Sorry ni awamu ya 5 ya bullzoda sio ya nne! Awamu ya 4 ilikuwa baba wa demokrasia.
Kabla ya 2015 angalau kulikuwa na uhuru wa kusema, ukweli ulijulikana na uliachwa usemwe kwa kiasi kikubwa, na wataalamu waliachwa watumie taaluma yao kutoa miongozo, lakini alipokuja Magufuli yeye aligeuka kuwa engineer, docta, mchumi, na kila kitu.
Kuna mambo mengi watanzania wenye akili nyepesi nyepesi hawawezi kuyaona. Matatizo mengi tuliyonayo sasa hivi kama uhaba wa dola, umeme, ukosefu wa sukari n.k. yalitokana na utawala wa kuburuza mambo wa awamu ya tano.
Mfano umeme: Wakati wa Magufuli mashine nyingi za kufua umeme kwa kutumia gesi zilifanya kazi na kupitiliza wakati wake wa kufanyiwa ukarabati. Tanesco walilazimika kuendelea kufua umeme na mashine zilizokuwa zinahitaji kufanyiwa ukarabati kwani Tanesco wangeondoa baadhi ya machine ili kufanya ukarabati kungesababisha upungufu wa umeme na mgao kitu ambacho kingepelekea wao kufukuzwa kazi mara moja. Hivyo waliendelea kuzalisha umeme na mashine zilizokuwa hoi.
Leo karibu nusu nzima ya mashine za kufua umeme wa gesi pale Ubungo na Kinyerezi zimeharibika kwa mkupuo baada ya kulazimishwa kufanya kazi zikiwa mbovu! Matokeo yake leo hii tuna mgao ambao hata viongozi wetu hawana lugha nzuri ya kuulezea; watasema ni upungufu wa mvua hata pale ambapo El Nino zilikuwa tele kuanzia mwaka jana mwishoni. Hutasikia wakisema ukweli huu kuhusu ubovu wa mashine zitu, utawasikia wakisema ni ongezeko la matumizi ya umeme, hilo nalo ni uongo tu.
Matatizo ya sukari na dola yana mkondo huo huo. Nani asiyejua namna Magufuli alivyoharibu biashara kwa kuwabambikizia kodi wafanyabiashara, kuwapora mitaji na kuwalazimisha kufunga biashara zao kwa visingizio vya kodi? Matokeo ya hayo ndio leo tunayaona. Biashara kati ya Tanzania na nchi za nje ilidorora mno wakati wa Magufuli. Si mnakumbuka jinsi Magufuli alivyowachukia "mabeberu"? Unategemea nini kibiashara unapowachukia bussiness partners na kufunga biashara zao nchini?
Ila kwakuwa watanzania wengi wamelishwa uongo na hawana jinsi ya kugundua uongo huo basi wataamini kuwa Magufuli angekuwepo mambo yangekuwa mazuri. Nawaambia, saa hii tungekuwa kwenye hali ya tahadhari na majanga makubwa kiuchumi na kijamii. Magufuli hakuwa na upeo mkubwa kiuchumi, yeye alilazimisha kila kitu kama alivyopenda bila kujali matokeo yake. Leo tunateswa na matatizo ambayo chimbuko lake ni awamu ya 5 na hakuna kiongozi atakayetuambia ukweli huu!
Kabla ya 2015 angalau kulikuwa na uhuru wa kusema, ukweli ulijulikana na uliachwa usemwe kwa kiasi kikubwa, na wataalamu waliachwa watumie taaluma yao kutoa miongozo, lakini alipokuja Magufuli yeye aligeuka kuwa engineer, docta, mchumi, na kila kitu.
Kuna mambo mengi watanzania wenye akili nyepesi nyepesi hawawezi kuyaona. Matatizo mengi tuliyonayo sasa hivi kama uhaba wa dola, umeme, ukosefu wa sukari n.k. yalitokana na utawala wa kuburuza mambo wa awamu ya tano.
Mfano umeme: Wakati wa Magufuli mashine nyingi za kufua umeme kwa kutumia gesi zilifanya kazi na kupitiliza wakati wake wa kufanyiwa ukarabati. Tanesco walilazimika kuendelea kufua umeme na mashine zilizokuwa zinahitaji kufanyiwa ukarabati kwani Tanesco wangeondoa baadhi ya machine ili kufanya ukarabati kungesababisha upungufu wa umeme na mgao kitu ambacho kingepelekea wao kufukuzwa kazi mara moja. Hivyo waliendelea kuzalisha umeme na mashine zilizokuwa hoi.
Leo karibu nusu nzima ya mashine za kufua umeme wa gesi pale Ubungo na Kinyerezi zimeharibika kwa mkupuo baada ya kulazimishwa kufanya kazi zikiwa mbovu! Matokeo yake leo hii tuna mgao ambao hata viongozi wetu hawana lugha nzuri ya kuulezea; watasema ni upungufu wa mvua hata pale ambapo El Nino zilikuwa tele kuanzia mwaka jana mwishoni. Hutasikia wakisema ukweli huu kuhusu ubovu wa mashine zitu, utawasikia wakisema ni ongezeko la matumizi ya umeme, hilo nalo ni uongo tu.
Matatizo ya sukari na dola yana mkondo huo huo. Nani asiyejua namna Magufuli alivyoharibu biashara kwa kuwabambikizia kodi wafanyabiashara, kuwapora mitaji na kuwalazimisha kufunga biashara zao kwa visingizio vya kodi? Matokeo ya hayo ndio leo tunayaona. Biashara kati ya Tanzania na nchi za nje ilidorora mno wakati wa Magufuli. Si mnakumbuka jinsi Magufuli alivyowachukia "mabeberu"? Unategemea nini kibiashara unapowachukia bussiness partners na kufunga biashara zao nchini?
Ila kwakuwa watanzania wengi wamelishwa uongo na hawana jinsi ya kugundua uongo huo basi wataamini kuwa Magufuli angekuwepo mambo yangekuwa mazuri. Nawaambia, saa hii tungekuwa kwenye hali ya tahadhari na majanga makubwa kiuchumi na kijamii. Magufuli hakuwa na upeo mkubwa kiuchumi, yeye alilazimisha kila kitu kama alivyopenda bila kujali matokeo yake. Leo tunateswa na matatizo ambayo chimbuko lake ni awamu ya 5 na hakuna kiongozi atakayetuambia ukweli huu!