Mwanamke wa type hiyo ni wanawake watafutaji,wapambanaji ndio huwa hivyo.
Unajua wanaume inatakiwa tuelewe wanawake wapo katika makundi binafsi mimi nimewagawa ktk makundi mawili tu.
1.Mwanamke Mwanamke
Huyu ni pure woman,sio fighter yeye ana behave kama mwanamke na heshima zake,anafanya kazi kawaida, sio mvivu lakini sio mchapakazi, Ule msemo wa Mwanamke huwezi mlinganisha na mwanaume, Wanawake wa kundi hili ndio ambao husemewa.
Wanawake flani Rojo Rojo sio rojo kwa maana ya uzembe au udhaifu la hasha ila ni wana ule ukike kike as how God Creates them.
70% ya wanawake chini ya Jua wapo kundi hili, na ndio wengi wengi wengi, wanahtaji mwanaume ili wafike sehemu hawawezi wao kama wao bila kuwezeshwa katika kila kitu. Pure Women.
2.Mwanamke Mwanaume
Huyu ni mwanamke aliekamilika ila ana kikwazo cha Jinsia,She is a fighter haswaa, anawaza positivity kwa mwanaume wake ktika mapambano yake, hawa ndio wale haoni shida kumpa mwanaume wake mshahara wake wote anaopokea ili huyo mwanaume afanikishe jambo Flani, anaamini mwanaume anaweza hivyo anafanya kila awezalo mwanaume wake afikie paleee.
Sio tu kumsapoti na kumpambania mumewe/mpenzi wake ila hata wanawake wa kundi hili sio Poa wanapush mno, wana ma idea ya biashara akikuomba hela afungue biashara ni kweli anaenda kufungulia biashara, hana matumizi ya hovyo na luxury kama wanawake wa pale juu.
Wana bajeti ya maisha hawa, kama ndio mama ako yupo kundi hili utakua shahidi ni mama ambae haoni shida kuwalisha ugali wiki nzima ila sio kwamba nyie n maskini ila n mama Saving, mna pesa na watu wanawakua hivyo huko nnje ila ndani ya nyumba ni bajeti sio kidogo. Strictly women wana kiu ya mafanikio.
Wanapenda wanaume wachakarikaji hawanaga time na mahandsome sijui six pack wao wanataka mwanaume mtafutaji anae ijua shilingi mambo ya muonekano wao wana deal nayo kwa uchache sana kwasababu wamefocus katka mafanikio Zaidi yake na Familia.
Wana ndoto za kufikia mbaliii wawe watu flani katika level zote kibiashara zao,familia zao,nk nk.
Huuu UZI umewaongelea wanawake Kundi no.2 ambao kwanza ni wachache (picha linaanzia hapo)
Kuwapata sio rahisi na ili uwapate hawa huwezi tu kukaa ukamuotea njiani umpate,hawa unawapata mkiwa ktk majukumu.
Either wewe upo na majukumu yako au yeye au wote mkaelewana.
Tofaut na kundi no 1 wale wapo kila kona,hata mdada anaetembea pembeni hapo ni no 1.
Balaaa la Kundi no 2 hawa bana wengi sio wazuri kimuonekano, ndio mana wanaume wengi wanao date na wanawake wa kundi hili Hufanikiwa na mwishowe huwaacha na kutafuta kundi no 1.
Ki ukweli kwenye mahusiano wanawake wa kundi hili wanaongoza kwa kuachiwa maumivu makali sana na wengi huachiwa maumivu kule mwishoni kwenye NDOA.
Shida kuu ya sisi wanaume tunashindwa waweka hawa wanawake wa kundi no 2 wawe kama wa kundi no 1, na badala yake tunawaacha na kurudi kule juu kundi no 1.
WANAUME
Ukiotea Pisi kali ile kali haswaa ipo kundi no 2 usi iache,ni chache sanaaaa, yani katika 100 unaweza otea hapo wawili au watatu.
Pata picha upate Chombooo Chombooo halafu ipo kundi no. 2 dunia yote utaiona yako, mziki ni kundi no 2 sura zao maumbo yao tunafanana nao kwa namna flani (natania bana)
Mapenzi ni kama Karata za kulamba huwezi Jua utalamba Nini, unaweza ukalamba weeee Mwisho ndio ukalamba JOKER.
Muhimu tuendeleee kuishi maisha yetu mtu sahihi atakuja tu,ila usikae unaanzisha mahusiano tofaut kisa kuna aina flani ya mtu unamtafuta,will cost you.