Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
1. CCM hadi hivi sasa imefanya juhudi kubwa za kuifanya CHADEMA ionekane kama chama chenye fujo na kinaharibu "utulivu na amani" wa Watanzania!
CHADEMA bila kujua hila za CCM kimeingia mkenge hasa viongozi wake wanapodai kwamba kura zikiibiwa "damu itamwagika!" Kauli hii iliwagharimu CUF na kilionekana ni chama kinachokusudia kuleta fujo, sasa hisia hizo zimehamia CHADEMA!
2. Kauli zinazoashiria kupunguza idadi ya wapiga kura:
- Nikiingia madarakani nitamtimua Mhariri wa Daily News: Mpiga kura huyo baada ya kuisikia kauli hiyo ataipigia kura CHADEMA?
- Nikiingia madarakani nitafuta vyeo vya U-DC: Hapa ina maana ma-DC wote hawatampigia kura Dkt Slaa kwa kuwa automatically vibarua vyao vitaota nyasi.
- Nikiingia madarakani nitawaburuza mahakamani mafisadi wote: Hapa ina maana kuwa wale wanaojihisi kuwa ni mafisadi (kwa bahati mbaya hawa wako wengi)hawataipigia kura CHADEMA!
nk.
Kauli hizi zirekebishwe ili zilenge electorate wote kwa ujumla na si kubagua kwa namna yoyote, hata kama nia ipo ya kufanya hayo! Lugha nzuri itumike ili kuwaelimisha watz maana kila jambo jipya huwa haliaminiki mwanzoni!
3. Ahadi za huduma za jamii (km elimu) kuwa bure: Ahadi hii imekuwa questioned hata na watu wasioenda shule (watu wa kawaida). Hapa yanahitajika maelezo ya ziada na si kudai kuwa tutachukua fedha za EPA ambapo hizo fedha zikiisha ndio inakuwaje! Majibu yangekaa kitakwimu zaidi, km kuna idadi kadhaa za wanafunzi, then kila mwanafunzi anagharimiwa kiasi fulani, then bajeti yetu ni kiasi fulani, etc.
Haya ndio yangu kwa leo wanaJF hasa wanaoitakia mema CHADEMA!
Tujadili!
CHADEMA bila kujua hila za CCM kimeingia mkenge hasa viongozi wake wanapodai kwamba kura zikiibiwa "damu itamwagika!" Kauli hii iliwagharimu CUF na kilionekana ni chama kinachokusudia kuleta fujo, sasa hisia hizo zimehamia CHADEMA!
2. Kauli zinazoashiria kupunguza idadi ya wapiga kura:
- Nikiingia madarakani nitamtimua Mhariri wa Daily News: Mpiga kura huyo baada ya kuisikia kauli hiyo ataipigia kura CHADEMA?
- Nikiingia madarakani nitafuta vyeo vya U-DC: Hapa ina maana ma-DC wote hawatampigia kura Dkt Slaa kwa kuwa automatically vibarua vyao vitaota nyasi.
- Nikiingia madarakani nitawaburuza mahakamani mafisadi wote: Hapa ina maana kuwa wale wanaojihisi kuwa ni mafisadi (kwa bahati mbaya hawa wako wengi)hawataipigia kura CHADEMA!
nk.
Kauli hizi zirekebishwe ili zilenge electorate wote kwa ujumla na si kubagua kwa namna yoyote, hata kama nia ipo ya kufanya hayo! Lugha nzuri itumike ili kuwaelimisha watz maana kila jambo jipya huwa haliaminiki mwanzoni!
3. Ahadi za huduma za jamii (km elimu) kuwa bure: Ahadi hii imekuwa questioned hata na watu wasioenda shule (watu wa kawaida). Hapa yanahitajika maelezo ya ziada na si kudai kuwa tutachukua fedha za EPA ambapo hizo fedha zikiisha ndio inakuwaje! Majibu yangekaa kitakwimu zaidi, km kuna idadi kadhaa za wanafunzi, then kila mwanafunzi anagharimiwa kiasi fulani, then bajeti yetu ni kiasi fulani, etc.
Haya ndio yangu kwa leo wanaJF hasa wanaoitakia mema CHADEMA!
Tujadili!