MSHINO
JF-Expert Member
- Jul 26, 2013
- 1,069
- 713
Sasa kubatizwa na kubadilishana majina kunakujaje hapa, fafanua tafadhali!
Kubalini tu kuwa Africa tumeshapoteza vitu vingi na vingine vya thamani zaidi hata ya huo ushoga.
Si kila kitu cha wenzetu ni kibaya, una maana hata magari na madawa tusitumie, lkn swala kuingilia utamadani wetu kwa lazima siyo sahihi, ndiyo maana mtu hashurutishwi kubadiri dini/imani yake. Ni kweli siku hizi tumebadiri majina ya asili na kuchukua hayo ya wageni, yaani ukisikia mtu anaitwa FRANK, MICHAEL, OWEN, WILDROD, ISA, JUMA, YAHYA, JAMAL NA NK basi hao wanaoneka kustaraabika. nasikia zamani wakristu wakipelka jina ambalo siyo la kidhungu wakati wa ubatizo yaani km mkama, kobwa, mkwawa ulikuwa hubatizwi. Nakubaliana na wewe huu wote ni ukoloni mambo leo. lkn kwenye swala la ushoga hapana, ukizoeana na mbwa atakufuata mpaka msikitini, sasa wametuzoea.