Ushauri tuendelee kujenga "metre gauge railway" sehemu nyingine

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,609
8,749
Watanzania na Waafrica kwa ujumla tunapenda vitu vizuri na vipya. Mimi naishi Texas, USA na nataka kuwajulisha reli zenye manufaa makubwa sana kwenye uchumi wa nchi hii ni reli za kizamani "metre gauge railway" na sio "Standard Gauge Railway" za umeme.

Hizi reli za kizamani ndizo zinasafirisha mafuta, magari, mifugo na mavuno mengi ya kilimo sehemu tofauti za nchi kwa bei rahisi.

Mfano kuna reli kutoka California mpaka Texas kote huko inapita kukusanya mafuta sehemu tofauti mpaka yanafika Houston, Texas ambako yanasafirishwa kwenda nje ya nchi au kusafishwa kwa matumizi ya ndani.

Nimesema yote hayo kuhimiza na kushauri upanuaji wa metre gauge railway hasa sehemu zenye kilimo kuanzia kusini mwa nchi yetu kote, Tanga mpaka Mwanza, Arusha mpaka Nairobi, Tanga mpaka Mombasa na sehemu nyingine muhimu.

Hii itasaidia sana kukuza Kilimo kwa kupunguza gharama kubwa za usafirishaji wa magari ya mizigo. Lakini uzuri hizi reli ni za bei nafuu kutengeneza. Lengo kubwa liwe Kilimo huu ni ushauri wangu.
 
Kwanza ukumbuke raiway za standard gauge haimaanishi ni railway inayotumika na train za umeme.
TAZARA ni standard gauge lakini hawatumii electric locomotive.. Unaweza kukuta hizo locomotive (train) za fuel uonazo Marekani zinatumia teknolojia za SGR kwenye railway yake. Electric locomotive siyo SGR.
Pili jiulize mahitaji ya SGR yanatokana na sababu zipi za kiteknolojia, kiuchumi na pia sababu ya train zilizopo sokoni na vipuri vyake.
 
Why SGR?
The SGR railway has the ability to carry heavy loads at high speed as opposed to the current Meter gauge Railway (MGR). Tanzania's SGR uses electric locomotives and has the capacity to transport passengers and cargo shipments at 160 kilometers per hour.
Source: www.tanzaniainvest.com link => SGR Archives.
 
Watanzania na Waafrica kwa ujumla tunapenda vitu vizuri na vipya. Mimi naishi Texas, USA na nataka kuwajulisha reli zenye manufaa makubwa sana kwenye uchumi wa nchi hii ni reli za kizamani "metre gauge railway" na sio "Standard Gauge Railway" za umeme.

Hizi reli za kizamani ndizo zinasafirisha mafuta, magari, mifugo na mavuno mengi ya kilimo sehemu tofauti za nchi kwa bei rahisi.

Mfano kuna reli kutoka California mpaka Texas kote huko inapita kukusanya mafuta sehemu tofauti mpaka yanafika Houston, Texas ambako yanasafirishwa kwenda nje ya nchi au kusafishwa kwa matumizi ya ndani.

Nimesema yote hayo kuhimiza na kushauri upanuaji wa metre gauge railway hasa sehemu zenye kilimo kuanzia kusini mwa nchi yetu kote, Tanga mpaka Mwanza, Arusha mpaka Nairobi, Tanga mpaka Mombasa na sehemu nyingine muhimu.

Hii itasaidia sana kukuza Kilimo kwa kupunguza gharama kubwa za usafirishaji wa magari ya mizigo. Lakini uzuri hizi reli ni za bei nafuu kutengeneza. Lengo kubwa liwe Kilimo huu ni ushauri wangu.


Reli za umeme hatuwezi kuweka kila mahali ushauri wangu uzingatiwe

mwigulu, Pascal Mayalla zitto junior
 
Back
Top Bottom