Jackwillpower
JF-Expert Member
- Oct 4, 2017
- 2,301
- 3,414
Habari za Jioni ndugu zangu, Amani ya Bwana iwe nanyi ,
Nisipoteze muda niseme hakika Mungu amenitendea Wema na muujiza katika maisha yangu ,sio kwamba Ni mwema au nini naweza kusema katika waovu ,wenye dhambi wa kutupwa nami Ni mmoja wapo ,ila huyu Mungu usipomuelewa utajihisi amekukataa kumbe sivyo, ukiuelewa upendo wa AGAPE utajua Nini naongea.
Mimi Ni muadventista Msabato , sio wa kuzaliwa. (Nitakuja kueleza siku Moja nilivyotoka katika Uislamu na kuingia katika Ukristo).
Mara kadhaa nilihangaika kupata ajira ,nilijiunga na Ajira portal na kweli niliitwa interview nyingi lakini zilikuwa zinaangukia Jumamos ambayo Ni siku yangu ya ibada ,Hali hii ilinipa tabu Sana , kusema kweli awali nilienda kufanya zile interview Hadi jumamos , sikufanikiwa japo nilikuwa naingia Hadi Oral interview, siku Moja nilihisi hatia baada yakuwa nasikiliza mahubiri na kusoma Maandiko,na historia nikiona mashujaa wa imani walivyojitoa kuacha ya dunia na kumtetea Mungu, niliazimia sitafanya Tena Interview jumamos kipindi hicho Sina ajira ,Nina mke na ana mimba , kula yangu ya tabu Sana, nilimwambia Mungu naomba Hadi mwezi ujao nipate ajira , Mwanamke wangu nyumbani alikuwa akinisimanga ,akininyanyapaa ,yote Ni sababu Sina ajira Sina kipato Kodi ya nyumba Sina na sijui nalipa Nini , niliendelea kushikilia msimamo sitafanya Tena Interview jumamos na rasmi naitelekeza akaunt ya ajira portal .
Kwakweli sijui hata nilikuwa nakulaje ,naishije ,maana sikuwahi kulala njaa ,hata mwenye nyumba Kodi yake ilipofika hakuwahi kuja kunidai had nikasahau nadaiwa Bei gan maana nilikuwa nimelimbikiza nahisi hata miezi 6-8, Siku Moja mwenye nyumba alikuja akasema hanidai Kodi Bali Kuna miezi Kama miwili mbele yeye ndiye namdai ,nilishangaa Sana , kipindi hicho nilikuwa napata interview makapuni mengi tu lakini tulikuwa tunashindwa kwenye Swala la IBADA , .Kuna wakati nilikuta kwenye Emali yangu meseji kutoka bodi yangu ya uhandisi ,nitume detail zangu na namba ya benki, kwakweli nilifanya vile , haikupita wiki nikawekewa laki 9 ,bila kufanya kazi yoyote ,na ndio Kipind ambacho ile miezi miwili ya Kodi niliyoambiwa inaishia ( japo binafsi kwakumbukumbu zangu nilikuwa nadaiwa miezi 6-8),ile laki 9 ilinisaidia Sana kipindi hicho.Nyingine nilianzisha biashara ya matunda lakini haikufanikiwa (ukisikia mtu anakwambia jiajiri wewe msikilize tu)
Lakini bado swala la ajira lililuwa gumu Sana hasa upande wa IBADA ,Kuhusu interview huwa naiitwa kila wiki hata Mara 2 ,Awali nikiwa nimehitimu nilitafuta ajira nikapata katika kampuni ya Uzalishaji mikaa ya briquette huko kusini, nilikutana na meneja mtata Sana, hofu yake kubwa ilikuwa nimekuja kuchukua cheo chake ,alihangaika kwa waganga kunifanyia figisu lakini alishindwa kabisa ,mwisho niliamua kuacha kazi, sio sababu yake ila sikupenda mazingira ,binafsi nakanuni Moja katika maisha , huwa simkimbii mchawi popote pale iwe kwenye kazi au nyumba ,maana kumkimbia mchawi Ni Kumdhalilisha Mungu ambaye tunajinasibu ana nguvu kuliko upande wao .,
Baada ya kurudi nyumbani ,nilisemwa na majirani na jamaa wanaonizunguka maana wanaona unaamka asubuhi had Jioni unarandaranda tu ,nikamwambia Mungu nataka mwezi fulani usipite nipate hata ajira kwanza iniweke sawa , Nilikuwa na rafiki yangu tumehitimu wote chuo darasa Moja , alikuwa hamuamini Sana Mungu, nayeye alihangaika Sana kuhusu maisha na Ajira , kipindi nipo kusini nilimtumia tangazo la ajira kampuni Moja kubwa hapa TZ ya Gesi , aliomba ,niliporudi Dar , tukawa wote majobless , lakini nilikuwa nae karibu kuhusu Mungu anavyofanya kazi, tukisoma Sana Maandiko, (huyu ana stori ndefu jinsi Mungu alivyomtendea,) ,alikata Sana tamaa alifikia hatua hata ya kujiua ,siku Moja akiwa amejiandaa amepaki mizigo yake na vyeti akijiandaa kurudi kwao Kaskazini mwa TZ , asubuhi anapigiwa simu kutoka ile kampuni ya Gesi aende kwa interview , alijiandaa tukiwa wote ,tuliomba , nami nilimwombea nilimwambia Mungu naomba apate hii kazi ili UTUKUFU WAKO UDHIHIRIKE
Kwakweli alifanya interview 3 na zote alitoboa na kupata kazi katika hiyo kampuni ya Gesi, Imani yake kwa Mungu iliongezeka Sana, hirizi na mafuta ya manabii ,maji yote nilikuta amezichoma .
Kwangu hali haikuwa nzuri niliendelea kuwa Jobless ,maisha ya kuungaunga ,biashara ya matunda ilikwama kabisa , .Nikamwambia Mungu Sasa nahitaji kazi ,maana maadui zangu wananisema vibaya na kusema ona anamtegemea Mungu mbona hamsaidii Sasa, binafsi najua hatua zote hizi za maisha Ni shule ,Maana hata Waisrael walikaa jangwani miaka 40 ili kufundishwa .
Siku moja nikaitwa interview katika kampuni Moja ya Tajiri mkubwa hapa TZ , nikafanya interview nikapita ,kosa nililofanya nilisahau kuweka masharti ya ibada wakati nasaini mkataba , Nilipoanza kazi nikawa nasumbuliwa Sana nije jumamos , Bosi akaniita nikamwambia siwezi kuja Jumamosi hata kazi nipo tayari kuacha , Bosi akachukua peni akapiga hesabu pesa ambayo nitakatwa kwa mwaka mzima kwasababu ya kutokwenda jumamos tu, akanikazia macho akasema upo tayari kupoteza kiasi hichi Cha Pesa kisa kusali tu? Je ukienda kanisani unapata Nini ? Mwisho akasema fine sikufukuzi kaz maana umeshasaini mkataba ila Tutakukata pesa .
Kuanzia hapo Bosi akaanza figisu, Pesa za bonus, hanipi anazuia, pesa za communication, n.k zote anazuia ,wenzangu wanapewa Mimi natengwa, mshahara ukija nimekatwa pakubwa Sana , .Wafanyakazi wenzangu na watu wakaribu wakasema fanya uje kazini jumamos tu utakatwa pesa na mshahara unabaki kidogo .,hata mke wangu pia akasema Nenda kazini Jumamosi.
Nikawaambia Sitaenda , Hali ikawa mbaya Sana, Bosi akazidi kunikazia kamba , Nikamuuliza Mungu Nimekutetea kwa watu na wewe nijibu Sasa, Nahitaji unijibu, Nikaweka ratiba nikawa nasoma Sana Zaburi ya 40 .,na maombi na kufunga , Haikupita muda nikapokea simu kutoka mgodi mmoja hapa Tanzania, nikaandaliwa interview online ,nikafanya ,nikaulizwa hapo unalipwa Bei gani nikajibu , lakini nikasema ngoja nimuulize Mungu je amenijibu yeye ,nikasema Kama wataniruhusu ibada jumamos Basi hiyo kazi imetoka kwa Mungu, kweli wakasema Hilo halina shida , nikatumiwa nauli na hela ya kula , nikafika nikagharamiwa accommodation ya Hali ya juu.
Nikaambiwa unataka tukulipe Bei gani nikataja mshahara mzuri tu nikaambiwa tunakuongeza zaidi, nikaambiwa tunataka uwe meneja hapa na tutakupa nyumba kubwa hapa.
Nikasema hakika Mungu umenijibu
NB: MIMI NI MDHAMBI SANA, ILA MUNGU AMEKUWA MWEMA KWANGU , NINAPOMKOSEA NATUBU KWA KUTAJA DHAMBI JINA LAKE BILA KUPEPESA MACHO ILI ANIREHEMU
Nimejifunza hii kutoka kwa Daudi ,nilijiuliza kwanini MUNGU alimpenda Sana Daudi kuliko sauli ?
Ukisoma Maandiko utagundua Kati ya Sauli na Daudi, Daudi ndiye kavurunda Sana , ameua ,amezini, amenyang'anya wake za watu, lakini alikuwa mtu wa toba ya kweli ,imefikia hatua Daudi ana mji /mtaa mbinguni
Unaitwa MJI WA SAYUNI
Nisipoteze muda niseme hakika Mungu amenitendea Wema na muujiza katika maisha yangu ,sio kwamba Ni mwema au nini naweza kusema katika waovu ,wenye dhambi wa kutupwa nami Ni mmoja wapo ,ila huyu Mungu usipomuelewa utajihisi amekukataa kumbe sivyo, ukiuelewa upendo wa AGAPE utajua Nini naongea.
Mimi Ni muadventista Msabato , sio wa kuzaliwa. (Nitakuja kueleza siku Moja nilivyotoka katika Uislamu na kuingia katika Ukristo).
Mara kadhaa nilihangaika kupata ajira ,nilijiunga na Ajira portal na kweli niliitwa interview nyingi lakini zilikuwa zinaangukia Jumamos ambayo Ni siku yangu ya ibada ,Hali hii ilinipa tabu Sana , kusema kweli awali nilienda kufanya zile interview Hadi jumamos , sikufanikiwa japo nilikuwa naingia Hadi Oral interview, siku Moja nilihisi hatia baada yakuwa nasikiliza mahubiri na kusoma Maandiko,na historia nikiona mashujaa wa imani walivyojitoa kuacha ya dunia na kumtetea Mungu, niliazimia sitafanya Tena Interview jumamos kipindi hicho Sina ajira ,Nina mke na ana mimba , kula yangu ya tabu Sana, nilimwambia Mungu naomba Hadi mwezi ujao nipate ajira , Mwanamke wangu nyumbani alikuwa akinisimanga ,akininyanyapaa ,yote Ni sababu Sina ajira Sina kipato Kodi ya nyumba Sina na sijui nalipa Nini , niliendelea kushikilia msimamo sitafanya Tena Interview jumamos na rasmi naitelekeza akaunt ya ajira portal .
Kwakweli sijui hata nilikuwa nakulaje ,naishije ,maana sikuwahi kulala njaa ,hata mwenye nyumba Kodi yake ilipofika hakuwahi kuja kunidai had nikasahau nadaiwa Bei gan maana nilikuwa nimelimbikiza nahisi hata miezi 6-8, Siku Moja mwenye nyumba alikuja akasema hanidai Kodi Bali Kuna miezi Kama miwili mbele yeye ndiye namdai ,nilishangaa Sana , kipindi hicho nilikuwa napata interview makapuni mengi tu lakini tulikuwa tunashindwa kwenye Swala la IBADA , .Kuna wakati nilikuta kwenye Emali yangu meseji kutoka bodi yangu ya uhandisi ,nitume detail zangu na namba ya benki, kwakweli nilifanya vile , haikupita wiki nikawekewa laki 9 ,bila kufanya kazi yoyote ,na ndio Kipind ambacho ile miezi miwili ya Kodi niliyoambiwa inaishia ( japo binafsi kwakumbukumbu zangu nilikuwa nadaiwa miezi 6-8),ile laki 9 ilinisaidia Sana kipindi hicho.Nyingine nilianzisha biashara ya matunda lakini haikufanikiwa (ukisikia mtu anakwambia jiajiri wewe msikilize tu)
Lakini bado swala la ajira lililuwa gumu Sana hasa upande wa IBADA ,Kuhusu interview huwa naiitwa kila wiki hata Mara 2 ,Awali nikiwa nimehitimu nilitafuta ajira nikapata katika kampuni ya Uzalishaji mikaa ya briquette huko kusini, nilikutana na meneja mtata Sana, hofu yake kubwa ilikuwa nimekuja kuchukua cheo chake ,alihangaika kwa waganga kunifanyia figisu lakini alishindwa kabisa ,mwisho niliamua kuacha kazi, sio sababu yake ila sikupenda mazingira ,binafsi nakanuni Moja katika maisha , huwa simkimbii mchawi popote pale iwe kwenye kazi au nyumba ,maana kumkimbia mchawi Ni Kumdhalilisha Mungu ambaye tunajinasibu ana nguvu kuliko upande wao .,
Baada ya kurudi nyumbani ,nilisemwa na majirani na jamaa wanaonizunguka maana wanaona unaamka asubuhi had Jioni unarandaranda tu ,nikamwambia Mungu nataka mwezi fulani usipite nipate hata ajira kwanza iniweke sawa , Nilikuwa na rafiki yangu tumehitimu wote chuo darasa Moja , alikuwa hamuamini Sana Mungu, nayeye alihangaika Sana kuhusu maisha na Ajira , kipindi nipo kusini nilimtumia tangazo la ajira kampuni Moja kubwa hapa TZ ya Gesi , aliomba ,niliporudi Dar , tukawa wote majobless , lakini nilikuwa nae karibu kuhusu Mungu anavyofanya kazi, tukisoma Sana Maandiko, (huyu ana stori ndefu jinsi Mungu alivyomtendea,) ,alikata Sana tamaa alifikia hatua hata ya kujiua ,siku Moja akiwa amejiandaa amepaki mizigo yake na vyeti akijiandaa kurudi kwao Kaskazini mwa TZ , asubuhi anapigiwa simu kutoka ile kampuni ya Gesi aende kwa interview , alijiandaa tukiwa wote ,tuliomba , nami nilimwombea nilimwambia Mungu naomba apate hii kazi ili UTUKUFU WAKO UDHIHIRIKE
Kwakweli alifanya interview 3 na zote alitoboa na kupata kazi katika hiyo kampuni ya Gesi, Imani yake kwa Mungu iliongezeka Sana, hirizi na mafuta ya manabii ,maji yote nilikuta amezichoma .
Kwangu hali haikuwa nzuri niliendelea kuwa Jobless ,maisha ya kuungaunga ,biashara ya matunda ilikwama kabisa , .Nikamwambia Mungu Sasa nahitaji kazi ,maana maadui zangu wananisema vibaya na kusema ona anamtegemea Mungu mbona hamsaidii Sasa, binafsi najua hatua zote hizi za maisha Ni shule ,Maana hata Waisrael walikaa jangwani miaka 40 ili kufundishwa .
Siku moja nikaitwa interview katika kampuni Moja ya Tajiri mkubwa hapa TZ , nikafanya interview nikapita ,kosa nililofanya nilisahau kuweka masharti ya ibada wakati nasaini mkataba , Nilipoanza kazi nikawa nasumbuliwa Sana nije jumamos , Bosi akaniita nikamwambia siwezi kuja Jumamosi hata kazi nipo tayari kuacha , Bosi akachukua peni akapiga hesabu pesa ambayo nitakatwa kwa mwaka mzima kwasababu ya kutokwenda jumamos tu, akanikazia macho akasema upo tayari kupoteza kiasi hichi Cha Pesa kisa kusali tu? Je ukienda kanisani unapata Nini ? Mwisho akasema fine sikufukuzi kaz maana umeshasaini mkataba ila Tutakukata pesa .
Kuanzia hapo Bosi akaanza figisu, Pesa za bonus, hanipi anazuia, pesa za communication, n.k zote anazuia ,wenzangu wanapewa Mimi natengwa, mshahara ukija nimekatwa pakubwa Sana , .Wafanyakazi wenzangu na watu wakaribu wakasema fanya uje kazini jumamos tu utakatwa pesa na mshahara unabaki kidogo .,hata mke wangu pia akasema Nenda kazini Jumamosi.
Nikawaambia Sitaenda , Hali ikawa mbaya Sana, Bosi akazidi kunikazia kamba , Nikamuuliza Mungu Nimekutetea kwa watu na wewe nijibu Sasa, Nahitaji unijibu, Nikaweka ratiba nikawa nasoma Sana Zaburi ya 40 .,na maombi na kufunga , Haikupita muda nikapokea simu kutoka mgodi mmoja hapa Tanzania, nikaandaliwa interview online ,nikafanya ,nikaulizwa hapo unalipwa Bei gani nikajibu , lakini nikasema ngoja nimuulize Mungu je amenijibu yeye ,nikasema Kama wataniruhusu ibada jumamos Basi hiyo kazi imetoka kwa Mungu, kweli wakasema Hilo halina shida , nikatumiwa nauli na hela ya kula , nikafika nikagharamiwa accommodation ya Hali ya juu.
Nikaambiwa unataka tukulipe Bei gani nikataja mshahara mzuri tu nikaambiwa tunakuongeza zaidi, nikaambiwa tunataka uwe meneja hapa na tutakupa nyumba kubwa hapa.
Nikasema hakika Mungu umenijibu
NB: MIMI NI MDHAMBI SANA, ILA MUNGU AMEKUWA MWEMA KWANGU , NINAPOMKOSEA NATUBU KWA KUTAJA DHAMBI JINA LAKE BILA KUPEPESA MACHO ILI ANIREHEMU
Nimejifunza hii kutoka kwa Daudi ,nilijiuliza kwanini MUNGU alimpenda Sana Daudi kuliko sauli ?
Ukisoma Maandiko utagundua Kati ya Sauli na Daudi, Daudi ndiye kavurunda Sana , ameua ,amezini, amenyang'anya wake za watu, lakini alikuwa mtu wa toba ya kweli ,imefikia hatua Daudi ana mji /mtaa mbinguni
Unaitwa MJI WA SAYUNI