Jamani wanajamvi naombeni ushauri.mimi ni mama wa familia japo bado sina mtoto naishi na mume wangu na dada anaenisaidia kazi nyumbani.ni mfanyakazi japo kwa muda sahivi nina likizo.nimepata dada wa kazi kama wiki tatu zimepita tatizo lake tangu nimeanza kukaa nae haongei,hali hata kwa siku nzima au anakula mlo mmoja then anagoma kula wakati mwingine.nikimtuma ua kumsemesha kanuna na hajibu chochote mpaka atakapotaka yeye kunisemesha.jana nikavunja ukimya kumuuliza nini tatizo mpaka anakuwa hivyo akaanza kulia.hakula akalala na njaa leo nimeamka nikakuta hayupo karudi muda huu kamm masaa mawili tangu nilipoaamka kumuuliza alikuwa wapi kaanza kulia na kunieleza mambo makubwa sijawahi dhani lama ni hayo.siku zote alikataa nieleza nini kinamsumbua mpaka leo nilipomwambia bora nimrudishe nyumbani naona kashindwa kukaa hapa.ananambia ana mashetani yanamkataza kuongea na mimi na yanamfanya anichukie hata nikimfanyia kitu gani kizuri.tatzo lake sahivi ananipigia magoti kuniomba nisimrudishe kwao jumla but nimpe kama likizo ya siku mbili akirudi atakuwa sawa.nahitaji mtu wa kunisaidia coz soon likizo yangu inaisha lakini kwa huyu nashindwa nichukue uamuzi gani.analia sana na anaomba msamaha kwa yote na anaahidi atabadilika baada ya kwenda kwao kutambikiwa kwa siku mbili.ananiogopesha na sijui nifanyaje.naombeni ushauri jamani.
Bi dada achana na habari za kukaa na mabinti iwapo huna mtoto unless kama ni mjamzito ila kama bado ishi wewe na mumeo jaribu kuboresha maisha kwa kuweka vitendea kazi vya kukusaidia. ukianza kuhangaika na mabinti wenye mapepo leo hi hata kachanga huna ukija kupata si ndo upakatiwa mtoto na shetan lenyewe??
huo mshahara unaomlipa na kula anakokula nk ni bora ununue dishwasher, na washing mashine, pamoja na mopa na blower. siku ya j1 unafua na kusafisha nyumba yako na kupanga kama zinakuzidi tafuta kijana wa kiume ambaye atakuja akupasie iyo siku ya j1 na kukufagilia uwanja basi.