Ushauri wenu, dunia naona mviringo!

Ushauri wenu, dunia naona mviringo!

PART V
Wana MMU, haka kastori ni ka mtiririko wa miaka mingi.
Na nakaleta ili walimwengu muone mwanaume anavyoweza kuwa mjinga kwa penzi.
Mwanamke anakufunga kamba kwa kukupa uroda unaoweza kukupumbaza, wewe ukawa unampenda lakini yeye anakupenda just enough kupata kile anachokipata kwako.
Kama amekuchoka au ndo unaelekea down, kuna wanawake ni wajanja sana ku jump a sinking ship na kudandia nyingine.

Kitendo cha Clara kuolewa kilinikera haswa.
Lakini kabla hajaolewa niliongea naye kinaga ubaga.
Nilimwambia wewe Clara nilikutongoza ukiwa huna hili wala lile huko mkoani, ila ulichokuwa nacho ni ule uzuri wako natural ulioufunika katika nguo zisizo na hadhi.

Nikakuanzishia biashara, nikakununulia gari, umenona umependeza sasa unaniacha.
Nilimwambia mimi simjui na sitaki kumjua anayetaka kukuoa, ila ujue amekuona baada ya mimi kukuibua.
Na vile vile kwa wewe mwanamke nimekuinua sana kimaisha, kwa vile nakupenda.
Nikaendelea kumwambia kuwa nitaendelea kumpa support kwa elimu ya mtoto wangu.
Ila nikamsisitizia, ili nisiumie moyo sitamsumbua kwa lolote.
Na nikamwambia kumtakia heri, hata ndoa yake nitachangia, na nilifanya hivyo.

Maneno yalikuwa ni mazito na hata Clara alikuwa na masikitiko, ila hakuweza kujibu lolote la maana bali kusema wajomba ndivyo walivyo amua.
Clara alikuwa na mama yake tu, baba yake alifariki kitambo.


Tukaachana, na mimi nikaendelea na hamsini zangu.
Clara alioana na kijana mwenziwe na mimi wala sikutaka kwenda harusini licha ya kualikwa.
Niliona ndoa yao kwenye Facebook, wenyewe wakiwa na furaha tele.

Baada ya ndoa alinitumia ujumbe kuwa wanahamia Dar, lakini nikaona hayanihusu.

Mimi nikaendelea kufukuzia shilingi katika mishe mishe zangu jijini na kimsingi mambo yangu Alhamdulillahi yalianza kuwa poa.
Mimi kubadili fashion ya gari ilikuwa kama kawa, na kwa kweli nilimshukuru Mungu.
Ikapita zaidi ya mwaka na nusu, mie sina hili wala lile, mara nikapata simu, namba siifahamu.
Nikatuma ujumbe wa sms kuwa atume ujumbe, niko mkutanoni.

Ikapita saa nzima simu ile ikaita tena, nikaona hebu niipokee.

Ikaanza"mwanangu hujambo"
Nikamjibu "sijambo mama shikamoo , ninani anaongea?"

Akanijibu "mimi mama yako, mama yake Clara"
Nikaitazama simu na kushangaa!
Nikamuuliza kama ni wazima wa afya pamoja na mtoto wangu.
Akanijibu kuwa ni wazima, ila Clara alikuwa anaumwa tumbo lake lile alilofanyiwa operation.
Nikataka ampe pole Clara na kumtakia apone haraka.

Hapo ndipo mama Clara akafunguka.
"Mwanangu mimi mama yako nakuomba radhi kwa yote. Uniwie radhi sana, Clara ana matatizo makubwa na nisipokuarifu ili utusaidie tutampoteza. Uniwie radhi mwanangu hatukuelewa.
Mimi naongea na wewe ndugu zangu hawafahamu, naomba baba, naomba utusaidie"
Nikamwuliza mama sasa itakuwaje mimi kumhudumia mke wa mtu, na mumewe yupo.

Mama akasema yule kijana hana uwezo wowote, na ugonjwa wa Clara unahitaji specialist wa magonjwa ya wanawake, na kuwa hivi tunavyoongea kalazwa, na wako pamoja hospitali moja binafsi.

Duh...nikapigwa mkanganyiko.
Clara hatujaonana zaidi ya mwaka na ushee!
Sasa napata simu toka kwa mama yake!
Lakini nikasema nitaenda kumwona.
Nilipoingia chumba alimolazwa nilimkuta binti ambaye alitoka nje ,na mama Clara yeye kakaa pembeni .
Nikamsalimia mama na nikaenda kitanda alipo Clara.
Nikambusu shavuni, kwa upande nilimwona mama anainama huku akitabasamu.
Clara alifurahi ila uso ulikuwa na hali ya kuonyesha maumivu.
Nikaomba bili ya matibabu na nikawapa fedha zote.
Haraka haraka nikamwambia mama siwezi kukaa zaidi hapo maana nisijeshikwa ugoni!
Mama ajacheka akasema nisijali sana.
Nikaondoka.

Clara alikuja toka hospitali ila hakupona.
Tumbo liliendelea kumsumbua.
Sasa alipungua mwili akawa kama ufito.

Ilibidi kuwaona madktari bingwa ambao walisema tatizo kubwa ni ile operation ya kujifungua na operation iliyofuatia.
Madaktari waliomfanyua upasuaji hawakuwa na ujuzi wa kutosha.
Hata hizi operation zilizofanyika karibuni hazikuwa nzuri.
Hivyo wakashauri apelekwe India.
Kizungumkuti ni kwamba mume wake Clara hana kitu na familia yake nayo ni ya watu wa kawaida sana.

Nikabeba tena majukumu, Clara nikamgharimia akaenda India ambako alifanyiwa upasuaji tena.
Madaktari India walimwambia watafanya operation hiyo katika stage mbili. Mara ya kwanza walifanya operation nzito na wakamwambia inabidi apumzike miezi mitatu halafu arudi tena wammalizie operation ya mwisho.

Ikawa hivyo, na ndio kupona kwa Clara.

Tatizo nimemtibu mke wa mtu, lakini ni mama wa mtoto wangu.

Mwisho wa yote, alipopona sasa Clara nikasema kwa nini nisijaribu mitambo!
Na kwa kweli tukaitesti, tukarudi tulikokuwa zamani, lakini mimi bado mwizi!
Penzi likawa moto sana sana, mpaka bibie sasa akaniambia anataka mtoto mwingine!

Walimwengu niishie hapo.
Ushauri wenu tafadhali.
 
Aisee...mi sina neno we kama unaendelea kuchakat chakata tuu na kama unaamua kuacha we acha tuu...
 
Hongera Sana kwanza kwa moyo huo
Hata ukichakata ni haki Kwanza ni mzaz mwenzako
Ila huyo dem anawenge angetulia na wewe tuu taamaa kama fis imemponza

Inamaana usinge ingilia kati angekufaa
Ushaur wangu usizae nae we endelea kula mbususu tuu
Usikubali kuzaa nae maana yupo kwenye ndoa huyo

Tomba tuu bas tena mama yake anajua!!!!!
Yaan we tomba tuu bas
 
Dah! Hspa mbona haya ni maradhi ya kawaida kabisa kwa wanaume mkuu?

Huyo mzazi mwenzio anakupenda sema tamaa na gubu vimemponza. Tukirudi kwenye maadili huyo Mama yake Clara na Clara mwenyewe sio watu wa ndoa, wangelitambua hilo wala asingehangaika na ndoa, ingekua una mke asiye rasmi.

Wife hajawahi kushtukia hata kwa mbali tu kwamba umezama sehem kwa Clara?
Yaani haijawahi kabisa kukuletea tafran kwenye familia yako? Kama jibu ni ndio itabidi ufungue tuisheni tuje kupata somo.

Ntatoa ushauri baadae sasa hivi ngoja kwanza tumalize jambo na Evelyn Salt
 
Kama bibilia inavyosema tu "Ndoa na iheshimiwe na watu wote" bhasi kwakua clara alishaolewa usingerudisha mahusiano nae tena ila ungebaki kama mwanaume uliezaa nae tu na heshima iwepo...
ukiheshimu ndoa yako na yake pia ndipo heshima yako itakapo onekana na kuheshimika pia.... ila huku unapoelekea mkuu unaenda dhalilika na kushuka heshima
 
Kila chenye mwanzo hakikosi mwisho....kikubwa aolewe ila uendelee kumega kama vp. Mchumba wake anakufaham?
 
Kama bibilia inavyosema tu "Ndoa na iheshimiwe na watu wote" bhasi kwakua clara alishaolewa usingerudisha mahusiano nae tena ila ungebaki kama mwanaume uliezaa nae tu na heshima iwepo...
ukiheshimu ndoa yako na yake pia ndipo heshima yako itakapo onekana na kuheshimika pia.... ila huku unapoelekea mkuu unaenda dhalilika na kushuka heshima
Lakini familia iliyomuoza ikarudi kwangu kwa msaada wa matibabu. Mi nilishasepa.
 
Kila chenye mwanzo hakikosi mwisho....kikubwa aolewe ila uendelee kumega kama vp. Mchumba wake anakufaham?
Ningeendelea Part VI lakini nangoja yaliyojiri.
Kimsingi na mimi sipendi kummega bibie aliyenisare ingawaje tumezaa.
Jamaa hatujawahi onana.
 
Dah! Hspa mbona haya ni maradhi ya kawaida kabisa kwa wanaume mkuu?

Huyo mzazi mwenzio anakupenda sema tamaa na gubu vimemponza. Tukirudi kwenye maadili huyo Mama yake Clara na Clara mwenyewe sio watu wa ndoa, wangelitambua hilo wala asingehangaika na ndoa, ingekua una mke asiye rasmi.

Wife hajawahi kushtukia hata kwa mbali tu kwamba umezama sehem kwa Clara?
Yaani haijawahi kabisa kukuletea tafran kwenye familia yako? Kama jibu ni ndio itabidi ufungue tuisheni tuje kupata somo.

Ntatoa ushauri baadae sasa hivi ngoja kwanza tumalize jambo na Evelyn Salt
Ulichoandika kweli kabisa.
Mpaka leo sielewi kwa nini Clara aliingia ndoa.
Kwa kawaida wanawake wakisha ingia matawi fulani kuolewa na mtu asiye na uwezo na yeye ni tegemezi, inakuwa ngumu.

Ila simlaumu mama kwa kunirudia kwa msaada wa matibabu.
Tungweza kumpoteza Clara na bado ingekuwa hasara kwangu na mwanangu.

Familia yangu bado haifahamu soo hili.
 
Ulichoandika kweli kabisa.
Mpaka leo sielewi kwa nini Clara aliingia ndoa.
Kwa kawaida wanawake wakisha ingia matawi fulani kuolewa na mtu asiye na uwezo na yeye ni tegemezi, inakuwa ngumu.

Ila simlaumu mama kwa kunirudia kwa msaada wa matibabu.
Tungweza kumpoteza Clara na bado ingekuwa hasara kwangu na mwanangu.

Familia yangu bado haifahamu soo hili.

Wewe tunakupa cheo cha ukufunzi! Wengine wakiwa hatua za awali kabisa, yani pale mwanzoni mwanzoni tu hali ya hewa inachafuka makao makuu kwa kukamatwa. Nashangaa wewe umeogelea mikasa yote hiyo na bado umevuka.

Sasa Jemedari, najua itakua ngumu sana kunielewa na sio rahisi (Hapa naongea kama mwanaume) haitakua kazi rahisi sana kukaa mbali na huyo mwanamke (Mzazi mwenzio.

Kwamba umeshakwepa mishale mingi sio kesi sana, ila nnachokuhakikishia, siku wife akigundua na ikaleta tafrani, hautakaa utulie na akili itakurudi. Ni fedheha sana watu wazima kuanza kukaa kukujadili kwa kesi ya michepuko. Na kitakachomuuma zaidi wife sio kuzaa mtoto, ni ile mnaendelea.

Kwa akili zetu wanaume zilivyo, hiyo hali ilivyo na ulivyomgharamia imeongeza sana intimacy kati yenu, sio rahisi kuzinduka kwa sasa ila inabidi ufanye maamuzi magumu. Hapo ulipo ukimuwaza Clara kidogo na mambo mliyopitia ni dakika moja tu unafunga safari kwenda kumuona.

Itakuathiri kwa muda kusitisha mahusiano na Clara, lakini utajenga msingi imara wa future yenu wote. Kumbuka hadi hapo Clara hana cha kupoteza kuendelea na wewe, hata huyo mme wake sifikirii anamjali au kuona ni tatizo. Lakini kwako vitu vingi vipo hati hati.

Pamoja na maongezi yote hayo...bado mpango wetu na Evelyn Salt uko pale pale.
 
Wewe tunakupa cheo cha ukufunzi! Wengine wakiwa hatua za awali kabisa, yani pale mwanzoni mwanzoni tu hali ya hewa inachafuka makao makuu kwa kukamatwa. Nashangaa wewe umeogelea mikasa yote hiyo na bado umevuka.

Sasa Jemedari, najua itakua ngumu sana kunielewa na sio rahisi (Hapa naongea kama mwanaume) haitakua kazi rahisi sana kukaa mbali na huyo mwanamke (Mzazi mwenzio.

Kwamba umeshakwepa mishale mingi sio kesi sana, ila nnachokuhakikishia, siku wife akigundua na ikaleta tafrani, hautakaa utulie na akili itakurudi. Ni fedheha sana watu wazima kuanza kukaa kukujadili kwa kesi ya michepuko. Na kitakachomuuma zaidi wife sio kuzaa mtoto, ni ile mnaendelea.

Kwa akili zetu wanaume zilivyo, hiyo hali ilivyo na ulivyomgharamia imeongeza sana intimacy kati yenu, sio rahisi kuzinduka kwa sasa ila inabidi ufanye maamuzi magumu. Hapo ulipo ukimuwaza Clara kidogo na mambo mliyopitia ni dakika moja tu unafunga safari kwenda kumuona.

Itakuathiri kwa muda kusitisha mahusiano na Clara, lakini utajenga msingi imara wa future yenu wote. Kumbuka hadi hapo Clara hana cha kupoteza kuendelea na wewe, hata huyo mme wake sifikirii anamjali au kuona ni tatizo. Lakini kwako vitu vingi vipo hati hati.

Pamoja na maongezi yote hayo...bado mpango wetu na Evelyn Salt uko pale pale.
Dah....we bro nashukuru kwa kunielewa.
 
Daah pole sana ndgu, wewe ni mkristo eeh?? Nadhani ungekua dini nyingine ungemuoa huyo bibie mke wa pili.

Mara ya kwanza nilidhani ni chai ila imenishawishi kuiamini na umeanzia mbali mkuu, sidhan km kuna mtu hataelewa hii situation yako.

Yote kwa yote na mimi naungana na jamaa hapo alosema fanya maamuzi magumu ua kumtema huyo mke wa mtu.
Hata kama mchizi wake hana kipande ila kumlia mkewe sio fresh kabisa na hata ivo mkeo akijua hilo varangati lake si la kitoto.
Kama ashapona na biashara zake zinaenda poa haina haja ya kuanza maisha mapya ya kujifichaficha ili mle vyenu huku mkiharibu ndoa zenu nyote 2.
 
Daah pole sana ndgu, wewe ni mkristo eeh?? Nadhani ungekua dini nyingine ungemuoa huyo bibie mke wa pili.

Mara ya kwanza nilidhani ni chai ila imenishawishi kuiamini na umeanzia mbali mkuu, sidhan km kuna mtu hataelewa hii situation yako.

Yote kwa yote na mimi naungana na jamaa hapo alosema fanya maamuzi magumu ua kumtema huyo mke wa mtu.
Hata kama mchizi wake hana kipande ila kumlia mkewe sio fresh kabisa na hata ivo mkeo akijua hilo varangati lake si la kitoto.
Kama ashapona na biashara zake zinaenda poa haina haja ya kuanza maisha mapya ya kujifichaficha ili mle vyenu huku mkiharibu ndoa zenu nyote 2.
Asante sana.
Ni kwa vile nimeishia hapo nilipoishia, lakini matibabu ya kuokoa maisha ya Clara na misaada mingine haijamfurahisha jamaa.

Sijutii kuokoa maisha ya Ckara.

Mi niko pembeni, ila hata Clara kanidokeza jamaa anataka talaka.
Hiyi Part VI bado inajifunua.
 
Back
Top Bottom