Ushawahi choka mkeo?

Ushawahi choka mkeo?

Siyo umemchoka ,umemzoea.Anafanya mambo yale yale kwa namna ileile kila siku so unazoea unahitaji something new,
Jitahidi kubadili mazingira msiwe pamoja kwa mada fulani then tafuta mshauri wa mambo ya mahusiano amfundishe mkeo ubunifu na kubadili ratiba .Kwa sababu ni mke mwema ukirudi utakuta mambo super mtalisongesha.Ila miloana mapema sana so unahitaji hekima ya hali ya juu kumtreat wife.
 
Ukimwacha ndio utajua umuhimu wake. Yaani hapo kama kwenye mechi saivi amekua kiungo mtibuaji asionekana akiumia timu inapoteza mwelekeo. Vumilia ndugu yangu mwombe Mungu yatakwisha
 
If you love your wife, you'll do anything you can to keep her. Kuchoka au kuwa bored ni kawaida but mnafanya nini kuspice up hayo maisha yenu? Mnaendanga safari pamoja? mnaenda hata dinner peke yenu bila watoto? yawezekana mmefanya maisha kuwa too routine kila mnachoongea ni habari za kawaida za kila siku (tule nini, gari limeharibika, fulani katutembelea ) and discuss nothing about your lives as couples --mnajisikiaje, mipango yenu, maisha yenu ya mapenzi, nk.

Ndoa na mapenzi ni kama mmea/ua tu jinsi unavyotunza ndio linavyositawi : kama hakuna juhudi zozote humo lazima mtachokana. Nakushauri msiachane bali mtafute njia za kujenga ndoa yenu iwe mpya.
Umeongea vizuri mkuu
 
Hata nyumba tu inachosha sembuse mke?

Mimi kuna siku nyingine huwa natamani nikalale nyumba ya jirani maana kwetu kunaboa hii nyumba nimeichoka kabisa

Ha ha ha ha..
 
Hiyo inatokea sana tu kwenye ndoa..Na moja ya sababu ya kuchokana ni kuwa na interest/hobbies tofauti...Mnajikuta hakuna intersection miongoni mwenu...Ukiwa na mwanamke ambaye mna vitu vingi vinaendana ni ngumu kumchoka

Miaka 35 bado ndoa ni changa sana, ninachokiona hapo probably mama ameshindwa ku-keep up baada ya kuzaa na hivyo jamaa anamwona kama amebadilika sana. Na hii inatokea sana, watoto wawili ni rahisi kumbadili shape mwanamke.

Ukiwa na wife ambaye anajua ku-keep up na mwili wake hasa hasa baada ya kuzaa huwezi kumchoka, kwanza ndo unazidi kumwonea wivu na kumpenda zaidi.

Gym na diet zinahusika hapo, shopping shopping pia.
 
Hebu twende taratibu Mpwa
  • Una miaka 34 na kidogo
  • Ndoa yako ina miaka 8 sasa
  • Unafanya kazi
  • Wife anafanya kazi (?)
  • Mmejaaliwa watoto wazuri wawili toka kwa MUNGU
  • "Umepoteza hamu na Mpenzi wako"
Haya tuanze moja baada ya jingine taratibu kabisa
Umri unaonyesha kuwa ulioa ukiwa na miaka 26-27, kwa uzoefu wa kidunia ya sasa (msisitizo uko kwenye dunia ya sasa) vijana wengi katika umri huo bado huongozwa na tamaa, sio wote ila walio wengi. Ni umri ambao ungeutumia vyema kujijenga kiakili na kupata exposure ya baadhi ya mambo ya dunia na mambo ya mbingu pia. Je katika umri huo wakati unaoa mkeo alikua na umri gani? 22? Umri huenda isiwe tatizo sana, hivyo hebu tuuache maana umri huenda sio ishu but maturity na exposure.

Umri wa ndoa yako ni miaka nane (8) ambapo ndio muda huu una experience hayo mambo ya "kujifanya kumchoka" dada wa mwenzio. Kwa utafiti mkubwa uliopo na kwa kuthibitisha kangu mimi mwenyewe, hichi ndichi kipindi ambacho ndoa nyingi sana hukumbwa na matatizo ya namna hio, hili (pengine) huenda likachangiwa na mambo mawaili au matatu; Moja, Mama huhamishia mapenzi kwa watoto Zaidi ya Baba, au Baba hupata majukumu mengi Zaidi kuanzia kazini, nyumbani na maisha kwa ujumla na hivyo kupoteza concentration ya ndoa, na jingine pia ni kwamba sasa kila mtu anaanza kuonekana uhalisia wake halisi sasa, sio ule uhalisiia wa maigizo, yaani yule Elli wa ndani sasa ndio anajitokeza, la mwisho katika hili pia huenda ikawa ni kule either kuijtoa ukaribu wako na MUNGU wako au kujisogeza kwa MUNGU Zaidi na ukayaacha ya familia. Hebu tufanye kama vile hili nalo si muhimu

Wakati mwingine (not always) baadhi ya kazi zetu hututenga sana na familia zetu kisaikolojia na kutufanya kuwa na "ulimwengu" tofauti na ulimwengu wa familia yako, yaani uko home lakini akili yako yote iko kwenye kazi, unawaza hili au unawaza lile hadi kuna kuccha, hili huweza kutokea kwa mkeo na kwako pia, lichunguze na badilisha mfumo wa utendaji kazi wenu


Je una kampani gani? Je marafiki hao wameoa wana familia je huchukuliaje suala la ndoa na mapenzi? Nini mitizamo yao juu ya ndoa, familia na mapenzi kwa ujumla? Jichunguze, hao nao wamechangia sana kwa baadhi ya ndoa na familia kuharibika.

Asikudanganye mtu eti umuache mkeo, imagine ni dada yako ndio anaacha na mtu, kisha ana watoto wako wa damu yako, imagine Mama yako angeachwa na Baba yako, asikudanganye mtu mapenzi ya mzazi mmoja yanawaumiza watoto sana kuliko tunavyoweza kudhani, kwanini ukubali kuharibu furaha ya watoto wako kwajili ya kutimiza matamanio yako ya mwili tu tena ya muda kwani uitese familia yako kwajili tu ya kutaka kujiona unaridhika? Hio selfishness itakuja kukugharimu.

Usikubali mtu aje kukulelea wanao ilihali wewe upo, usikubali wanao walelewe na Mama wa kambo ilihali mama wa watoto wako yupo, you will one day pay for that when it is too late. Ushauri wangu wa mwisho, ulishasikia watu wanasema tunaishi kama Kaka na Dada? unaelewa maana yake? Jifunze toka kwao, nakusihi sana sana usimuache mke wako uliepewa na MUNGU na zawadi nzuri ya watoto. hebu tizama video hii hapa chini, mimi ilinigusa sana nikabadilika, hope na wewe itakubalisha pia...


 
Miaka 35 bado ndoa ni changa sana, ninachokiona hapo probably mama ameshindwa ku-keep up baada ya kuzaa na hivyo jamaa anamwona kama amebadilika sana. Na hii inatokea sana, watoto wawili ni rahisi kumbadili shape mwanamke.

Ukiwa na wife ambaye anajua ku-keep up na mwili wake hasa hasa baada ya kuzaa huwezi kumchoka, kwanza ndo unazidi kumwonea wivu na kumpenda zaidi.

Gym na diet zinahusika hapo, shopping shopping pia.
Yeah hiyo inaweza kuchangia..Ila saanyingine kuchokana wala hakuhusiani ni muonekano wa mtu..Wengine wana wake wazuri ila still wamewachoka...Hilo la kutokuwa na common interest linachangia nalo kwa kiasi kikubwa..Ndo mana utakuta watu wapo ndani ya ndoa lakini hawana story au story ni zile zile deile

Imagine labda we ni mtu ambaye unapenda kudiscuss trending issues lakini wife wako hata hajui kinachoendelea uraiani..Utajikuta unatafuta watu nje wa kujadili nao...Au unakuwa na mke antisocial wakati we unapenda kujamiana ..We unapenda burudani lakini wife hamjui hata Diamond ni nani..

Wife akiwa rafiki yako kumchoka ni kazi..Na hawezi kuwa rafiki kama hamuendani
 
Yeah hiyo inaweza kuchangia..Ila saanyingine kuchokana wala hakuhusiani ni muonekano wa mtu..Wengine wana wake wazuri ila still wamewachoka...Hilo la kutokuwa na common interest linachangia nalo kwa kiasi kikubwa..Ndo mana utakuta watu wapo ndani ya ndoa lakini hawana story au story ni zile zile deile

Imagine labda we ni mtu ambaye unapenda kudiscuss trending issues lakini wife wako hata hajui kinachoendelea uraiani..Utajikuta unatafuta watu nje wa kujadili nao...Au unakuwa na mke antisocial wakati we unapenda kujamiana ..We unapenda burudani lakini wife hamjui hata Diamond ni nani..

Wife akiwa rafiki yako kumchoka ni kazi..Na hawezi kuwa rafiki kama hamuendani

Sure sure, ila haya mambo wakati mwingine yanatokea bila sababu. Wanaume ni kati ya viumbe ambao hata haijulikani wanataka nini kwa mwanamke. Case nyingi ni mwanaume kumchoka mwanamke kuliko mwanamke kumchoka mwanaume.

Ni kumwomba sana Mungu asaidie tu kulinda ndoa maana kuna kama mdudu anamwingia mtu kichwani anaenda kuharibu haribu mawazo.
 
Nafikiri wazee zamani walikuwa hawaachi wake zao sababu walikuwa na wake wengi
huwezi kumchoka mkeo kama ungekuwa unapata mda wa kum miss...
wanasema 'how can i miss you if you are always here'

labda ni phase tu itapita
au labda umemchoka kweli for good....

hebu safiri alone kama wiki mbili ujitathmini
Dunia ni nyingine sasa hivi ukioa wanawake wengi cha moto utakiona.wanaume mmekuwa mnalalamika sana Lkn ninyi ndio mlioanzisha vita.wanawake ni wavumilivu sana lkn wakigeuza shingo zao huwa wanaharibu jumla hata wasiohusika watahusika.mnatuumiza sana jamani
 
Mkuu kwanini usitafute kijiholiday muende sehem mbali kidogo na mazingira uliyoyazoea mkae huko hata mwezi mzima, mkutane na watu tofauti muongee vitu tofauti na mlivyozoea kuongea and have some fun..... am sure mkirudi mtakua kama mmeanza upya

Chukua karatasi orodhesha mambo kumi yaliyokupendeza kwake mpaka ukaamua kumuoa upande mmoja na upande wa pili andika mambo ambayo yanakufanya umchoke (Naamini humchukii).
baada ya hapo nakuomba kaa ongea nae mkeo mpendwa kuhusu usiyoyapenda ili ajirekebishe na wewe akikuambia asiyoyapenda kwako uwe tayari kujirekebisha. Na yale kumi ambayo yalikufanya umpende hakikisha una ya re inforce, mpende mkeo haya ya kuchokana ni kawaida kwa binadamu. Pia kumbuka miaka inakwenda na mnakuwa watu wazima, inawezekana kuna vitu mlikuwa mnafanya wakati wa uv=chumab sasa kuna watoto na majukumu yameongezeka vimepungua.. kumbushia mara moja moja.
Kila lakheri.
 
Hata nyumba tu inachosha sembuse mke?

Mimi kuna siku nyingine huwa natamani nikalale nyumba ya jirani maana kwetu kunaboa hii nyumba nimeichoka kabisa
Hata Mme anachosha pia.mana unatamani hata asirudi kutoka kazini.wote tumechokana tu na hivi kila kukicha maisha yanabadilika na kuwa magumu zaidi ndio kabisaa.pia ukiona mwanaume hayuko responsible na family wanawake tunamchoka Mara mbili.
 
Sure sure, ila haya mambo wakati mwingine yanatokea bila sababu. Wanaume ni kati ya viumbe ambao hata haijulikani wanataka nini kwa mwanamke. Case nyingi ni mwanaume kumchoka mwanamke kuliko mwanamke kumchoka mwanaume.

Ni kumwomba sana Mungu asaidie tu kulinda ndoa maana kuna kama mdudu anamwingia mtu kichwani anaenda kuharibu haribu mawazo.
Sure aiseee..Vipi we bado hujachoka?
 
Back
Top Bottom