba , Nikamuuliza Mungu Nimekutetea kwa watu na wewe nijibu Sasa , Nahitaji unijibu , Nikaweka ratiba nikawa nasoma Sana Zaburi ya 40 .,na maombi na kufunga , Haikupita muda nikapokea simu kutoka mgodi mmoja hapa Tz, nikaandaliwa interview online ,nikafanya ,nikaulizwa hapo unalipwa Bei gani nikajibu , lakini nikasema ngoja nimuulize Mungu je amenijibu yeye ,nikasema Kama wataniruhusu ibada jumamos Basi hiyo kazi imetoka kwa Mungu, kweli wakasema Hilo halina shida , nikatumiwa nauli na hela ya kula , nikafika nikagharamiwa accommodation ya Hali ya juu,

Nikaambiwa unataka tukulipe Bei gani nikataja mshahara mzuri tu nikaambiwa tunakuongeza zaidi, nikaambiwa tunataka uwe meneja hapa na tutakupa nyumba kubwa hapa .

Nikasema hakika Mungu umenijibu

NB: MIMI NI MDHAMBI SANA , ILA MUNGU AMEKUWA MWEMA KWANGU , NINAPOMKOSEA NATUBU KWA KUTAJA DHAMBI JINA LAKE BILA KUPEPESA MACHO ILI ANIREHEMU

Nimejifunza hii kutoka kwa Daudi ,nilijiuliza kwanini MUNGU alimpenda Sana Daudi kuliko sauli ?

Ukisoma Maandiko utagundua Kati ya Sauli na Daudi, Daudi ndiye kavurunda Sana , ameua ,amezini, amenyang'anya wake za watu, lakini alikuwa mtu wa toba ya kweli ,imefikia hatua Daudi ana mji /mtaa mbinguni

Unaitwa MJI WA SAYUNI
SHUJAA WA BWANA UMEANDIKA VIZURI ILA MWISHONI UMEHARIBU HUJASOMA BIBLIA VIZURI KUMHUSU DAUDI MTU WA MUNGU _Kosa Moja ambalo Biblia Imemuelezea Daudi kwamba Ni La Uria Mhiti Wewe umemtaja daudi alikuwa muuaji wale walikuwa ni adui zake wa kimwili na walikuwa waovu ambao walitolewa na Bwana Katika Mikono ya daudi apate kuwauwa. YOTE YA YOTE HONGERA SHUJAA WA BWANA
 
SHUJAA WA BWANA UMEANDIKA VIZURI ILA MWISHONI UMEHARIBU HUJASOMA BIBLIA VIZURI KUMHUSU DAUDI MTU WA MUNGU _Kosa Moja ambalo Biblia Imemuelezea Daudi kwamba Ni La Uria Mhiti Wewe umemtaja daudi alikuwa muuaji wale walikuwa ni adui zake wa kimwili na walikuwa waovu ambao walitolewa na Bwana Katika Mikono ya daudi apate kuwauwa. YOTE YA YOTE HONGERA SHUJAA WA BWANA
Mtu wa Mungu ,unajua Daudi alimuua Uriah pia Mungu alimkatalia Daudi asijenge hekalu sababu mikono yake imemwaga damu nyingi

Sauli kosa lake kubwa Ni kwenda kwa mchawi wa Endori na kutowaangamiza wote alipoagizwa na Mungu


Lakin Daudi hata Abigaili yule mke alinyang'anya kasome vizur, hata Bethsheba hakuwa mke wake ,kachukua mke wa Uria ,kazini nae , pili kamuua Uriah mhiti

Daudi alishasababisha dhambi yake iangamize taifa .

Kama ukiambiwa ujaji Kama tunavyofanya binadamu Basi SAULI anaonekana mwema zaidi ya Daudi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom