So what? Wewe uko CCM bado unajitetea dhidi ya Ufukuzwaji wako CHADEMA? Mbowe ni dhaifu. Sawa Tunakubaliana na wewe Mbowe ni dhaifu. Naomba nijibu maswali yafuatayo:
1. Kwanini udhaifu wa Mbowe unaifanya CHADEMA inaendelea kuka kwa kasi kwa kupata idadi ya KURA za Urais, idadi ya wabunge, madiwani na mameya.
2. Kwanini udhaifu wa Mbowe unamyima usingizi Mh.Rais wa Tanzania mpaka anawafungia Mbowe na wenzake kufanya mikutano? anamuhofia dhaifu?
3. Kwanini udhaifu wa Mbowe unawafanya watu shupavu kama wewe Shonza, Zito na wenzako kuondoka CHADEMA?
4. Kwanini ninyi mashupavu mliofukuzwa CHADEMA mlishindwa kumuondoa Mbowe kwenye uenyekiti wa Chama cha CDM?
5. Kwanini ninyi mlio mashupavu msianzishe chama chenu cha Upinzani na kuonyesha udahaifu wa Mbowe kwa kuipiku CHADEMA?
Majibu Tafadhali