Ushauri mie nipo njia panda

Ushauri mie nipo njia panda

mmmmhhh kwenye miti hakuna wajenzi...ni kumbembeleza mpaka atulie ukitumia nguvu na hasira umemkosa huyo
 
Hapana usimwulize angalia kitu gani anaweza kusimamia. Fanya kumwekea M-PESA ama mfungulie kingine zaidi, MPE ufundi cherehani ajue kushona vyote, kuanzia Mapazia mpaka suti. Usimwache atapotea, Maisha yana changamoto sana
 
kama kila mtu akisoma na akafaulu sidhani kama dunia itakuwa ni mahala pazuri pa kuishi. lazima kuwepo na matabaka. na wengi wetu hatujui kwamba watu wa elimu ya kawaida ndio wanaoendesha maisha ya sisi tunaojiona tumesoma. mfano mdogo tu ni hiyo kitimoto ulioagiza ilifugwa na mtu wa kawaida tu na huenda hata la saba hakumaliza.

so back tu ushauri, ongea nae na athibitishe miradi mitatu tofauti anayoweza kufanya (mmojawapo ukiwa mradi wa kilimo) arafu kwa mradi utaopata maksi kubwa hakikisha unaanza nae kwa usimamizi. ni hayo tu.
 
Huyo sasa........inabidi umuulize yeye binafsi anataka kufanya nini........vinginevyo unaweza kumchinja hadharani.........

Sidhani kama hajamuuliza hilo swali mpaka sasa.
Dogo kashajichagulia fungu lake lililo jema ambalo analiweza
 
Nieleweke ni ndugu yangu 'Damu' mtoto wa Baba Mkubwa.

Kamaliza form four mwaka 2010 kafail alipata ziro na 'D' moja tu, 2011 akareseat ndo kavurunda kabisa, 2012 nikamwambia njoo huku nchi jirani nilipo mie akaja akaanza kusoma Diploma ya HR kaharibu mbaya semister ya kwanza kachemsha na vitabia fulani sio vizuri.

Nikamrudisha home nikamwambia chagua usome nini he jibu nililopata nusu nizimie 'Dada mie kusoma siwezi' nikasema wataka nini sasa. Ngoja nifikirie mie haya he kaenda kwa Mdingi wangu ambaye ni Mdogo kwa Baba yake kawashiwa moto hatari kwa ujinga wake na ushauri wa kipumbavu wa marafiki katoroka akaenda kuishi hostel na rafiki anayesoma CBE.

Jana nimekwenda mahali kula kiti ya moto mara namuona kabeba tray anakuja kunihudumia mie mdomo wazi. Namuuliza hii ndo kazi uliyotaka kufanya ama?? Anaanza kulia eti dada nisamehe nimekosa pesa ya kula imebidi nifanye hii kazi nisaidie.

Mwenzenu mate yalinikauka, maneno yalipotea sikujibu hata neno moja kiti ya moto yenyewe ilikuja nikafunga hata apetite yote iliyeyuka.

Naomba ushauri wenu nifanyeje


kusomesha mtoto asiye wako mara nyingi ni kujinunulia lawama na matusi. Usirudie tena.
 
Nieleweke ni ndugu yangu 'Damu' mtoto wa Baba Mkubwa.

Kamaliza form four mwaka 2010 kafail alipata ziro na 'D' moja tu, 2011 akareseat ndo kavurunda kabisa, 2012 nikamwambia njoo huku nchi jirani nilipo mie akaja akaanza kusoma Diploma ya HR kaharibu mbaya semister ya kwanza kachemsha na vitabia fulani sio vizuri.

Nikamrudisha home nikamwambia chagua usome nini he jibu nililopata nusu nizimie 'Dada mie kusoma siwezi' nikasema wataka nini sasa. Ngoja nifikirie mie haya he kaenda kwa Mdingi wangu ambaye ni Mdogo kwa Baba yake kawashiwa moto hatari kwa ujinga wake na ushauri wa kipumbavu wa marafiki katoroka akaenda kuishi hostel na rafiki anayesoma CBE.

Jana nimekwenda mahali kula kiti ya moto mara namuona kabeba tray anakuja kunihudumia mie mdomo wazi. Namuuliza hii ndo kazi uliyotaka kufanya ama?? Anaanza kulia eti dada nisamehe nimekosa pesa ya kula imebidi nifanye hii kazi nisaidie.

Mwenzenu mate yalinikauka, maneno yalipotea sikujibu hata neno moja kiti ya moto yenyewe ilikuja nikafunga hata apetite yote iliyeyuka.

Naomba ushauri wenu nifanyeje
Mfanye house girl!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom