Mkuu, kuna mama ntilie mmoja alikuwa akiuza sana chakula kuliko wenzake wote, yaani watu wanamiminika na mpaka amalize yeye ndio wengine waanze kuuza.
Sasa juzi kuna mzee alienda pale kwa yule mama ila mama akakataa kumuuzia na kumwambie nenda kibanda cha pili, yule mzee akamwambia yule mama "acha mchezo wako," kisha mzee akaondoka na mwiko wa yule mama na kumwacha amepigwa na butwaa.
Baadae nilipokutana na yule mzee kwa kuwa namfahamu nikamuuliza maana ya mambo yale, akaniambia yule mama ni mwanga na anauzia watu michanga na vitu vingine vichafu pale......akasema ule mwiko aliouchukua sio mwiko bali ni fuvu la mtoto.
Mkuu inawezekana hii?