Ushuhuda binafsi: Awamu ya tano niliishi kwa hofu

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,341
51,907
USHUHUDA BINAFSI: AWAMU YA TANO NILIISHI KWA HOFU.

Kwa Mkono wa, Robert Heriel.

Nikiri wazi kuwa, licha ya kuwa mimi sio mwoga lakini siwezi ongopa kuwa sina hofu au wasiwasi. Hakuna binadamu asiye na mashaka, hofu na wasiwasi, labda kutofautiana kiwango cha hayo.

Moja ya mambo ninayoyapenda kwa kiwango cha juu kabisa basi ni "Kuandika na kusoma" mambo mbalimbali. Tangu nikiwa mtoto mdogo nilipenda sana mambo hayo. Kuandika kwangu ni kama mchezo, kusoma kwangu ni kama starehe. Haiwezi kupita siku pasipo kuandika chochote na kusoma. Ingawaje, nilipokuwa nasoma, nilikuwa sipendi kuanzika Notes za darasani, sio ajabu kunikuta katika adhabu za wanafunzi wasio andika notes kila mara. Hata hivyo nilikuwa na daftari moja kubwa ambalo nilikuwa naandikia somo la Hisabati, Fizikia, Kemia na Biology. Hata hivyo sio lengo langu kueleza haya.

Kama nitaulizwa, nini utakumbuka kwenye awamu ya tano, basi jibu langu ni "HOFU"

Kwangu awamu ya tano ilikuwa awamu iliyoninyima amani. Nilikuwa mtu wa hofu sana. Pengine ukajiuliza hofu hiyo ilisababishwa na nini?

Kama nilivyotangulia kusema hapo awali kuwa, mimi hobby yangu ni "KUANDIKA" na "KUSOMA" basi kama mnavyojua kitu upendacho kukifanya huwezi kukizuia hata ufanyeje kwani kukizuia ni kuyafanya maisha kuwa magumu. Nilikuwa naandika makala za hapa na pal, zipo za kijamii, kiuchumi, kisiasa, riwaya, mashairi, na maandiko ya kitoto, yakizee, maandiko ya kusadikika basi ilimradi akilli yangu itakavyonituma.

Katika maandiko yangu mara nyingi nalenga kuijenga jamii, kuifundisha na kuielimisha. Kuikosoa, kuikemea na kuiburudisha. Mara zingine naandika bila dhamiri, naandika kwa vile roho yangu inataka niandike tuu yale yote yaliyomo akilini mwangu. Hivyo ndivyo nilivyo, na hiyo ndio furaha yangu.

Sasa kasheshe linakujaga pale ninapoandika makala za kisiasa hasa zenye maudhui ya kukemea, kukosoa na kuonya. Hapa ndipo kulinifanya niishi kwa hofu na kwa tahadhari kubwa sana.

Hofu yangu haikutoka ndani bali ilitoka nje kutoka katika sehemu zifuatazo;

1. Watu wanaonizunguka
Wazazi, ndugu, jamaa na marafiki walikuwa wakiniambia niache kuandika mambo ya kisiasa, hasa yenye lengo la kukosoa, na kuwaonya wakubwa. Nakumba Mama yangu alinipigia simu akanikanya sana, na kunikemea, tuligombana sana, nikijaribu kumwambia asinifundishe kuwaogopa waovu, akaniambia kwa sauti ya kukata tamaa, akasema " Shauri yako hutatimiza ndoto yako" Mimi nikamjibu ndoto yangu ni kuona jamii yangu inaishi kwa haki na uhuru. Basi Mama yangu akasema amenawa mikono na kamwe hataongea na mimi tena kwa habari hizo.

Sisemi sikumuelewa mama yangu, nilimuelewa sana, alikuwa hataki nikutwe na madhila kama yaliyokuwa yanatokea, alionyesha upendo kama Mama. Mama yangu Mkubwa naye mara zote tuliingia kwenye migogoro ya namna hiyo hiyo, nilijaribu kumueleza lakini hakuweza kunielewa kama mimi nilivyoshindwa kumuelewa. Mjomba wangu mmoja naye kwa kujali alinipigia simu siku moja usiku wa manane, nilishangaa simu yake kwani hatukuwa na ukaribu wa kupigiana simu. Hivyo kuiona simu yake usiku ule ilinipa wasiwasi. Yeye naye alinisihi niachane na mambo hayo kwani ni hatari kwangu, aliongea kwa kilugha nafikiri ili nimuelewe vizuri kabisa.

Bibi yangu aliyenilea naye hakuwa nyuma, aliniambia niachane na hayo kwani maisha yangu yatakuwa mafupi, nakumbuka nilimjibu na kumuambia hivi " Bibi ni ipi faida uliyoipata kuishi miaka mingi na ipi hasara ya mtu aliyezaliwa akaishi siku moja?" Bibi hapo alipata kigugumizi. Nilijadiliana sana na Bibi yangu, hakutaka kunielewa.

Mchumba wangu naye hakuwa nyuma mara kwa mara alikuwa akinisihi nisiandike mambo hayo, kwani hataki kuniona katika hatari. Nilimuelewesha akanielewa kishingo upande. Marafiki zangu pia wanaonijua na wasionijua kwa sura(ana kwa ana) nao walinitisha na kunitia hofu..

2. MATUKIO YALIYOKUWA YAKIENDELEA
Baadhi ya matukio kama vile mauaji, utekaji na kutiwa korokoroni kwa baadhi ya wakosoaji nako kulikuwa sehemu ya kunitia hofu katika awamu ya tano. Hata hivyo kila tukio lililokuwa likitokea lazima awepo mtu wa kuniambia; unaona mwenzako, bado wewe. Yaani hiyo ilikuwa ni lazima.

Jambo moja ni kuwa mimi nilichokuwa najaribu kukieleza ndani ya jamii yangu ni kuamsha ari na ujasiri wa kukemea waovu, nilikuwa nahamasisha vijana wasioogope waovu hata kama wangekuwa na nguvu kiasi gani. Jambo moja nililowaambia watu wanitishiapo lilikuwa; sifundishwi kumheshimu na kumuogopa Muovu.

Hata hivyo nilikuwa mtu wa tahadhari, na kama nitakuwa mbali na nyumbani basi nilichunga mienendo yangu na wanaonizunguka, sikuweza kukaa chumbani pasipo kufunga mlango, sikuweza kufungua mlango unaobishwa pasipokusikia sauti ya mtu anayebisha. Sisemi tahadhari hizo zilinisaidia au zingeisaidia hashaa! nilifanya hayo kuepukana kukamatwa kizembe.

MAMBO NILIYOJIFUNZA KIPINDI HICHO;

1. Maovu yanazidi kwenye jamii kwa sababu ya watu wanaogopa kukemea waovu

2. Watu wa karibu wakiwemo wazazi , ndugu na marafiki ndio huwa waalimu wakuu wakufundisha watu uoga wa kumuogopa muovu. Hii ni kutokana na kukupenda na kuona usumbufu unaoweza kukupata na kuwapata

3. Uovu ukizoeleka unakuwa utamaduni ndani ya jamii kiasi kwamba waovu hutukuzwa na kupewa sifa au kujipa sifa

4. Hakuna mtu mwema anayenyamaza aonapo maovu, isipokuwa wanafiki

5. Waovu hutumia mbinu ya kuzima wasema ukweli ili kuhalalisha uovu wao uonekane ni wema

6. Uovu ukishatamalaki, akili ya jamii huwa yakiovu, waovu husifiwa na wenye haki hupondwa.

7. Kutokana na waovu kupenda kamera na kutenda wema mbele ya media, jamii ni hujikuta ikiwaona ni watu wema kumbe ni wabaya.

8. Uovu haufichiki kama vile ulivyo wema. Waovu hutumia nguvu kubwa kuficha ubaya wao, ila kadiri wanavyouficha ndivyo wanavyouibua uovu wao mwingine

9. Hata waovu hufa, tena hufa kabla ya wakati wao.

10. Muovu hana uhuru, kwani uhuru upo hivi; ukiuzuia nao unakuzuia, ukiuachia nao unakuachia. Waovu huzuia uhuru na kujikuta kumbe nao hawapo huru kupitia kuficha uhuru.

11. Muovu hawezi kuwa huru hata siku akifa, bado ataishi kama mtumwa huko aendako

Nilishawahi kusema na kila siku nasema; Taikon atakuheshimu na kukuogopa ukitenda haki na kufuata sheria za Mungu. Lakini kamwe dunia ingalipo, Taikon hataogopa mtu muovu hata angekuwa ni nani. Taikon haogopeshwi na elimu ya mtu, kazi ya mtu, cheo cha mtu, uzuri wa mtu au mamlaka. Ukitenda wema nitakupongeza, ukitenda mabaya nitakukemea na kukuonya, ukiwa na kiburi shauri yako.

Tuishi kwa upendo, upendo ndio utatufanya tuishi milele.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Iringa Mjini
 
Sio muumini wa kusoma maandiko marefu lakn nimejitahidi kumaliza.

Siku zote mtu muoga ni mnafiki, mnafiki ni adui wa mkweli, umeishi kwa hofu na utaendelea kuishi kwa hofu sababu ni mnafiki.

Mambo ya watu kufa, kukimbia nchi zao, kuwekwa ndani yameanza hata kabla uhuru na yameendelea kuwepo na yataendelea kuwepo mpaka wanafiki watakapoisha.
 
Sio muumini wa kusoma maandiko marefu lakn nimejitahidi kumaliza.

Siku zote mtu muoga ni mnafiki, mnafiki ni adui wa mkweli, umeishi kwa hofu na utaendelea kuishi kwa hofu sababu ni mnafiki.

Mambo ya watu kufa, kukimbia nchi zao, kuwekwa ndani yameanza hata kabla uhuru na yameendelea kuwepo na yataendelea kuwepo mpaka wanafiki watakapoisha.

Nashukuru,

Hata Yohana Mbatizaji aikuwa mnafiki ndio maana alikatwa kichwa, karibu sana
 
Uovu ukizoeleka unakuwa utamaduni ndani ya jamii kiasi kwamba waovu hutukuzwa na kupewa sifa au kujipa sifa,,,,,


Hiyo palagraph inaelezea hali halisi kabisa ambayo ilikuwepo kabla jiwe hajatwaliwa,,ashukuriwe Mungu mkuu kwa kusikia kilio chetu.

Naam Mkuu
 
Siyo wewe tu, hofu ilikuwa kwa kila mtu anayetaka kuwa huru kifikra.

Kuna wakati, kwenye jukwaa moja ambalo tunatumia majina yetu halisia, niliwahi kuandika makala moja ya kuikosoa serikali. Wengi walinipongeza.

Kwa kiwango cha kipimo changu, niliona nimetumia lugha ya kistaarabu na kiungwana. Cha ajabu, baada ya siku 2 nilipigiwa simu na mtu ambaye alijitambulisha kuwa anatoka ikulu (sikuweza kuthibitisha kama ni kweli au hapana, na sikuwa na namna ya kuthibitisha). Nikaambiwa, 'tumeupata ushauri wako, hongera sana, tumeuzingatia, titaufanyia kazi LAKINI nakushauri, punguza ukali wa maneno.

Niliwaambia baadhi ya jamaa zangu wa karibu, juu ya simu ile. Nilipata ushauri wa namna mbalimbali, lakini kwa kiasi kikubwa, kila mmoja alijawa na hofu, na walinipa hofu mimi pia. Wengine wakasema, tayari ujue unafuatiliwa. Simu yako hiyo sasa siyo salama. Ukisafiri ni aheri uizime, n.k. Yawezekana kabisa hakukuwa na nia ovu dhidi yangu lakini hali ile iliashiria hali iliyopo katika jamii, yaani watu wanahofu kuwa ukinena chochote, kisichowapendeza watawala, maisha yako yapo hatarini.

Ni vema sasa, utawala mpya, ukawathibitishia wananchi wote, wawe wanapongeza au wanakosoa, kuwa wapo salama.
 
Siyo wewe tu, hofu ilikuwa kwa kila mtu anayetaka kuwa huru kifikra.

Kuna wakati, kwenye jukwaa moja ambalo tunatumia majina yetu halisia, niliwahi kuandika makala moja ya kuikosoa serikali. Wengi walinipongeza.

Kwa kiwango cha kipimo changu, niliona nimetumia lugha ya kistaarabu na kiungwana. Cha ajabu, baada ya siku 2 nilipigiwa simu na mtu ambaye alijitambulisha kuwa anatoka ikulu (sikuweza kuthibitisha kama ni kweli au hapana, na sikuwa na namna ya kuthibitisha). Nikaambiwa, 'tumeupata ushauri wako, hongera sana, tumeuzingatia, titaufanyia kazi LAKINI nakushauri, punguza ukali wa maneno.

Niliwaambia baadhi ya jamaa zangu wa karibu, juu ya simu ile. Nilipata ushauri wa namna mbalimbali, lakini kwa kiasi kikubwa, kila mmoja alijawa na hofu, na walinipa hofu mimi pia. Wengine wakasema, tayari ujue unafuatiliwa. Simu yako hiyo sasa siyo salama. Ukisafiri ni aheri uizime, n.k. Yawezekana kabisa hakukuwa na nia ovu dhidi yangu lakini hali ile iliashiria hali iliyopo katika jamii, yaani watu wanahofu kuwa ukinena chochote, kisichowapendeza watawala, maisha yako yapo hatarini.

Ni vema sasa, utawala mpya, ukawathibitishia wananchi wote, wawe wanapongeza au wanakosoa, kuwa wapo salama.

Kweli kabisa,

Wengine kusema ukweli ndio kipaji tuichojaliwa.

Wengine unafiki ulitushinda tukiwa tumboni mwa mama zetu
 
USHUHUDA BINAFSI: AWAMU YA TANO NILIISHI KWA HOFU.

Kwa Mkono wa, Robert Heriel.

Nikiri wazi kuwa, licha ya kuwa mimi sio mwoga lakini siwezi ongopa kuwa sina hofu au wasiwasi. Hakuna binadamu asiye na mashaka, hofu na wasiwasi, labda kutofautiana kiwango cha hayo.

Moja ya mambo ninayoyapenda kwa kiwango cha juu kabisa basi ni "Kuandika na kusoma" mambo mbalimbali. Tangu nikiwa mtoto mdogo nilipenda sana mambo hayo. Kuandika kwangu ni kama mchezo, kusoma kwangu ni kama starehe. Haiwezi kupita siku pasipo kuandika chochote na kusoma. Ingawaje, nilipokuwa nasoma, nilikuwa sipendi kuanzika Notes za darasani, sio ajabu kunikuta katika adhabu za wanafunzi wasio andika notes kila mara. Hata hivyo nilikuwa na daftari moja kubwa ambalo nilikuwa naandikia somo la Hisabati, Fizikia, Kemia na Biology. Hata hivyo sio lengo langu kueleza haya.

Kama nitaulizwa, nini utakumbuka kwenye awamu ya tano, basi jibu langu ni "HOFU"

Kwangu awamu ya tano ilikuwa awamu iliyoninyima amani. Nilikuwa mtu wa hofu sana. Pengine ukajiuliza hofu hiyo ilisababishwa na nini?

Kama nilivyotangulia kusema hapo awali kuwa, mimi hobby yangu ni "KUANDIKA" na "KUSOMA" basi kama mnavyojua kitu upendacho kukifanya huwezi kukizuia hata ufanyeje kwani kukizuia ni kuyafanya maisha kuwa magumu. Nilikuwa naandika makala za hapa na pal, zipo za kijamii, kiuchumi, kisiasa, riwaya, mashairi, na maandiko ya kitoto, yakizee, maandiko ya kusadikika basi ilimradi akilli yangu itakavyonituma.

Katika maandiko yangu mara nyingi nalenga kuijenga jamii, kuifundisha na kuielimisha. Kuikosoa, kuikemea na kuiburudisha. Mara zingine naandika bila dhamiri, naandika kwa vile roho yangu inataka niandike tuu yale yote yaliyomo akilini mwangu. Hivyo ndivyo nilivyo, na hiyo ndio furaha yangu.

Sasa kasheshe linakujaga pale ninapoandika makala za kisiasa hasa zenye maudhui ya kukemea, kukosoa na kuonya. Hapa ndipo kulinifanya niishi kwa hofu na kwa tahadhari kubwa sana.

Hofu yangu haikutoka ndani bali ilitoka nje kutoka katika sehemu zifuatazo;

1. Watu wanaonizunguka
Wazazi, ndugu, jamaa na marafiki walikuwa wakiniambia niache kuandika mambo ya kisiasa, hasa yenye lengo la kukosoa, na kuwaonya wakubwa. Nakumba Mama yangu alinipigia simu akanikanya sana, na kunikemea, tuligombana sana, nikijaribu kumwambia asinifundishe kuwaogopa waovu, akaniambia kwa sauti ya kukata tamaa, akasema " Shauri yako hutatimiza ndoto yako" Mimi nikamjibu ndoto yangu ni kuona jamii yangu inaishi kwa haki na uhuru. Basi Mama yangu akasema amenawa mikono na kamwe hataongea na mimi tena kwa habari hizo.

Sisemi sikumuelewa mama yangu, nilimuelewa sana, alikuwa hataki nikutwe na madhila kama yaliyokuwa yanatokea, alionyesha upendo kama Mama. Mama yangu Mkubwa naye mara zote tuliingia kwenye migogoro ya namna hiyo hiyo, nilijaribu kumueleza lakini hakuweza kunielewa kama mimi nilivyoshindwa kumuelewa. Mjomba wangu mmoja naye kwa kujali alinipigia simu siku moja usiku wa manane, nilishangaa simu yake kwani hatukuwa na ukaribu wa kupigiana simu. Hivyo kuiona simu yake usiku ule ilinipa wasiwasi. Yeye naye alinisihi niachane na mambo hayo kwani ni hatari kwangu, aliongea kwa kilugha nafikiri ili nimuelewe vizuri kabisa.

Bibi yangu aliyenilea naye hakuwa nyuma, aliniambia niachane na hayo kwani maisha yangu yatakuwa mafupi, nakumbuka nilimjibu na kumuambia hivi " Bibi ni ipi faida uliyoipata kuishi miaka mingi na ipi hasara ya mtu aliyezaliwa akaishi siku moja?" Bibi hapo alipata kigugumizi. Nilijadiliana sana na Bibi yangu, hakutaka kunielewa.

Mchumba wangu naye hakuwa nyuma mara kwa mara alikuwa akinisihi nisiandike mambo hayo, kwani hataki kuniona katika hatari. Nilimuelewesha akanielewa kishingo upande. Marafiki zangu pia wanaonijua na wasionijua kwa sura(ana kwa ana) nao walinitisha na kunitia hofu..

2. MATUKIO YALIYOKUWA YAKIENDELEA
Baadhi ya matukio kama vile mauaji, utekaji na kutiwa korokoroni kwa baadhi ya wakosoaji nako kulikuwa sehemu ya kunitia hofu katika awamu ya tano. Hata hivyo kila tukio lililokuwa likitokea lazima awepo mtu wa kuniambia; unaona mwenzako, bado wewe. Yaani hiyo ilikuwa ni lazima.

Jambo moja ni kuwa mimi nilichokuwa najaribu kukieleza ndani ya jamii yangu ni kuamsha ari na ujasiri wa kukemea waovu, nilikuwa nahamasisha vijana wasioogope waovu hata kama wangekuwa na nguvu kiasi gani. Jambo moja nililowaambia watu wanitishiapo lilikuwa; sifundishwi kumheshimu na kumuogopa Muovu.

Hata hivyo nilikuwa mtu wa tahadhari, na kama nitakuwa mbali na nyumbani basi nilichunga mienendo yangu na wanaonizunguka, sikuweza kukaa chumbani pasipo kufunga mlango, sikuweza kufungua mlango unaobishwa pasipokusikia sauti ya mtu anayebisha. Sisemi tahadhari hizo zilinisaidia au zingeisaidia hashaa! nilifanya hayo kuepukana kukamatwa kizembe.

MAMBO NILIYOJIFUNZA KIPINDI HICHO;

1. Maovu yanazidi kwenye jamii kwa sababu ya watu wanaogopa kukemea waovu

2. Watu wa karibu wakiwemo wazazi , ndugu na marafiki ndio huwa waalimu wakuu wakufundisha watu uoga wa kumuogopa muovu. Hii ni kutokana na kukupenda na kuona usumbufu unaoweza kukupata na kuwapata

3. Uovu ukizoeleka unakuwa utamaduni ndani ya jamii kiasi kwamba waovu hutukuzwa na kupewa sifa au kujipa sifa

4. Hakuna mtu mwema anayenyamaza aonapo maovu, isipokuwa wanafiki

5. Waovu hutumia mbinu ya kuzima wasema ukweli ili kuhalalisha uovu wao uonekane ni wema

6. Uovu ukishatamalaki, akili ya jamii huwa yakiovu, waovu husifiwa na wenye haki hupondwa.

7. Kutokana na waovu kupenda kamera na kutenda wema mbele ya media, jamii ni hujikuta ikiwaona ni watu wema kumbe ni wabaya.

8. Uovu haufichiki kama vile ulivyo wema. Waovu hutumia nguvu kubwa kuficha ubaya wao, ila kadiri wanavyouficha ndivyo wanavyouibua uovu wao mwingine

9. Hata waovu hufa, tena hufa kabla ya wakati wao.

10. Muovu hana uhuru, kwani uhuru upo hivi; ukiuzuia nao unakuzuia, ukiuachia nao unakuachia. Waovu huzuia uhuru na kujikuta kumbe nao hawapo huru kupitia kuficha uhuru.

11. Muovu hawezi kuwa huru hata siku akifa, bado ataishi kama mtumwa huko aendako

Nilishawahi kusema na kila siku nasema; Taikon atakuheshimu na kukuogopa ukitenda haki na kufuata sheria za Mungu. Lakini kamwe dunia ingalipo, Taikon hataogopa mtu muovu hata angekuwa ni nani. Taikon haogopeshwi na elimu ya mtu, kazi ya mtu, cheo cha mtu, uzuri wa mtu au mamlaka. Ukitenda wema nitakupongeza, ukitenda mabaya nitakukemea na kukuonya, ukiwa na kiburi shauri yako.

Tuishi kwa upendo, upendo ndio utatufanya tuishi milele.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Iringa Mjini
Kongole Taikon, mshukuru Mungu kwa kukukinga na waovu, sasa muovu kafa, kazi iendelee kwani waovu bado wako wengi sana
 
Kongole Taikon, mshukuru Mungu kwa kukukinga na waovu, sasa muovu kafa, kazi iendelee kwani waovu bado wako wengi sana

Nashukuru sana Mkuu.
Huo ndio ukweli, hakuna asiye na hofu lakini wapo waliojaliwa kuidhibiti hofu yao
 
Itoshe tu kusema kuanzia 2015-2021 nchi yetu ilikuwa na Wanaume wawili tu,waliotunishiana misuli kwelikweli.Hawa ni JM(mfalme Juha) na mwanasheria msomi TUNDU ANTIPASS LISSU,nadhani mshindi ametangazwa.
Dunia inachukua walio dhaifu.
Tabia uipendayo Sana ndiyo itakayokuua.
 
Umeandika ukweli mtupu, binafsi nilikuwa msomaji tu hapa jf na hata huko kwenye mitandao mingine. Sikutaka kuiletea matatizo familia yangu kisa kuandia au kuongea jambo ambalo ni la kweli ila halimfurahishi mtawala.

Mungu ni mwema siku zote na kamwe Hawezi acha uovu kutawala lazima auangamize
 
Kweli kabisa,
Wengine kusema ukweli ndio kipaji tuichojaliwa.
Wengine unafiki ulitushinda tukiwa tumboni mwa mama zetu
naomba hizo Mada uziweke hapa Jukwaani zilizokutia hofu, kwani tulikuona km CHAWA tu kwa Mwenzazake maana ulijikomba sana
Eti leo upo upande gani mpaka Nyanya yako anakulaumu?
PASKALI Mayalla pasco Mayalla yeye link zake zote anaziweka mnaziona jinsi alivyokuwa Mtabiri, mkweli au alipoangukia kwa Wasukuma
wewe tuwekee tujue maswali ya kukugonga
 
USHUHUDA BINAFSI: AWAMU YA TANO NILIISHI KWA HOFU.

Kwa Mkono wa, Robert Heriel.

Nikiri wazi kuwa, licha ya kuwa mimi sio mwoga lakini siwezi ongopa kuwa sina hofu au wasiwasi. Hakuna binadamu asiye na mashaka, hofu na wasiwasi, labda kutofautiana kiwango cha hayo.

Moja ya mambo ninayoyapenda kwa kiwango cha juu kabisa basi ni "Kuandika na kusoma" mambo mbalimbali. Tangu nikiwa mtoto mdogo nilipenda sana mambo hayo. Kuandika kwangu ni kama mchezo, kusoma kwangu ni kama starehe. Haiwezi kupita siku pasipo kuandika chochote na kusoma. Ingawaje, nilipokuwa nasoma, nilikuwa sipendi kuanzika Notes za darasani, sio ajabu kunikuta katika adhabu za wanafunzi wasio andika notes kila mara. Hata hivyo nilikuwa na daftari moja kubwa ambalo nilikuwa naandikia somo la Hisabati, Fizikia, Kemia na Biology. Hata hivyo sio lengo langu kueleza haya.

Kama nitaulizwa, nini utakumbuka kwenye awamu ya tano, basi jibu langu ni "HOFU"

Kwangu awamu ya tano ilikuwa awamu iliyoninyima amani. Nilikuwa mtu wa hofu sana. Pengine ukajiuliza hofu hiyo ilisababishwa na nini?

Kama nilivyotangulia kusema hapo awali kuwa, mimi hobby yangu ni "KUANDIKA" na "KUSOMA" basi kama mnavyojua kitu upendacho kukifanya huwezi kukizuia hata ufanyeje kwani kukizuia ni kuyafanya maisha kuwa magumu. Nilikuwa naandika makala za hapa na pal, zipo za kijamii, kiuchumi, kisiasa, riwaya, mashairi, na maandiko ya kitoto, yakizee, maandiko ya kusadikika basi ilimradi akilli yangu itakavyonituma.

Katika maandiko yangu mara nyingi nalenga kuijenga jamii, kuifundisha na kuielimisha. Kuikosoa, kuikemea na kuiburudisha. Mara zingine naandika bila dhamiri, naandika kwa vile roho yangu inataka niandike tuu yale yote yaliyomo akilini mwangu. Hivyo ndivyo nilivyo, na hiyo ndio furaha yangu.

Sasa kasheshe linakujaga pale ninapoandika makala za kisiasa hasa zenye maudhui ya kukemea, kukosoa na kuonya. Hapa ndipo kulinifanya niishi kwa hofu na kwa tahadhari kubwa sana.

Hofu yangu haikutoka ndani bali ilitoka nje kutoka katika sehemu zifuatazo;

1. Watu wanaonizunguka
Wazazi, ndugu, jamaa na marafiki walikuwa wakiniambia niache kuandika mambo ya kisiasa, hasa yenye lengo la kukosoa, na kuwaonya wakubwa. Nakumba Mama yangu alinipigia simu akanikanya sana, na kunikemea, tuligombana sana, nikijaribu kumwambia asinifundishe kuwaogopa waovu, akaniambia kwa sauti ya kukata tamaa, akasema " Shauri yako hutatimiza ndoto yako" Mimi nikamjibu ndoto yangu ni kuona jamii yangu inaishi kwa haki na uhuru. Basi Mama yangu akasema amenawa mikono na kamwe hataongea na mimi tena kwa habari hizo.

Sisemi sikumuelewa mama yangu, nilimuelewa sana, alikuwa hataki nikutwe na madhila kama yaliyokuwa yanatokea, alionyesha upendo kama Mama. Mama yangu Mkubwa naye mara zote tuliingia kwenye migogoro ya namna hiyo hiyo, nilijaribu kumueleza lakini hakuweza kunielewa kama mimi nilivyoshindwa kumuelewa. Mjomba wangu mmoja naye kwa kujali alinipigia simu siku moja usiku wa manane, nilishangaa simu yake kwani hatukuwa na ukaribu wa kupigiana simu. Hivyo kuiona simu yake usiku ule ilinipa wasiwasi. Yeye naye alinisihi niachane na mambo hayo kwani ni hatari kwangu, aliongea kwa kilugha nafikiri ili nimuelewe vizuri kabisa.

Bibi yangu aliyenilea naye hakuwa nyuma, aliniambia niachane na hayo kwani maisha yangu yatakuwa mafupi, nakumbuka nilimjibu na kumuambia hivi " Bibi ni ipi faida uliyoipata kuishi miaka mingi na ipi hasara ya mtu aliyezaliwa akaishi siku moja?" Bibi hapo alipata kigugumizi. Nilijadiliana sana na Bibi yangu, hakutaka kunielewa.

Mchumba wangu naye hakuwa nyuma mara kwa mara alikuwa akinisihi nisiandike mambo hayo, kwani hataki kuniona katika hatari. Nilimuelewesha akanielewa kishingo upande. Marafiki zangu pia wanaonijua na wasionijua kwa sura(ana kwa ana) nao walinitisha na kunitia hofu..

2. MATUKIO YALIYOKUWA YAKIENDELEA
Baadhi ya matukio kama vile mauaji, utekaji na kutiwa korokoroni kwa baadhi ya wakosoaji nako kulikuwa sehemu ya kunitia hofu katika awamu ya tano. Hata hivyo kila tukio lililokuwa likitokea lazima awepo mtu wa kuniambia; unaona mwenzako, bado wewe. Yaani hiyo ilikuwa ni lazima.

Jambo moja ni kuwa mimi nilichokuwa najaribu kukieleza ndani ya jamii yangu ni kuamsha ari na ujasiri wa kukemea waovu, nilikuwa nahamasisha vijana wasioogope waovu hata kama wangekuwa na nguvu kiasi gani. Jambo moja nililowaambia watu wanitishiapo lilikuwa; sifundishwi kumheshimu na kumuogopa Muovu.

Hata hivyo nilikuwa mtu wa tahadhari, na kama nitakuwa mbali na nyumbani basi nilichunga mienendo yangu na wanaonizunguka, sikuweza kukaa chumbani pasipo kufunga mlango, sikuweza kufungua mlango unaobishwa pasipokusikia sauti ya mtu anayebisha. Sisemi tahadhari hizo zilinisaidia au zingeisaidia hashaa! nilifanya hayo kuepukana kukamatwa kizembe.

MAMBO NILIYOJIFUNZA KIPINDI HICHO;

1. Maovu yanazidi kwenye jamii kwa sababu ya watu wanaogopa kukemea waovu

2. Watu wa karibu wakiwemo wazazi , ndugu na marafiki ndio huwa waalimu wakuu wakufundisha watu uoga wa kumuogopa muovu. Hii ni kutokana na kukupenda na kuona usumbufu unaoweza kukupata na kuwapata

3. Uovu ukizoeleka unakuwa utamaduni ndani ya jamii kiasi kwamba waovu hutukuzwa na kupewa sifa au kujipa sifa

4. Hakuna mtu mwema anayenyamaza aonapo maovu, isipokuwa wanafiki

5. Waovu hutumia mbinu ya kuzima wasema ukweli ili kuhalalisha uovu wao uonekane ni wema

6. Uovu ukishatamalaki, akili ya jamii huwa yakiovu, waovu husifiwa na wenye haki hupondwa.

7. Kutokana na waovu kupenda kamera na kutenda wema mbele ya media, jamii ni hujikuta ikiwaona ni watu wema kumbe ni wabaya.

8. Uovu haufichiki kama vile ulivyo wema. Waovu hutumia nguvu kubwa kuficha ubaya wao, ila kadiri wanavyouficha ndivyo wanavyouibua uovu wao mwingine

9. Hata waovu hufa, tena hufa kabla ya wakati wao.

10. Muovu hana uhuru, kwani uhuru upo hivi; ukiuzuia nao unakuzuia, ukiuachia nao unakuachia. Waovu huzuia uhuru na kujikuta kumbe nao hawapo huru kupitia kuficha uhuru.

11. Muovu hawezi kuwa huru hata siku akifa, bado ataishi kama mtumwa huko aendako

Nilishawahi kusema na kila siku nasema; Taikon atakuheshimu na kukuogopa ukitenda haki na kufuata sheria za Mungu. Lakini kamwe dunia ingalipo, Taikon hataogopa mtu muovu hata angekuwa ni nani. Taikon haogopeshwi na elimu ya mtu, kazi ya mtu, cheo cha mtu, uzuri wa mtu au mamlaka. Ukitenda wema nitakupongeza, ukitenda mabaya nitakukemea na kukuonya, ukiwa na kiburi shauri yako.

Tuishi kwa upendo, upendo ndio utatufanya tuishi milele.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Iringa Mjini
Umeongea madini sana kaka..big up. Nimependa kuanzia point ya 5-10. Upo sahihi
 
Itoshe tu kusema kuanzia 2015-2021 nchi yetu ilikuwa na Wanaume wawili tu,waliotunishiana misuli kwelikweli.Hawa ni JM(mfalme Juha) na mwanasheria msomi TUNDU ANTIPASS LISSU,nadhani mshindi ametangazwa.
Dunia inachukua walio dhaifu.
Tabia uipendayo Sana ndiyo itakayokuua.
Ukweli Tundu Lisu ni Mtanzania pekee liuwa kiboko ya Jiwe

Pamoja na risasi zote zile Lisu alirudi na kumsema Jiwe hadharani ufisadi wake haswa wa vitambulisho hewa mpaka Jiwe akawa anakatisha kampeni kwa pressure

Pamoja na mabunduki ya Jiwe Lisu aliondoka salama

Hapo ndiyo utajuwa Jiwe alikuwa limbukeni wa kutupwa
 
Back
Top Bottom