USHUHUDA: Hivi ndivyo mafuta yanavyoibiwa Bandarini Dar...

Status
Not open for further replies.
Ni makosa kama watu wa usalama wa taifa walioko bandarini bado ni wale wale wa awamu iliyopita.

Rais au Waziri mkuu aweke siku ya kukutana ikulu au popote na wanyetishaji habari muhimu kama hizi. Hata mimi nitampa yangu moja ya uhakika.
Mkuu itoe hapa hapa....
 
Do hii ni hatari.... yaani mpaka nimeogopa.... 80m
kila mmoja cash! !..... inahitaji moyo kuzikataa.... na hawa wanajua hakuna atakae kataa.... inahitajika total overhaul ya utaratibu wa mafuta hapa nchini....
Na hao watu 9 ni toka tra, tpa na tiss sasa huoni bado mfumo ni shida, kiudwe chombo cha kumulika vyombo hivi vya uchunguzi hata tukishindwa basi mkuu wa nchi atoe ajira kwa experts waje wapewe vitengo kama sie tumeshindwa kujilinda. Ni mawazo yangu binafsi
 
mkuu nitakupa namba ya simu au email ya Mh. Rais ili umfafanulie vizuri na kwa lugha rahisi zaidi ili ajue pa kuanzia.

Asante.
Nakubaliana na wewe kwa mara ya kwanza mkuu.

umeandika kwa hekima sana...

itakuwa jambo la msingi, our President akapata taarifa muhimu kama hii..

uwe na siku njema kiongozi
 
For the first time nakaa na wewe meza moja kula bia, jamaa ameelezea vizuri sana na natamabi gazeti la jamhuri waiandike hii kama ilivyo ila wasisahau kutupa credit huku, hivi yule mmiliki wake tulie nae humu aitwa nani vile
@Deudatus Balile
 
Barbarosa mbn kama unafanana na jipu maana unaonekana as if hutaki tueleze madhambi yenu, subiri tu mtakoma tutaeleza kila uozo mlioufanya usitutishe kwa eti magufuli anajua kila kitu eti ili tusiwataje tutasema tuuu
 
taarifa ni muhimu sana,japo haina support evidence lakini inatoa picha namna deals zinachezwa mle na hivyo kuwafanya wahusika kubuni mbinu za kupambana na hizo deals
 
Do hii ni hatari.... yaani mpaka nimeogopa.... 80m
kila mmoja cash! !..... inahitaji moyo kuzikataa.... na hawa wanajua hakuna atakae kataa.... inahitajika total overhaul ya utaratibu wa mafuta hapa nchini....
Kama huyo ISLAM ana uwezo wa kuwapa hiyo 80 wote kwa wakati mmoja in cash, ebu piga picha pesa anayopiga hapo. Waarabu wengi wapo mchini hapa kimaslahi zaidi.
 
Wewe wala usijali sidhani kama Raisi Magufuli na Waziri Mkuu Majaliwa hawayajui hayo uliyoyaeleza wanayajua sana kwanza wanayajua kabla hata WM hajaenda hapo kwenye hiyo mitambo ya mafuta na ndiyo maana unaona hawakuweza kumdanganya ingawaje yeye WM siyo mtaalamu wa mambo ya mafuta, alikuwa na data zote na hata ukifwatilia maagizo aliyoyatoa siyo ya mtu ambaye hakuwa amejitayarisha na asiyejua alichokuwa anakifanya!

Hata ukiangalia huyo Masamaki uliyemtaja alishachomolewa zamani na ana kesi hivyo ninaweza kukutoa hofu wanajua kila kitu na ni swala la muda tu kwani lazima ujue kwamba wahalifu nao pia ni werevu hivyo ni lazima kwenda nao kwa umakini na mwisho wa siku sisi tunachotaka na fedha zetu ninakwambia kwa Magufuli kila jiwe litafunuliwa kama alivyosema Mzee Slaa, hao akina Oil Com, Lake Oil wote wako kwenye radar utasikia tu mdu siyo mrefu!

Hivyo wewe chill na relax Raisi na Serikali yake wanafahamu yote hayo na zaidi kuna sababu kwa nini Maswi aliletwa halafu akaondolewa baada ya kumaliza kazi yake hivyo sasa kazi ndiyo imeanza na haponi mhalifu yoyote yule amini usiamini!
Tutaaminije haya maelezo yako mkuu?

usijekuwa nawe ni miongoni mwa walengwa,so unataka kuua soo....

Huwezi jua nani ni nani...
 
Duuh hii kali mkuu!Yaani umeshusha nondo za uhakika
Hapo ni Bandarini tu...Bado hatujaja Jeshini(Japo tutaambiwa ni siri ya Usalama wa nchi),Lakini tutaongelea juu ya yule Muhindi wa "Duty Free Shop" anavyotumia kibali cha jeshi kuingiza bidhaa nchini bila ushuru na matokeo yake anaingiza na bidhaa za Wafanyabiashara Wahindi wenzake kwa jina la "Jeshi" na wao wanaziuza mtaani kana kwamba zimeingia kwa ushuru.Bati na vifaa vingine vinaingia kwa gia ya "Duty free mali ya maduka ya Jeshi" lkn vinapelekwa mtaani.Data zake bado tunazikusanya mpaka maduka yanayofaidika na uhuni huu.
Kuna data pia juu ya "uhuni" wa mashirika ya ndege ya binafsi na namna yanavyokwepa kulipa kodi zetu stahiki,uozo uliopo kwenye Mamlaka ya Viwanja vya ndege Tanzania,kuanzia ujenzi wa viwanja vya mikoani,ajira zinavyotolewa kwa upendeleo na nani anayeuongoza huo upendeleo,wizi kwa safari za nje na jinsi zabuni za kihuni kama za wale porters pale JNIA,viza za kihuni uhamiaji uwanja wa ndege jinsi wanavyopitisha wachina na wahindi kwa rushwa,namna gani eneo la Cargo uwanja wa ndege linavyopitisha magendo kwenda na kutoka nje ya nchi hasa madini na nyara mbalimbali za serikali ambapo TRA uwanja wa ndege wakishirikiana na wafanyakazi wa kampuni ya Swissport.
 
Nimejikuta natokwa machozi baada ya kusoma taarifa hii....yaani kila nikiona gari la OIL COM au kituo cha mafuta cha OIL COM.... najikuta natetemeka kwa hasira....
Hivi kwanini tusiwe tunawachinja hawa majizi jamaani....haaaaaaaaa......
 
Tukipata watu kama wewe angalau hata hamsini wa kutoa taarifa za kina kutoka sehemu mbalimbali kuliko na majipu hakika tutakuwa tumesaidia sana watendaji pa kuanzia, kweli Tanzania ni tajiri kinachotakiwa tu ni uzalendo na uwajibikaji
Tatizo sio taarifa bali ni uwajibikaji wa baada ya kutoa hizo taarifa...
 
Taarifa murua! Muhimu ni kwamba sio kuwa namna huu wizi unavyofanyika haijulikani kwa wahusika. Hivi ndivyo rushwa ya kitaasisi (institutional corruption) inavyofanya kazi. Na nchi inapokuwa na pengo kubwa kati ya matajiri na maskini, ujue kuna mambo kama haya yanafanyika. Oilcom ni kati ya wafadhili wakubwa wa CCM.
 
Tutaaminije haya maelezo yako mkuu?

usijekuwa nawe ni miongoni mwa walengwa,so unataka kuua soo....

Huwezi jua nani ni nani...


Hauna haja ya kuniamini mambo mengine ni common sense tu, kwa mfano unafikiri WM alikwenda pale akiwa hajui kinachoendelea? Rejea maswali aliyokuwa anamuuliza yule mama Magdalena na maagizo aliyotoa, Je ni maagizo ya mtu ambaye alikuwa hajajiandaa? Iangalie clip vizuri kuna mahali mama Magdalena alitaka kumchenga na WM akamuuliza vipi kuhusu mashine ile nyingine mbona inafanya kazi?

Hata huyo mama kusimamishwa ninavyodhani walishaamua kumsimamisha kitambo sema ilikuwa sasa ni lazima wamshike ili asilie kuonewa na kama ujuavyo sasa hakuna wa kusema kaonewa!
Wewe fikiria ishu nzima ndiyo utaelewa kwamba WM alikwenda pale akijua kila kilichokuwa kinaendelea, unafikiri ni kwa nini ameiamruru Hazina pale pale kupitia Mwanasheria Mkuu kuangalia jinsi ya kuvunja Mkataba na TIPER na kuirudsiaha Serikalini kwa 100% Unafikiri maamuzi kama haya aliyatolea pale pale?
 
Nashauri kuwe na jukwaa la WHISTLE BLOWING, kwa ajili ya wale wazalendo walio ktk mfumo na wanaona madudu yakifanywa ila hawana pa kuanzia, wadondoshe nondo humu, NINA uhakika Magufuli habari zitamfikia tu. Jf ni zaidi.
 
Nahisi kuna kitu kimenikaba kooni kwa hasira, bandarin na TRA HR manual yao iwe tofauti na watu wasainishwe failure to adhere, mhusika anyongwe hadi kufa. Manake kwa style ya kufukuza baadhi ile spirit ipo had kwa watumishi wadogo sana na kila anaefanyakaz humo ana means ya kuwezesha mchakato.
 
zamani kabla watu hawajaingizwa usalama wa taifa walichunguzwa kwa ukaribu lakini toka walipogeuza hizi kazi kupeana kishikaji hayo ndio matokeo yake ndio maana tunawaona wengine bar wakitamba unanijua mi ni nani
Wizi wa mafuta ni biashara inayohusisha watu wengi hao walioondolewa ni mfano tu wengine wanajua kuwa serikali ya sasa haijalala
 
Hivi Pombe ana akaunti JF? Anatakiwa awe anazipata nyuzi kama hivi moja kwa moja.
 
Hizi taarifa zingekuwa zinaandikwa kama maombi ya kazi na kupelekewa moja kwa moja kwenye ikulu...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom