Ushauri wako ni muhimu zaidi kwangu

Ushauri wako ni muhimu zaidi kwangu

Bila shaka huyo mumeo yuko JF na anausoma huu ujumbe. Ni matumani yangu kuwa atakujibu
 
Ahsante sana ndugu kwa usahuri wako huu.
Mie lakini bado sijampa DB go ahead manake pia wanangu sijui nitawaambia nini jamani

dada pole sana!
kwa ushaur mdogo tu!
kwa nafasi uliyonayo sasa kimaisha naamin unaweza safar popote dunian!

mruhusu bwana DB aje ila kwa kushauriana yafutayo:- (ILI ASIKUONE UNAMAMBO MENGI)
1:-Mwambie kwa kipindi chote kuna uliyo yasikia juu ya mme wako lakn unahitaji kuthibitisha ili ujue maamuz yako hayatoleta maumivu kwa mwingine

2:- unahitaji kuwaandaa watotot kisaikolojia ili wasiumie watakapoanza kuona mazingira mengine ( kama maamuzi yenu yatafikia huko)

3: hapa ndo muhimu!
take time mama mtafute mumeo ujue yuko wapi? anaishije? why no mawasiliano? coz naamin unauwezo wa kumpta tu ukizingatia kuna source za uhakika za info zinazo weza kukusaidia na naamini hao aliosoma nao bado anawasiliana nao watumie hao kumpata.
hapa unatafuta future end ya maisha yako kama ulifait kumpta na kuwa naye then fait kujua hatima yenu,

dada usikae ukasubir kurud kwake kwa siku na saa tusioijua kama Yesu bhana (kwa iman yangu)

andaa mazingira chukua likizo nenda! tena hapo hata bwana DB anaweza kukusaidia kama kwel anakupenda ili hata mkianzisha mahusiao yenu hakuna wakuwabughudhi!!! stand up mama mtafute!! unamapenz naye sawa lakn nakuhakikishia hakupend tenaaaaaaa!

watoto wataelewa tu na thank God unasema ni wakubwa omba Mungu kwa ajili yao watakuelewa mama!!!

hata wao wenyewe wanajiuliza mbona baba hatujamuona ili wanahis may be nyie mnawasiliana they have to know kwanini baba yao hawajamuona! hao ndo aina ya wazazi ambao wanatelekeza watoto later yakiwashinda walikojuwa wanabak mtoto wangu huyu!!

yeye atabaki kuwa mtoa mbegu kiunoni kwake lakni si baba yao!!
nasikia kulia kwa ajili yako!!
 
Polee dada!
Kimsingi huyo DB ni hatari kwako ingawa wengi wamehisi kama ni bahati kwako. Huyo DB ana matatizo yake tena huenda anadhamira tofauti na wewe unayoifikiria. Tena kutoka ukanda ule ? Think twice.

Wewe ndiye kichwa cha familia kwa sasa,tumaiini la watoto wako lipo kwako. Usifanye maamuzi yatakayoathiri saikolojia ya wanao kwa lolote lile. Acha watoto wasubiri baba arudi hata kamma itakuwa miaka kumi ijayo.

Hakikisha unapata mawasiliano ya mumeo ikiwezekana hata uende alipo. Ujue ukweli halisi wa mumeo kuliko kusikia maneno ya watu. Maana huenda hata mumeo kaolewa na dume huko. Hivyo jitahidi upate sauti ya mumeo ktk mustakabali wako.

Achana na DB moyo wako usipate mashaka. Sidhani kama unashindwa kujizuia na mihemko kwa umri huo.
 
BD mie najiuliza ivi huyu dada kwanza ni mzima ama ni ndondocha?

mwanaume miaka 5 sijui 3 hana mawasiliano?? ..............................

alee wanae baasi aachane nae kama vipi aka file divorce basi.
atavumilia ndo yale ya mtu anamjia na visukari na presha

Don't blame her mimi mwenyewe nina mwaka wa 5 sasa tumeseparate na mume, niko kwenye hali hiyo hiyo ya sintofahamu na tuko nae mji mmoja, hajaoa bado...pengine na mimi nianzishe uzi nipate ushauri....
 
Embu kwa tenganisha hizi mada mbili akilini mwako, yaani usitafute conclusion kwa pamoja ["Hatma ya ndoa yako" na "Suala la DB"]....................., kumbuka mumeo alishawahi kukupenda zaidi ya anavyoonekana DB sasa, nini kilitokea??? je mazungumzo baada ya habari hii yatakuwaje tena???
 
kwanza kabisa usikimbilie kwenye ndoa ukaamini ndiyo kuna furah, wakati hapo ulipo unapata furaha sema ni upweke unaohitaji subira, imagine huyo anayetaka kukuoa ujamjua vizur, je anawatoto wangapi? Na ushawah hisi kitu kuwa kuna watu kama hao wakifa mtoto wako harithi kitu hapo? Atarithi wake tu. Utajikuta umemtumikia yeye ila mtoto wako hapati faida, unaweza pia pata upinzani toka family yake kuhusiana na hiyo ndoa ukajikuta rafik ni wewe na yeye tu ila ndugu hawasaport ndoa hiy na we upo ugenini. Cha kwanza kabisa dada mwambie unafanya kaz na haupo tayar kuacha, mwambie hata mkioana we hautaondok tz na unahitaji uendelee ishi hapa hapa tz, then mume uliyenaye unatakiwa ukaombe talaka mahakamani kuwa mume wak ametelekeza family 3 yrs hivyo unakosa haki zako kama mwanandoa mfano haki ya tendo la ndoa konjugal rights, matunzo ya mtoto, so unahitaji court devorce pale utachukua sumons ya kuita ndugu zake kuisaidia mahakama kujua ukweli juu ya maisha ya huyu bwana, kisha ndugu wataamriwa kumwita kadri itakavyopangwa na mahakama. Na kama hatotokea bila sabab ya msingi basi mahakama itaamua kesi kwa upande mmoja. So tafuta wakili apa atakapoandika pertion ataiomba mahakama itengue ndoa, watoto wapewe haki ya kumwona baba yao anapowahitaj, ila baba hatoshiriki tendo la ndoa na wewe. Pia kushea mali na wewe ila mtoto anaruhusiwa kurithi mali pale baba atakapoona inafaa kufanya hivyo. kisha jipange zako tulia fanya mambo yako ikitokea ndoa yako inafanyikia tz na huyu bwana hapo guarantee ya maisha yasiyo na usumbufu ipo kuliko ndoa ikifungwa ugaibuni we ukaacha kazi ukaenda huko kumbe mwanaume kuna vitu amekudanganya unakuja kujua wakat upo kwenye ndoa utakuwa umepoteza mwelekeo wa maisha alafu utaingia kwenye matatizo.
 
Kwanini usiwe unachepuka na DB ukitaka kuondoa mihemko yako, ndoa ni jina tu....dushe ndo kila kitu unachohitaji kwa sasa.
 
nadhani pia ni vema kupata kauli au talaka ya mume wako dada, maana kama yupo silence, ina maana kamdanganya hata huyo alie nae huko.talaka ndo safe side yako.
 
Terminate hiyo ndoa, terminate huyo DB, jipange upya kama mama Wa watoto watatu sijui wawili na baba yao

Kamwe usiende kuolewa mbali na kuacha kazi dada yangu cause ugenini na ndoa hiyo Mpya plus watoto wanaokutegemea aah! Utalemewa na mengi. Kama utahidi kuolewa subiri upate mtu utakayeweza kumsoma kwanza siyo huyo aliyembali hivyo labda kama atahamia huku OK, pendaneni.
 
hivi gfsonwin na BADILI TABIA, Mtu miaka 3+ hakuna barua wala nini halafu eti asijicommit hadi ajue hatma? Kama uko na ndoa hamna mawasiliano, umekuwa blocked kwa maneno na matendo, na mtu amerudi hadi mtaa wa tatu hana habari na wanae wala wewe. Halafu ati unaendelea kumpenda? Unampenda nini hapo kwa mfano?
King'asti kupenda hakuna macho,kwa mfano mtu akiyapenda hayo mapaja,hawezi kuona bunduki unayomlenga.
 
Last edited by a moderator:
twende taratibu dada (nakuchukulia kama mdogo wangu).

Unampenda huyu bwana? Manake moyo nao una kiherehere. Tulia kwanza mchecheto upite, manake kuchat na mtu miezi sita sio sababu ya kumpenda. Wewe uko lonely and vulnerable (take note, kwa hiyo husisha akili kwenye maamuzi)

Nimefurahi unaangalia mambo ya msingi:

1. Unahitaji kujua kama unampenda huyu ndugu. Lakini still wewe sio binti mdogo na kukimbilia ndoa sio muhimu sana ( angalia usiwe unakimbilia sex pia). Ndoa ni commitment ya maisha.

2. Hakikisha jamaa anaonana na ndugu wachache sana unaowaamini, pamoja na wanao. Waambie watoto that is your good friend na uwaone wanamchukuliaje. Na wewe unahitaji kukutana na wanae

3. Nafurahi kuwa unawaza kazi yako pia. Come what may, usiache kazi. tafuta kazi ya hadhi hiyo hiyo ama zaidi na hiyo ndio condition ya kuhamia huko. Hata kama itabidi msioane hadi upate kazi. Kubalianeni mambo ya msingi ikiwemo wewe kufanya kazi. Hao wenzetu wana tamaduni tofauti, ukimuambia mtoto wa binamu wa mjukuu wa ukoo wao baba kwa upande wa mama anahitaji msaada hawaelewagi. So kazi yako ishikilie haswaa.

4. Wakati huo mnaendeleana kujuana na huyu ndugu, unaweza kufanya mipango ya talaka. Lakini ningekuwa wewe, nisingesaka talaka ili niolewe na DB. Ningesaka talaka kwa sababu nimechoka kuishi kwa suspension ya kungojea mtu ndio nianze kuishi wakati huo yeye anaendelea kuishi na kufurahia malimwengu. Huyu DB asiwe sababu ya kutaka talaka manake nae akikuacha utaumia sana

Haya maneno yako, kuwa its too early kujicommit yanaonyesha maturity yako. Nimekupenda bure kabisa. Muambie ni mapema sana kufunga ndoa, ni muhimu tuongee mambo yote na kuyamaliza, na tukutane na ndugu pia.

Kila la kheri. Mwisho wa siku trust your guts. Ni sawa kukosea kuamua, ila utakosea usipoamua kabisa na kupelekwa kama jahazi bovu

I second you!!!
 
Back
Top Bottom