Ushindi wa CHADEMA Ukonga waleta neema

Ushindi wa CHADEMA Ukonga waleta neema

Waache hao maCCM yaendelee kuwekeana kiporo hadi kitakapochacha ndio watajua kuwa kiporo hakiliki tena baada ya kuchacha.
Wameshazoea kula vilivyochacha hao ndio maana wanaonga sana makamanda ili kuwapata
 
Ngoja Nimuulize kamanda Thomas Nyahende kama kweli Mwita Mwikabe ndio mwenyekiti wa Kivule, pia aniambie kama huyu ndie alikuwa Raisi wa Daruso nilipokuwa mwaka wa kwanza 2005, kama ni kweli basi tuna under utilize resources, maana jamaa anauwezo mkubwa sana katika uongozi
 
Goooood!!!! Chadema ni ukweli, uwazi na uwajibikaji kwa VITENDO.
 
Ngoja Nimuulize kamanda Thomas Nyahende kama kweli Mwita Mwikabe ndio mwenyekiti wa Kivule, pia aniambie kama huyu ndie alikuwa Raisi wa Daruso nilipokuwa mwaka wa kwanza 2005, kama ni kweli basi tuna under utilize resources, maana jamaa anauwezo mkubwa sana katika uongozi

Ndio yeye mkuu
 
Haya ndio mambo Wananchi wanayotaka, hawataki personality za watu n.k bali wanataka hali walizokuwa nazo ziboreshwe, wanataka mabadiliko chanya
 
Kuna watu walikuwa wanasema yeye ndio yule MM3.

Hata kama yeye ndio MM3 inawezekana kabisa yeye ndiye aliyefanikisha kupatikana zile taarifa za usaliti za akina Zitto, Mwigamba na Kitila kwani yeye alikuwemo humo kama kiungo kwa utoaji wa taarifa kwa viongozi wa chama, kwa kukupa kumbukumbu nzuri kumbuka lile tukio la wale akina Tamimu, Macghee na Maganga walipotaka kumpindua Nyerere lakini waliweza kugundulika kutokana tu na uwepo wa watu/Mtu aliyekuwa akitoa taarifa kwa Serikali ndani ya kundi lao na ndiye aliyefanikisha wao kukamatwa kama kuku.
 
Piga kazi Kamanda Mwita, saa ya ukombozi imeshafika. Huu ni mwaka wa hitimisho.
 
Ahsante sana kamanda Molemo kwa taarifa hii nzuri na yenye kuamsha ari.

Nampongeza kwa dhati kabisa Mwenyekiti wangu wa Mtaa wa Kivule kwa namna alivyoanza kazi za kuwatumikia wananchi mara moja baada ya kuchaguliwa kuwaongoza, hakusubiri mkurugenzi ajitafutie posho ya kumuapisha.

Na huu ndio mwelekeo kwa wenyeviti wangu wote wa mitaa tuliyoshinda Jimbo la UKONGA kufanya kazi kwa bidii, kwa kushirikisha wananchi lakini kwa ubunifu wa hali ya juu ili kutimiza matarajio ya waliowachagua.

Kazi yangu ni kuhakikisha kuwa nafuatilia hatua kwa hatua kutendaji na utekelezaji wa majukumu ya kila mwenyekiti wa mtaa anayetokana na Chadema katika jimbo la UKONGA na kuhakikisha kuwa wanatoa huduma bora kwa wananchi.
 
Last edited by a moderator:
jamani ccm wasilaumiwe wamechoka miaka 53 sio mchezo...
ni mda wao sasa wapumzike wala sio kwa machafuko
 
Wananchi wa Kata ya Kivule wamefurahishwa na ushindi wa Mwenyekiti wa Mtaa wa Kivule Mwita Mwikabe Waitara kutokana na kuanza kutumikia wadhifa huo kwa kishindo kikubwa.

Ni wiki moja sasa kuna ukarabati mkubwa wa barabara za mitaa ya Kivule na ile itokayo Banana kwenda Kivule.

Taarifa zinasema mara baada ya kuapishwa Mwenyekiti wa mtaa huo Mwita Waitara alivamia ofisi za Manispaa kuelezea kero za wananchi wa Kivule kutokana na ubovu mkubwa wa barabara.Waitara alitaka kuona bajeti nzima ya miundombinu ya manispaa.

Kutokana na hali hiyo Waitara aliahidiwa ukarabati wa barabara hiyo na kesho yake ukarabati ukaanza.

Akikagua ukarabati huo Mwita Waitara aliwaeleza wananchi waliomzunguka kwamba hiyo ndiyo CHADEMA na kuwaambia kamwe hatalala huku wananchi wake wakitembea kwa miguu kwa ubovu wa barabara.

Diwani wa Kivule na mbunge wa Ukonga Eugene Mwaiposa wanatoka CCM lakini siku zote wamepuuza kilio cha wananchi kuhusu ubovu wa barabara.

Picha chini ni Mwenyekiti wa mtaa wa Kivule Mwita Mwikabe Waitara

Hongera Waitara . Kaza buti .
 
Kweli siasa ni mchezo mchafu Mwita leo hii ni mwenyekiti wa mtaa tena sio Mchafu Koge au Barack Obama bali ni Kivule.
 
Chizi pekee ndiyo anaweza kuiamini hoja kama hii.
Hiyo avatar umeivamia ndugu, haiendani na akili ulizo nazo. Akili yako inaendana na ile avatar uloitoa. irudishe sababu unaabisha kichwa ulichokiweka hapo. Huna kitu wewe kichwani hadi kuweka avatar hiyo. Weka ya JK si ya Mwalimu! Ova!
 
Ahsante sana kamanda Molemo kwa taarifa hii nzuri na yenye kuamsha ari.

Nampongeza kwa dhati kabisa Mwenyekiti wangu wa Mtaa wa Kivule kwa namna alivyoanza kazi za kuwatumikia wananchi mara moja baada ya kuchaguliwa kuwaongoza, hakusubiri mkurugenzi ajitafutie posho ya kumuapisha.

Na huu ndio mwelekeo kwa wenyeviti wangu wote wa mitaa tuliyoshinda Jimbo la UKONGA kufanya kazi kwa bidii, kwa kushirikisha wananchi lakini kwa ubunifu wa hali ya juu ili kutimiza matarajio ya waliowachagua.

Kazi yangu ni kuhakikisha kuwa nafuatilia hatua kwa hatua kutendaji na utekelezaji wa majukumu ya kila mwenyekiti wa mtaa anayetokana na Chadema katika jimbo la UKONGA na kuhakikisha kuwa wanatoa huduma bora kwa wananchi.

Asante sana Mwenyekiti Mwita Maranya kwa uongozi mzuri uliosababisha wananchi wa Ukonga nao wajihesabu ni watu katika Taifa lao.

Ukonga imedharauliwa vya kutosha.Ukonga imepuuzwa vya kutosha.

Kila mwanaKivule anafurahia utendaji uliotukuka.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom