Ushuhuda: Freeman Mbowe ni kiongozi dhaifu

Ushuhuda: Freeman Mbowe ni kiongozi dhaifu

Hawezi kujibu
Pamoja na ukweli kwamba wahadhi wa chuo chetu chenye sifa lukuki kukataa agizo la mwenyekiti wako wa Chama kukagua Vyeti vyoa vya kidato cha nne bado naona kuna haja!

A) Juliana wewe ni binti uliyekuwa blinded na ambition ambaye hata unachokitaka hujui, huenda hata kwa huyo mume umeenda tu kwa kuwa wenzio wenye umri kama wako waliolewa na wewe ukafuata mkumbo!

B) Unajitanabaisha kwamba una elimu,tena ya Sociology ambayo pamoja na mambo mengine inatakiwa uwe na ability ya kutambua chimbuko la matatizo ya jamii yako, ili uwezo kuitoa jamii kutoka hatua moja kwenda nyingine na kuzuia viashiria vingine kuibuka kwa kutoa elimu ya kujitambua. Badala yake umeendelea ku take advantage ya kutojua kwa jamii inayokuzunguka kuzidi kuwarudisha kwenye tope badala ya kuwaanza hata watumie common sense kujinasua!

C) Umeshindwa kuainisha ni kwa namna gani udhaifu wa Mbowe asiye wa chama chako umekuwa kero kwa Chama chenu CCM hadi kushindwa kutatua kero za wananchi na badala yake mkizidishia kero wananchi kwa kuwa watumishi wa propaganda kwenye chama kingine mkitumia muda na rasilimali za chama tofauti!

D) Umeshindwa kutambua unaoita udhaifu wa Mh. Mbowe ndiyo umesababisha serikali ya chama ambacho wewe ni mchepuko kwa sasa ikashindwa kutekeleza ilani yake na badala yake ikitekeleza ilani ya Chama ambacho wewe usiyeijua CCM unamwona mwenyekiti wake ni dhaifu ilihali watu waandamizi wa chama chako hawaishi kuweweseka wasikiapo jina lake!

E) Nakufananisha na askari uliyeingia vitani kujifunza kushika bunduki wakati hakuna vita ya majaribio,so ni vyema ukahifadhi akiba ya maneno yako ya shombo maana siku moja utatafuta akiba yake ukose. Wewe umeamua kuwa mtumwa, its fine, wengine wamekataa utumwa haina haja ya kutumia muda mwingi kuwaeleza waliokataa utumwa jinsi bwana wako anavyokutenda vyema japokuwa ni mtumwa! Wewe endelea tu time will tell!
 
Mtu yeyote anaye mtuhumu Mh Mbowe namshangaa sana na inawezekana anaupungufu wa akili (Zezeta ) au ndo kwanza anaanza kujifunza siasa. Tanzania inavyama vyenye wenyeviti zaidi ya 22, hivyo njoo na data halisi tueleze ni mwenyekiti gani tokea awe mwenyekiti wa chama husika amepoteza au amepata. Kwa takwimu Mh Mbowe tokea awe mwenyekiti wa chama kilichokuwa hakifahamiki kabisa kwa watu mwaka 2004( watu wengi walikuwa wanajua vyama vya siasa tanzania ni CCM, TLP, CUF, UDP na NCCR Mageuzi tu) kwa miaka 10 tu ya uongozi wake CHADEMA kimekuwa chama chenye nguvu kuliko hata Chama tawala yaani CCM, kila uchaguzi wabunge wanaongezeka ( pekee tanzania), Madiwani wanaongezeka (pekee tanzania), Wenyeviti wa mitaa na vijiji wanaongezeka (pekee Tanzania), Kura za wagombea Urais zinaongezeka (pekee Tanzania). Sasa kama angekuwa Dhaifu yote haya yangetokea. Mpeni Mh Mbowe haki yake , amefanya kazi kubwa sana Tanzania na sijui kama kuna Mwenyekiti atakuja kumfikia kwa mafanikio kwenye Chama chochote. Nasema leo wewe JS utalaaniwa kabisa , huwezi kumtukana mtu aliye leta mafanikio makubwa hivyo. Je Mh Mbowe baada ya kuwa Mwenyekiti 2004 angekiua kabisa chadema kama alivyofanya TLP, UDP, nk huo umaarufu unaokutesa ungeupata wapi? Naapa utalaaniwa kabisa hii ni sawa na kumtukana mama yako aliye kuzaa na kukulea kwa kuwa angeamua kukuua angekuua tu hivyo hivyo kwa Mbowe angeiua CDM sijui kama ungekuwa hapo ulipo wewe ******.
 
mimi nasema, siku ambayo CHADEMA walijidanganya wakaruka mkojo na kukanyaga mavi ni siku ile waliyokubali kumpokea mamvi kwenye chama chao. mimi mwenyewe niliondoka na Dr. Slaa. Gia ya angani ilituponza chama chetu. CHADEMA original sio hii ya sasa, na kama kulikuwa kuna uchaguzi rahisi wa raisi chadema kushinda ilikuwa ni mwaka jana, wangemsimasha Dr. Slaa awe rais na Mamvi awe anam support tuu kama Mhe. Sumaye alivyokuwa.

hizo operation ukuta wataenda wenyewe, sasa hivi tunataka maendeleo sio bla bla bla tuuu.
Hilo lilikuwa kosa moja kubwa sana la kiufundi sijui nani aliwashauri kuchukua kinyesi chooni Na kukileta sebuleni.
 
Why don't you celebrate having weak opponents? Why spend sleepless days and nights because of some weak inconsequential opposition party? Why is your chair (and prez), the whole cabinet and the rest of you up to the most down-to-dust JF-CCM fanatic conjuring some kind of scheme to oppress the "already powerless" CHADEMA. What's the fear?
Hawezi kujibu huyu mama WA familia isiyo na watoto
 
Unasoma PhD ama "permanently head destruction".?
Angalia hapo juu makosa yako ya uandishi halafu utuambie kweli kuwa na mtunga sheria kama wewe hii nchi maana yake ina stink na ime sink tayari?
1. U!!!
2. u have as a leaders!!!!
Hawezi kujibu!
 
Ile hali tu ya Mbowe kuwa mwenyekiti wa kudumu dhama hizi ni ishara kwamba Chadema na Mbowe mwenyewe wana matatizo.

Kama wanachadema wanaamini hakuna mtu mwingine mwenye uwezo wa kuwa mwenyekiti wa chama tofauti na Mbowe basi kelele zao hizi za kila siku ni kazi bure.
Watu ambao chama kinawandaa kuja kuwa viongozi wa juu serikalini iwapo Chadema itashinda uchaguzi wataonekana vipi na wananchi ikiwa watu wameng'ang'ania vyeo? Wanapatikana Vijana wakionyesha uwezo wao wanapewa majina mabaya na kisha kufukuzwa Chadema anabaki Mbowe na vijana wa kuchongwa na yeye.

Chadema kuna matatizo mengi ila tatizo la kwanza na liko wazi ni Mbowe, huyu lazima aondoke ndipo mabadiliko yataanza kuonekana.
 
The real question is why are you volunteering to advise your opponents? If all you are saying is true re. udhaifu wa Mbowe, one would expect you to be rejoicing for a "job well done" if he remains in control of CDM - because you guys are working day and night to weaken the opposition. Right? What am I missing? And what makes you think that the people you are trying to advise will listen to you? And why should they listen while they clearly know yours is a project to drive them to extinction? This is pretty much like Hillary Clinton offering political advise to Donald Tump and/or vice versa and expect the opposing party to heed to the advise. We are indeed living in strange times. By the way, do you consider yourself a competent politician?

Ps. Just out of curiosity. Why did you choose to list your qualifications here upfront? It is not like it is illegal or I care. A sign of weakness? A defensive mechanism? What are you defending yourself from? Plus the "Masters on sociology"[sic] that you claim to carry on your shoulders. Clearly you have more than one degree at master's level, if I understand what "masters on sociology" [sic] means. How many degrees in sociology do you have exactly? Why did you decide to get more than one master's degree in sociology?
hawezi kujibu pia.
 
Kwa mtazamo wangu, i think Umejieleza vyema sana. hongera.
Bila kuwashambulia wana cdm.


Hata hivyo upo msemo:-

linaloiva haraka huvunda haraka vilevile.


Nguvu ya ghafla ya Ukawa na cdm iliyotokana na ujio wa El, haikua na mzizi wa asili. Kwasababu ule mzizi wa asili uliojengwa na akina mbowe na dk slaa ulishalegea. Hawa walikua Watu wenye historia moja, waliovuja jasho pamoja kupigwa mabomu pamoja walikua ndugu kwelikweli na hawakua na doa. Cdm hii ilishasambaratika. Ikajitokeza nguvu mpya ya waliokua wana CcM. Ambao miongoni mwao wana madoa, Ikaundwa cocktail ya haraka haraka na upendo na mshikamano wa haraka kama ndoa ya wapenzi wasiosomana tabia kabla ya kuoana.

Ni wazi nguvu hii ililenga kushika dola..ndio maana wako walioamini kua cdm wakikosa dola chama kitakufa. Kwasababu hii ni kama natural law.
Nakumbuka kuna watu walijenga majimbo yao lakini kwenye mgao wa kugombea ubunge na nafasi nyingine walilazimika ku-sacrify nafasi hizo ili waliohamia kutoka ccm wapewe wagombee wakiwemo member wanaounda ukawa.

Sasa mgogoro unaofukuta sasa hivi ni baada ya kukutana wale wasiofahamiana., Wakitambua lengo lililowaunganisha la kushika dola limekufa. Kwahiyo baadhi yao hawana wala hawakua na lengo la kukubali kubeba msalaba wa kua mpinzani daima, tena mpinzani asiye na cheo wala ujiko mtaani.

Na wanautazama ule umachachari waliokua nao wakati wanajuana kipindi cha uchaguzi ndio mahaba halisi tofauti na sasa. Na kwasababu serikali imezuia siasa. Basi hawana pa kufanyia siasa za kiuhanaharakati. Ndio manung'uniko kua Chama kinaonekana kudhohofu.
Ingawa unaonekana una personal attack kwa mh. mbowe. Ila sidhani kama mbowe ndiye anayeamua hizo movement bila kuwashirikisha washauri wake.
Hongera kwa kufunguka mkuu, afadhali sasa hivi mmeanza kidogo kidogo kufunguka watu wa aina yenu..... maana hapo Nyuma mawazo kama haya mlikuwa mnatolea chumbani .
 
Big up Shonza..Huyu DJ kwa wengi tunaemjua kiundani akitoa matamko yake huwaga tunacheka tu..zaidi nashangaa wasomi kama Baregu na Lisuu kuburuzwa na huyu jamaa..siwashangai watu kama Lema cos kichwa chake na mbowe vipo sawa tu
 
Uzuri wa Freeman anapiga za uso tu... Watanunuliwa haohao ma Dr., sijui Prof, lakini sio Freeman.

Na wanakomaa Freeman aondoke ili waweke kibaraka wao.
mimi ninakuelewa Sana unachomaanisha,just imagine mtu kama mpendazoe kawa kiongozi
 
NI hiyo miaka 5 uliyobebwa na walliokuwa wanakutumia, ikiisha hiyo ccm wanakumwaga rasmi na najua huna ubavu wa kupata kura za uchaguzi kwa kupitia jimbo
 
Big up Shonza..Huyu DJ kwa wengi tunaemjua kiundani akitoa matamko yake huwaga tunacheka tu..zaidi nashangaa wasomi kama Baregu na Lisuu kuburuzwa na huyu jamaa..siwashangai watu kama Lema cos kichwa chake na mbowe vipo sawa tu
Kweli sasa kichekesho, sasa wewe Halima mbona usiandike kwa hoja badala yake unakuja na umbea wako wa kike tena wa Tandale?
 
Chura anapojichanganya na kujitia fundi wa kupiga mbizi ndani ya mafuta ya alizeti yaliyochemka 100% +....
 
Cdm imeingiliwa na mdudu unaitwa
Fuata mkumbo
Zidumu fikra za Mbowe hatakama ni Ugoro mtupu.

Vijana wengi CHADEMA hawatumii akili kitafakari anayo yaropoka Mwenyekiti wao.

Mbowe Hana uwezo kuiongoza cdm ya sasa
Anatumia ubabe

"Akili ndogo kuongoza Akili kubwa"
Chama cha UPINZANI Tanzania ni CHADEMa tu?
 
CHADEMA inahitaji uongozi mpya wenye kitu kipya ambacho kitaacha legacy ambayo ni tangible. Aliyoyafanya Mbowe mpaka sasa ni mengi lakini kwa faida ya upinzani na chama chenyewe, ni bora akaja kiongozi mwingine ambaye pengine hulka zake za kisiasa zitakuwa na mwanga mpya wa upinzani.

Lakini asili ya watu wanaomuunga mkono mwenyekiti huyu, ni ubishi na matusi mengi ya kitoto. Kwao kuweza kufikiria tu kwamba chama CHADEMA haiwezi tena kutegemea CCM wajikwae eti ndipo wao wajitokeza hadharani na kuwa wapingaji na wakosoaji, mbinu hizi haziwezi kuwa na msaada mkubwa kwa chama cha siasa chenye ndoto ya kuja kuwa na sera zinazoiongoza nchi hii.
 
Jina: JULIANA SHONZA

Kabila: Mnyiha wa Mbozi

Elimu: Shahada ya Uzamili (Masters on Sociology) – Shahada ya Uzamivu ( Phd – UDSM) on progress.

Ndoa: Nimeolewa

Umri: Miaka 30

Dini: Mkristo wa Dhehebu la Pentekoste

Kazi: Mbunge wa Bunge Tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
====================================================


Kama ilivyoelekeza Sheria, na kwa Matakwa ya Kikatiba ninaanza Andiko langu kwa “Kiapo” ili itakapolazimu maneno yangu ya leo yatumike katika mabaraza ya Sheria na Mahakama kama rejea rasmi.

Maana ya neno “kiapo” kama nilivyolitumia linamaanisha kuwa ni maelezo anayotoa mtu ambayo mtu huyo anaamini kuwa ni sahihi na ya kweli. Na kwa kuwa inakubalika katika Sheria (Sheria ya Ushahidi, Sura ya 6 ya Sheria za Tanzania, kifungu cha 231) kutoa kiapo kwa njia ya maandishi, kama ifuatavyo;

’’Mimi, JULIANA SHONZA, Mtu mzima, Mkristo, Mama wa familia, Mkazi wa Songwe, nikiwa ninaelewa vya kutosha juu ya jambo ninalotaka kulitolea kiapo na hivyo NAAPA kuwa;

NIKIWA NA AKILI TIMAMU BILA KUSHAWISHIWA NA MTU AU KIKUNDI CHA WATU, NAAPA KUWA MAELEZO NITAKAYOYATOA HAPA KUHUSU MHE. FREEMAN AIKAELI MBOWE, (Mb) MWENYEKITI WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO NI SAHIHI, NA YA KWELI”

Ndugu wana jamvi wenzangu, nikiwa ndani ya kiapo naomba nieleze yafuatayo kuhusu UDHAIFU na UDHALIMU wa NDG. MBOWE, nitajitahidi nielekeze kwa ushahidi wa matukio na kwa ufupi kadri itakavyowezekana.

Nianze kwa kueleza kuwa wengi katika watu wanafahamu (ingawa kuna upotoshaji mkubwa ktk ufahamu huo) kuwa niliondoka / kuondolewa CHADEMA kwa sababu moja tu, nilidiriki kumnyooshea kidole MWENYEKITI MBOWE. Nikikosoa namna ya utendaji wake, nilitia shaka juu ya uwezo, maono, ufundi na maarifa yake katika kumudu aina ya siasa za sasa na hatma ya CHADEMA..nilifanya hivyo kwa maslahi mapana ya CHAMA hicho na NCHI yetu kwa ujumla.

Lakini kama ilivyo kwa viongozi WAOGA (cowards), mkuu wangu huyo (ambae hakuzoea kunyooshewa kidole) aliona nimemtusi, nimemkebehi na nimefanya jambo la kumvua nguo na kumshushia heshima na hakuwa tayari kuvumilia DHIHAKA hiyo..hakuwa tayari kukiri MAKOSA, hakuwa TAYARI kuruhusu UHURU wa kikatiba ulio kwa kila mwanachama wa CHADEMA kutumika, hakuwa tayari kuuona UKWELI, kwa kuwa tu UKWELI huo ulisemwa na JULIANA.

Nitaeleza matukio mawili (kati ya mengi) ambayo nilimkosoa MBOWE na ikawa mwanzo wa mtafaruku baina yetu na baina yangu na CHADEMA.

(a) Mnamo tarehe 16 Mei, 2012; (Kwa maelekezo ya MBOWE) Aliyekuwa Mwenyekiti wa BAVICHA Mhe John Heche alitoa tamko la kumtuhumu Ndg John Magale Shibuda kuwa ni MSALITI kwa kitendo chake cha kutangaza hadharani kuwa atagombea URAIS kupitia CHADEMA mwaka 2015.


Baada ya TAMKO hilo, (nikiwa Makamu Mwenyekiti wa BAVICHA) nilijitokeza hadharani kumpinga HECHE, na kumkosoa kuwa TAMKO lake halina Baraka za BAVICHA kwani hajamshirikisha Kiongozi yeyote wa BAVICHA na halikupitia vikao rasmi vya kikatiba, hivyo nikasema kuwa TAMKO hilo ni la HECHE na wala sio la BAVICHA, na nikasema kuwa hatuko tayari BAVICHA kutumika na MTU ndani ya Chama kupambana na MTU mwingine.


Mnamo tarehe 26/5/2012, Mnadhimu na Mjumbe wa Kamati Kuu wa CHADEMA Mhe Tundu Lissu (kwa maelekezo ya Mbowe) akajitokeza hadharani na kusema HECHE yuko sahihi, na kwamba SHIBUDA ni pandikizi na msaliti. Kwa mara nyingine nikapinga hoja ya Lissu iliyonukuliwa kwenye Gazeti la Mwananchi la tarehe 27/5/2012 ukurasa wa 7. Nilisema Mwenyekiti HANA Absolute Mandate ya kuitumia BAVICHA anavyopenda.


(b) Mnamo tarehe 2, february 2013 katika vuguvugu la Mhe Zitto Kabwe kutangaza kuwania UENYEKITI wa CHADEMA na mimi kuhisiwa kuwa ni miongoni mwa wanaomuunga mkono, niliitwa na kutakiwa kujieleza hasa kutokana na hekaya iliyoitwa Ripoti ya Siri ya Mwenendo wa Kisiasa wa Zitto Z. Kabwe ndani na nje ya CHADEMA.


Kwa kuwa niliamini katika kweli, sikushindwa kutamka mbele ya kikao kile ambacho Mhe Baregu alikuwepo, Mbowe mwenyewe alikuwepo na Dr Kitila (akiwa bado CHADEMA) alikuwepo kuwa sina IMANI na uwezo na maarifa ya Mwenyekiti kukivusha Chama katika wakati huu, ni vyema na ni kutokana na utaratibu wa kidemokrasia ndani ya Chama uliokuwepo kikatiba watu wengine waruhusiwe kugombea na ikiwa wanachama wengi watakubali kufanya mabadiliko ya Mwenyekiti, UAMUZI wao uheshimiwe, miongoni mwa wanaotaka mabadiliko hayo ni pamoja na Mimi.

Baada ya Mjadala mrefu, nilijiengua/kuenguliwa CHADEMA kwa jina maarufu la wakati huo la MSALITI, maana kila aliyempinga MBOWE wakati huo na hata sasa aliitwa hivyo.

Baada ya kueleza kwa ufupi matukio hayo mawili yaliyothibitisha udhalimu wa Mbowe wa kutumia mabavu kuendesha Chama na kufanya maamuzi na kuonyesha alivyo Kiongozi Dhaifu, mwenye Woga na asiyejiamini (maana siku zote amekuwa akituma watu badala ya kujitokeza yeye mwenyewe), nirudi katika kadhia ya maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA iliyokutana Juzi na kuunda UKUTA.

Kwanza ieleweke kuwa sio mara ya kwanza CHADEMA kuunda opresheni zisizo na mbele wala nyuma, ila mwaka huu operesheni hii imezidi kuwa ya hovyo kuwahi kufanywa ndani ya CHADEMA..eti ya kuzuia UDIKTETA..Hivi baada ya yoooote aliyoyafanya MBOWE ndani ya CHADEMA anapata wapi authority, ama legitimacy ya kukemea Udikteta..?

Mimi najua kuwa CHADEMA ya sasa sio ile niliyokuwa mimi miongoni mwa Viongozi, maana sisi tulikuwa tunahoji na wakati mwingine kupinga UJINGA na UONEVU ndani ya Chama, hii ni CHADEMA ya ma-ZOMBIE yanayofuata kama WAFU wasio na roho wala maono. Chadema yenye Katibu Mkuu aliyefungwa hatamu, akivutwa kulia anakwenda na akivutwa kushoto ndio unakuwa muelekeo wake, yenye Viongozi wa BAVICHA waoga, wajinga, wasiofikiri, wasiojiuliza, wenye njaa na wanaojali maslahi ya matumbo yao na matumbo ya waliowaweka madarakani.

Ili nifanye thread hii kuwa fupi naomba nifanye marejeo ya Thread yangu ya tarehe 24 february, 2016 yenye anuani Ushauri kwa Jirani: Mbowe must be disposed! na nyingine ni hii Waraka kwa vijana wa UKAWA: Ni wakati wa Mabadiliko hizo nyuzi mbili zinawatosha kabisa kuwa ni hadidu za rejea juu ya mwenendo na tabia zinazoonyesha udhaifu mkubwa wa MBOWE na matendo yake.

Kimsingi, operesheni hii nayo itakufa kifo cha kimya kimya kama ilivyo zingine zilizowahi kutangazwa huko nyuma bila kuacha mafanikio ya aina yeyote, ila kitu cha kipekee sana ambacho nikiri kuwa huko nyuma hakikuwahi kujitokeza ni jina lenyewe la operesheni, inaitwa Operesheni UKUTA...woow, what a brand name..!!!
Mdada nimekupenda bure!!!!![emoji16]
 
Ahsante Juliana Shonza kwa bandiko lako hii itakua rejea, kwa kizazi kijacho juu ya usaniii wa MBOWE katika Tanzania, na wote wafuasi wake wakawa fuata mkumbo, nakumbuka kipindi kile ambacho Zitto alimwambia LISU TUNDU kua anataka mama kuku atoke nje, hasitume viranga.

Inaonekana mpaka Leo Mbowe hajaacha tabia ya kutuma vifaranga vyake..
 
Back
Top Bottom