Ahsante sana kamanda
Molemo kwa taarifa hii nzuri na yenye kuamsha ari.
Nampongeza kwa dhati kabisa Mwenyekiti wangu wa Mtaa wa Kivule kwa namna alivyoanza kazi za kuwatumikia wananchi mara moja baada ya kuchaguliwa kuwaongoza, hakusubiri mkurugenzi ajitafutie posho ya kumuapisha.
Na huu ndio mwelekeo kwa wenyeviti wangu wote wa mitaa tuliyoshinda Jimbo la UKONGA kufanya kazi kwa bidii, kwa kushirikisha wananchi lakini kwa ubunifu wa hali ya juu ili kutimiza matarajio ya waliowachagua.
Kazi yangu ni kuhakikisha kuwa nafuatilia hatua kwa hatua kutendaji na utekelezaji wa majukumu ya kila mwenyekiti wa mtaa anayetokana na Chadema katika jimbo la UKONGA na kuhakikisha kuwa wanatoa huduma bora kwa wananchi.