Ushauri wako ni muhimu zaidi kwangu

Ushauri wako ni muhimu zaidi kwangu

Shikamoo dada gfsonwin,
ama baada ya salamu nikuulize kwa nini mimi sijaitwa? Halafu tangu nirudi mjini sijakuona...u hali gani???!

BACK TO TOPIC...
Namfahamu mmama mmoja ambaye hakuolewa tena tangu mumewe amuache, hadi leo ana matumaini mumewe atarejea. Sijawahi kuelewa mental psychology ya mwanamke ila nikiwaza huyo mama anachofikiria kumtegemea mumewe 10+ years after amemuacha na watoto (halafu watatu..coincidence!!!???) sipati jibu.

My thought ni...kama huyo DB (BD?) anakuja aje...wakae tu pamoja waongee tena, kwa kirefu...amweleze hofu yake...wahenga wanasema 'two heads are better than one'. wakikaa pamoja wakaongea nadhani watapata suluhisho.

From there filing for divorce na mengine yatafuata.

Hofu yangu tu ni mwanamke ambaye bado ana mapenzi kwa mtu mwingine -in my view - ni hatari kuliko mwanaume mwenye mapenzi na mtu mwingine. Ni heri angebaki single tu kuliko kumuingiza DB (BD?) kwenye maumivu kama aliyonayo yeye.

Ni hayo tu...!

Cc: Paloma Watu8 ....

Ahsante sana ndugu kwa usahuri wako huu.
Mie lakini bado sijampa DB go ahead manake pia wanangu sijui nitawaambia nini jamani
 
Mmmmmmmmmmmmh! KUNA APPROACH 2 HAPO!

1. KATE MIDLETON APPROACH! Hii ilimlipa sanaa Kate, hii unatuliza mpapa tuliiiiiiiiiiiii kama unanyolewa vuzi mpaka hio siku isio na jinaaa atakaporudi huyo mume. Believe atarudi even fter 10 years. Mungu anajibu japo kwa kuchelewa mda mwingine lakini anajibuuu. Akirudi hio siku iso na jina na kukuta umekituliza mambo byeeeeeeeeeeee! Akikuta umekitembeza ana ghairi. Kate aliachana na prince akakituliza tuliiii, wenzie wanaolewa miaka ishirini na ngapi huko yeye anafukuza upepo wa prince tu, siku iso na jina ikafika bwanaa. Angtia tamaa kujichulia looser si ingekula kwake?

2. MTAANI UNTD! Hii unakuwa a woman of double faces. Huku kwa wanao kujua unajitia kuendelea kumngoja mumeo kwa unyonge, huku kwa bwana BD mnakandamiza mavituz kama kawaidaaaaaaaa. Kwa raha zenu. Unacheza ligi international! Dubai, South, Nairobi hivo yani. Unapata kitu roho inapenda huku unafukia tracks zako. Siku iso na jina ikifika kama sio yule uliejiachia na boloyanki la DB! Hahahaaaaaa! HII NI WIN WIN! Ila usiwe mzembe tu, na uwe na roho ya korosho hubby akirudi unamuangalia usoni kama sio yule ulieshika mic ya DB! Hahahaaaaaaaaaaa!

Hahahaha!! Mdogo wangu lara1 unafiki huu wa wanauweza malegend kama wewe hapa unaweza ukaharibu MTU kabisa akamkosa DB na hubby kabisaa mwisho hata mambo mengine ya maisha akashindwa kuyaendesha kabisaa!!!
 
Last edited by a moderator:
Maisha ya Ndoa/mahusiano yoyote yana wakati mzuri na wakati mbaya.yana changamoto zake ambazo hatuna budi kukabiliana nazo.
nashauri asifanye maamuzi ya haraka kumkubali huyu mtu.nikiongezea tu wengine walivyosema--
1. lazima ajue nia ya dhati kabisa ya huyo bwana DB, yawezekana pengine pia ana janja yake tu ndio maana anampelekesha kwa kasi namna hiyo. Yaani ana uhakika 100% kwamba DB hana mchepuko mwingine huko aliko hata kama mkewe alikufa. isije akaruka jivu akakanyaga moto.
2. Jingine sasa asiwe kimya-Dada aongee suala hili sasa kwa uwazi kabisa na familia zote mbili upande wake na wa mumewe, ili wafike muafaka ambao baadae utamsaidia.
3. Jingine ni watoto wake-aongee nao ikiwa ni wakubwa aone jinsi gani pia watalichukulia suala hili.Naamini atakuwa na watoto wenye zaidi ya miaka 15, aongee nao aone jinsi gani wataweza kumkubali huyu 'baba mpya'. Nafasi yao, ikitokea mama analazimika kuhamia huko kwa 'mumewe mpya' watoto mustakabli wao utakuwaje
4. Pamoja na kuwa mama utakuwa unatafuta kujipa raha mwenyewe 'kupendwa'-ambayo ni haki ya kila mtu kupendwa; lakini lazima uwafikirie na wengine. Na hapa tunasemea watoto wake. Lazima pia ufikirie mwisho wao, na si kuwasambaratisha. Watoto wengi wakiishajielewa hata kama wanabaki na mama tu bila kuingiliwa ingiliwa na akina baba wageni wanaweza kuwa na mustakabali mzuri wa maisha.
5. Lazima ujue pia kwamba jambo lolote linalokupata, linakupata kwa wema-it happens for good. Pengine sasa ni muda muafaka sana wa kumrudia MUNGU wako na kuomba uongozi wake kwa kila uamuzi unaotaka kufanya kwa furaha yako, wanao, na uwapendao-wa zamani na mpya
5. Akili za mbayuwayu changanya na za kwako. Mapenzi yana nguvu ya ajabu. Mapenzi ni upofu, huoni wala huambiwi kitu ukishapenda.inawezekana umeshafika kweny point of no return, na watu wakawa wanashauri hakuna linaoingia
 
Yaani wewe hao wakwe ambao wananiona kila siku nahangaika na wajukuu zao. Halafu mtoto wao amekuja na mie nikasikia tu mtaani (tena wala hawajaniambia wao wala kuniita nimshuhudie), halafu isitoshe huyo mtoto wao alikuja na wakakaa nae wala hawajamuona akija na wanae wala mimi. Wanapewa taarifa kivipi, kwa barua, kwa email ama niende na kitenge na sukari kuulizia kama mtoto wao bado ni mume wangu?:heh::heh:
Mi naona DB asipewe nafasi bila taarifa, taarifa ninayoiongelea hapa, ni wewe kwenda kwa wazazi wa mume wako na kuwajulisha situation ya ww na mumeo kwa kipindi chote, na kama pia unampenda DB basi ni wakati muafaka wa mumeo kukupa talaka kwasababu katika hali ya kawaida ata kama ndoa za kanisani hawaachani lakini still huwezi kukaa na mume katika maisha ya ukatili, mume hajui watoto wake wala mkewe hiyo sio kweli, so take advantage ya kumwagana kabisa na huyo Hubby umpendae na amishia feelings kwa DB inawezekana DB akawa faraja na pumziko la moyo wako, wanaume wa bongo wengi wakienda Ulaya wanaishia kwa style hiyo sijui ni ulimbukeni au upuuzi, lakini mwisho wasiku wanarudi kupiga magoti, hivo unampigiaje magoti mwanamke uliemjeruhi kiasi hiki? atakusamehe lakini hayataisha kichwani kuna mambo mengine psychologically hayaondokagi kichwani na yanajenga chuki sana ukiyakumbuka, my advise ni kuwa lazima uweke clear upande wa mumeo ndio uanze maisha na DB ili kuhepuka maneno, maana hapo yatasemwa mengi ya mtoto wao hayatoonekana


Kwani mtoto wao alipokuja hawakusema maneno? Khaaa!
 
Ndugu yangu ninahitaj faraja jamani, hebu niambie for 5 yrs mtu amekuwa nje, na katika miaka iyo amewah kurudi nchini kuonana na mie mara 2 tu na kwa maiaka 3 hana mawasiliano na mie kabisaa. Ivi kweli hata yale mahaitaj ya kimwili pesa zitanisaidia nini?

Nina fanya kazi sehemu nzuri sana niasafiri kila mwezi nje ya nchi nalala mahoteli makubwa nakutana na watu wa kila aina ivi nisipokuwa na wangu si ndio nitajikuta natembea na kila ninayekutana naye kwenye mikutano sijui ama mahotelini?

Mumy kumbe unajua unachokihitaji kwanini ujipe mateso follow your heart lakini kuwa tayari kwa lolote litakalotokea.......

Kwenye maelezo yako kuna mahali mahali umesema ulijarib kuwa na mchepuko lakini ukaipiga chini unafikiri nini kilifanya uachane na mambo hayo?
 
Kwani huyo DB imeshaonekana anafaa ama anataka commitment kwa matendo? Kabla ya kuamua kuwa na DB kuna haja ya kumuobserve etc. Hapa nilitegemea approach ya kufanyaje usitapeliwe mapenzi.

Huyu baba why anataka aandikiwe email kuwa anatakiwa aende kwa bibie? Yeye sio mtoto mdogo, akitaka kwenda kwa gf wake si anachukua likizo ofisini na anatafuta visa anaenda kumuona? Why mambo ya emails za ofisi? Mie siamini katika wanaume wote waliowahi kumtongoza huyu toka huyo looser apotee kwa vijisenti vyake kuuguza mwanae, kuwa huu ndio uamuzi mgumu. By the way alishawahi chepuka akaona myeyusho akapiga chini (she aint a virgin). Halafu hiyo excuse ya atawaambia nini wanae, kwani anashindwa kudate huku analea watoto? Single mothers hawatoki?Wooi:eyebrows::eyebrows:

Sasa akienda kumripoti ubalozi anaenda kusema nini? Kuwa hampendi, hamtaki, hatumi matumizi ama? Stress za kujidhalilisha manake dada yuko swaafi financially. Huyo looser akafilie mbele huko, mie wala ningekutana nae barabarani ningemsalimia ili anione ila nisingempa hata dakika 5 za kunipotezea

ivi sasa King'asti unategemea nini akisema ajicommit kwa DB ?
hebu niambie kwa jinsi alivyosema ni wazi wanawe ni wakubwa atawaambia nini?? Lakin jamani muda mwingine anahitaj tu kuwa huru, ayafurahie maisha yake yeye kama yeye, kama kweli mume hana mawasiliano na watoto, kwa muda wote huo tusemeje sasa??
BTW ivi akienda kumripoti kwa dawati la wanawake ubalozi wa nchi aliyopo hauwez kumsaidia??
aaarrgggggggggggghhhhhhh.....................jamani aachanae nae tuu kama alivyoachwa akajianzie maisha yake.

(sijui hata kama nimeeleweka manake nimeandika kama naongea vile)
 
Mumy kumbe unajua unachokihitaji kwanini ujipe mateso follow your heart lakini kuwa tayari kwa lolote litakalotokea.......

Kwenye maelezo yako kuna mahali mahali umesema ulijarib kuwa na mchepuko lakini ukaipiga chini unafikiri nini kilifanya uachane na mambo hayo?

HAhah besti, anachokihitaji huyu wala hakiendani na moyo....moyo wake unamtuma kwa 'mumewe' mwili wake unamtuma kwa 'DB (BD?)'...see where the problem lies!??

Angekuwa mwanaume ingekuwa rahisi sana kumshauri..sema nyie wadada bwana, saikolojia yenu iko so different! As a man, unachukua moyo unafungia kabatini mnaanza misele na huyo DB (BD?)...hata akirudi huyo 'mumewe' hakuna msamaha cha maana tu wanae wamwone...moyo usiutoemo huko kabatini tena...Life is too short to give it to some individual to destroy it!!!!
 
Chiomaizwe, good luck and all the best in your decision making process. It's my hope that you'll be able to make the right decision for you and your kids.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu yangu ninahitaj faraja jamani, hebu niambie for 5 yrs mtu amekuwa nje, na katika miaka iyo amewah kurudi nchini kuonana na mie mara 2 tu na kwa maiaka 3 hana mawasiliano na mie kabisaa. Ivi kweli hata yale mahaitaj ya kimwili pesa zitanisaidia nini?

Nina fanya kazi sehemu nzuri sana niasafiri kila mwezi nje ya nchi nalala mahoteli makubwa nakutana na watu wa kila aina ivi nisipokuwa na wangu si ndio nitajikuta natembea na kila ninayekutana naye kwenye mikutano sijui ama mahotelini?

Huyo mpya na yeye yuko ng'ambo siyo? mtakuwa mnafanya kwa viber?
 
Kwani huyo DB imeshaonekana anafaa ama anataka commitment kwa matendo? Kabla ya kuamua kuwa na DB kuna haja ya kumuobserve etc. Hapa nilitegemea approach ya kufanyaje usitapeliwe mapenzi.

Huyu baba why anataka aandikiwe email kuwa anatakiwa aende kwa bibie? Yeye sio mtoto mdogo, akitaka kwenda kwa gf wake si anachukua likizo ofisini na anatafuta visa anaenda kumuona? Why mambo ya emails za ofisi? Mie siamini katika wanaume wote waliowahi kumtongoza huyu toka huyo looser apotee kwa vijisenti vyake kuuguza mwanae, kuwa huu ndio uamuzi mgumu. By the way alishawahi chepuka akaona myeyusho akapiga chini (she aint a virgin). Wooi:eyebrows::eyebrows:

Hahahahahahaha!! Kwahiyo aendelee kukitembeza kwa DB tu??😉 halafu huyu DB hata mimi ananipa mashaka sana inamaana yeye ameshindwa kweli kuomba likizo na maujanja yote mpaka kuutangazia uma wote anaenda kwa bibie? Kuna nyuma ya pazia ya DB, haki ya nani kuna wanaume wanajua kuvuta attention ya mwanamke yaani unajiona bongeee la malkia kumbe ana yake!!!!!
 
Huyo BD sijui nani nae asikupeleke mbio bwana. Why anataka kuoa haraka haraka, ana nia gani? Na huko kazini kwake unamuombea ruhusa ya kuja kuoa ama? si achukue likizo aje muonane? you should date kwanza na kujuana vizuri, muangalie kama ataclick na wanao pia. Baadae ufanye mpango wa talaka ndio muoane. Umri huo utakimbizwaje na masuala ya ndoa bibie, chuo cha pili hakina haraka.

Kuwa muangalifu wanaume wengi wanakujaga na gia ya ndoa akishakutumia aingie mtini.
uhakika ya kwamba mume wangu kaoa ninao toka kwa dada yake alompokea alipokujaga pamoja na rafiki yake walikwendaga wote masomoni lakin yeye amesharusi baada ya kumaliza.

DB yuko na haraka sana manake hapa nilipo anataka kuja Tanzania kuniona na kuwaona wazazi wangu ili aoe kabisa na yeye tayari kesha nitumia email ya kampuni yake ili nimuombee ruhusa
 
Kwani huyo DB imeshaonekana anafaa ama anataka commitment kwa matendo? Kabla ya kuamua kuwa na DB kuna haja ya kumuobserve etc. Hapa nilitegemea approach ya kufanyaje usitapeliwe mapenzi.

Huyu baba why anataka aandikiwe email kuwa anatakiwa aende kwa bibie? Yeye sio mtoto mdogo, akitaka kwenda kwa gf wake si anachukua likizo ofisini na anatafuta visa anaenda kumuona? Why mambo ya emails za ofisi? Mie siamini katika wanaume wote waliowahi kumtongoza huyu toka huyo looser apotee kwa vijisenti vyake kuuguza mwanae, kuwa huu ndio uamuzi mgumu. By the way alishawahi chepuka akaona myeyusho akapiga chini (she aint a virgin). Halafu hiyo excuse ya atawaambia nini wanae, kwani anashindwa kudate huku analea watoto? Single mothers hawatoki?Wooi:eyebrows::eyebrows:

Sasa akienda kumripoti ubalozi anaenda kusema nini? Kuwa hampendi, hamtaki, hatumi matumizi ama? Stress za kujidhalilisha manake dada yuko swaafi financially. Huyo looser akafilie mbele huko, mie wala ningekutana nae barabarani ningemsalimia ili anione ila nisingempa hata dakika 5 za kunipotezea

Huu ndo mwiba wa kijidunga.
DB kiukweli mpaka sasa japo kanitumia na iyo Email niwaandikie ofsin kwao kwamba namuhitaj lakni sijaweza kufanya ivyo manake sijielewei to be frank.
Pia kanipa adi hadi namba ya mwanae nimpigie simu sijui nisalimie blah blah nyingiii nikasema nitampigia though bado.

Approach zote hisi na apply delaying technique manake sijielewi niamue nini. Nashuru sana japo hizi sindano zinauma lakin zinanitibu kimtindo.
 
HAhah besti, anachokihitaji huyu wala hakiendani na moyo....moyo wake unamtuma kwa 'mumewe' mwili wake unamtuma kwa 'DB (BD?)'...see where the problem lies!??

Angekuwa mwanaume ingekuwa rahisi sana kumshauri..sema nyie wadada bwana, saikolojia yenu iko so different! As a man, unachukua moyo unafungia kabatini mnaanza misele na huyo DB (BD?)...hata akirudi huyo 'mumewe' hakuna msamaha cha maana tu wanae wamwone...moyo usiutoemo huko kabatini tena...Life is too short to give it to some individual to destroy it!!!!

Hahahaha!!! Ni kweli kwa sisi wanawake ni mgumu katika hili na tunaweza haribu kabisa tukakosa yote, basi moyo uko kwa mumewe aendelee tu kumngoja kama tunavyomngoja Yesu tukiamini atarudi hakika huyu ajibuye kwa moto atamjibu tu na siku isiyo na jina baba watoto wake atarudi,wanasema mateso yakizidi ndipo Neema huja......
 
Huyo BD sijui nani nae asikupeleke mbio bwana. Why anataka kuoa haraka haraka, ana nia gani? Na huko kazini kwake unamuombea ruhusa ya kuja kuoa ama? si achukue likizo aje muonane? you should date kwanza na kujuana vizuri, muangalie kama ataclick na wanao pia. Baadae ufanye mpango wa talaka ndio muoane. Umri huo utakimbizwaje na masuala ya ndoa bibie, chuo cha pili hakina haraka.

Kuwa muangalifu wanaume wengi wanakujaga na gia ya ndoa akishakutumia aingie mtini.
Hapa ndipo na mie panapo nipa mashaka yaani nataman ningekuwa naweza kuonyesha mawasiliano yangu na yeye hapa ila basi tu siwez kufanya hivyo.
Mie najua kila jambo huwa lina muda wake wa kukua, na sasa sitaki kukimbizwa manake huo mguu wa kati mbona sio ishu sana ikiwa hakuna mapenzi ya kweli?
Mchana huu nimemwabia in one of the chats kwamba anaposema aje anioe such urgently je mie carrier yangu naitupa wapi? Nimemwambia kama yuko radhi abaki TZ anasema haijui vyema Tz so angependa tukaish kwenye nchi yao, ....................:mmph:
Nikamwambia unless nime secure kazi kwenye gas&oil drilling company ndo nitanyunyua mguu wangu hapa Tz. Though hajaipenda hii kauli as he is claiming that I don't trust his love and all those shits ...............lakin bado naona ugumu hasa kwamba mie nina familia yeye mwenzangu hana so he has nothing to lose.

Ana demand kuandikiwa email simply kwasabb kwenye geocompany yao wana respect zaid women concerns especially socially related na mie ilo sio tatizo kwangu ila its too early kwa mimi kujicommit in such a way.
 
Kuwa na relationship ni kukitembeza? Miaka 5 bila bila atatia aibu sasa hivi (kuna mtu unaangalia matendo tu unajua huyu ana sexual deprivation hehehe).

Ndio maana mie sitaki tuangalie habari ya huyo looser mpotevu wala ndoa. Kama unamdate mtu kuna hatua za uhusiano. Hao wanae nao wanamisi kuwa na baba nyumbani bwana. Ila bibie aende taratibu, wajuane kiswahili. Hii mambo ya kutongozana asubuhi na kuoana saa mbili usiku mie sitaki. Lazma ukanyagie miaka 4, wa tano ndo nakupa jibu afu wa sita tuoane (@platozoom umebakisha miaka 4 sio?)
Hahahahahahaha!! Kwahiyo aendelee kukitembeza kwa DB tu??😉 halafu huyu DB hata mimi ananipa mashaka sana inamaana yeye ameshindwa kweli kuomba likizo na maujanja yote mpaka kuutangazia uma wote anaenda kwa bibie? Kuna nyuma ya pazia ya DB, haki ya nani kuna wanaume wanajua kuvuta attention ya mwanamke yaani unajiona bongeee la malkia kumbe ana yake!!!!!
 
Mumy kumbe unajua unachokihitaji kwanini ujipe mateso follow your heart lakini kuwa tayari kwa lolote litakalotokea.......

Kwenye maelezo yako kuna mahali mahali umesema ulijarib kuwa na mchepuko lakini ukaipiga chini unafikiri nini kilifanya uachane na mambo hayo?
Its definitely true that every woman needs happiness, love, care and respect. Cross puzzle comes when a new man pops in. Huwez kujua uchague lipi. Hasa ukikumbua ule msemo usemao umekimbilia kulia ukakuta kushoto kumebomoka...........
Nimejiuliza maswali mengi sana nikaishia kucheka manake rafiki yangu mmoja alikuwa anasoma hizi comments apa akaniambia bibie ....................................'Uzuri wa mkakazi ndani kipande cha mti"

Na nikifikiria zaid "a rolling stone gathers no moss " nashindwa kuchagua
 
Kuwa na relationship ni kukitembeza? Miaka 5 bila bila atatia aibu sasa hivi (kuna mtu unaangalia matendo tu unajua huyu ana sexual deprivation hehehe).

Ndio maana mie sitaki tuangalie habari ya huyo looser mpotevu wala ndoa. Kama unamdate mtu kuna hatua za uhusiano. Hao wanae nao wanamisi kuwa na baba nyumbani bwana. Ila bibie aende taratibu, wajuane kiswahili. Hii mambo ya kutongozana asubuhi na kuoana saa mbili usiku mie sitaki. Lazma ukanyagie miaka 4, wa tano ndo nakupa jibu afu wa sita tuoane (@platozoom umebakisha miaka 4 sio?)

You have said it all correct...............no need to rush ila sasa mtego uko hapa................
life is not certain my dear...................I may say let me wait, but what if tomorrow wont come? Na je kwa umri huu do I need to act like a virgin girl? kwamba niwe na kihere here cha ndoa??
I cant make proper decision at this moment.
 
Sasa iyo L.M.A hairuhusu na mie ninavyo vyeti vya ndoa hapa nilipo manake hakuondoka navyo lakin je nitasaidika vipi ikiwa ndo amesha zamia huko na huyo mwanamke mwingine? Natamani arudi nyumban hata leo.
DB ukweli japo ndo ivyo sijampa msimamo wangu lakin ukweli amekuwa akinishauri vingi sana na hasa juu ya hatma ya hii ndoa yangu manake yeye amesema kama kaoa basi na wewe nikuoe kwakua hatuna haja ya watoto wengine tulepo maisha basi.

Ugumu kwangu mpendwa wangu unakuja kwa wanangu, ivi ninaanzaje kuwaambia kwamba nimeachana na baba yao na sasa watalelewa na baba mwingine?

hamna ndoa hapo kati yako na mmeo
maana for five yrs ht hamu na watoto hana duh huyo ni mme wa aina gani sasa
na hao ndg zake hasa huyo dada ni mnafki kawezaje kukaa na kaka ake alivyokuja TZ badala ya kumshauri aende kwa mkewe
mi nakushauri omba talaka najua wampenda ila ndo hakupendi mama we utajipa moyo atarudi atarudi lini...?
hao watoto wataelewa tu
maana hapo we umebaki unaongezeka uzito wa mwili tu kwa kuvaa pete ya gold ya ndoa
mi ushauri wangu fanya yako "people learn to live"
 
Kuwa muangalifu wanaume wengi wanakujaga na gia ya ndoa akishakutumia aingie mtini.

Madam King'asti naomba urekebishe hapo bold!!!!

Wanaotumia ni yule anakukopa hadi nauli na pesa za gesti..wa huku uswahilini kwetu! Huyo ambaye ku-do mnaenda Serena utasema anakutumia kweli!???
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom