PART V
Wana MMU, haka kastori ni ka mtiririko wa miaka mingi.
Na nakaleta ili walimwengu muone mwanaume anavyoweza kuwa mjinga kwa penzi.
Mwanamke anakufunga kamba kwa kukupa uroda unaoweza kukupumbaza, wewe ukawa unampenda lakini yeye anakupenda just enough kupata kile anachokipata kwako.
Kama amekuchoka au ndo unaelekea down, kuna wanawake ni wajanja sana ku jump a sinking ship na kudandia nyingine.
Kitendo cha Clara kuolewa kilinikera haswa.
Lakini kabla hajaolewa niliongea naye kinaga ubaga.
Nilimwambia wewe Clara nilikutongoza ukiwa huna hili wala lile huko mkoani, ila ulichokuwa nacho ni ule uzuri wako natural ulioufunika katika nguo zisizo na hadhi.
Nikakuanzishia biashara, nikakununulia gari, umenona umependeza sasa unaniacha.
Nilimwambia mimi simjui na sitaki kumjua anayetaka kukuoa, ila ujue amekuona baada ya mimi kukuibua.
Na vile vile kwa wewe mwanamke nimekuinua sana kimaisha, kwa vile nakupenda.
Nikaendelea kumwambia kuwa nitaendelea kumpa support kwa elimu ya mtoto wangu.
Ila nikamsisitizia, ili nisiumie moyo sitamsumbua kwa lolote.
Na nikamwambia kumtakia heri, hata ndoa yake nitachangia, na nilifanya hivyo.
Maneno yalikuwa ni mazito na hata Clara alikuwa na masikitiko, ila hakuweza kujibu lolote la maana bali kusema wajomba ndivyo walivyo amua.
Clara alikuwa na mama yake tu, baba yake alifariki kitambo.
Tukaachana, na mimi nikaendelea na hamsini zangu.
Clara alioana na kijana mwenziwe na mimi wala sikutaka kwenda harusini licha ya kualikwa.
Niliona ndoa yao kwenye Facebook, wenyewe wakiwa na furaha tele.
Baada ya ndoa alinitumia ujumbe kuwa wanahamia Dar, lakini nikaona hayanihusu.
Mimi nikaendelea kufukuzia shilingi katika mishe mishe zangu jijini na kimsingi mambo yangu Alhamdulillahi yalianza kuwa poa.
Mimi kubadili fashion ya gari ilikuwa kama kawa, na kwa kweli nilimshukuru Mungu.
Ikapita zaidi ya mwaka na nusu, mie sina hili wala lile, mara nikapata simu, namba siifahamu.
Nikatuma ujumbe wa sms kuwa atume ujumbe, niko mkutanoni.
Ikapita saa nzima simu ile ikaita tena, nikaona hebu niipokee.
Ikaanza"mwanangu hujambo"
Nikamjibu "sijambo mama shikamoo , ninani anaongea?"
Akanijibu "mimi mama yako, mama yake Clara"
Nikaitazama simu na kushangaa!
Nikamuuliza kama ni wazima wa afya pamoja na mtoto wangu.
Akanijibu kuwa ni wazima, ila Clara alikuwa anaumwa tumbo lake lile alilofanyiwa operation.
Nikataka ampe pole Clara na kumtakia apone haraka.
Hapo ndipo mama Clara akafunguka.
"Mwanangu mimi mama yako nakuomba radhi kwa yote. Uniwie radhi sana, Clara ana matatizo makubwa na nisipokuarifu ili utusaidie tutampoteza. Uniwie radhi mwanangu hatukuelewa.
Mimi naongea na wewe ndugu zangu hawafahamu, naomba baba, naomba utusaidie"
Nikamwuliza mama sasa itakuwaje mimi kumhudumia mke wa mtu, na mumewe yupo.
Mama akasema yule kijana hana uwezo wowote, na ugonjwa wa Clara unahitaji specialist wa magonjwa ya wanawake, na kuwa hivi tunavyoongea kalazwa, na wako pamoja hospitali moja binafsi.
Duh...nikapigwa mkanganyiko.
Clara hatujaonana zaidi ya mwaka na ushee!
Sasa napata simu toka kwa mama yake!
Lakini nikasema nitaenda kumwona.
Nilipoingia chumba alimolazwa nilimkuta binti ambaye alitoka nje ,na mama Clara yeye kakaa pembeni .
Nikamsalimia mama na nikaenda kitanda alipo Clara.
Nikambusu shavuni, kwa upande nilimwona mama anainama huku akitabasamu.
Clara alifurahi ila uso ulikuwa na hali ya kuonyesha maumivu.
Nikaomba bili ya matibabu na nikawapa fedha zote.
Haraka haraka nikamwambia mama siwezi kukaa zaidi hapo maana nisijeshikwa ugoni!
Mama ajacheka akasema nisijali sana.
Nikaondoka.
Clara alikuja toka hospitali ila hakupona.
Tumbo liliendelea kumsumbua.
Sasa alipungua mwili akawa kama ufito.
Ilibidi kuwaona madktari bingwa ambao walisema tatizo kubwa ni ile operation ya kujifungua na operation iliyofuatia.
Madaktari waliomfanyua upasuaji hawakuwa na ujuzi wa kutosha.
Hata hizi operation zilizofanyika karibuni hazikuwa nzuri.
Hivyo wakashauri apelekwe India.
Kizungumkuti ni kwamba mume wake Clara hana kitu na familia yake nayo ni ya watu wa kawaida sana.
Nikabeba tena majukumu, Clara nikamgharimia akaenda India ambako alifanyiwa upasuaji tena.
Madaktari India walimwambia watafanya operation hiyo katika stage mbili. Mara ya kwanza walifanya operation nzito na wakamwambia inabidi apumzike miezi mitatu halafu arudi tena wammalizie operation ya mwisho.
Ikawa hivyo, na ndio kupona kwa Clara.
Tatizo nimemtibu mke wa mtu, lakini ni mama wa mtoto wangu.
Mwisho wa yote, alipopona sasa Clara nikasema kwa nini nisijaribu mitambo!
Na kwa kweli tukaitesti, tukarudi tulikokuwa zamani, lakini mimi bado mwizi!
Penzi likawa moto sana sana, mpaka bibie sasa akaniambia anataka mtoto mwingine!
Walimwengu niishie hapo.
Ushauri wenu tafadhali.