Ushauri: Rais Samia apumzike Urais 2025

technically

JF-Expert Member
Jul 3, 2016
11,975
48,843
Kwa mtazamo wangu binafsi napendekeza Rais wetu Mama Samia apumzike mwaka 2025 kama analo wazo la kuendelea kutuongoza.

Kwanza niseme wazi Mama ni moja ya Marais bora kabisa kuwai kutokea katika taifa letu. Sijawai kusikia kashifa yeyote ya wizi na ufisadi kutoka kwake, ni Rais mwadilifu kweli kweli.

Ila shida yake ipo kwenye kuchukua hatua juu ya watu wanaomzunguka na kufanya mambo ya hovyo katika utawala wake.

Naunga mkono michakato yote ya kodi inayoanzishwa kufanyika Ila shida ipo kwenye matumizi yake ni jinsi gani tunaitumia hiyo pesa inayopatikana kwenye kodi, mfano serikali kwa ujinga imetumia bilioni 629 kwenye zoezi la sensa pekee huu ni ufisadi.

Zoezi lenyewe watu wengi bado hawajahesabiwa mpaka sasa. Leo ni siku ya 6 ndani ya zile siku saba zilizopangwa maana yake kesho ni siku ya mwisho. Zoezi limegubikwa na wizi na ufisadi wakati zoezi lingewatumia mabalozi wa nyumba kumi tu na mwenyekiti wa kijiji lingekuwa limeshakamilika kwa 100%.

wangetumia karatasi za kawaida kujaza taarifa za watu, then kwenye kata ndio wangeweka mfumo wa TEHAMA wa kuingiza zile taarifa kwa kutumia tablet tungefanikiwa kwa 100%

Kukwama kwa zoezi la katiba na tume huru ya uchaguzi kabla ya 2025, ili nalo ni donda ndugu. Watu wanakushauri kwamba utashindwa uchaguzi 2025 ukileta sasa Katiba mpya na tume huru ya uchaguzi.

Wanakudanganya ungeweka mazingira sawa ya uchaguzi na katiba lazima watu wangukupigia kura 2025 ili kulipa mema uliyowafanyia hata kama wasingekuchagua mema yako yangeandikwa duniani na mbinguni.

Swala ya mfumuko wa bei ndio bomu kuu, watu hawakatai kwamba vitu vinapanda duniani lakini watu wanachokataa ni kwanini vitu muhimu ndio vipande tu kwani vitu vingine ambavyo havipandi vitu havisafirishwi?

Mfano unakuta kiberiti kinauzwa shilingi 100 Tanzania nzima hakipandi bei zaidi ya miaka 10, wakati na chenyewe kinatumia mafuta kuzalishwa. Ila Ngano, mafuta ya kula na sembe inapanda kila muda kila mwaka.

Utasikia usafirishaji, kwanini mafuta ya alizeti yanayozalishwa Rukwa na Singida hapo hapo kiwandani ukiyafuata yana bei ile ile kama unayoinunua Dar es salaam?

Mh. Rais hapa tukubaliane kwamba umeshindwa ku control inflation kwa sasa, mwezi umepita mafuta yanashuka kila siku kwenye soko la dunia kwanini sisi mafuta yanazidi kupanda tu?

Kwanini uwashughulikii wafanyabiashara Ili waache ulafi wa kutaka faida kubwa?

Tofauti yetu na Zanzibar iko wapi, kwanini Zanzibar kila kitu kinachoingizwa kwenye visiwa hivyo bei zake zipo chini, hata bei zao za mafuta zipo chini kuliko sisi au ndio kusema Zanzibar ni taifa tofauti na sisi?

Basi Kama hivyo Rais Mwinyi ana uwezo wa kupambana na mfumuko wa bei vile, bora tumchukue aje atusaidie huku bara baada ya 2025.

Mambo ni mengi, Ila naomba nikushauri kama unahitaji heshima ya milele basi pumzika 2025 aje mtu mwingine afanye kazi ya Urais. Inawezekana watu wanakushauri vibaya kwa sababu haukuchaguliwa na wananchi ili kukuchonganisha kwa watanzania.
 
Kuchukua hatua juu ya watu anaowaongoza anaweza, ndio maana aliwaondoa kina Kabudi na Lukuvi.

Tatizo lake kuwachukulia hatua wale vipenzi vyake wa karibu aliowateua yeye ndio anakuwa mgumu kuwachukulia hatua.

Matokeo yake jamaa sasa wanajiamini wanajua hayupo wa kuwafanya chochote kwani ulinzi wanao.

Hii hali ikiendelea, ndio mbele ya safari itaenda kuzalisha mafisadi wa utawala wake, hao "untouchables" wataanza kufanya ujanja na baadhi yao naona wameshaanza.

Hao mafisadi wapya ndio watakuja kuchafua taswira yake siku itakapofika akaondoka madarakani hataacha legacy yoyote, kwa namna alivyoonesha kiu ya kuutaka Urais 2025, sidhani kama ataondoka kabla ya 2030.
 
Mkuu technically iko hivi;
1. Ni kweli mama ni kiongozi muadilifu sana na mpenda haki. Aidha, ni mara chache sana kusikia kiongozi toka zbar asiye mwadilifu.

2. Kuwa na kiongozi mmoja bora peke yake hakutoshi kufanya mambo yaende sawa. Kutegemea mtu mmoja pekee ili kila kitu kiende sawa, ni sawa na kutegemea injini zuri kwenye gari yenye tairi zenye pancha.

3. Kuhusu kuchukulia watu hatua; unapaswa kuelewa kuwa nchi ina sheria lakini pia kuna actors tofauti tofauti waliopewa majukumu tofauti tofauti na mengine ya kitaalamu. Ni kweli kuna maeneo yenye matatizo ila kufikiri kama Rais anaweza kuingilia kila kitu na kuface mtu mmoja mmoja na kumchukulia hatua sio sahihi. Kiongozi mkubwa kazi yake ni kutoa maelekezo sahihi.

4. Kuhusu mfumuko wa bei; kabla ya kupendekeza solution kwenye jambo lolote, ni muhimu sana kuelewa chanzo sahihi cha tatizo.

Mwisho, ili kila kitu kiwe sawa, ni muhimu kila mtu atekeleze wajibu wake kulingana na uwezo wake na sehemu alipo. Tukiwa na watu wengi wanaofanya hivyo, ndio tutaweza kupiga hatua kwa haraka.

Vinginevyo ni sawa na kuwa na kocha mzuri na wachezaji hawana mbio, tutabakia kulaumu makocha tu kumbe ishu sio kocha bali wachezaji.
 
Mkuu technically iko hivi;
1. Ni kweli mama ni kiongozi muadilifu sana na mpenda haki. Aidha, ni mara chache sana kusikia kiongozi toka zbar asiye mwadilifu...
Sheria zinawabana sana wanaokosoa matendo ya serikali kama aliyetumbuliwa juzi tu kisa kuongelea tozo, na kiongoz aliyetamka nchi itapigwa mnada. Ila kwa wezi sheria nchi inasheria ambazo ni ngumu kuzifuata.

NB: Mwezi agosti tuliambiwa kwenye soko la dunia mafuta yalishuka bei na sisi kuambiwa yatashuka mwezi wa 9 maana ya agosti yaliagizwa kipindi bei iko juu. Tunasubiria kuona hiyo septemba
 
Mama Samia kama anasoma humu namshauri jambo moja kubwa...

Weka pembeni mawaziri wako ambao uliwateua kama kuwafuta machozi kwa kutumbuliwa na mtangulizi wako.

Kuna wawili watatu ni sumu mbaya kwako dhidi ya wananchi. Wanautaka urais na wanatumia nafasi zao ulizowateua kuhakikisha lengo lao kinatimia lakini wanakuangusha kwenye utendaji.

Wapo karibu sana nawe kwenye mambo mengi lakini walimvuruga sana Muungwana na alipokuja Buldozer aliwastukia akawapiga wino.

Unahitaji kujenga nchi ili matumaini yakue na siyo kuwasikiliza wasaidizi wako wanaokuombea uanguke kila wanaposali
 
Mama hana ujasiri wa kuchukua hatua kwa wezi na wazembe, tunamshukuru kwa miaka yake aliyotufusha 2025 apumzike tu
Kazi ya kiongozi mkubwa kama Rais sio kuchukua hatua kwa mtu mmoja mmoja ispokuwa kwa wateule wake tu wa moja kwa moja. Kazi ya Rais ni kutoa miongozo, maelekezo na muelekeo wa taifa kwenye mambo makubwa makubwa.

Then kuna mifumo ya kitaasisi ambayo inatakiwa ifanikishe masuala ya kiutendaji kama hayo ya kuchukuliana hatua na.k.

Kwa bahati mbaya kwenye jamii yetu tuna watu wachache wa maana na wengi wa ovyo. Hivyo kutoka kwenye sample hiyo, ndio tunapata wawakilishi wa maeneo mbalimbali. Na tunachoona ni matokeo ya kuwa na jamii ya aina hiyo.

Hivyo pamoja na kuwa na kiongozi mzuri, mabadiliko ya kijamii yanayolenga kila mtu kuwa na utamaduni wa kutekeleza wajibu wake ni muhimu kuliko kitu kingine chochote.
 
Mkataa pema pabaya panamuita. CCM hii tunayoijua haitosita kutuletea nduli mwingine.
Mtu anayelalamikia kila kitu, anastahili kupewa chochote. Ndio maana wengine tunashauri kuwa, ni kuhimu kuwa principles. kiongozi yoyote anayefanya jambo linalokubalika kwa mujibu wa principle husika aungwe mkono.

Sasa kuna wenzangu na mie, wao ikiwa ya moto wanalalamika inachoma, ikiwa ya vuguvugu wanalalamika inatia uvivu, ikiwa ya baridi wanalalamika itawaua; hatimae mfanyaji anapoteza incentive anaamua kufanya vyovyote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom