Ushindi wa Lema, aibu kwa Clouds FM

Ushindi wa Lema, aibu kwa Clouds FM

Tutor B

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2011
Posts
9,025
Reaction score
6,614
Leo asubuhi kwenye kipindi cha Power breakfast watangazaji wa Clouds FM wameongea mengi ya kumbeza Lema na kesi yake. Sijui sasa hivi wanajisikiaje baada ya hukumu kusoma.

Ombi langu kwa vyombo vya habari:
Msioneshe waziwazi kwamba mnaegemea upande fulani wa chama cha kisiasa kwani vyombo vyenu hivyo ni vya kibiashara. Jamii ikigundua kuwa mna mlengo flani itawasusa.

Mwana JF aliyesikiliza kipindi hicho anaweza akaongeza yale yalokuwa yakiongelewa..
 
Hivi waandishi na watangazaji wa kituo hiki wana taaluma gani? Kwao ushambenga na maneno ya jikoni kwa kwenda mbele!
 
Clouds ovyooo! Na huenda wakawa wanafagilia CCM mafisadi!

Sio hili tu kunakipindi tena walishawahi kumkejeli kiongozi mmoja wa serikali! Mkomeee!
 
Hiyo wafu fm kwani inawachambuzi,wana taaluma gani

Siwezi kupoteza muda kuwasikiliza watangazaji wajinga
 
Walibeza sio kesi ya kihistoria, wakisahau kuna Watanzania walimwaga damu kwa vurugu za kisiasa huko Arusha.

Kwa wanasheria wanatambua kuwa precedent imekuwa set, extent ya udhalilishaji na kuathiri matokeo. case law, bwana Gerald Hando vp bwana? nakaribia kuhama Pb kama siku hizi nilivyojimuvuzisha kutoka jahazi kwenda maskani ya Times Fm, kazi kwenu wapiga debe.
 
That's chap chap media hawana weredi hata kidogo. They luck professionalism hawana contents kwenye habari zao. We sikiliza kuanzaia asubuhi mpaka usiku ndio utajua Clouds hawana contents ni full upuuzi ila jamii ya Kitanzania ndio inapenda kuambiwa upuuzi kama wa Clouds.

Ndio maana hawajatoa mwandishi au mtangazaji kwenda kwenye international media kama BBC au DW.
 
hao ndo kawaida yao mim mwenyewe nimewasikia kiukwel iafike mahal vyombo vya habar katika mambo ya ushabik visionyeshe upande vinakoegemea.
 
hapa nadhani mnawachafua clauds bure,tafadhali mfanye tena utafiti wa kina kujua mnachokisema kama ni sawa
 
Hao ni wachambuzi wa magazeti,sio wachambuzi wa habari

litakaloandikwa la kipropaganda wanatiririka nalo,hawajitegemei kiakili,kiuelewa
 
Hakuna umakini , taaluma inapofanyika kienyeji unategemea nini?? Mfumo mzima umeoza, hadi Media inakosa dira ! aibu yao.Waombe msamaha kwa Lema .
 
Pamoja na baadhi ya masuala ya kijamii kufanya anglau vizuri, masuala ya kisiasa waachane nayo kwani wanaboa kweli kweli. Nafikiri wanafagilia rushwa!!!.
 
Aibu yao, lakini si mliwaona ndio walitoa ofa ya Public Address - system kwenye mkutano mkuu wa CCM?
 
Back
Top Bottom