Johnson12345
JF-Expert Member
- May 29, 2023
- 206
- 422
Habari,
Kuna rafiki yangu mmoja nilizoeana nae mda kidogo na tunafamianane kutoka na biashara zetu yeye anaumri wa 43 now. Ila kwa sasa anahali mbaya ya kiafya anaumwa magojwa yasiotibika haya kupona haiwezakani kabisa.
Sasa miaka kadhaa ya nyuma alipata mchepuko, katika kukutana na mchepuka akampatia ujauzito akafanikiwa kupata mtoto wa kiume, kafananae sana maana nimemwona kwenye picha. Baada ya miaka miwili akachepuka tena na huyo huyo mchepuko wake akampa tena ujauzito alimlumu, ila mchepuko alimwambia kuwa mimi nakupenda.
Akaamua kuvunja mahusiano na mchepuko. Ila baadae akaona ngoja tuu awatambulishe watoto kwa kaka zake na dada yake. Alifanikiwa kuwatambulisha ila kwa mkewe hakufanya hivyo. Kutokana na kuaminiana na mke wake.
Sasa ni mogonjwa yeye na mkewe wamejenga nyumba tatu na biashara zao na vitu vingine kama magari. Yeye na mkewe wamezaa watoto 2 tuu.
Shida inakuja hizo mali zote limeandikwa jina lake ila ameshirikiana na mkewe wa ndoa kabisa. Yeye kaniambia tangu aishi na mkewe hajawahi kugombana nae wala kumuona mkewe anashida yoyote. Amenikambia kuwa ni mke mzuri sana na mama bora, hana shida yoyote, hicho ndio kilipelekea hata kuwaambia kaka zake na dada yake wasimwambie mkewe. Hataki mkewe aumie.
Wadau ushauri, maana anaona akiacha tuu mali watagawana na kumuacha mkewe na maumivu makubwa sana. Yeye hilo hataki, sasa alikuwa ananiambia mimi kuwa abadilishe hati ya nyumba na mali zingine kwenda kwa majina ya watoto wa ndoa tuu. Mimi nilikuwa sina cha kumjibu nilibaki namwangalia tuu.
Nikaona isiwe shida ngoja nije hapa JF. Maoni yenu wadau anataka afanye sasa.
Kuna rafiki yangu mmoja nilizoeana nae mda kidogo na tunafamianane kutoka na biashara zetu yeye anaumri wa 43 now. Ila kwa sasa anahali mbaya ya kiafya anaumwa magojwa yasiotibika haya kupona haiwezakani kabisa.
Sasa miaka kadhaa ya nyuma alipata mchepuko, katika kukutana na mchepuka akampatia ujauzito akafanikiwa kupata mtoto wa kiume, kafananae sana maana nimemwona kwenye picha. Baada ya miaka miwili akachepuka tena na huyo huyo mchepuko wake akampa tena ujauzito alimlumu, ila mchepuko alimwambia kuwa mimi nakupenda.
Akaamua kuvunja mahusiano na mchepuko. Ila baadae akaona ngoja tuu awatambulishe watoto kwa kaka zake na dada yake. Alifanikiwa kuwatambulisha ila kwa mkewe hakufanya hivyo. Kutokana na kuaminiana na mke wake.
Sasa ni mogonjwa yeye na mkewe wamejenga nyumba tatu na biashara zao na vitu vingine kama magari. Yeye na mkewe wamezaa watoto 2 tuu.
Shida inakuja hizo mali zote limeandikwa jina lake ila ameshirikiana na mkewe wa ndoa kabisa. Yeye kaniambia tangu aishi na mkewe hajawahi kugombana nae wala kumuona mkewe anashida yoyote. Amenikambia kuwa ni mke mzuri sana na mama bora, hana shida yoyote, hicho ndio kilipelekea hata kuwaambia kaka zake na dada yake wasimwambie mkewe. Hataki mkewe aumie.
Wadau ushauri, maana anaona akiacha tuu mali watagawana na kumuacha mkewe na maumivu makubwa sana. Yeye hilo hataki, sasa alikuwa ananiambia mimi kuwa abadilishe hati ya nyumba na mali zingine kwenda kwa majina ya watoto wa ndoa tuu. Mimi nilikuwa sina cha kumjibu nilibaki namwangalia tuu.
Nikaona isiwe shida ngoja nije hapa JF. Maoni yenu wadau anataka afanye sasa.