Kweli tu
JF-Expert Member
- Dec 25, 2022
- 397
- 441
-Polisi hawakumkomalia, ndio maana wakampa dhamana maana ni haki ya mtuhumiwa.Humu tuliongea wengine kuwa Polisi lazima wakukomalie na kuwa lazima utawekwa ndani nenda na wadhamini wengine wakakujaza ujinga humu wakabeza Yako wapi ndani umeenda .Polisi wa Sasa wanajua Sheria sio utani
Mke Yuko sahihi kuondoka Kwa usalama wake na wanawe
Kuondoka na watoto ni ushahidi kuwa anajali wanawe angekuwa hajali asingeondoka nao angekuachia
Ngoma bado mbichi kwako kisheria subiri mziki wake mahakamani uko nje Kwa dhamana kesi Iko palepale ni ya kanisa dhidi Yako sio ya mkeo dhidi Yako.Unalo hilo
-Polisi ni kazi yao kupokea kila taarifa itolewayo kituoni na kuichukulia hatua na ndio maana kwa uzito wa kosa walitumia busara ya wito na sio kwenda kumfuata.
Polisi hakuepo eneo la tukio, kimpasacho ni kupokea taarifa na kuifanyia kazi, yaani kuchunguza namna kosa lilivyo tokea, na kwavile chanzo hapo ni mgogoro wa kifamila, na polisi wanajua kua kosa la shambuli anaetakiwa kulalamika mi mke na sio mchungaji wa kanisa, pia polisi sio wajinga wakapeleke kosa hilo mahakamani wakati wanajua kua ndoa itakua na mpasuko na tabu itakua kwa watoto, na Polisi ndie mlinzi wa watoto kisheria.
Pia kwa kosa la shambulio ni mahakama ya mwanzo na hukumu yake ni faini, na faini ni pesa ya serekali na sio ya alie lalamika, kosa hilo hafungwi.
Kosa la kufanya fujo pia nalo sana, hata kanisa wafanyeje, hawawezi kulifanya kua kubwa, na hukumu itategemea na thamani ya uharibifu wa mali, tofauti na hapo kama hakuna thamani nayo ni kupigwa faini, kwa kwa makosa yote hayo faini haivuki laki 2 hata kama kuna uharibifu wa mali. Hiyo ndio kisheria.
Polisi wanajua fika kua ili udhaminiwe unatakiwa ktk wadhamini kuwe na mwanaume, na kama ni mdhamini ni mmoja basi awe mwanaume, lakini polisi walimdhaminisha kwa mama mkwe yani mwanamke, hio ni dalili kua hapo hakuna kesi.
Pia hapo kanisani mchungaji sio msemaji wa mwisho na iko wazi kabisa kua kanisa ndio linaiharibu hiyo ndoa, mzee wa kanisa hawezi kutia aibu kanisa lake kwa kwenda mahakamani kuaibika kwa kusimamia kukosa haki ya msingi ya watoto wa miezi minne kunyonya. Atakosa waumini.
Na polisi hawataacha kuuliza swali la msingi kwa mchungaji ktk maelezo yake ya kua, je! Huoni kwamba wewe utakua chanzo cha ndoa hii kufa?