Ninazo hoja kidogo ambazo nadhani zinaonshesha mahakama ya kadhi itakuwa na maslahi kwa watanzania wote 1. Sheria nyingi za serikali zilirithiwa kutoka ukoloni amba zo pia zilikuwa influenced zaidi na ukristo kwa hiyo haziwafai waislamu. 2. Pia kitu cha kufahamu ni kuwa mambo yakiamuliwa kijamii hayana uzito kisheria kwa hiyo ni muhimu mahakama ya kadhi kupewa. 3. Kila mtanzania ana haki ya kupata haki mahakamani kwa mujibu wa sharia , kwa hiyo mahakama ya kadhi inastahiki kusimamiwa na kugharamiwa na serikali sababu ni wajibu wa serikali kuhakikisha haki inatendeka 4. Mahakama ya kadhi sina sifa ya kusikiliza kesi na kutoa hukumu kwa mda mchache kuliko mahakama za serikali kwa hiyo hii itapunguza gharama serikalini na pia kupunguza idadi za kesi zinazongoja kusikilizwa.. 5. Mahakama ya kadhi haitatumika pale mtu wa dini nyingine anapo husika kama mdai au mshutumiwa au wote watake na wakubali uamuzi. 6. Hizi mahakama zipo nchi nyingi na zina fanya bila tatizo 7. Makosa ya jinai yatakuwa ni jukumu la mahakama za serikali